ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 30 Januari 2016

Mahakama ya mafisadi yaiva

SERIKALI imewahakikishia Watanzania kuwa mchakato wa kuanzishwa kwa Mahakama Maalumu ya mafisadi na wezi, umefikia hatua nzuri. Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe alisema hayo juzi bungeni mjini hapa, wakati akichangia Hotuba ya Rais ya Ufunguzi wa Bunge.
Akizungumzia mchakato wa kuanzishwa kwa mahakama hiyo maalumu, Mwakyembe alisema unakwenda vizuri na utakapokamilika Watanzania watafahamishwa. “Kiongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano, akitoa tamko lazima litekelezwe.
Kama tunakumbuka Rais, kwa nyakati tofauti kipindi cha kampeni, aliahidi kuanzisha Mahakama Maalumu ya Mafisadi na Wezi,” alisema Mwakyembe. Akiizungumzia hotuba ya Rais, Mwakyembe alisema ikiachwa hotuba ya Mwalimu Nyerere, ya Magufuli pia ni bora na iligusa mioyo ya Watanzania wenye nia njema na Taifa.
“Wakati rais anatoa hotuba yake iliyokuwa na aya 160, alipigiwa makofi na vigelegele mara 137, ni zaidi ya asilimia 86, ya Dk Martin Luther ambaye ni Mmarekani mweusi,” alisema na kuongeza kuwa hatua hiyo, imewaweka pabaya wapinzani waliokuwa wanapinga kila kitu.
Dk Mwakyembe alisema tatizo ni kwamba kwa hotuba hiyo, yeyote akijaribu kuipinga, wananchi watamuona wa hovyo. Aliendelea kusema; “Wamejaribu (upinzani) kutoka kwenye mjadala, kwa hoja tu ya TBC (Shirika la Utangazaji Tanzania), ili wasiwepo kwenye mjadala, kwani wakiwepo lazima wataisifia tu.”
January na Tanzania Mpya
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), January Makamba alisema safari ya kutengeneza Tanzania Mpya, haitakuwa nyepesi na ni lazima wajaribiwe, watiwe shaka na kukatishwa tamaa kuhusu mwelekeo wao.
Akijibu hoja za wabunge zilizotolewa wakati wa kujadili hotuba hiyo ya Rais Magufuli ya ufunguzi wa Bunge, aliyoitoa Novemba mwaka jana, January alisema;“ni kama kutengeneza keki ya mayai, lazima upasue mayai”.
Aliendelea kusema, “watu wasipate mashaka wala wasiwasi kwamba nchi inaelekea katika mwelekeo usiofaa. Tulifika mahala tukahitaji Rais wa namna hii, tumempata na tumuunge mkono.”
Kauli ya Waziri inalenga kujibu kauli za baadhi ya watu, ikiwemo wabunge wa vyama vya upinzani, ambao hivi karibuni walikosoa kazi ya ‘kutumbua majipu’ inayofanywa na Rais Magufuli pamoja na waziri, wakidai kwamba haizingatii taratibu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Utumishi na Utawala Bora, George Simbachawene alisema kazi ya Rais Magufuli ya kuisuka Serikali haijakamilika, kwani anaendelea kwa wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi hadi kwa wakuu wa idara, watakaochujwa kuhakikisha wanaendana ya kaulimbiu yake ya ‘Hapa Kazi Tu’.
Alisema Tanzania mpya ya Magufuli inayokuja ni ya watu wanaofanya kazi. Tunataka tuwahakikishie kwamba Rais anaendelea kuisuka serikali na mtambue kwamba serikali bado haijakamilika, bado tunahitaji wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya lakini tunakwenda vizuri zaidi tunataka kusuka wakurugenzi.
“Tunakwenda mbali kusuka mpaka wakuu wa idara, tunataka tuwachuje vizuri kabisa na siyo kuokotana okotana. Tunataka Tanzania mpya tukianzia juu tukisema hapa kazi tu basi ni hapa kazi,” alisema.
Hotuba ya Rais Bungeni Akizungumzia Mapambano Dhidi ya Rushwa na Ufisadi, alipofungua rasmi Bunge mjini Dodoma, Novemba 20, mwaka jana, 2015, Rais Magufuli alisema, “Jambo moja nililolisemea kwa nguvu kubwa wakati wa kampeni ni mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi.
Sikufanya hivyo kwa sababu nilitaka tu kuwarubuni wananchi ili wanipe kura zao na kunifanya kuwa Rais wao. Nililiongea jambo hili kwa dhati kabisa, na nilichokisema na kuwaahidi wananchi ndicho hasa nilichokikusudia. Wananchi wanachukia sana rushwa na ufisadi, na wamechoshwa na vitendo hivyo.
Mimi pia ninachukia rushwa na ufisadi. Sifurahishwi kabisa na vitendo vya rushwa na ufisadi vinavyoendelea hapa nchini. Vitendo vya rushwa na ufisadi vinawanyima haki wananchi na kuitia hasara serikali kwa mamilioni ya fedha ambazo zingeweza kutumika kwa ajili ya kujenga miradi ya maendeleo kwa ajili ya watu wetu.”
Magufuli alisema “Mimi nimewaahidi wananchi, na nataka nirejee ahadi yangu kwao mbele ya Bunge lako tukufu, kwamba nitapambana na rushwa na ufisadi bila kigugumizi na bila haya yoyote. Dawa ya jipu ni kulitumbua, na mimi nimejipa kazi ya kuwa mtumbua jipu. Najua kutumbua jipu kuna maumivu lakini bahati mbaya halina dawa nyingine.
Hivyo ninaomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote mniombee na muniunge mkono wakati natumbua majipu haya.” Alieleza kuwa anafahamu ugumu wa vita aliyoamua kuipigana na anafahamu ugumu na changamoto zake kwa sababu wanaojihusisha na rushwa, sio watu wadogo wadogo.
Alisema Vitendo vya rushwa na ufisadi vyenye madhara makubwa kwa nchi na ustawi wa nchi yetu, hutendwa na watu wenye dhamana kubwa za uongozi na utumishi, ambazo wamezipata kutokana na ridhaa ya watu.
“Katika kushughulikia tatizo hili, nimeahidi kuunda Mahakama ya Rushwa na Ufisadi. Ni matumaini yangu vyombo husika katika jambo hili havitanikwamisha,” alisema Magufuli.

Hoja ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa yaondolewa bungeni

WAZIRI wa Fedha, Dk Philip Mpango ameondoa hoja ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa kwa kipindi cha miaka mitano 2016/17 mpaka 2020/21 aliyoiwasilisha bungeni jana.
Hatua hiyo ilitokana na mwongozo uliotolewa kwa nyakati tofauti na wabunge; Mbunge wa Kigoma Mjini, Kabwe Zitto (ACT Wazalendo) na wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema).
Wabunge hao walisema Waziri amewasilisha hoja kinyume na kanuni za kudumu za Bunge, zinazosema katika mkutano wa bunge wa kila Oktoba na Novemba, Serikali inatakiwa kuwasilisha mpango wa maendeleo wa taifa wa kila mwaka.
“Kutokana na maelezo uliotoa (Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge) na kwa kutumia kanuni ya hamsini na nane, tano ya kanuni za kudumu za Bunge toleo la 2016, naomba ruhusu kuondoa hoja niliyoiwasilisha leo (jana) asubuhi ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa kwa kipindi cha miaka mitano 2016/17 mpaka 2020/21,” alisema Dk Mpango.
Hoja hiyo iliondolewa baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Chenge kutoa mwongozo na kisha kuahirisha Bunge hadi kesho kutwa. Awali katika maelezo yao bungeni na nje ya Bunge, wakati wakizungumza na waandishi wa habari, Zitto na Lissu walisema uwasilishwaji wa hoja ya Waziri Mpango, umekiuka Katiba. Hata hivyo akitoa mwongozo, Chenge alisema suala hilo halikukiuka katiba.
“Nimelitafakari sana jambo hili, na baada ya kutafakari hakuna ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.” Alisema kilicholetwa na serikali ni mchakato wa kushirikisha wawakilishi wa Tanzania ili watoe maoni, ushauri na mapendekezo yao kuhusu na mpango unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali katika mwaka wa fedha 2020/16/17.
Alisema kitu ambacho wabunge lazima wakubali, ni kwamba kulingana na Kanuni ya 94 (1), Bunge linapofanya kazi hiyo huwa haliketi kama Bunge, bali linaketi kama kamati ya mipango. “Hiyo ni dosari ambayo tumeiona,” alisema na kukiri kwamba hapa ilikuwa ni mpango wa muda mfupi.
Hata hivyo alisema Ibara ya 63 haisemi ni lini huo mpango uletwe. Alikiri kuwa mpango mfupi unatokana na wa mwaka mitano, ambao hitimisho lake ni pale waziri atakaposoma mpango wa serikali kwa mwaka unaofuata wa fedha na jioni yake, Waziri anaposoma bajeti ya serikali.
Akihimiza kuwa Kanuni ya 94 (1) lazima izingatiwe, Chenge alisema, “Bunge halikuweza kukutana Oktoba na Novemba kama kanuni hiyo inavyotaka kwa sababu kulikuwa na shughuli kubwa ya uchaguzi.
Alisema Serikali na Bunge hawakuwa na njia nyingine, jambo ambalo ilikuwa lazima mchakato ufanyike sasa ili Machi 11, serikali iwasilishe mbele ya wabunge kama ilivyofanyika mwaka jana katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam.
“Waziri mwenye dhamana anawasilisha mipango na ukomo wa bajeti. Wakishawasilisha, katibu wa bunge ndiye anapeleka kwa spika ili aelekeze ipelekwe kwenye kamati ya bajeti hadi watakapokuja kutoa taarifa,” alisema.
Kwa mujibu wa kanuni, siku ya kusoma bajeti ya serikali, waziri anawasilisha hoja yake ya mpango; utekelezaji wa hali ya mwaka jana na mwaka unaofuata. Hivyo kunakuwa na hoja mbili ambazo hujadiliwa kwa pamoja; hoja ya mpango na ya bajeti ya serikali.
“Haya ndiyo yanapaswa yafanyike,” alisema na kusihi wabunge kuelewa kanuni. Baada ya maelezo hayo, Chenge alimuita Waziri mtoa hoja; Waziri wa Fedha, aombe idhini ya Bunge ya kuondoa hoja. Kabla ya kutoa hoja hiyo, wabunge walihojiwa, na wote waliridhia.

Magufuli awateua Chagonja, Mtweve makatibu tawala

RAIS John Magufuli amefanya uteuzi wa makatibu tawala wawili wa mikoa ya Mwanza na Katavi, ili kujaza nafasi za makatibu tawala wa mikoa hiyo. Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema Dar es Salaam jana kuwa Rais amemteua Kamishna wa Polisi, Clodwing Mtweve kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, ambako anakwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Faisal Issa ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Kabla ya uteuzi huo, Kamishna Mtweve alikuwa Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Polisi Tanzania. Balozi Sefue alisema Rais Magufuli pia amemteua Kamishna wa Polisi, Paul Chagonja kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, ambako anakwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Madeni Kipande, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Kabla ya uteuzi huo, Kamishna Chagonja alikuwa Kamishna wa Mafunzo na Operesheni wa Jeshi la Polisi Tanzania. Aidha, Balozi Ombeni Sefue alisema Rais Magufuli ameamua kuwateua Makamishna hao wa Polisi, kama alivyowateua Majenerali wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania kuwa Makatibu Wakuu wa Wizara, kwa lengo la kujenga nidhamu katika utumishi wa umma.
Makamishna Clodwing Mtweve na Paul Chagonja pamoja na Mahadhi Juma Maalim ambaye ameteuliwa kuwa Balozi mpya wa Kuwait, wataapishwa jijini Dar es Salaam leo saa nne asubuhi.

Jumatatu, 25 Januari 2016

MAPENZI SHIDA PART 2

KWA HISANI YA OMBENI LONGO&HELMAN MHANGA

Baada ya JENIFER na wenzake kukamatwa na mwalimu na kupewa adhabu hiyo ya kwenda na wazazi wao shuleni siku ya Ijumaa tatu na kupelekea kupoteza mudi ya kuendelea kufurah usiku huo ikawabidi waondoke kabisa sehemu hiyo ya CLUB usiku huo huo na kwenda kulala kwenye chumba cha rafiki yao CHRISTINA waliekuwa nae katika kundi lao usiku huo, ilipofika kesho yake siku ya ijumaa pili asubuhi kila mtu alirejea nyumbani kwao huku wakiwa na sura za hudhuni na mawazo kibao kichwani wakijiuliza itakuaje kesho yake ambayo ni siku ya Ijumaa tatu wanatakiwa waende shule na wazazi wao?!. Jenifer alipofika kwao moja kwa moja alielekea chumbani kwake na kujilaza kitandani huku akiwa na mawazo kibao hata chakula hakuweza kula siku hiyo muda wote alikua kajifungia chumbani analia. Ghafla akasikia mlango wa chumbani kwake unafunguliwa aliposhtuka akamuona mama yake Mrs. Brown. Mrs. Brown alimsogelea binti yake Jenifer kuanza kuzungumza nae kama ifuatavyo:-
MRS. BROWN: "Jenifer binti yangu mbona unaonekana leo hauko sawa, nini tatizo mwanangu?! Na mbona unalia? 
JENIFER: "Hapana mama, wala usijali hamna kitu chochote naomba uwe na amani mama yangu, niko sawa tu!" 
MRS. BROWN: "Jenifer mwanangu lazima kutakuwa kuna kitu ila unaficha. Mwanangu nakuomba unieleze usinifiche niambie tu mwanangu wala usiogope" 
JENIFER: "Mama wala usijali hakuna kitu chochote kile" 
MRS. BROWN: "Sidhani binti yangu kama kweli hakuna tatizo sasa mbona unalia, Au umepata ujauzito?! 
JENIFER: "Mama bora ningekua nina ujauzito ila kwa hiki kilichonipata mama yangu najuta tena najuta hata sijui kwanini mlinipeleka shule mama yangu" 
MRS. BROWN: "Mwanangu mbona unasema hivyo kwani kuna tatizo limetokea shule?! 
JENIFER: "Ndio mama, kuna mwalimu shuleni alinitongoza nikamkatalia sasa kila siku huwa ananichapa fimbo bila makosa na ananitesa sana shule na kaniahidi kuwa atanitafutia kosa lolote la uongo ili nifukuzwe shule anikomoe na juzi siku ya Ijumaa kuna wanafunzi kawakamata usiku CLUB akawaambia kuwa atawafukuza shule sasa kaniambia namimi ataniingiza katika hilo kosa la hao wanafunzi kesho shuleni ili nifukuzwe namimi" 
MRS. BROWN: "Haiwezekani mwanangu wewe nyamaza acha kulia tumsubiri baba yako aje nimuelezee ikiwezekana kesho akupeleke shule akamkomeshe huyo mwalimu, wala usiwaze sana mwanangu Jenifer looooo, huyo mwalimu hana hata aibu" 
Baada ya Jenifer kutumia uongo wa kumdanganya mama yake Mrs. Brown kwa dhumuni la kujitetea kutokana na kosa alilolifanya usiku wa jana yake walipokutwa na mwalimu wao wa shule CLUB ikamlazimu kumpa kesi ya uongo yule mwalimu kwa wazazi wake ili wasimuone yeye anamakosa. Mama yake na Jenifer Mrs. Brown alihamaki na kuingiwa na hasira akawa anamsubiria mume wake arudi ili amuelezee kilichotokea. Ghafla baba yake na Jenifer Mr. Brown akaingia nyumbani kwake na kumkuta mke wake Mrs. Brown akiwa na binti yao Jenifer, Jenifer alipomuona baba yake Mr. Brown akaanza kuangua kilio huku akisema "BABA NAJUTA MIMI MWANAOO, NAJUTA BABA HIVI KWANINI ULINIPELEKA NIKASOME ILE SHULE BABA YANGUUUUUU" Jenifer alikua analia huku akitoa sauti kubwa ya kumlalamikia baba yake. Mr. Brown alipigwa na butwaa hakujua nini kinachoendelea ikabidi akae chini na kumuuliza mke wake "MKE WANGU NINI KIMEMPATA BINTI YETU JENIFER?" Mrs. Brown akamjibu mume wake "MUME WANGU NENDA KWANZA KAKOGE KISHA ULE HALAFU NDIO NIKUELEZEE KILICHOTOKEA" Mr. Brown nae akamjibu "HAPANA MKE WANGU NIELEZEE KWANZA NIJUE TATIZO NINI?". Mrs. Brown ikabidi aanze kumuhadithia kama alivyohadithiwa na binti yao Jenifer kuwa kuna mwalimu wa shule alimtongoza binti yao akamkataa sasa huyo mwalimu anamtesa sana Jenifer shuleni na kamuahidi atamfanyia njama yoyote ili binti yao afukuzwe shuleni. Pale pale Mr. Brown nayeye akapandwa na hasira akamnyamazisha binti yake Jenifer na kumwambia "JENIFER BINTI YANGU NYAMAZA, KESHO IJUMAA TATU ASUBUHI TUTAKWENDA WOTE MPAKA SHULENI KWENU UKANIONESHE HUYO MWALIMU. ATANITAMBUA" baada ya hapo wakatawanyika Jenifer akaingia chumbani akaanza kushangilia peke yake kimya kimya akiwa na imani kuwa kishamaliza kesi aliyokuwa nayo na akawa na furaha tele akaendelea kufanya mambo yake kama kawaida.

VICHWA VYA MAGAZETI YA LEO TAR 25JANUARY 2016

MAPENZI SHIDA PART ONE

 Hadithi inayomuhusu binti wa kitanzania alietunukiwa uzuri wa asili na mvuto wa kipekee aliojaaliwa na mungu ama hakika uzuri aliokuwa nao ulikuwa ni kishawishi tosha kwa mwanaume yoyote aliemtazama binti huyu na kutamani kuwa nae kutokana na mvuto aliokuwa nao binti huyu anaitwa Jenifer na amezaliwa katika familia duni ya Mr. Brown na Mrs. Brown yenye watoto watatu (3). Ambao ni Peter, Joseph na Jenifer na katika watoto hawa watatu mwanamke alikua ni Jenifer peke yake na ndie alikua mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia hii yenye watoto watatu ambapo Peter na Joseph walikua ni wadogo zake na Jenifer na walikuwa bado ni wadogo sana. Na wazazi wa Jenifer Mr. Brown na Mrs. Brown walitokea kumpenda sana binti yao Jenifer kwani ndio mtoto pekee wa kike hivyo walionesha upendo mwingi kwa binti yao kwa kumtimizia mahitaj yote muhimu na kumpa kila alichokitaka binti yao ili wamridhishe na kuhakikisha wanampa malezi bora na kujenga upendo imara kwa binti yao. Kutokana na hali ya ngumu ya maisha iliyokuwepo katika familia hiyo ya Mr. Brown na Mrs. Brown, wazazi hawa walikaa na kujadili njia sahihi ya kuweza kukabiliana na umasikini walio nao na kuweza kujikwamua kimaisha wakapata wazo la kumpeleka shule binti yao Jenifer ili hapo baadae aje kuwasaidia wazazi wake kupitia elimu atakayoipata shule hivyo wazazi wakakubaliana na kuanza mipango ya kumuandikisha shule binti yao ili aanze kusoma, wazazi wa Jenifer walijitahidi kutafuta pesa kwa hali na mali ikapelekea wazazi wa Jenifer kujiunga na kampuni zinazotoa mikopo ya fedha lengo kupata pesa waweze kumtimizia mahitaji binti yao aweze kuanza shule. Mungu alileta kheri kwa wazazi hao na kufanikisha kuipata pesa ya kumpatia binti yao kwa ajili ya matumizi madogo madogo ya shule na binti yao akafanikiwa kuanza elimu ya msingi akasoma darasa la kwanza mpaka darasa la saba lakini alipo maliza darasa la saba matokeo yake hayakua mazuri hivyo hakuweza kuchaguliwa katika shule za serekali kwa ajili ya kuendelea na elimu ya sekondari lakini wazazi wa Jenifer hawakukata tamaa na waliendelea kuwa na moyo wa kumsaidia binti yao Jenifer kwa vyovyote vile mpaka waone mwisho wake kwani malengo yao binti yao asome mpaka daraja la juu afike mpaka chuo kikuu, baada ya Jenifer kumaliza elimu ya msingi na hakufanikiwa kufanya vizuri katika mitihani yake ikabidi wazazi wajipange upya kutafuta ada ya kumlipia binti yao ili aweze kujiunga na elimu ya sekondari kwa dhumuni la kuhakikisha binti yao Jenifer anaendelea na elimu. Mungu hakuitupa familia hii ya Mr na Mrs. Brown aliwajaalia wakafanikiwa kuipata pesa ya kumlipia ada binti yao na wakamuandikisha katika shule ya kulipia ya sekondari iliyofahamika kwa jina la "GARDEN SECONDARY SCHOOL" Jenifer alijiunga na shule hii na kuanza elimu yake ya sekondari lakini kama ilivyo kwa vijana wengi wa kisasa kutofahamu umuhimu wa elimu na kushindwa kujua nini wanapaswa kukifanya pindi wanapo kuwa shule ndivyo ilivyokuwa kwa Jenifer. Jenifer hakujua umuhimu wa elimu na hakuona juhudi za wazazi wake kwake za kutafuta pesa kwa ajili ya kumlipia ada ili aje kuwasaidia baadae na kuwasaidia wadogo zake Peter na Joseph. Kipindi Jenifer alipokua shuleni hapo akiendelea na elimu ya sekondari tabia yake ilibadilika akawa anautumia muda wake mwingi wa shule kujichanganya na marafiki ambao hawakuwa na msaada mzuri kwake na wakati mwingine alikua akiaga kwao anakwenda shule lakini alikua hafiki shule alikua anakwenda kwa marafiki anashinda na kurudi nyumbani wazazi wake hawakujua kinachoendelea kwa binti yao. Wakati mwingine Jenifer alikuwa ni mtu wa kupenda sana kwenda kwenye kumbi mbali mbali za starehe wakati alikua anatoka nyumbani kwao usiku akiwaaga wazazi wake kuwa anakwenda kwa marafiki zake anaosoma nao wanakwenda kukesha wakisoma na kujadiliana yale waliyofundishwa shuleni, wazazi wa Jenifer hawakuwa na kipingamizi kwa binti yao walikua ridhwaa kukubaliana na kila anachohitaji binti yao ili mradi kumridhisha na kumfanya awe huru ili mwisho wa siku aweze kutimiza ndoto za wazazi wake hivyo wazazi walikua wakimpa ruhusa binti yao atoke usiku wakidhani anaenda kusoma na wenzake kumbe Jenifer alikua anatumia muda huo kutoka na kwenda CLUB (kumbi za starehe) na marafiki zake wanaenda kujirusha na alikua anarudi nyumbani kwao kesho yake asubuhi, na ilikua kila ikifika siku ya Ijumaa mosi ndio anatoka usiku na wenzake, siku moja kama kawaida yake Jenifer na wenzake wametoka na kwenda kwenye kumbi za starehe huku nyumbani wazazi wanajua watoto wao wameenda katika masomo yao kama ilivyozoeleka, kipindi wapo CLUB kuna mwalimu wao wa shule alikuwepo katika ukumbi huo wa starehe na akakutana na kundi hili la wakina dada kama wanne akiwemo na Jenifer wakiwa wamevaa mavazi mafupi ya ajabu kama machangudoa wanaojiuza, yule mwalimu wao alichokifanya akawaita kisha akawaambia "NAOMBA SIKU YA IJUMAA TATU MKIFIKA SHULE CHA KWANZA NAOMBA NIWAKUTE OFISINI KWANGU KAMA MLIVYO WANNE TENA MJE MKIWA MMEVAA HIZI NGUO MLIZO ZIVAA NA KILA MMOJA WENU AJE NA MZAZI WAKE" kisha mwalimu akawaambia wawe huru waendelee na mambo yao ila ikifika siku ya Ijumaa tatu siku ya shule wafanye kama alivyo agiza mwalimu huyo pale pale Jenifer na wenzake wakakosa amani na mudi ya kuendelea kufurahi usiku ule ikatoweka na kila mmoja wao akawa anawaza itakuaje hiyo siku ya Ijumaa tatu na wataanzia wapi kuwaeleza wazazi wao juu ya kosa hili walilofanya mpaka wamekutana na mwalimu kawaomba waende shule na wazazi wao.....?!