ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 1 Januari 2016

Wasomi wapongeza makatibu wakuu

  Imeandikwa na Waandishi Wetu
WAKATI makatibu wakuu wateule na manaibu wao wanaapishwa leo Ikulu jijini Dar es Salaam, baadhi ya wasomi wamesema uteuzi wao ambao ameufanya Rais John Magufuli unalenga kuisaidia nchi iweze kuingia kwenye uchumi wa Viwanda.
Profesa Emrod Elisante wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) alisema kwamba uteuzi huo ni mzuri kwani umezingatia utaalamu zaidi. Alisema lazima wizara ziwe na wasimamizi madhubuti ambao wataisaidia nchi kuwa yenye viwanda.
“Nikiwaangalia watu kama Dk Chamriho (Leonard, Katibu mkuu Uchukuzi) Profesa Mkenda (Adolf, Katibu mkuu katibu Mkuu Biashara na Uwekezaji) hawa ni watu makini na ni watendaji wazuri naamini wataisaidia nchi,” alisema.
Alisema iwapo watapewa malengo na rais, wana uwezo wa kuyatekeleza hasa kuifanya Tanzania iwe sekta ya viwanda kama alivyoahidi Rais Magufuli wakati wa kampeni.
Profesa Elisante alisema licha ya nchi kuwa na changamoto mbalimbali kama za kifedha na rasilimaliwatu, lakini alisema uteuzi huo umejaa wataalamu ambao wengi wamepelekwa kwenye fani zao.
“Unajua hata waliopita ni wazuri, ila tatizo waliingia kwenye siasa, Rais Magufuli akiweza kuwadhibiti hawa wasiingie kwenye siasa na wakafanya kazi yao kwa weledi na kujua malengo ya wizara na nchi naamini tutachomoka,” alisema.
Naye Mwanaharakati za haki za Binadamu, Onesmo Olengurumwa alisifu uteuzi wa makatibu wakuu hao kwa maelezo kuwa umewapeleka watu katika fani walizosomea.
“Mfano Profesa Mchome (Sifuni ambaye ni Katibu mkuu wizara ya katiba na sheria) yule ni mwanasheria aliyebobea naamini ataisaidia nchi kwa kutumia taaluma yake,” alisema Olengurumwa.
Alisema kitendo cha Rais Magufuli kujaza wataalamu kama maprofesa na madaktari katika Serikali yake kunaonesha kuwa anathamini wataalam hao na angependa kuona wanatumia taaluma yao kuisaidia nchi.
“Utakuta katika wizara kwa mfano ya Madini, kuanzia Waziri hadi makatibu wakuu ni profesa na daktari, wakikaa pamoja wanaweza kufanya vizuri lakini pia wanaweza kufanya vibaya,” alisema Olengurumwa.
Alisema dhamira ya rais ni nzuri, hata hivyo alikosoa wingi wa makatibu wakuu hao hasa uteuzi wa manaibu makatibu wakuu kuwa haukuwa na maana kwani kila kitengo na idara kina mkurugenzi ambaye kama katibu mkuu hayupo anaweza kufanya kazi zake.
“Alipunguza baraza la mawaziri tukafurahi, lakini amerudi nyuma kwa kuleta makatibu wakuu wengi tofauti na alivyotangaza kuwa makatibu wakuu pia wangepungua, kwa hiyo tuko kule kule,” alisema Olengurumwa.
Naye Katibu Mkuu mteule wa Afya katika wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Mpoki Ulisubisya amesema ameupokea uteuzi wake kwa mshituko mkubwa kwa kuwa ni jambo ambalo hakuwahi kulifikilia.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi yake ya Ukurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya, Dk Ulisubisya alisema uteuzi wake umekuja kwa ghafla huku akiwa na mipango aliyokuwa amejiwekea ya kuendeleza hospitali hiyo.
Alisema mawazo yake yote ilikuwa ni kujipanga kuhakikisha anatekeleza majukumu aliyokuwa ameachiwa na aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii majuma mawili yaliyopita, Dk Donan Mbando aliyefanya ziara ya kushtukiza katika hospitali hiyo.
Dk Ulisubisya alisema agizo lingine lilikuwa kuhakikisha hospitali hiyo inaanzisha Chuo Kikuu kwa ajili ya kuongezea taaluma kwa madaktari na kuboresha huduma za dharura na kupunguza foleni kwa wagonjwa, mambo ambayo tayari alianza kuyafanyia kazi na kuyawekea mikakati.
Wakati huo huo, leo Rais Magufuli anawaapisha makatibu wakuu na manaibu katibu wakuu wa wizara mbalimbali aliowateua juzi. Kazi ya kuwaapisha inafanywa leo Ikulu na kwa hatua hiyo, Rais atakuwa amekamilisha kazi ya kupata watendaji wa ngazi za juu katika wizara mbalimbali, ambazo ni moja ya vyombo vinavyotegemewa kuleta maendeleo ya watanzania ikiwa kila mmoja kwa nafasi yake, atatimiza wajibu wake. Imeandikwa na Shadrack Sagati, Dar na Joachim Nyambo, Mbeya.

Alhamisi, 24 Desemba 2015

Pengo kuongoza misa mkesha wa Krismasi


ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Policapy Kardinali Pengo leo saa tatu usiku anatarajiwa kuongoza misa ya mkesha wa sikukuu ya Kuzaliwa Yesu Kristo.
Wakati Wakristo wakifanya mkesha wa Krismasi kote nchini leo, wenzao Waislamu wote nchini leo wanaadhimisha sikukuu ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W), ambapo Kitaifa Baraza litafanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam kuanzia saa tisa alasiri na mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Misa ya mkesha wa Krismasi itafanyika katika makanisa yote yaliyopo jimboni humo na kote Tanzania, lakini kwa Jimbo la Dar es Salaam, Askofu Pengo ataongoza misa hiyo katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph.
Ratiba ya ibada hiyo iliyotolewa na Katibu wa Jimbo hilo, Padri Aidan Mubezi ilisema siku ya Krismasi ambayo ni kesho, Askofu Pengo ataadhimisha misa hiyo katika Kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay, Dar es Salaam.
Padre Mubezi alisema kuwa misa hiyo itaanza saa 3 asubuhi na kwamba Wakristo wote wanakaribishwa kusali katika misa hiyo. Alisema Askofu Pengo anawatakia Wakristo wote duniani sikukuu njema ya kuzaliwa Kristo na kwamba washerehekee siku hiyo kwa utulivu na amani.
Pamoja na hayo, jimbo hilo kwa kushirikiana na majimbo mengine duniani, wanasherehekee sikukuu hiyo huku wakiadhimisha mwaka wa Huruma ya Mungu uliozinduliwa hivi karibuni na Baba Mtakatifu Francis.
Alisema katika sikukuu hiyo Wakristo wote hususan Wakatoliki, wanatakiwa kufanya matendo ya huruma kwa watu wasiojiweza ili kupata baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Kwa upande wa Waislamu, baada ya mkesha wa Maulid uliofanyika jana usiku, leo Baraza la Maulid litafanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee, huku Mufti wa Tanzania Shehe Abubakar Zuber akiwataka Waislamu kujitokeza kwa wingi katika sherehe hizo.
Mufti Zuberi alisema ujio wa Mtume Muhammad (S.W.A) ni kudumisha amani na hekima ya kumjua Mungu.

Mawaziri wapya wanne wateuliwa

RAIS John Magufuli amemalizia kujaza nafasi za uteuzi wa Mawaziri na Naibu Waziri alizobakiza wakati akitangaza Baraza la Mawaziri la Kwanza katika awamu ya tano ya utawala wake.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Gerson Msigwa kwa vyombo vya habari, Dar es Salaam jana, katika uteuzi wake Rais Magufuli amemteua Profesa Jumanne Maghembe kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.
Aidha, Dk Philip Mpango aliyekuwa Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ameteuliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango. Amemteua kuwa Mbunge na kumteua pia kuwa Waziri.
Rais Magufuli pia amemtangaza Profesa Makame Mbarawa kuwa Waziri mpya wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, akimhamisha kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Naibu Waziri wa zamani wa Ujenzi, Gerson Lwenge ameteuliwa kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji.
Aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi ni Dk Joyce Ndalichako ambaye mapema jana aliteuliwa kuwa Mbunge. Dk Ndalichako aliwahi kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza na Mitihani la Taifa (NECTA).
Katika uteuzi wake mwingine, Rais Magufuli amemteua Hamad Masauni kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Waziri wake ni Charles Kitwanga. Rais Magufuli, Desemba 9 mwaka huu alitangaza kuunda wizara 18 zenye mawaziri 19. Mawaziri hao na wizara zao kwenye mabano ni George Simbachawene na Angela Kairuki (Ofisi ya Rais-Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora) wakati Naibu wa wizara hiyo na Selemani Jaffo.
Wengine ni Mwigulu Nchemba (Kilimo, Mifugo na Uvuvi) na Naibu wake ni William ole Nasha, Jenista Mhagama (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Balozi Augustine Mahiga (Mambo ya Nje na Afrika Mashariki). Naibu wake ni Dk Suzan Kolimba.
William Lukuvi (Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi) ambaye Naibu wake ni Angelina Mabula, Ummy Mwalimu (Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto) na Naibu wake ni Dk Hamisi Kigwangalla.
Waziri wa Nishati na Madini ni Profesa Sospeter Muhongo ambaye Naibu wake ameteuliwa Dk Medard Kalemani. Waziri wa Katiba na Sheria ni Dk Harison Mwakyembe na Waziri wa Ulinzi ni Dk Hussein Mwinyi.
Aidha, Nape Nnauye aliteuliwa kuwa Waziri wa Habari na Michezo na Naibu wake ni Anastazia Wambura. January Makamba aliteuliwa Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) na Naibu wake ni Luhaga Mpina.
Katika uteuzi wa awali, Rais Magufuli alimteua Charles Mwijage kuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Wengine walioteuliwa kuwa Naibu Mawaziri, wakati wizara zao zikisubiri mawaziri kamili ni Edwin Ngonyani (Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano), Ashantu Kijaji (Wizara ya Fedha), Ramo Makani (Maliasili na Utalii) na Stella Manyanya (Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi).
Naibu Waziri mwingine ni Isack Kamwela wa Maji na Umwagiliaji. Wakati huo huo, Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Alphayo Kidata ameteuliwa kuwa Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA.
“Mbali ya kukamilisha uteuzi wa Baraza lake la Mawaziri, Rais Magufuli pia amewatakia heri Watanzania wote katika Sikukuu za Maulid, Krismasi na Mwaka Mpya na kuwataka washerehekee kwa amani na utulivu,” ilieleza taarifa hiyo ya Ikulu.

KHERI YA SIKUKUU




Nawatakieni watazamaji na wasomaji wa blog hii furaha na amani katika sikukuu hizi za MAULIDI, KRISMASI NA MWAKA MPYA ni matumaini yangu kwamba mwaka tuliouaga ulikuwa ni wa mafanikio na wenye heri na baraka tele bila kusahau changamototulizopata . tumuombe mungu atujarie baraka katika mwaka ujao 2016 uwe na baraka tele na tufanye kazi kwa juhudi zote

happy new year to all.

BY kikot blog managements

Jumatatu, 21 Desemba 2015

EDUCATION :AFRICAN AND CAPITALIST CRISIS


Crisis in capitalist countries were the conflict which occurred in Europe and America and spraed world wide. This crisis includes:

1. First world war(ww1)

2. Great economic depression(GED)

3. Second world war(WW2)
FIRIST WORLD WAR was the greatest imperialist war which occurred between two camps triple alliance and triple entente and fought between 28/7/1914 up to the 11/11/1918.

TRIPLE ALLIENCE INCLUDE: Germany, Italy, Austria Hungary and turkey

TRIPLE ENTENTE INCLUDE: British, France and Russia with full support from U.S.A and JAPAN.

BACKGROUND OF THE WAR

This war was a root of many political and economic tendencies of the big capitalist nation.

CAUSES OF THE FIRIST WORLD WAR

1. Development of capitalist in Europe ,after the development of capitalism in Europe all European nation started to struggle so as to get the demand of their industrial such as raw material, market, cheap labour, and areas for investment, this struggle for the resources led to land conflict which resulted to the war.

2. Rise of nationalism, after completion of European unification especially in British and Germany led the capability of expansion and acquire more colonies in Africa and other part of the world this led the conflict with other imperialist nation which were also interested in potential colonies example French hence war.

3. Dissatisfaction of territorial arrangement, by the 19th c almost were under big capitalist nation but the division of the colonies were never satisfied with their political and territory boundary in their given colonies hence imperialist nation started eying other territories with the aim of expand to annex them for example .British was interested in Mesopotamia, Iraq, and Palestine which were the territory of turkey also Germany interested in Ukraine and Baltic which were under French hence war

4. Development of military alliance ,European developed the military union hence made them trust to fight together against the common enemies

5. Moroccan crisis in 1904 and 19011, this conflict was between Germany and French which planted by the Franco Prussia war 1840-1870.germany attempting not primary to keep France out of the morocco but the conference of 1906 which attended by British and supported the French claims in morocco so conflict between Germany and British and France.

6. Assassination of archduke Ferdinand in Sarajevo the capital city of Bosnia , on June 28, 1918 a young Bosnian revolutionary and the member of secrete society known as union death or black death by the name of Gavilo princip assassinate Ferdinand who would soon became the emperor (king) of Austrian throne after that Australian sent drastic ultimatum to the Serbia captain in Belgrade demanding satisfactory other within fourth eight (48) hours, the Australian ultimatum contain three demand :

-Serbia was to explain for the assassination and suppress all societies organizing ant Austrian propaganda

-Serbia was to dismiss all officials to whom Austrian suspect to have involved in murder

-Austrian officials and police were to be permitted to take a part of investigation and punishing the course of the assassination

NOTE: Serbia accept all near term that were given out except third condition that they should allow Austrian official to take part of investigation and suggest that third term should be subjected by international court of justice at the Hague from that Austrian declared the war on Serbia on 28, July 1914 and world war began.
Other causes of ww1 include

· Franco Prussia war1870-1871

· Balkan crisis

· Russian expansionism

· Germany unification.

EFFECT OF FIRIST WORLD WAR

o Depopulation

o Destruction of infrastructure

o Led to the great economic depression

o Led to formation of dictatorship regime

o Formation of league of nation of 1919

WHY USA JOINED THE WAR 6/04/1917.

o Cultural reason, British colonized America so wanted to help British so as to avoid shy.

o USA was a chief supplier of food ad weapons to triple entente

o The USA president ambition of creating peace and security

o Germany sunk of USA submarines in march 1917(u-boat)

THE GREAT ECONOMIC DEPRESSION OF (GED) IN 1929-1933

Was an economic problems which was affected the whole world especially capitalist countries like USA, British, Germany
CAUSES OF GREAT ECONOMIC DEPRESSION.

o The effect of the first world war, this war ended and left the capitalist countries with a lot of debt to pay to USA which provided as an assistance during the war

o Over production and under consumption of commodities, this was both industrial countries and colonies so all good produced lack a market

o Unequal distribution of income in the capitalist world , normally capitalist aimed at profit in produced goods some areas got more income than other so fail to balance the income

o Fall rate of profit, profit for goods produced decline hence tax tend to decrease

o Closure of industries, due to unprofitable of produced goods led more industries to close hence rise the problems of produced raw material

o The fall of stock exchange in USA ,this was the areas where different businessman and seller buy different goods but most of the stock in USA closed and fall down cause the decline of trade.

EFFECT OF GREAT ECONOMIC DEPRESSION ON AFRICA

o Fall of price of African raw materials

o Unemployment

o Increase of taxation

o Intensification of exploitation under the company grow more and sell me

o Low wages and salaries to both workers and labourers.

EFFECT OF GREAT ECONOMIC DEPRESSION IN EUROPE

o Unemployment

o Decline of financial institution

o Decline of trade

o Decline of industries

o Over production
SECOND WORLD WAR (WW2)

Was the second imperialist war fought between the axis power allies or democratic forces, this war was fought with the aim of dividing and re-dividing the world to among the impeliast nation the war fought in 01/09/1939 up to 02/09/1945
Was the complex wide spread and deadly war in the history because use advanced technology in fighting

Axis power include GERMANY, ITALY, JAPAN and AUSTRIA

Allies power include BRITIAN, FRENCH, RUSSIA and USA

CAUSES OF THE SECOND WORLD WAR

Effect of great economic depression

Rise of dictatorship in Europe

Failure of league of nation

Weakness of Versailles treat

Development of military alliances

Germany invasion in Poland

Economic rivalry of imperialist nation

EFFECT OF SECOND WORLD WAR IN AFRICA

Intensification of exploitation of African human resources

Influx of whitmen in Africa

Cut down of colonial expenditure

Introduction of new agricultural policies

Introduction of colonial development plan and scheme such as Nile

Change of colonial labour and mechanization in agriculture

Intensification of African nationalism

Led to the formation of UNO in 1945

Emergence of USA as a superpower
EFFECT OF SECOND WORLD WAR IN EUROPE

Collapse of European capitalist economy

Emergence of USA dominance

Formation of UNO IN 1945

Creation of multilateral financial institution IMF and WOLD BANK

Depopulation

Destruction of infrastructure

Division of the world into two camps CAPITALIST and SOCIALIST Spread of socialism ideologies

Mkuu wa Upelelezi TANAPA achinjwa

POLISI mkoani Arusha imewatia mbaroni watu wawili wanaohusishwa na tukio la kuuawa kinyama kwa kuchinjwa shingo kwa Mkuu wa Idara ya Upelelezi ya Ulinzi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Stephen Kisamo.
Kifo cha Kisamo kinahusishwa na mambo mengi yakiwemo vita ya kupambana na ujangili, ikielezwa mkuu huyo alikuwa na siri nzito juu ya watu wanaojihusisha na ujangili wakiwemo wafanyabiashara wakubwa wa ndani na nje ya Arusha, watumishi wa serikali na wanasiasa.
Habari kutoka ndani ya Jeshi la Polisi Arusha zilieleza tayari imewatia ndani watu wawili ambao ni marafiki wakubwa wa Kisamo na wanajua siri nzito kutokana na kunaswa kwa mawasiliano ya simu ya kiganjani kati ya marehemu na watu fulani muda mfupi kabla ya mauti kumfika ambao polisi inawachunguza kwa karibu.
“Wasiliana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas sisi tumeshakamata watu wawili wa karibu na marehemu na sms na mawasiliano yanatia shaka, lakini ukweli utajulikana muda si mrefu,” kilieleza chanzo chetu cha habari ndani ya Jeshi la Polisi.
Kamanda Sabas alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo Desemba 18, mwaka huu asubuhi katika eneo la Kikwakwaru jijini Arusha muda mfupi baada ya Kisamo kutoka nyumbani kwake akiwa na gari aina ya Mazda.
Hata hivyo, jana hakupatikana kuelezea kukamatwa kwa watu hao wawili baada ya simu yake ya kiganjani kuita bila ya mafanikio, lakini mwandishi wa gazeti alithibitishiwa na maofisa wa Polisi Arusha kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa, lakini wao si wasemaji wa jeshi hilo Arusha.
Awali, Sabas alisema siku hiyo hiyo jioni alifika kituoni hapo mke wa marehemu na kueleza juu ya kutoweka kwa mumewe ambapo mara moja polisi walianza kufuatilia jambo hilo bila mafanikio.
Kamanda Sabas alisema usiku, Polisi ilipokea taarifa kutoka kwa raia wema wa eneo hilo la Kikwakwaru kuhusu kuonekana kwa gari hilo likiwa limeegeshwa maeneo hayo kwa muda mrefu bila kuonekana mtu yeyote ambapo walifika na kulikuta gari hilo, lililovutwa hadi katika Kituo Kikuu cha Polisi usiku huo na baadaye lilitambuliwa na mke wa Kisamo.
Baadaye walirejea eneo la tukio kwa lengo la kutafuta mwili wa marehemu huyo, lakini hawakufanikiwa kuupata mwili wala kumuona kachero huyo ambapo walilazimika kuomba ruhusa ya kupekua gari hilo.
Alisema baada ya kuomba ruhusa hiyo, mke wa marehemu alipowasilisha ufunguo wa akiba wa gari na Polisi walipofungua na kuanza upekuzi walikuta mwili wa marehemu ukiwa umekunjwa kwenye buti, huku shingo yake ikiwa imechinjwa eneo la nyuma ya shingo yake.
Aidha, Kamanda Sabas alisema kwa mujibu wa maelezo ya mkewe, mumewe alikuwa mgonjwa na alikuwa akijiandaa kwa safari ya India kwa matibabu, hivyo kabla ya tukio walidhani alitekeleza gari baada ya kuzidiwa na ugonjwa.
Mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru

YANGA NA AZAMU MIKIKI MIKIKI

TIMU ya soka ya Azam FC imezidi kujiimarisha zaidi katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifunga Majimaji ya Songea mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Majimaji.
Matokeo hayo yanaipa timu hiyo pointi tatu muhimu zinazoiweka kwenye nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 29 nyuma ya Yanga inayoongoza ligi kwa pointi 30 lakini ikiwa mbele kwa mechi moja.
Mabao ya Azam iliyokuwa ikipewa nafasi kubwa ya kushinda mchezo huo yote yalifungwa katika kipindi cha kwanza. Ame Ali alifunga bao la kuongoza katika dakika ya 10 huku mwenzake Didier Kavumbagu akifunga katika dakika ya 20.
Mchezo huo ulichezwa huku kukiwa na mvua kubwa iliyosababisha mpira kukwama kwenye madimbwi ya maji uwanjani. Ligi hiyo ilichezwa tena kwenye uwanja wa Karume Ilala Dar es Salaam ambapo wenyeji JKT Ruvu walilazimishwa sare ya mabao 2-2 na Coastal Union.
Mabao ya Coastal yalifungwa na Miraji Selema katika dakika ya 20 na Nassoro Kapama dakika ya 75. Wafungaji wa JKT ni Musa Juma katika dakika ya 61 na Samuel Kamuntu katika dakika ya 63.