Kikoti.com

Kikoti.com: habari za uhakika

ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 19 Desemba 2015


CHAPTER 5
RESEARCH
INTRODUCTION: concept of research
Research derived from the French word “recherché” which means to search
So research defined as  Is the act of inquiring making experiment, gathering, or investigating information aimed at discovering new theories and laws.
OR  Is a systematic investigation and study of materials in order to establish fact and reach conclusion
GENELLARY: research is the systematic and scientific process of collecting, analyzing, and interpreting data from the field or from a certain phenomenon.

OBJECTIVE OF RESEARCH
- To search for the new knowledge or to be familiar with a phenomenon.
- To gain familiarity with a certain phenomenon
-To develop theories about a social economic phenomenon
- To test hypothesis so as to find out the reliability and validity with the given cultural setting
-To make evaluation of a certain issues
- to reveal accurate features of certain aspects of social life
- test or approve hypotheses of casual relationships between phenomena

- Importance of Research
- Provides policy makers with accurate information about the subject matter
- used to provide accurate solutions to social problems, used to direct social activities,
-providing reliable information to the data bank,
- members of society become well informed about their society
- remove preconceived ideas in the researchers mind
-creates a spirit of investigation,
-finds accurate solutions to problems,
- provides sources for future
-It allows the identification of problems and finds it is solution.
- It bring awareness in the societies about the social problems
- It emphasize on the prediction of the future of the society
  -Helps in solving different conflict in the societies example land conflict.
TYPES OF RESARCH
Types of research according to the aim or purpose of research:
i. Basic/pure research
ii. Applied research
iii. Evaluative research
iv. Analytical research
v. Fundamental research

i. Basic /pure research is the types of research which is conducted to correct, advance or develop a certain scientific knowledge always done through implication of theories
ii. Applied research , is the types of research used to seek specific knowledge necessary to find the solution to solve a certain problems in the society
iii. Evaluative research is the types of research which is conducted with the purpose to measure or asses the achievement of a certain scientific purpose
iv. Analytical research is the types of research uses fact already available and so analyses this fact to make critical evaluation of the materials
v. Fundamental research is types of research aim the studies of life processes that are universal in their application to scientific knowledge.
TYPES OF RESEARCH ACCORDING TO DATA COLLECTED

i. Qualitative research - is the types of research concern with qualitative phenomenon, - it applicable to the phenomenon that can be expressed in term of quality , - the data gathered are purely in form of description being that why sometimes called descriptive research/- Deals with the quality of a phenomenon.
ii. Quantitative research. Is the research that applicable to phenomenon that can be expressed in term of quantity like population data/ Research which deals with the measurement of quantity or amount in numerical form.
Other types of research include:
- Empirical research Is the research based on experimentation or observation -
 Conceptual research is the research based on concept or theory that describe or explain phenomenon
Ø Exploratory research is the research based on the extensive investigation or is the research conducted for the problem that is not clearly defined
Research Tools
- Methods of data collection including
· observation,
· interviews,
· questionnaires
IMPORTANCE OF RESEARCH
STAGES IN CONDUCTING RESEARCH.
1) Problems identification or formulation of research problems
2) Literature review or statement of objective
3) Formulation of hypothesis
4) Preparation for the field work
5) Actual field research
6) Data analysis
7) Hypothesis testing
8) Presentation of data
9) Report writing
1) Problems identification is the title of the topic to be discussed or topic where the research focus example a study of land form in the areas around the schools
2) Literature review or statements of the objective. - Involves the finding of the more detail aspect of the problems to be studied. - Possible process involved in the formation of such land form. - Economic importance of that land form. - Relationship of that land form and soil from different written documents
3) Formulation of hypothesis is the tentative answer to the problems is a theories which has not yet approved there are two types of hypothesis:
NULL HYPOTHESIS
ALTERNATIVES HYPOTHESIS
Null hypothesis is the statement which started in negatives form example you formulate that there has no relationship between land form and soil;
Alternatives hypothesis is the statement which started in positively example there is a relationship between land form and soils.
4) Preparation for the field work before going up the field work the following process should be done
- Researcher should seek permission from the authority within the school and were he/ she want to visit
- Pre visits
- Cost
- Time
- School calendar
- Preparation of research equipments
IMPORTANCE OF PRE VISTS
Familiarize learners or researcher
Help the researcher to decide the kind of equipment to be used
Help in identification of problems those researchers likely to be encountered during the research process.
Help to estimate cost
Help to design working schedules
5) Actual field research - involves data collection
-the aim of doing research is to get information to be used to explain any phenomenon this information known as research data
Research data divided into two
a) Primary data
b) Secondary data
a)primary data is the original or fresh data collected by researcher direct from the field, primary data can be collected through ;
i. Observation method is the research data which involves the researcher use his/her own eye in learning, testing and smelling during the collection of data. In this case use his/her own eye to look at the phenomenon and record what is seen.
ADVANTAGES OF OBSERVATION.

A researcher can determine the behavior and mood of respondents
Suitable even to illiterate people
void report bias
Overcome language behavior
First hand information are easily collected
A researcher gets to know ideas of the group he/she observing or studying.
DISADVANTAGES OF OBSERVATION.
Misinterpretation of what observed
It is cost fully in term of time and money and sometimes involves risk talking especially when your observing something wrong
The disable people cannot work easily example blind people.
B) INTERVIEW
Is the verbal interaction between interviewer and interviewee. Designing a list of question and asking respondents this done in two ways
Face to face interview
Telephone interview
ADVANDAGES OF INTERVIEW METHOD
A researcher can get first hand information
Provide in depth data which is not possible to get through questionnaire
It is not restricted to literacy people only, used to the whole group in the societies.
A researcher can participate in change the mood of the respondents.
Interview can also employ other method such as observation technique.
DISADVANTAGES OF INTERVIEW
· It is time consuming
· Data collected are difficult to analyze
· Bias and untruth
· It cannot provide reliable information
· It is cost fully
Interview can be analyzed in two ways
Unstructured interview and structured interview.
Unstructured interview is the interview in which there is no special set of question that the interviewer ask when interviewing
Structured interview is the types of interview in which interviewer had a set of question that asked to all respondents
C) QUESTIONNAIRE.
Is a set of question written and then submitted to respondent and respondents supposed to answer it, they consist the list of question concern the topic
ADVANTAGES OF QUESTIONNAIRE
· Data can be collected as the first hand
· It saves time especially when a close ended question is used
· Easily to analyze data
· Low cost
· Respondents are in great chance of expression
· It avoids bias.
DISADVANTAGES OF QUESTIONNAIRE
· It used only to literacy people
· The question may not being understood there for the respondent may provide wrong data
· Cheating may be involved
· Respondent may dislike in answering the questions
· It is time consuming
TYPES OF QUESTIONNAIRE
v Close ended questionnaire
v Open ended questionnaire

Close ended questionnaire is the types of question which a compared by a list of all possible alternatives answers example yes or no question: QUESTION INCLUDE DO YOU GROW MAIZE IN FARMS.
ADVANTAGES OF CLOSE ENDED QUETIONNAIRE
v Easier to analyze since they are in immediate useable form.
v Easier to administer or to organize because each items followed by alternatives answer
v They are economically to use since they saves time and cost.
DISADVANTAGES OF CLOSE ENDED QUESTIONNAIRE.
v They are more difficult to construct because categories must be well structured
v The responses question are limited and respondent is completely for answer question without explanations
OPEN ENDED QUESTIONNAIRE
This refers to the questions which gives respondents completely freedom responses. These questions include WHAT CROPS YOU GROW.
ADVANTAGES OF OPEN ENDED QUESTIONNAIRE
v They permit a great response when respondent asked the question.
v Simple to formulate mainly because the research do not have common answer
v May gives insight and wide expression
v It stimulate personal thinking
DISADVANTAGES OF OPEN ENDED QUETIONNAIRE
v There is a tendency of providing information which does not reflect to the aim of research
v It is time consuming because it need more explanation
6. DATA ANALYSIS data collected should be analyzed in order to remove unnecessary materials.
7. HYPOTHESIS TESTING. After the data analysis collect the research needs to test the hypothesis formulated the questions here is that the data collected support hypothesis
8. PRESENTATION OF DATA. After getting correct information about the study topic the analyzed data is interpreted and presented in different statistical graphs and what it can be understood to everyone.
9. REPORT WRITING At the end of research , the researcher has to prepare report of what has been done, the research finding has to be presented to the public
Report writing should include the following;
- TITLE it deals with the topic of your research
- CONTENTS should be organized in chapters thing that you write
- Preface objective the things that you write.
- Acknowledgements other contribution from other people
- Introduction of topics
- Abbreviation and meaning of key terms
- Reference of the book bibliography
SAMPLE AND SAMPLING TECHNIQUE.
· Sample is the representative information from a given population
· Sampling is the process of obtaining sample ,
SAMPLING TECHINIQUE
Is the technique used in data collection where by a representation portion of phenomenon under research is selected and analyzed
Selection of representatives in the population is essential because the study of the total population may be expansive and time consuming.
TYPES OF SAMPLING TECHNIQUE
Random sampling
Systematic sampling
Stratified sampling
Snowball sampling
Accidentally sampling
RANDOM SAMPLING.
Is the selection of an individual into interplay to a choice where every people had a chance to be selected example the researcher need the population from the people of 100 so everyone had a chance of been selected.
MERITS OF RANDOM SAMPLING
This method is usefully in the areas where the number of population is large and unevenly population.
It minimize bias tendency for the part of research
It reduce misunderstanding to among the population
DEMERTS OF RONDAM SAMPLING

A poor selection of sample can led mislead information
SYSTEMATIC SAMPLING
Are the types of sampling techniques in which selection of individual done in regular form example after every three people you select one personal.
ADVANTAGES OF SYSTEMATIC SAMPLING.
Accurate representation is done
It reduce the element of bias
It is easily to be conducted
DISADVANTAGES OF SYSTEMATIC SAMPLING.
It will involves the selection of the people who base
Sometimes sample selected may not consider the ratio of sex, and age.
Some respondent may not be aware about the research topic
STRATIFIED SAMPLING
Are the types of sampling which involves the selection of sample on the bases of group or categories of similar elements of the phenomenon. This classification may base on age, education status, or tribes bases.
ADVANTAGES OF STRATIFIED SAMPLING
It considers a large number of samples so it is easily to get the facts.
The fact obtained because different strata participate
It reduce time consuming
DISADVANTAGES OF STRATIFIED SAMPLING.
Poor organization may led to inaccurate data
Some time people may contain the same idea.
NECTA QUESTION
NECTA 2008 Qn no 5
In 2007, form four students from kibaigwa secondary schools conducted a research about road accident between Morogoro and Dodoma. Finally they submitted the report to the head of school.
a) What were the main three (3) objectives of the research?
b) Propose three (3) methods which might be used to collect.
c) Explain three (3) problems that possibly faced them when collecting the data.
Necta 2010 Qn no 5
Hypothesis formulation can be used in both qualitative and quantities research. Example the problems faced in hypothesis formulation.
NECTA 2011 Qn no 5
a) What is hypothesis formulation?
b) Explain the importance of hypothesis in research.
Research Proposal
- A systematic plan which plans what will be needed to accomplish the main objective of the research
Functions of a research proposal
· Guideline to show how to proceed with a project,
· shows where the research should end,
· shows how the research will be evaluated in the future
Components of a research proposal
· title,
· problem and setting,
· hypothesis,
· literature review
· work plan,
· budget chart,
· references
Qualities of a good research proposal
- Should be clearly written,
- precise,
- reasonable length,
- worth time/money being used

By teacher kikoti m














Soma zaidi >>>>>>>>>>
Imechapishwa na Unknown kwa 18:00:00 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

MAPENZI: mjue mwanamke bora

Na mwandishi wetu;Kijangai y
Wengi wangekuja na orodha isiyokuwa na mwisho ambayo inaeleza tofauti tofauti kuhusu tabia nzuri za mwanamke.

Hapa tumekuja na orodha ya sifa nzuri na muhimu zaidi ambazo zinafaa kutumiwa kama kuwa kigezo cha kupima tabia nzuri za mwanamke.
Kwa kuwa wanawake huwa na tabia tofauti tofauti, hatuwezi kusema lazima mwanamke awe na tabia zote hizi ili asomeke kama mwanamke mwenye tabia nzuri. La. hizi ni baadhi tu ya tabia ambazo mwanamke anaweza kuwa nazo, na nyingine kutokuwa nazo na bado akaorodheshwa kuwa na tabia nzuri. Zama nami.

Baadhi ya sifa nzuri kutoka kwa mwanamke

1. Kusamehe
Ni vigumu kuwa katika uhusiano halafu uwe hauna moyo wa kumsamehe mpenzi wako. Kawaida katika mahusiano, huwa kuna changamoto kadhaa ambazo hujitokeza hivyo lazima uwe na tabia ya kuweza kusamehe. Hii inaweza kuanzia kukosana kwa mambo ya kinyumbani, ama mambo mengine yanayofanana.
Mwanamke mzuri ni yule ambaye ana uwezo wa kumsamehe mpenzi wake bila kuweka kinyongo. Iwapo mpenzi wako umemshika katika fumanizi nk na bado unampenda, basi jambo zuri la kufanya ni kumsamehe na kuendelea na maisha.
2. Msikilizaji mzuri
Mara nyingi migogoro ambayo inatokea majumbani kati ya wapenzi wawili husababishwa na kutosikilizana. Huyu akiambiwa hivi huyu anajibu hivi. Well, iwapo mwanamke anataka mahusiano yake yake marefu na ya kufaana, basi anapaswa kuwa msikilizaji mzuri.
Mwanamke ambaye huwa anatulia na kumsikiliza mpenzi wake, mahusiano yake na mpenzi wake huwa ya furaha zaidi ukilinganisha na ya yule ambaye hatilii maanani maoni ya mwenzake.
3. Mwaminifu
Hii ni kuanzia kuongea ukweli bila kudanganya hadi maswala ya chumbani. Iwapo mwanamke ana mchepuko mahali fulani ama anamwendea kinyume mpenzi wake, basi aina hii ya tabia haifai kabisa.
Sifa ya mwanamke mzuri ni ile ambayo ni ya uaminifu. Mwanamke mwaminifu kwa mpenzi wake haitofika wakati fulani ambapo atakosana na mpenziwe.
4. Msaidifu
Katika mahusiano, kuna wakati fulani hufika ambapo lazima wapenzi wawili wasaidiane kufanya jambo ama kutimiza kitu fulani. Hivyo mwanamke mzuri ni yule ambaye anatoa msaada wa kumsaidia mpenzi wake na jambo fulani. Mathalan inaweza kuwa kumsaidia kimawazo, kifedha ama jambo tofauti. Mwanamke mwenye tabia hii humpendeza sana mpenzi wake kwa kuwa inaonyesha ya kuwa mwanamke kama huyu ana uwezo wa kumtumikia mpenzi wake wakati ambapo anaweza kupatwa na majanga.
5. Mwenye imani
Kuna tabia za wanawake ambazo huwachosha wanaume, nazo ni kukosa imani. Iwapo wewe una tabia za kutokuwa na imani basi tabia kama hio unafaa kuiacha mara moja. Tabia za kutokuwa na imani ni kama vile kuharakisha jambo, kulazimisha kitu ambacho hakiwezekani nk.
Hali kadhalika, mwanamke mwenye imani ni yule ambayo ana subira. Iwapo ameambiwa na mpenzi wake kuhusu jambo fulani, basi yeye hutulia hadi kungojea matokeo yake.
6. Kuhamasisha
Wanaume humpenda mwanamke ambaye anatoa motisha ili kumsaidia kutimiza lengo lake. Vile vile kwa kawaida kuna wanaume ambao wanahitaji kiinua mgongo ili kutimiza mambo fulani. Hivyo wewe kama mwanamke, mara moja au nyingine unafaa kuonyesha umotisha wako kwa kumuelekeza mpenzi wako mara moja au nyingine.
7. Mcha Mungu
Mwanamke mcha Mungu bila shaka maisha yake huwa ya kufanikiwa. Mtu yeyote yule lazima awe mcha Mungu ili awe na sifa nzuri ya maisha katika jamii.
8. Heshima
Heshima haimaanishi ni kwa mpenzi wako pekee bali kwa jamii nzima. Mwanamke ambaye anapenda kugombana na majirani kila kukicha halafu ikifika jioni anamheshimu mpenzi wake hafai. 
Tabia za mwanamke mzuri ni yule ambaye anaheshimu na kuishi na majirani zake vizuri bila kuwa na mivurutano yeyote ile.
9. Anajiamini
Mwanamke mzuri ni yule anajiamini na anaamini mahusiano yake. Mwanamke mzuri ni yule ambaye hatasikia maneno ya watu halafu akampakizia mpenzi wake. Iwapo kuna swala tata ambalo linafanyika, basi mwanamke aina hii atamwekea kikao mpenzi wake na kujaribu kumuuliza maswali na kutaka kufafanua chochote ambacho kitakuwa kinamkwaza. Mwanamke aina hii hupendwa na wanaume kwa sababu anajua ya kuwa akifanya jambo fulani basi mpenzi wake atataka kuelezewa bila kuwa na hisia zozote mbaya.
10. Anajua mapenzi
Ikija katika swala la mapenzi, mwanamke mzuri ni yule ambaye anaujua mwili wake vizuri, hivyo si mwoga wa kuonyesha sehemu yake ya ndani ya mapenzi. Mwanamke huyu haoni aibu ya kujaribu mitindo tofauti tofauti ya kufanya mapenzi nk.
Wanawake ambao wanajua mapenzi ni moja wapo wa sifa nzuri ambayo wanaume wanapenda.
Hizi ni baadhi tu ya sifa za mwanamke mzuri. Iwapo unataka kuongezea ama kuchangia, angusha comment yako hapo chini.
Imechapishwa na Unknown kwa 14:41:00 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

Ijumaa, 18 Desemba 2015

Ajali yaua 12 Iringa, 28 taabani

Basi la kampuni ya New Force baada ya kugongana

Imechapishwa na Unknown kwa 18:17:00 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

Rwanda wafanya uamuzi


Friday, December 18, 2015

Kwa ufupi

  • Shughuli za kuapishwa wabunge Dodoma leo

    Habari Mpya
  • 1 Kitaifa Ajali yaua 12 Iringa, 28 taabani
  • 2 Kitaifa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar yaparaganyika
  • 3 Kitaifa Rwanda wafanya uamuzi
  • 4 Kitaifa Kasi ya mawaziri wa JPM watia shaka
  • 5 Kitaifa Waziri wa Afya ajiweka kitanzi kwa Magufuli
  • 6 Kitaifa Nyumba 100 zabomolewa Msimbazi
  • 7 Kitaifa Aga Khan aishukuru Serikali ya Uganda
  • 8 Kitaifa Wizara ya Afya yawasaka waliokaidi amri ya Magufuli
  • 9 Kitaifa Vigogo wa TRA kesi ya makontena nje
  • 10 Kitaifa Wataja mambo manne kuongeza kodi

  • Imechapishwa na Unknown kwa 17:38:00 Hakuna maoni:
    Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

    Kasi ya mawaziri wa JPM watia shaka






    Rais John Magufuli 
     Kwa ufupi

    Tangu walipoapishwa Desemba 12, mawaziri wengi wamekuwa wakitembelea taasisi zilizo chini yao kufuatilia utendaji na utoaji huduma kwa wananchi na kutoa matamko.
    By Fidelis Butahe na Kalunde Jamal

    Dar es Salaam. Licha ya mawaziri wa Serikali ya Awamu ya Tano kutokaa ofisini wakishughulikia matatizo ya wananchi, wasomi bado wana shaka kuwa huenda kasi waliyoanza nayo ni ya muda na kwamba baadhi yao wanafanya kwa nidhamu ya woga.

    Tangu walipoapishwa Desemba 12, mawaziri wengi wamekuwa wakitembelea taasisi zilizo chini yao kufuatilia utendaji na utoaji huduma kwa wananchi na kutoa matamko.

    Mathalan, mara baada ya kuapishwa, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu na naibu wake, Hamisi Kigwangalla hawakwenda ofisini na badala yake mmoja alikwenda Hospitali ya Amana na mwingine Hospitali ya Mwananyamala kukagua utoaji huduma.

    Ziara kama hizo zilifanywa na mawaziri wengi, ambao walifika sehemu zinazowahusu na kuhoji masuala kadhaa na baadhi kutoa muda ili wapewe majibu, wengine wakitangaza kusimamisha watendaji au kusitisha zabuni.

    Lakini wachambuzi waliohojiwa wametilia shaka kasi hiyo, baadhi wakisema mawaziri hao walihitaji kupata ripoti kutoka ofisi zao kabla ya kuanza ziara za ufuatiliaji na wengine wakienda mbali zaidi kusema kuna dalili za kutaka waonekane wanafanya kazi.

    “Kufanya kazi siyo kwenda mbio na kutoa maagizo lukuki kwa wakati mmoja. Kinachofanyika sasa ni kufuata maagizo zaidi kuliko utendaji wa dhati. Hali hiyo ipo katika ngazi zote na inasababisha baadhi ya watendaji kukiuka Katiba na sheria za nchi,” alisema mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Hamad Salim. Msomi huyo alisema nchi haihitaji mtu kujionyesha kuwa anafanya kazi. “Anayefanya kazi anatakiwa kutambuliwa na watu wanaomzunguka.”

    Katika kutekeleza kauli mbiu ya Rais John Magufuli ya “hapa kazi tu”, mawaziri wamekuwa wakifanya ziara hizo za ‘kushtukiza’ wakiwa wameambatana na waandishi wa habari na kuwahoji watendaji wa Serikali kuhusu utekelezaji wa majukumu yao.

    Wakati Mwalimu na Kigwangalla walianzia hospitalini, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na naibu wake Dk Medard Kalemani wameanza kazi kwa kutembelea vituo vinavyozalisha umeme kwa kutumia maji.

    Muhongo, ambaye alishughulikia madini na nishati kwenye Baraza la Mawaziri la Serikali ya Awamu ya Nne kabla ya kujiuzulu mapema mwaka jana, alitumia fursa hiyo kueleza mikakati yake na kutoa maagizo kuwa kila mteja aliyeomba kuunganishiwa umeme na hahitaji nguzo, afanyiwe hivyo.

    Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa akikutana na wadau wa maji, kutembelea Ruvu pamoja na Dawasa.

    Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga alianzia ofisini kwake akipokea taarifa ya ndani na juzi alikuwa na kikao na maofisa wa polisi huku akiwataka kutoa taarifa za sababu ya Jeshi la Polisi kutolinda Bandari ya Dar es Salaam, kazi inayofanywa na kampuni binafsi.

    Naye Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Utumishi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jaffo alikuwa wilayani Bahi ambako alikutana na tatizo la utoro wa watendaji wa Halmashauri ya Bahi.

    Tofauti na mawaziri wengine walioamua kufanya ziara za kushtukiza, Mwigulu Nchemba anayeongoza Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, alilazimika kusafiri kwenda Mvomero, Morogoro baada ya kutokea mapigano kati ya wakulima na wafugaji, yaliyosababisha mtu mmoja kufariki, wanne kujeruhiwa na ng’ombe 72 kuuawa.

    Lakini alipofika huko aliahidi kushughulikia matatizo ya wakulima na wafanyakazi huku akiwaomba wananchi hao waache kujichukulia sheria mkononi.

    Jenister Mhagama, ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, pia alilazimika kutoka ofisini baada ya mvua iliyonyesha kwa kipindi kisichozidi saa nne, iliposababisha mafuriko jijini Dar es Salaam.

    Waziri huyo aliagiza kusitishwa kwa zabuni ya mkandarasi wa mfereji wa Buguruni na kutaka maelezo ya ujenzi wa mfereji wa Boko Basihaya.

    Wanatumia nguvu nyingi

    Lakini wachambuzi wanaona kuna nguvu kubwa inatumika ambayo inaweza kutoa matokeo madogo.

    “Mtu akipewa kazi ya kukata mti mkubwa, atakaa siku sita mezani akipanga jinsi ya kuukata,” alisema mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (Sua), Profesa Damian Gabagambi, akimnukuu Rais Barack Obama wa Marekani.

    “Utendaji wa kulipuka utatumia nguvu nyingi na kuleta matokeo madogo kwa sababu maeneo yanayohitaji kurekebishwa na kufanyiwa kazi ni mengi na yanahitaji upeo wa kina kuyafahamu, kwanza kwa kushirikisha wataalamu na wadau ili kujadili na kupata ufumbuzi wa pamoja,” alisema Profesa Gabagambi.

    Lakini mtaalamu wa mambo ya Katiba, Profesa Ruth Meena alionyesha shaka kama utendaji huo ni nidhamu ya kazi au ya woga.

    “Kuna vitu viwili; nidhamu ya kazi na nidhamu ya woga, hivyo inahitaji muda kulibaini hilo. Siwezi kusema mengi kuhusu utendaji kazi unaoonyeshwa na walioteuliwa kwa sababu siamini katika vitu vya mbiombio na tabia ya mtu ya kupenda kazi huonekana bayana, muda utaeleza yote.

    “Wapewe muda na mimi nawapa muda pia tuone. Wenye nidhamu ya woga na nidhamu ya kazi wataonekana tu, hawatajificha.”

    Mhadhiri wa OUT, Hamad Salim alisema mawaziri hao wanafanya kitu ambacho hakitokani na utashi wao, bali kuiga uchapakazi wa Rais.

    “Nafikiri tunahitaji kubadili sheria na taratibu mbalimbali ili kuendana na mfumo uliopo wa kuchapa kazi. Kinachofanyika sasa si sawa. Lakini wasaidizi wa Rais hawafanyi kazi kwa utashi, wanafanya kwa amri na kuimba wimbo wa mtu mwingine wakijiaminisha kuwa ni wimbo wao.”

    Hoja ya mfumo pia ilizungumziwa na Profesa Bakari Mohammed wa UDSM: “Ili kuwe na utendaji kazi endelevu, tunatakiwa kuwa na mifumo itakayofanya utendaji kazi wa kasi walioanza nao uendelee hata kama Rais Magufuli ataondoka madarakani,” alisema.

    Alisema yanatakiwa mabadiliko ya sheria na kanuni na kuwe na Katiba yenye maelezo ya utendaji kazi wa mawaziri.

    Alisema hata Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete naye alianza na kasi kubwa, lakini kutokana na utendaji kazi kutokuwapo kimfumo, ilifikia mahali kasi ikashuka na kuwa ndogo.
    Imechapishwa na Unknown kwa 17:14:00 Hakuna maoni:
    Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

    Jumamosi, 8 Agosti 2015

    USIKU KUNA MAMBO: SIMULIZI YA MAPENZI






    Kuna siku nilikuwa maeneo ya Mjini kati (City Center), nikaipenda suruali moja ya shilingi 15,000/= na pesa sikuwa nayo ikabidi niende kutoa kwenye ATM ya Postal.
    Nimefika pale sikukuta mtu hivyo niliingia moja kwa moja, nimefika mle ndani nikakuta Pesa Kibao zimemwagika pale kwenye kitundu cha kutolea pesa, ATM Card ilikuwepo pale imetokezea na Pembeni kulikuwa na Pochi ya Kike iliyoonekana kutuna vilivyo.
    Kwa woga mimi huku nikitetemeka mapigo ya moyo yakiwa yameongezeka nikatizama nyuma yangu sikuona mtu, nikachukua zile Pesa harakaharaka, ATM na ile pochi.
    Ile natoka nje kuna dada mmoja alikuwa anakuja kwa kasi maeneo yale nikapata uoga nikamuuliza “Samahani dada, kuna kitu umesahau humu”, yule dada hakunijibu kitu kaingia kwenye chumba cha ATM akachomeka Kadi kutoa hela mi nikaondoka zangu fasta kuelekea home.
    Nimefika home nikajifungia ndani na kuzibwaga zile pesa kitandani, nikafungua wallet nikakuta imejaa dollar, Vipodozi, iphone na ki-Nokia kidogo cha tochi, ATM Card mbili za Benki tofauti ambazo zilikuwa zimezungushiwa karatasi iliyokuwa na namba za siri za ATM zote, moyo ukanilipuka paaaa!!! Nikaona bora Nipumzike kwanza kitandani!!
    Muda si mrefu ile iphone ikaanza kuita, nilipoangalia halikutokea jina nikaona bora nipokee nimsikilize anasemaje, ilikuwa sauti ya kike iliyoongea kwa huzuni kwa kubembeleza huku akilia na alijitambulisha vizuri kuwa ile mali ni ya kwake! Huruma ilinijia nikamwelekeza nilipo aje kuchukua...
    Hakuchukua muda akawa amefika nami nikamkabidhi vitu vyote naye akavihakiki na kukuta viko sana: Milioni 3 za Kibongo na Dollar 500. Dada kanishukuru na kunipa ile Millioni 3 ya kibongo mi nikazikataa kwasababu ni mali yake na alizisahau tu.
    Alinitoa hofu kwa kunisihi nichukue tu, mi kama binadamu mwenyezi Mungu atanilipa, nikakataa... Mwishowe akaomba namba yangu na kuondoka zake, akawa ameniacha ndani huku njaa sasa nikaanza kuisikia, nilikuwa na buku mbili nikaenda kula viepe kavu na soda nikawa powa.
    Sasa jana kanipigia simu kuwa anakuja nimsubiri, dakika tano tu akanipigia tena kuwa ameshafika yupo nje yupo ndani ya Prado mpyaa nikaingia tukaondoka akaenda kunionyesha kwake kisha tukaelekea kwenye nyumba nyingine iliyokuwa ndo imekamilika kujengwa akaniambia hii itakuwa yako akanikabidhi baadhi ya nyaraka na funguo zote sikuamini...!!
    Akanisindikiza kwangu, kufika home ananiambia hiyo gari (Prado) nayo ananiachia ni kwa mema tu niliyomfanyia, ndani ya ile gari kulikuwa na brifcase iliyokuwa na pesa akaniambia pia hii pesa itakuwa yako ya kuanzia maisha, na kumbe yule dada alikuwa kanipenda akanikumbatia kwa nguvu nikiwa pale kwenye seat oooh!! umasikini baibai...
    Akiwa kanikumbatia akihema kwa kasi juu ya kifua changu nikahisi mtu akinishika begani na kuniita kwa sauti.
    “Anko ankoo we ankoo... amka rafiki yako Salim anakuita!!!”.
    “ALIKUWA MTOTO WA SISTA ALIKUWA ANANIAMSHA !!”.
    Kumbe muda wote nilikuwa nikiota Dah..
    Imechapishwa na Unknown kwa 12:47:00 Hakuna maoni:
    Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

    LIPUMBA ANGESEMA ADC WANGEMWACHIA URAIS


    Profesa Ibrahimu Lipumba
    Kwa ufupi

    Profesa Ibrahimu Lipumba juzi alitangaza rasmi kuachia nafasi ya Uenyekiti wa CUF Taifa
    By Kalunde Jamal na Borrice Bwire

    Dar es Salaam. Mgombea urais kupitia tiketi ya Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) Chifu Lutalosa Yemba, amemkaribisha aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kujiunga na chama hicho.

    Chama hicho juzi kilifanya mkutano wa kuwatambulisha wagombea wake wa nafasi ya urais, Yemba anayewania urais wa muungano na mgombea mwenza wake Said Miraj Abdullah, pia alitambulishwa Hamad Rashid Mohamed, anayewania urasi wa Zanzibar.

    Yemba kwenye mkutano huo alisema anaufahamu uwezo wa Lipumba katika siasa, ujasiri na uvumilivu wake, hivyo hatakuwa na kinyongo kufanya naye kazi ya kusukuma mbele gurudumu la siasa za upinzani.

    Alisema hakujiunga na chama hicho kwa ajili ya kuwa rais, amejiunga kwa ajili ya kutengeneza dola ya uongozi itakayoondoa dhiki na mateso wanayopata Watanzania, hivyo kutokana na uzowefu alionao katika siasa anaamini watafanikisha hilo kwa ufanisi.

    “Walinifukuza mwezi wa sita , mwezi wa nane Lipumba amejing’atua kwenye uongozi, watafahamu sasa kuwa kwenye chama kile kuna udhalimu, namkaribisha Lipumba na ninampongeza kwa uvumilivu wake, ingawa ninaumia kuona kiongozi shupavu aliyekuwa na uwezo wa kuhakikisha wananchi wanaamini katika vyama vingine vya upinzani kukatishwa tamaa na watu wachache wenye uroho wa madaraka, ”alisema Yemba.

    Alisema kuwa anaingia katika kinyang’anyiro cha kuwania urais akipambana na chama kimoja tu, CCM, hivyo vilivyobaki hakuna wa kumtisha kwa sababu wenyewe kwa wenyewe wameanza kuvurugana.

    “Sisi ADC kama bahari, tunachukua maovu yao tunameza, baadaye tunayatema, wakati ukifika wa kufanya hivyo tutafanya kwa sasa , nawaomba Watanzania mpime kwa makini na kuchagua kiongozi anayefaa.

    “Mchagueni asiyekuwa mwizi, fisadi, mnyang’anyi asiye na kashfa na hakuna unapoweza kumpata kiongozi wa namna hiyo zaidi ya ADC, pimeni sikilizeni sera zetu, ilani yetu mtuunge mkono. ”alisema Yemba.

    Jana, Yemba alichukua fomu za kuwania urais wa chama hicho, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), huku akiwasisitiza Watanzania kukipa nafasi chama hicho ili kuifanyia nchi mabadiliko ya haki na kuondokana na ukandamizaji.

    Kabla ya kufikia uamuzi wa kuchukua fomu Nec, Yemba alinukuliwa akisema kama Lipumba angejitokeza jana, angemwachia nafasi ya kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano. Hata hivyo kuna taarifa Lipumba alisafiri juzi usiku kwenda nje ya nchi.

    Said Miraj Abdulla

    Kwa upande wa mgombea mwenza wa chama hicho Said Miraj Abdulla, alisema kuwa anamualika Maalim Seif awaeleze Watanzania anataka nini katika siasa, kwa nini anavuruga utaratibu wa kuwapo kwa upinzani wa kweli.

    Alieleza kuwa pamoja na kuunga mkono kilichofanywa na Lipumba kutokana na udhalimu unaofanywa na wanasiasa wachache wanaokatisha tamaa wengine, lakini hafurahi kumuona au kusikia anakaa nje ya ulingo wa siasa.

    “Nani asiyejua mchango wa Lipumba katika siasa za upinzani wa nchi, arudi kwenye siasa aje kuendeleza safari aliyoianza mwaka 1995, kukaa kwake nje ya siasa kunapunguza nguvu ya Watanzania kufikia kilele cha mafanikio ya kupata rais atakayejali shida zao, kuwasikiliza, kuwanufaisha na rasilimali zinazopatikana nchini mwao, ”alisema Abdulla.

    Hamad Rashid Mohamed

    Kwa upande wa mgombea urais wa Zanzibar, Hamad Rashid Mohamed, aliwataka wananchi kuwa makini wanaposhabikia vyama na kuviepuka visivyoheshimu Katiba.

    Alisema alipokuwa kwenye Bunge la Katiba alisema hakuna upawa wala Ukawa, matokeo yake ndiyo hayo watu wanalumbana, Wazanzibar wanahitaji mabadiliko wamekaa kwenye umasikini usiowahusu kwa sababu hakuna ajira.

    Alieleza kuwa kwa wakazi wa Zanzibar wanaohitaji ajira, akijenga viwanda vitano tu hakutakuwa na kijana atakayekosa kazi na huo ndiyo mkakati wake katika miaka mitano ya uongozi.

    “Watanzania shabikieni vyama huku mkiwapima wagombea wana nia gani na nyinyi, maslahi yao binafsi au kuwasaidia, maana “Tumbili akimaliza miti anakuja mwilini” kuweni makini, ”alisema.

    Imechapishwa na Unknown kwa 11:35:00 Hakuna maoni:
    Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
    Machapisho Mapya Machapisho ya Zamani Nyumbani
    Jisajili kwenye: Machapisho (Atom)

    KIKOTI EDUCATION CENTRE

    KIKOTI EDUCATION CENTRE

    kwa afya bora

    kwa afya bora

    Tafuta taarifa

    Orodha Yangu ya Blogu

    • KIKOTI EDUCATION CENTRE
      Tangazo kwa walioomba ajira KIKOTI EDUCATION CENTRE

    WAZO LA LEO

    usiombe pesa, omba kazi
    powered by KIKOTI EDUCATION CENTRE

    Habari mchanganyiko

    • ▼  2018 (42)
      • ▼  Septemba (4)
        • Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya...
        • Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya...
        • Msukuma Asema Lowassa Anampango wa Kurudi CCM
      • ►  Julai (2)
      • ►  Aprili (8)
      • ►  Machi (5)
      • ►  Februari (6)
      • ►  Januari (17)
    • ►  2017 (357)
      • ►  Desemba (13)
      • ►  Novemba (7)
      • ►  Oktoba (10)
      • ►  Septemba (16)
      • ►  Agosti (27)
      • ►  Julai (31)
      • ►  Juni (27)
      • ►  Mei (41)
      • ►  Aprili (32)
      • ►  Machi (59)
      • ►  Februari (53)
      • ►  Januari (41)
    • ►  2016 (593)
      • ►  Desemba (36)
      • ►  Novemba (31)
      • ►  Oktoba (37)
      • ►  Septemba (58)
      • ►  Agosti (57)
      • ►  Julai (82)
      • ►  Juni (75)
      • ►  Mei (95)
      • ►  Aprili (80)
      • ►  Machi (17)
      • ►  Februari (6)
      • ►  Januari (19)
    • ►  2015 (62)
      • ►  Desemba (11)
      • ►  Agosti (3)
      • ►  Julai (6)
      • ►  Juni (7)
      • ►  Mei (21)
      • ►  Aprili (14)

    Jisajili Kwenye

    Machapisho
    Atom
    Machapisho
    Maoni Yote
    Atom
    Maoni Yote

    Kurasa

    • facebook
    • misael B kikoti

    Advertise with us:

    Advertise With Sponsored Post

    I can publish a sponsored post about your business,website,blog, start up, OR add your website address into an existing blog post as a sponsor of the post. />PHONE:+255769694963

    Machapisho Maarufu

    • SIMULIZI FUPI YA MAPENZI
            Kijana mmoja alitokea kumpenda sana dada mmoja ijapokuwa dada huyo alikuwa akimtolea nje mara kwa mara lakini ...
    • SHAIRI YA KWANZA YAITWA TITI LA MAMA
      Titi la mama litamu,hata likiwa la mbwa, Kiswahili naazimu,sifayo iliyofumbwa, Kwa wasiokufahamu,niimbe ilivyo kubwa, Toka kama ml...
    • Makonda ataja majina mengine ya washukiwa wa madawa ya kulevya
    • USIKU KUNA MAMBO: SIMULIZI YA MAPENZI
      Kuna siku nilikuwa maeneo ya Mjini kati (City Center), nikaipenda suruali moja ya shilingi 15,000/= na pesa sikuwa nayo ikabidi niende k...
    • Magazeti ya ijumaa ya Leo tarehe 15/09/2017
    • HAO NDIO MAWAZIRI VIVULI
      Imeandikwa na Stella Nyemenohi, Dodoma ...
    • Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera
      JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU ...
    • Kuona Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Chuo Kikuu 2016/2017,
      UPDATED!: List Ya Vyuo Vilivyotoa Selection Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Vyuo Vikuu Mbalimbali 2016/2017 ...
    • Magazeti ya Leo jumamosi ya tarehe 07/05/2016
      Headline hizi za magazeti ya Leo zimeletwa Kwa hisani kubwa ya Airtel jipime kifurushi cha yatosha na kampuni ya uuzaji na utenge...
    • Makonda: Mashoga wanataka kuniangamiza
      MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amesema tangu alipotangaza kuanza kukamatwa kwa mashoga, ameb...

    Chapisho Lililosomwa sana

    Jipu jipya shule za sekondari zilizopo katika mji mdogo wa ilula -kilolo laanza kuiva

    Na mwandishi wetu , kilolo         Picha:( kushoto) wanafunzi wakijisomea       kulia: prof ndalichako akiapa kuwa W/ elimu.(maktaba y...

    -

    -
    --

    Habari mchanganyiko

    • ▼  2018 (42)
      • ▼  Septemba (4)
        • Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya...
        • Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya...
        • Msukuma Asema Lowassa Anampango wa Kurudi CCM
      • ►  Julai (2)
      • ►  Aprili (8)
      • ►  Machi (5)
      • ►  Februari (6)
      • ►  Januari (17)
    • ►  2017 (357)
      • ►  Desemba (13)
      • ►  Novemba (7)
      • ►  Oktoba (10)
      • ►  Septemba (16)
      • ►  Agosti (27)
      • ►  Julai (31)
      • ►  Juni (27)
      • ►  Mei (41)
      • ►  Aprili (32)
      • ►  Machi (59)
      • ►  Februari (53)
      • ►  Januari (41)
    • ►  2016 (593)
      • ►  Desemba (36)
      • ►  Novemba (31)
      • ►  Oktoba (37)
      • ►  Septemba (58)
      • ►  Agosti (57)
      • ►  Julai (82)
      • ►  Juni (75)
      • ►  Mei (95)
      • ►  Aprili (80)
      • ►  Machi (17)
      • ►  Februari (6)
      • ►  Januari (19)
    • ►  2015 (62)
      • ►  Desemba (11)
      • ►  Agosti (3)
      • ►  Julai (6)
      • ►  Juni (7)
      • ►  Mei (21)
      • ►  Aprili (14)

    Wikipedia

    Matokeo ya utafutaji

    Jisajili kikoti m blog

    Machapisho
    Atom
    Machapisho
    Maoni Yote
    Atom
    Maoni Yote

    Tafuta katika Blogu Hii

    Translate

    we are strong

    To fight for
    Powered By Blogger

    matukio yenye uhakika

    ubora sanifu ndani yake

    Kunihusu

    Unknown
    Tazama wasifu wangu kamili
    kikoti. Mandhari ya Alama maalum. Inaendeshwa na Blogger.