ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 25 Januari 2016

MAPENZI SHIDA PART 2

KWA HISANI YA OMBENI LONGO&HELMAN MHANGA

Baada ya JENIFER na wenzake kukamatwa na mwalimu na kupewa adhabu hiyo ya kwenda na wazazi wao shuleni siku ya Ijumaa tatu na kupelekea kupoteza mudi ya kuendelea kufurah usiku huo ikawabidi waondoke kabisa sehemu hiyo ya CLUB usiku huo huo na kwenda kulala kwenye chumba cha rafiki yao CHRISTINA waliekuwa nae katika kundi lao usiku huo, ilipofika kesho yake siku ya ijumaa pili asubuhi kila mtu alirejea nyumbani kwao huku wakiwa na sura za hudhuni na mawazo kibao kichwani wakijiuliza itakuaje kesho yake ambayo ni siku ya Ijumaa tatu wanatakiwa waende shule na wazazi wao?!. Jenifer alipofika kwao moja kwa moja alielekea chumbani kwake na kujilaza kitandani huku akiwa na mawazo kibao hata chakula hakuweza kula siku hiyo muda wote alikua kajifungia chumbani analia. Ghafla akasikia mlango wa chumbani kwake unafunguliwa aliposhtuka akamuona mama yake Mrs. Brown. Mrs. Brown alimsogelea binti yake Jenifer kuanza kuzungumza nae kama ifuatavyo:-
MRS. BROWN: "Jenifer binti yangu mbona unaonekana leo hauko sawa, nini tatizo mwanangu?! Na mbona unalia? 
JENIFER: "Hapana mama, wala usijali hamna kitu chochote naomba uwe na amani mama yangu, niko sawa tu!" 
MRS. BROWN: "Jenifer mwanangu lazima kutakuwa kuna kitu ila unaficha. Mwanangu nakuomba unieleze usinifiche niambie tu mwanangu wala usiogope" 
JENIFER: "Mama wala usijali hakuna kitu chochote kile" 
MRS. BROWN: "Sidhani binti yangu kama kweli hakuna tatizo sasa mbona unalia, Au umepata ujauzito?! 
JENIFER: "Mama bora ningekua nina ujauzito ila kwa hiki kilichonipata mama yangu najuta tena najuta hata sijui kwanini mlinipeleka shule mama yangu" 
MRS. BROWN: "Mwanangu mbona unasema hivyo kwani kuna tatizo limetokea shule?! 
JENIFER: "Ndio mama, kuna mwalimu shuleni alinitongoza nikamkatalia sasa kila siku huwa ananichapa fimbo bila makosa na ananitesa sana shule na kaniahidi kuwa atanitafutia kosa lolote la uongo ili nifukuzwe shule anikomoe na juzi siku ya Ijumaa kuna wanafunzi kawakamata usiku CLUB akawaambia kuwa atawafukuza shule sasa kaniambia namimi ataniingiza katika hilo kosa la hao wanafunzi kesho shuleni ili nifukuzwe namimi" 
MRS. BROWN: "Haiwezekani mwanangu wewe nyamaza acha kulia tumsubiri baba yako aje nimuelezee ikiwezekana kesho akupeleke shule akamkomeshe huyo mwalimu, wala usiwaze sana mwanangu Jenifer looooo, huyo mwalimu hana hata aibu" 
Baada ya Jenifer kutumia uongo wa kumdanganya mama yake Mrs. Brown kwa dhumuni la kujitetea kutokana na kosa alilolifanya usiku wa jana yake walipokutwa na mwalimu wao wa shule CLUB ikamlazimu kumpa kesi ya uongo yule mwalimu kwa wazazi wake ili wasimuone yeye anamakosa. Mama yake na Jenifer Mrs. Brown alihamaki na kuingiwa na hasira akawa anamsubiria mume wake arudi ili amuelezee kilichotokea. Ghafla baba yake na Jenifer Mr. Brown akaingia nyumbani kwake na kumkuta mke wake Mrs. Brown akiwa na binti yao Jenifer, Jenifer alipomuona baba yake Mr. Brown akaanza kuangua kilio huku akisema "BABA NAJUTA MIMI MWANAOO, NAJUTA BABA HIVI KWANINI ULINIPELEKA NIKASOME ILE SHULE BABA YANGUUUUUU" Jenifer alikua analia huku akitoa sauti kubwa ya kumlalamikia baba yake. Mr. Brown alipigwa na butwaa hakujua nini kinachoendelea ikabidi akae chini na kumuuliza mke wake "MKE WANGU NINI KIMEMPATA BINTI YETU JENIFER?" Mrs. Brown akamjibu mume wake "MUME WANGU NENDA KWANZA KAKOGE KISHA ULE HALAFU NDIO NIKUELEZEE KILICHOTOKEA" Mr. Brown nae akamjibu "HAPANA MKE WANGU NIELEZEE KWANZA NIJUE TATIZO NINI?". Mrs. Brown ikabidi aanze kumuhadithia kama alivyohadithiwa na binti yao Jenifer kuwa kuna mwalimu wa shule alimtongoza binti yao akamkataa sasa huyo mwalimu anamtesa sana Jenifer shuleni na kamuahidi atamfanyia njama yoyote ili binti yao afukuzwe shuleni. Pale pale Mr. Brown nayeye akapandwa na hasira akamnyamazisha binti yake Jenifer na kumwambia "JENIFER BINTI YANGU NYAMAZA, KESHO IJUMAA TATU ASUBUHI TUTAKWENDA WOTE MPAKA SHULENI KWENU UKANIONESHE HUYO MWALIMU. ATANITAMBUA" baada ya hapo wakatawanyika Jenifer akaingia chumbani akaanza kushangilia peke yake kimya kimya akiwa na imani kuwa kishamaliza kesi aliyokuwa nayo na akawa na furaha tele akaendelea kufanya mambo yake kama kawaida.

VICHWA VYA MAGAZETI YA LEO TAR 25JANUARY 2016

MAPENZI SHIDA PART ONE

 Hadithi inayomuhusu binti wa kitanzania alietunukiwa uzuri wa asili na mvuto wa kipekee aliojaaliwa na mungu ama hakika uzuri aliokuwa nao ulikuwa ni kishawishi tosha kwa mwanaume yoyote aliemtazama binti huyu na kutamani kuwa nae kutokana na mvuto aliokuwa nao binti huyu anaitwa Jenifer na amezaliwa katika familia duni ya Mr. Brown na Mrs. Brown yenye watoto watatu (3). Ambao ni Peter, Joseph na Jenifer na katika watoto hawa watatu mwanamke alikua ni Jenifer peke yake na ndie alikua mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia hii yenye watoto watatu ambapo Peter na Joseph walikua ni wadogo zake na Jenifer na walikuwa bado ni wadogo sana. Na wazazi wa Jenifer Mr. Brown na Mrs. Brown walitokea kumpenda sana binti yao Jenifer kwani ndio mtoto pekee wa kike hivyo walionesha upendo mwingi kwa binti yao kwa kumtimizia mahitaj yote muhimu na kumpa kila alichokitaka binti yao ili wamridhishe na kuhakikisha wanampa malezi bora na kujenga upendo imara kwa binti yao. Kutokana na hali ya ngumu ya maisha iliyokuwepo katika familia hiyo ya Mr. Brown na Mrs. Brown, wazazi hawa walikaa na kujadili njia sahihi ya kuweza kukabiliana na umasikini walio nao na kuweza kujikwamua kimaisha wakapata wazo la kumpeleka shule binti yao Jenifer ili hapo baadae aje kuwasaidia wazazi wake kupitia elimu atakayoipata shule hivyo wazazi wakakubaliana na kuanza mipango ya kumuandikisha shule binti yao ili aanze kusoma, wazazi wa Jenifer walijitahidi kutafuta pesa kwa hali na mali ikapelekea wazazi wa Jenifer kujiunga na kampuni zinazotoa mikopo ya fedha lengo kupata pesa waweze kumtimizia mahitaji binti yao aweze kuanza shule. Mungu alileta kheri kwa wazazi hao na kufanikisha kuipata pesa ya kumpatia binti yao kwa ajili ya matumizi madogo madogo ya shule na binti yao akafanikiwa kuanza elimu ya msingi akasoma darasa la kwanza mpaka darasa la saba lakini alipo maliza darasa la saba matokeo yake hayakua mazuri hivyo hakuweza kuchaguliwa katika shule za serekali kwa ajili ya kuendelea na elimu ya sekondari lakini wazazi wa Jenifer hawakukata tamaa na waliendelea kuwa na moyo wa kumsaidia binti yao Jenifer kwa vyovyote vile mpaka waone mwisho wake kwani malengo yao binti yao asome mpaka daraja la juu afike mpaka chuo kikuu, baada ya Jenifer kumaliza elimu ya msingi na hakufanikiwa kufanya vizuri katika mitihani yake ikabidi wazazi wajipange upya kutafuta ada ya kumlipia binti yao ili aweze kujiunga na elimu ya sekondari kwa dhumuni la kuhakikisha binti yao Jenifer anaendelea na elimu. Mungu hakuitupa familia hii ya Mr na Mrs. Brown aliwajaalia wakafanikiwa kuipata pesa ya kumlipia ada binti yao na wakamuandikisha katika shule ya kulipia ya sekondari iliyofahamika kwa jina la "GARDEN SECONDARY SCHOOL" Jenifer alijiunga na shule hii na kuanza elimu yake ya sekondari lakini kama ilivyo kwa vijana wengi wa kisasa kutofahamu umuhimu wa elimu na kushindwa kujua nini wanapaswa kukifanya pindi wanapo kuwa shule ndivyo ilivyokuwa kwa Jenifer. Jenifer hakujua umuhimu wa elimu na hakuona juhudi za wazazi wake kwake za kutafuta pesa kwa ajili ya kumlipia ada ili aje kuwasaidia baadae na kuwasaidia wadogo zake Peter na Joseph. Kipindi Jenifer alipokua shuleni hapo akiendelea na elimu ya sekondari tabia yake ilibadilika akawa anautumia muda wake mwingi wa shule kujichanganya na marafiki ambao hawakuwa na msaada mzuri kwake na wakati mwingine alikua akiaga kwao anakwenda shule lakini alikua hafiki shule alikua anakwenda kwa marafiki anashinda na kurudi nyumbani wazazi wake hawakujua kinachoendelea kwa binti yao. Wakati mwingine Jenifer alikuwa ni mtu wa kupenda sana kwenda kwenye kumbi mbali mbali za starehe wakati alikua anatoka nyumbani kwao usiku akiwaaga wazazi wake kuwa anakwenda kwa marafiki zake anaosoma nao wanakwenda kukesha wakisoma na kujadiliana yale waliyofundishwa shuleni, wazazi wa Jenifer hawakuwa na kipingamizi kwa binti yao walikua ridhwaa kukubaliana na kila anachohitaji binti yao ili mradi kumridhisha na kumfanya awe huru ili mwisho wa siku aweze kutimiza ndoto za wazazi wake hivyo wazazi walikua wakimpa ruhusa binti yao atoke usiku wakidhani anaenda kusoma na wenzake kumbe Jenifer alikua anatumia muda huo kutoka na kwenda CLUB (kumbi za starehe) na marafiki zake wanaenda kujirusha na alikua anarudi nyumbani kwao kesho yake asubuhi, na ilikua kila ikifika siku ya Ijumaa mosi ndio anatoka usiku na wenzake, siku moja kama kawaida yake Jenifer na wenzake wametoka na kwenda kwenye kumbi za starehe huku nyumbani wazazi wanajua watoto wao wameenda katika masomo yao kama ilivyozoeleka, kipindi wapo CLUB kuna mwalimu wao wa shule alikuwepo katika ukumbi huo wa starehe na akakutana na kundi hili la wakina dada kama wanne akiwemo na Jenifer wakiwa wamevaa mavazi mafupi ya ajabu kama machangudoa wanaojiuza, yule mwalimu wao alichokifanya akawaita kisha akawaambia "NAOMBA SIKU YA IJUMAA TATU MKIFIKA SHULE CHA KWANZA NAOMBA NIWAKUTE OFISINI KWANGU KAMA MLIVYO WANNE TENA MJE MKIWA MMEVAA HIZI NGUO MLIZO ZIVAA NA KILA MMOJA WENU AJE NA MZAZI WAKE" kisha mwalimu akawaambia wawe huru waendelee na mambo yao ila ikifika siku ya Ijumaa tatu siku ya shule wafanye kama alivyo agiza mwalimu huyo pale pale Jenifer na wenzake wakakosa amani na mudi ya kuendelea kufurahi usiku ule ikatoweka na kila mmoja wao akawa anawaza itakuaje hiyo siku ya Ijumaa tatu na wataanzia wapi kuwaeleza wazazi wao juu ya kosa hili walilofanya mpaka wamekutana na mwalimu kawaomba waende shule na wazazi wao.....?!

Jumapili, 10 Januari 2016

ngoja ngoja utakuta mwana si wako

1st year

nikiwa nimekaa leacture room nikimuangalia msichana aliyekaribu yangu,niliyekuwa nikimuita "Bestfriend"nilikuwa nikimuangalia nywele zake nzuri na sura yake ya upole huku nikitamani awe wangu,lakini yeye hakuwa akitamani hilo na nilikuwa nikilitambua hilo.
Baada ya leacture,alikuja kwangu na kuniomba notes za siku ya nyuma kwa sababu hakuweza kuingia darasani hiyo siku iliyopita.baada ya kumpa akasema "asante" na kushikana mikono na mimi.I wanted to tell her,i want her to know that i don't want us to be just friends,i love her but i'm just to shy,and i don't know why

2nd year

Simu yangu iliita,kupokea alikuwa yeye alikuwa akilia akinielezea jinsi gani boyfriend wake broke her heart,she asked me to come over because she didn't want to be alone,kwa kuwa ni rafiki yangu kipenzi ilinibidi kwenda kumfariji,as i sat next to her on the sofa,nilikuwa nikimuangalia Machoni nikitamani awe wangu.Baada ya masaa mawili baada ya kuangalia nae movie mbili tatu na kula nae chakula pamoja akarudi katika hali yake ya kawaida,hivyo akaamua kwenda kulala,before akaniangalia na kuniambia "asante" na kunipa tabasamu tamu,i want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why.

3rd year

Siku moja kabla ya Tamasha la muziki chuoni alikuja kwenye meza yangu leacture room na kuniambia "Boyfriend wangu amepata udhuru hivyo naomba unipe campan katika tamasha la muziki leo usiku" kwa kuwa tuliwekeana promice kwamba ikitokea kila mmoja wetu amekosa mtu wa ku-date nae basi tutaenda pamoja just as "bestfriends".hivyo tukaenda.
katika tamasha baada ya kila kitu kuisha na muziki kufungwa,nilikuwa nimekaa nje ya ukumbi nikimuangalia jinsi alivyokuwa akicheka na rafiki zake,she saw me looking to her she smiled at me,i want her to be mine lakini yeye alikuwa hafikirii hilo kabisa na nilikuwa nikilitambua hilo,then she said to me "nimekuwa na muda mzuri na wewe asante sana" and she gave me a sweet smile.I want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why.

Graduation Day

siku,wiki kisha mwezi ukapita ilikuwa ni mahafali yetu tukimaliza masomo ya chuo,akiinuka kwenda kutunukiwa shahada yake ya uchumi nilikuwa nikimuangalia akiwa amependeza sana siku ile,i wanted her to be mine,but she didn't notice me like that,and i knew it.
kabla watu hawajatawanyika kwenda makwao,alikuja kwangu akiwa na vazi lake la mahafali,na kulia pale nilipomkumbatia akainua kichwa chake na kuniambia "you are my bestfriend asante sana" i want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why.

Miaka michache baadae

Nikiwa kanisani Yule Msichana akiwa anaolewa sasa,nilimuangalia akisema "ndiyo nakubali " and drive off to new life,kaolewa na mwanaume mwingine,i wanted her to be mine,but she didn't see me like that,and i knew it.
but before she drove away,alikuja kwangu na kusema "asante sana" and kissed me on the cheek.I want to tell her to know that i dont us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why.

Kwenye Mazishi

Miaka ilipita i looked down katika jeneza lilokuwa na msichna ambaye alikuwa ni "bestfriend" wangu,Katika Service ya mazishi wakasoma diary ya Bestfriend ambayo alikuwa akiiandika enzi za maisha ya chuo'

Diary yake ilikuwa Ilikuwa ikisomeka hivi
I stare at him napenda awe wangu,but he doesn't notice me like that,and i know it,i want to tell him,i want him to know that i dont want us to be just friends,i love him but i'm just to shy,and i dont know why.I wish he would tell me he loved me!

Nilipiga magoti huku nikilia nikijisemea moyoni i wish ningemwambia tu ukweli,nimeshachelewa sipo nae tena katangulia mbele za haki i cried!!

Vunja ukimya

Karibu elimumsingi bila malipo


KAMA Mzazi inapenda kuanza mwaka huu mpya wa 2016 kwa kuwapongeza wote waliobahatika kwa mapenzi ya aliyetuumba kuwa hai na salama na kuendelea kuomba Mungu awalinde kwa mwaka huu tangu mwanzo hadi mwisho wake.
Tunawajibika kushukuru kwa sababu kuna wenzetu hawakubahatika kuuona mwaka huu kutokana na sababu mbalimbali zilizo nje ya uwezo wetu. Lakini kubwa kwa Januari hii ya 2016 ni zawadi ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa wazazi na walezi kwa kuanzisha elimumsingi bila malipo kwa vitendo.
Elimumsingi inajumuisha elimu ya awali,ya msingi na sekondari, kuwa bure kwa gharama za serikali kwa shule za ngazi hiyo zinazomilikiwa na serikali ispokuwa shule 11 tu nchi nzima. Hongera sana serikali ya Rais Magufuli kwa kuishi kwa vitendo.
Kwa mujibu wa waraka wa serikali uliotolewa katikati ya Desemba mwaka jana, uliainisha wazi majukumu ya serikali katika utekelezaji wa elimumsingi bila malipo lakini pia ulioanisha majukumu ya wazazi katika utekelezaji wa jambo hili ili watoto waweze kusoma bila kupata changamoto zisizo za lazima.
Kama Mzazi nataka kuwakumbusha majukumu ya wazazi na walezi katika utekelezaji wa jambo hili kwani yale ya serikali, yenyewe inayajua vilivyo na tayari imeshaanza kutekeleza kwa kutenga fedha za kugharimia elimu hiyo.
Wazazi na walezi kwa mujibu wa waraka wa serikali wanatakiwa kununua sare za shule na vifaa vya michezo,vifaa vya kujifunzia ikiwa ni pamoja na daftari na kalamu, vifaa vya usafi binafsi, chakula kwa wanafunzi wa kutwa na bweni na gharama za matibabu.
Gharama nyingine kwa wazazi na walezi ni kulipia nauli ya kwenda na kurudi shule kwa wanafunzi wa kutwa na wanafunzi wa bweni kwa wakati wa likizo, kununua magodoro, shuka na vifaa vya usafi.
Ili kuhakikisha kwamba hayo yanafanyika bila kuleta manung’uniko kwa kutumbukiza gharama zisizokuwemo katika orodha hiyo, wazazi na walezi wanatakiwa kukemea na kutoa taarifa kwa vyombo husika juu ya mienendo inayokwenda kinyume na utaratibu wa elimumsingi bila malipo.
Kwa uhalisia wake kila mzazi na mlezi anatakiwa kuwa macho kwa kuwa msimamizi wa utekelezaji wa sera hiyo ya serikali ya elimumsingi bila malipo huku watoto wakibakiwa na jukumu la kusoma kwa bidii na uwezo waliojaliwa kwa ajili ya kujipatia ufunguo wa maisha yaani elimu. Visingizio na figisufigisu zisipewe nafasi katika hili ili tuweze kunufaika vilivyo.
Visingizio vya watoto kutokwenda shule kwa sababu ya wazazi au walezi kushindwa kumlipia ada mwanafunzi katika ngazi hizo tatu visipewe nafasi kama ilivyokuwa kabla ya utaratibu huu mpya. Kila mmoja wetu, hususan ni wazazi na walezi wajiandae kwa gharama zilizoorodheshwa ili watoto wetu wote waingie madarasani kwa kazi moja ya kujifunza. Hapa Kazi Tu sasa!

Jumamosi, 9 Januari 2016

Prof. Ndalichako ameipa NECTA siku 7 itoe maelezo kwanini mfumo wa kupanga matokeo kwa GPA ni bora kuliko wa Divisheni uliokuwa unatumika tokea awali.

WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ametoa siku saba kwa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limpe sababu za kubadili mfumo wa utunuku viwango vya ufaulu wa awali( Division) na kwenda wa wastani wa pointi (GPA) unaotumika sasa Kidato cha Nne na Sita.

Aidha, ametaka litoe maelezo ya kitaalamu juu ya sababu za kuanzisha mtihani wa pili kwa watahiniwa wa kujitegemea na kwamba zisipomridhisha, mwaka huu wasifanyishwe mtihani huo.

Mfumo wa GPA ulianza kutumika kwa wanafunzi waliofanya mtihani wa mwaka 2014 ambao matokeo yao yalitoka mwaka jana.Vile vile mitihani miwili kwa watahiniwa wa kujitegemea, ilianza mwaka 2014 na 2015.

Ndalichako ambaye aliwahi kuwa Katibu Mtendaji wa baraza hilo kwa miaka tisa, alitoa maagizo hayo jana ambako pamoja na masuala mengine, alishuhudia namna alivyojaribiwa na kuletewa vishawishi jambo ambalo alisema, alilishinda kwa kusimamia taaluma.

Maagizo hayo aliyatoa alipotembelea na kuzungumza na viongozi, wafanyakazi wa NECTA ambako hakuridhishwa na maelezo yaliyotolewa na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde.

Alisema tangu alipoteuliwa kuwa Waziri, amepokea malalamiko mengi kutoka kwa wadau wa elimu na wananchi juu ya mfumo wa sasa wa upangaji matokeo wa GPA ambao umekuwa haueleweki na kwamba hawakushirikishwa katika mabadiliko hayo.

“ Nataka nijue sababu za kitaalamu za kubadilisha mfumo wa upangaji wa matokeo kutoka kwenye ule wa Division (madaraja) kwenda kwenye ule wa GPA na kama huo mfumo una tija kwa elimu yetu,” alisema.

Awali , Dk Msonde alisema mfumo huo ulipitishwa baada ya vikao kati yake, Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Baraza la Vyuo vya Ufundi (Nacte) na Wizara.

Alisema baraza lilitakiwa kuendesha mfumo huo ili kwenda na mifumo mingine ya elimu ya juu katika kurahisisha udahili wa wanafunzi kwenda sanjari na mfumo wa serikali mtandao na ajira.

Watahiniwa kujitegemea
Kuhusu uanzishwaji wa mtihani wa pili kwa watahiniwa wa kujitegemea, Ndalichako alisema, “Nataka sababu za watahiniwa wa kujitegemea kupewa mtihani wa pili ambao unachukuliwa kama alama upimaji endelevu kwa mwanafunzi.

“ Kama baraza ambalo ndio wataalamu, mnasema mmeamua kutoa mtihani wa pili kutokana na kupokea malalamiko ya kufeli na mtihani mgumu, basi hatuwezi kuendelea nao, nataka nipate sababu za kitaalamu na kama sababu haziridhisha basi mwaka huu wasifanyishwe mtihani wa pili,” alisema.

Alisema kwa kawaida, mtihani wa pili kwa watahiniwa wa kujitegemea hauwezi kuwa mbadala wa alama endelevu kwa wanafunzi. Alisema unaongeza mzigo kwa watahiniwa na gharama za kulipa wasimamizi na wasahihishaji wa mitihani hiyo.

Ashuhudia alivyojaribiwa
Ndalichako aliwataka viongozi wa baraza hilo kutokukurupuka katika kutoa uamuzi na kufanya mabadiliko yasiyo na tija kwa taifa. Badala yake, alisisitiza watumie utaalamu wao kushauri na kukataa maagizo yasiyo na tija kusaidia katika kuboresha elimu.

Katika hatua nyingine, Ndalichako aliwataka watendaji wa Baraza hilo kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu na kuepuka vishawishi. “ Baraza la Mitihani ni sehemu ngumu sana, hasa kutokana na kuhudumia watu na hasa katika suala zima la mitihani.

"Na ni eneo ambalo lina vishwishi vingi, hata mimi nilijaribiwa kuletewa vishawishi lakini nilisimama misimamo ya taaluma,” alisema.

Ndalichako pamoja na kuwapongeza Baraza kwa kutoa vyeti mbadala, ametaka kuwa makini katika suala hilo kuzuia udanganyifu.

Alisisitiza watoe tathmini ya kina katika matokeo ya wanafunzi ambayo yatasaidia wizara kufanya uboreshaji. “Nilipokuwa hapa, kuna wakati nilikuwa nakosa usingizi linapokuja suala la kutangaza matokeo, unakuta matokeo ya wanafunzi 30 yote ni mbaya, sasa hapa si kuwa wanafunzi wote walikuwa hawafundishiki ila kuna tatizo la ziada, na hilo ndio tunatakiwa kushughulikia,” alisema.

Alisema, “ Nilikuwa naumia sana na ubora wa elimu iliyokuwa ikitolewa kwa baadhi ya shule, sasa nimepewa kazi ya kuhakikisha elimu inakuwa bora, tunaondoa watu wa kuchora mazombi na ule wakati wa shule kugeuka vituo vya kulelea watoto badala ya kutoa elimu umefika mwisho.”