ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 6 Februari 2016

India waomba radhi kwa Watanzania kudhalilishwa

Imeandikwa na Sifa Lubasi, Dodoma
Imechapishwa: 06 Februari 2016
SERIKALI ya India imeiomba radhi serikali ya Tanzania, kufuatia kudhalilishwa na kupigwa kwa wanafunzi wa Tanzania wanaosoma nchini humo.
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika, Kikanda na Uhusiano wa Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga, aliliambia Bunge, jana, mjini hapa, wakati akitoa taarifa ya serikali kuhusu hatua zilizochukuliwa serikali ya India kufuatia tukio hilo.
Alisema tayari serikali ya India, imewachukulia hatua wote waliohusika na tukio hilo na wamefikishwa mahakamani.
Balozi Mahiga alisema serikali ya India, imeagiza kuwa wanafunzi wa Watanzania wapewe ulinzi maalumu kwenye maeneo wanakoishi na wasindikizwe wanapokwenda masomoni.
Aidha alisema serikali ya India ilimtaka balozi wa Tanzania afuatane na maofisa waandamizi, wa Wizara ya Mambo ya Nje ya India kwenda Bangalore ili kukutana na wanafunzi wa Tanzania na wengine wa Afrika kufanya mikutano na wanafunzi hao.
Balozi Mahiga alisema tukio hilo lilitokea baada ya uendeshaji mbaya wa gari uliofanywa na mwanafunzi kutoka Sudan ambaye aligonga pikipiki tatu na baada ya hapo kumgonga mama wa kihindi aliyekufa papo hapo.
Alisema baada ya tukio hilo, mwanafunzi huyo alikimbia na wananchi waliokuwa jirani walichoma gari lake moto na kwamba baada ya muda lilitokea gari lingine likiwa na wanafunzi wanne Watanzania akiwemo msichana mmoja.
Balozi Mahiga alisema wananchi hao walilisimamisha gari hilo na kuwatoa nje wanafunzi hao ambapo mwanafunzi wa kike alivuliwa nguo na kutembezwa mitaani uchi, huku wanaume wakipigwa sehemu mbalimbali za miili yao na gari lao lilichomwa moto.
“Katika gari hilo kulikuwa na simu zao na document (nyaraka) mbalimbali ambazo ziliteketea,” alisema.
Alisema baada ya muda, polisi walifika lakini walishindwa kutoa ushirikiano ingawa waliwachukuwa na kuwapeleka hospitali. Balozi Mahiga alisema, “Kule hospitali walionekana wana majeraha makubwa, walitibiwa lakini ikabidi waondoke kwa sababu walikuwa hawana fedha za kutosha za kugharamia matibabu”.
Alisema baada ya hapo, Balozi wa Tanzania aliyeko India aliandika dokezo la kidiplomasia kwa serikali ya India kulaani kitendo hicho na kuitaka serikali ya India, ichukue hatua za kisheria na za haraka katika kupeleleza tukio hilo.

ILULA KWETU

welcome small city ILULA- HOME OF HOSPITALITY

Population of Ilula:

29 193 people

Latitude of Ilula:

-7,6833 (740'59.988"S)

Longitude of Ilula:

36,0333 (361'59.880"E)

Altitude of Ilula:

1 505 m

Article: Tanzania

Biggest cities: Tanzania

Photos, pictures: Tanzania

All cities: Tanzania


The biggest cities of the World

GMT time in Ilula:

+3 hours

Distance from city Ilula to 25 biggest cities of country: Tanzania

Distance (Km)
 Ilula - Dar Es Salaam  372 km
 Ilula - Unguja Ukuu  398 km
 Ilula - Mwanza  671 km
 Ilula - Zanzibar  387 km
 Ilula - Arusha  485 km
 Ilula - Mbeya  315 km
 Ilula - Morogoro  204 km
 Ilula - Tanga  447 km
 Ilula - Dodoma  170 km
 Ilula - Kigoma  774 km
 Ilula - Moshi  503 km
 Ilula - Moschi  503 km
 Ilula - Tabora  464 km
 Ilula - Songea  336 km
 Ilula - Musoma  731 km
 Ilula - Mazama  731 km
 Ilula - Iringa  38 km
 Ilula - Katumba  317 km
 Ilula - Shinyanga  531 km
 Ilula - Mtwara  539 km
 Ilula - Ushirombo  648 km
 Ilula - Kilossa  141 km
 Ilula - Sumbawanga  488 km
 Ilula - Bagamoyo  346 km
 Ilula - Bagamojo  346 km

Distance from city: Ilula to Top 10 cities of the world

Distance (Km)
 Ilula - Berlin  6 992 km
 Ilula - London  7 385 km
 Ilula - Los Angeles  16 065 km
 Ilula - Moscow  6 973 km
 Ilula - New York  12 262 km
 Ilula - Paris  7 034 km
 Ilula - Peking  9 691 km
 Ilula - Rio De Janeiro  8 565 km
 Ilula - Sydney  11 806 km
 Ilula - Tokyo  11 679 km
 Ilula - Prague  6 761 km

HAO NDIO MAWAZIRI VIVULI

KAMBI rasmi ya upinzani bungeni, imetangaza baraza lake la mawaziri kivuli ambalo Chama cha ACT Wazalendo, chenye mbunge mmoja, Kabwe Zitto, ndicho hakikuingizwa kwenye baraza hilo. Kiongozi wa kambi hiyo, Freeman Mbowe alitangaza jana bungeni baraza hilo.
Chadema chenye wabunge wengi katika kambi hiyo, kina mawaziri vivuli wengi ikilinganishwa na vyama vingine na wakati huo huo, kina wizara nyingi ambazo kinaongoza peke yake kwa maana ya kuwa na mawaziri na naibu mawaziri vivuli.
Mawaziri, naibu mawaziri vivuli wa Chadema ni katika Wizara ya Ofisi ya Rais, Tamisemi, ambayo Waziri Kivuli ni Mbunge wa Moshi Mjini, Japhary Michael (Chadema) na Naibu wake ni Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi (Chadema).
Wizara ya Fedha na Mipango inaongozwa na wabunge wa Chadema ambao ni Halima Mdee wa Kawe na Mbunge wa Momba, David Silinde. Kwa upande wa Wizara ya Nishati na Madini pia inaongozwa na wabunge wote wa Chadema. Waziri kivuli ni Mbunge wa Kibamba, John Mnyika na Naibu wake ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche.
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaongozwa na Mbungewa Siha, Dk Godwin Mollel (Chadema) na naibu wake ni Mbunge wa Viti Maalumu, Zubeda Sakuru (Chadema).
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo inaongozwa na wabunge wa Chadema; ambao ni Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ambaye ni waziri kivuli akisaidiana na wa Viti Maalumu, Devotha Minja.
Kwa upande wa wizara ya Utumishi, Utawala Bora inaongozwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Ruth Mollel (Chadema) pekee bila naibu.
Mawaziri Chadema kuhusu wizara ambazo mawaziri vivuli ni wa Chadema na manaibu ni wa vyama vingine, ni Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu inaongozwa na Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema). Bulaya anasaidiana na manaibu ambao wote ni wa CUF.
Nao ni Mbunge wa Chake Chake, Yusuf Kaiza Makame na Abdallah Maftah wa Mtwara Mjini .
Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa inaongozwa na Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa na Naibu wake Mbunge wa Viti Maalumu, Riziki Mngwali (CUF).
Mambo ya Ndani ya Nchi amepangiwa Mbunge wa Arusha, Godbless Lema (Chadema) akisaidiwa na Mbunge wa Mtambile, Masoud Abdallah Salim (CUF), Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaongozwa na Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare (Chadema) na naibu wake ni Mbunge wa Viti Maalumu, Salma Mwassa (CUF).
Waziri kivuli mwingine ni Suzane Lyimo wa Viti Maalumu anayeongoza Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi akisaidiana na Mbunge wa Mgogoni, Dk Ali Suleiman Yusuf (CUF) ambaye ni naibu.
Wizara ya Katiba na Sheria inaongozwa na Mbunge Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema ) akisaidiana na Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolela (CUF).
Mawaziri wa CUF, Wizara zinazoongozwa na CUF kwa maana ya waziri kivuli kutoka chama hicho, ni Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, ambayo Mbunge wa Malindi, Ali Saleh Ali(CUF) anasaidiana na Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul (Chadema).
CUF imepata pia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambayo Waziri kivuli ni Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya (CUF) na naibu ni Mbunge wa Viti Maalumu, Dk Immaculate Semesi (Chadema).
Kwa upande wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi laKujenga Taifa, inaongozwa na Mbunge wa Ole, Juma Hamad Omary (CUF) na naibu wake ni Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema). Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali (CUF) anaongoza wizara ya Maji na Umwagiliaji akisaidiwa na Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali (Chadema).
Mbunge wa Vunjo, James Mbatia (NCCR) amepangiwa wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano akisaidiwa na Naibu ambaye ni Mbunge wa Karatu, Qambalo Qulwi (Chadema). Kiongozi wa Upinzani bungeni, Mbowe aliomba wote wanaohusika watoe ushirikiano kwa baraza hilo kadri inavyowezekana.

Jumamosi, 30 Januari 2016

Simba, Yanga leo tena

DURU la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara linaanza leo wakati timu 12 zikiwemo za Yanga na Simba kushuka kwenye viwanja tofauti kusaka pointi tatu muhimu. Hata hivyo, Azam FC inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo, leo ilitakiwa kucheza na Prisons ya Mbeya, haitashuka dimbani kwa sababu inashiriki mashindano ya timu nne nchini Zambia.
Yanga wenyewe wako kileleni wakiwa na pointi 39 sawa na Azam FC, lakini wanaongoza kwa uwiano wa tofauti ya magoli, leo watakuwa wageni wa Coastal Union katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
Katika mchezo wa raundi ya awali, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Yanga watataka kudhihirisha kuwa hawakubahatisha kuifunga Coastal katika mchezo wa kwanza, huku Wagosi hao wa Kaya nao watataka kudhihirisha wao sio wanyonge mbele ya mabingwa hao watetezi.
Vijana hao wa Jangwani wakishinda leo watakuwa wamejikusanyia pointi 42 na kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo na kuiacha Azam FC ikibaki na pointi zake 39 katika nafasi ya pili.
Kwa upande wa Simba, wenyewe katika mchezo wa kwanza dhidi ya African Sports uliochezwa Mkwakwani, iliibuka na ushindi kiduchi wa bao 1-0, hivyo na leo itataka kuendeleza ubabe dhidi ya vijana hao wa Tanga.
Simba yenye pointi 33, inazihitaji sana pointi tatu kutoka kwa African Sports ili angalau izidi kujisogeza katika nafasi ya tatu nyuma ya Azam katika mbio hizo za ubingwa wa ligi hiyo.
Kwa sasa Simba inafundishwa na Mganda Jackson Mayanja aliyechukua nafasi ya Muingereza Dylan Kerr aliyetimuliwa licha ya timu hiyo kuwa katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi hiyo.
Mayanja alisema pamoja na ugumu wa mchezo huo, watajitahidi kuibuka na ushindi ili kuendelea kuzifukuza Yanga na Azam FC zilizoko kileleni. Coastal Union na African Sports ziko katika nafasi ya 14 na 15 baada ya kucheza mechi 15 na kuambulia pointi tisa na 10 badala ya kuwa na pointi 45 kutoka katika mechi hizo 15 za duru la kwanza.
Mechi zingine leo ni JKT Ruvu watakuwa wenyeji wa Majina ya Songea, huku Mtibwa Sugar wakiikaribisha Stand United, wakati Mwadui FC itaikaribisha Toto African wakati Kagera Sugar watacheza na Mbeya City na Mgambo JKT watakuwa wenyeji wa Ndanda FC.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa Mgambo kuikaribisha Ndanda FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga. Kwa upande wa ufungaji mabao, Amis Tambwe ndiye anayeongoza hadi duru la kwanza linapomalizika baada ya kupachika mabao 13 huku Hamisi Kiiza wa Simba akifuatia kwa mabao 10.

Mahakama ya mafisadi yaiva

SERIKALI imewahakikishia Watanzania kuwa mchakato wa kuanzishwa kwa Mahakama Maalumu ya mafisadi na wezi, umefikia hatua nzuri. Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe alisema hayo juzi bungeni mjini hapa, wakati akichangia Hotuba ya Rais ya Ufunguzi wa Bunge.
Akizungumzia mchakato wa kuanzishwa kwa mahakama hiyo maalumu, Mwakyembe alisema unakwenda vizuri na utakapokamilika Watanzania watafahamishwa. “Kiongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano, akitoa tamko lazima litekelezwe.
Kama tunakumbuka Rais, kwa nyakati tofauti kipindi cha kampeni, aliahidi kuanzisha Mahakama Maalumu ya Mafisadi na Wezi,” alisema Mwakyembe. Akiizungumzia hotuba ya Rais, Mwakyembe alisema ikiachwa hotuba ya Mwalimu Nyerere, ya Magufuli pia ni bora na iligusa mioyo ya Watanzania wenye nia njema na Taifa.
“Wakati rais anatoa hotuba yake iliyokuwa na aya 160, alipigiwa makofi na vigelegele mara 137, ni zaidi ya asilimia 86, ya Dk Martin Luther ambaye ni Mmarekani mweusi,” alisema na kuongeza kuwa hatua hiyo, imewaweka pabaya wapinzani waliokuwa wanapinga kila kitu.
Dk Mwakyembe alisema tatizo ni kwamba kwa hotuba hiyo, yeyote akijaribu kuipinga, wananchi watamuona wa hovyo. Aliendelea kusema; “Wamejaribu (upinzani) kutoka kwenye mjadala, kwa hoja tu ya TBC (Shirika la Utangazaji Tanzania), ili wasiwepo kwenye mjadala, kwani wakiwepo lazima wataisifia tu.”
January na Tanzania Mpya
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), January Makamba alisema safari ya kutengeneza Tanzania Mpya, haitakuwa nyepesi na ni lazima wajaribiwe, watiwe shaka na kukatishwa tamaa kuhusu mwelekeo wao.
Akijibu hoja za wabunge zilizotolewa wakati wa kujadili hotuba hiyo ya Rais Magufuli ya ufunguzi wa Bunge, aliyoitoa Novemba mwaka jana, January alisema;“ni kama kutengeneza keki ya mayai, lazima upasue mayai”.
Aliendelea kusema, “watu wasipate mashaka wala wasiwasi kwamba nchi inaelekea katika mwelekeo usiofaa. Tulifika mahala tukahitaji Rais wa namna hii, tumempata na tumuunge mkono.”
Kauli ya Waziri inalenga kujibu kauli za baadhi ya watu, ikiwemo wabunge wa vyama vya upinzani, ambao hivi karibuni walikosoa kazi ya ‘kutumbua majipu’ inayofanywa na Rais Magufuli pamoja na waziri, wakidai kwamba haizingatii taratibu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Utumishi na Utawala Bora, George Simbachawene alisema kazi ya Rais Magufuli ya kuisuka Serikali haijakamilika, kwani anaendelea kwa wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi hadi kwa wakuu wa idara, watakaochujwa kuhakikisha wanaendana ya kaulimbiu yake ya ‘Hapa Kazi Tu’.
Alisema Tanzania mpya ya Magufuli inayokuja ni ya watu wanaofanya kazi. Tunataka tuwahakikishie kwamba Rais anaendelea kuisuka serikali na mtambue kwamba serikali bado haijakamilika, bado tunahitaji wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya lakini tunakwenda vizuri zaidi tunataka kusuka wakurugenzi.
“Tunakwenda mbali kusuka mpaka wakuu wa idara, tunataka tuwachuje vizuri kabisa na siyo kuokotana okotana. Tunataka Tanzania mpya tukianzia juu tukisema hapa kazi tu basi ni hapa kazi,” alisema.
Hotuba ya Rais Bungeni Akizungumzia Mapambano Dhidi ya Rushwa na Ufisadi, alipofungua rasmi Bunge mjini Dodoma, Novemba 20, mwaka jana, 2015, Rais Magufuli alisema, “Jambo moja nililolisemea kwa nguvu kubwa wakati wa kampeni ni mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi.
Sikufanya hivyo kwa sababu nilitaka tu kuwarubuni wananchi ili wanipe kura zao na kunifanya kuwa Rais wao. Nililiongea jambo hili kwa dhati kabisa, na nilichokisema na kuwaahidi wananchi ndicho hasa nilichokikusudia. Wananchi wanachukia sana rushwa na ufisadi, na wamechoshwa na vitendo hivyo.
Mimi pia ninachukia rushwa na ufisadi. Sifurahishwi kabisa na vitendo vya rushwa na ufisadi vinavyoendelea hapa nchini. Vitendo vya rushwa na ufisadi vinawanyima haki wananchi na kuitia hasara serikali kwa mamilioni ya fedha ambazo zingeweza kutumika kwa ajili ya kujenga miradi ya maendeleo kwa ajili ya watu wetu.”
Magufuli alisema “Mimi nimewaahidi wananchi, na nataka nirejee ahadi yangu kwao mbele ya Bunge lako tukufu, kwamba nitapambana na rushwa na ufisadi bila kigugumizi na bila haya yoyote. Dawa ya jipu ni kulitumbua, na mimi nimejipa kazi ya kuwa mtumbua jipu. Najua kutumbua jipu kuna maumivu lakini bahati mbaya halina dawa nyingine.
Hivyo ninaomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote mniombee na muniunge mkono wakati natumbua majipu haya.” Alieleza kuwa anafahamu ugumu wa vita aliyoamua kuipigana na anafahamu ugumu na changamoto zake kwa sababu wanaojihusisha na rushwa, sio watu wadogo wadogo.
Alisema Vitendo vya rushwa na ufisadi vyenye madhara makubwa kwa nchi na ustawi wa nchi yetu, hutendwa na watu wenye dhamana kubwa za uongozi na utumishi, ambazo wamezipata kutokana na ridhaa ya watu.
“Katika kushughulikia tatizo hili, nimeahidi kuunda Mahakama ya Rushwa na Ufisadi. Ni matumaini yangu vyombo husika katika jambo hili havitanikwamisha,” alisema Magufuli.

Hoja ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa yaondolewa bungeni

WAZIRI wa Fedha, Dk Philip Mpango ameondoa hoja ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa kwa kipindi cha miaka mitano 2016/17 mpaka 2020/21 aliyoiwasilisha bungeni jana.
Hatua hiyo ilitokana na mwongozo uliotolewa kwa nyakati tofauti na wabunge; Mbunge wa Kigoma Mjini, Kabwe Zitto (ACT Wazalendo) na wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema).
Wabunge hao walisema Waziri amewasilisha hoja kinyume na kanuni za kudumu za Bunge, zinazosema katika mkutano wa bunge wa kila Oktoba na Novemba, Serikali inatakiwa kuwasilisha mpango wa maendeleo wa taifa wa kila mwaka.
“Kutokana na maelezo uliotoa (Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge) na kwa kutumia kanuni ya hamsini na nane, tano ya kanuni za kudumu za Bunge toleo la 2016, naomba ruhusu kuondoa hoja niliyoiwasilisha leo (jana) asubuhi ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa kwa kipindi cha miaka mitano 2016/17 mpaka 2020/21,” alisema Dk Mpango.
Hoja hiyo iliondolewa baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Chenge kutoa mwongozo na kisha kuahirisha Bunge hadi kesho kutwa. Awali katika maelezo yao bungeni na nje ya Bunge, wakati wakizungumza na waandishi wa habari, Zitto na Lissu walisema uwasilishwaji wa hoja ya Waziri Mpango, umekiuka Katiba. Hata hivyo akitoa mwongozo, Chenge alisema suala hilo halikukiuka katiba.
“Nimelitafakari sana jambo hili, na baada ya kutafakari hakuna ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.” Alisema kilicholetwa na serikali ni mchakato wa kushirikisha wawakilishi wa Tanzania ili watoe maoni, ushauri na mapendekezo yao kuhusu na mpango unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali katika mwaka wa fedha 2020/16/17.
Alisema kitu ambacho wabunge lazima wakubali, ni kwamba kulingana na Kanuni ya 94 (1), Bunge linapofanya kazi hiyo huwa haliketi kama Bunge, bali linaketi kama kamati ya mipango. “Hiyo ni dosari ambayo tumeiona,” alisema na kukiri kwamba hapa ilikuwa ni mpango wa muda mfupi.
Hata hivyo alisema Ibara ya 63 haisemi ni lini huo mpango uletwe. Alikiri kuwa mpango mfupi unatokana na wa mwaka mitano, ambao hitimisho lake ni pale waziri atakaposoma mpango wa serikali kwa mwaka unaofuata wa fedha na jioni yake, Waziri anaposoma bajeti ya serikali.
Akihimiza kuwa Kanuni ya 94 (1) lazima izingatiwe, Chenge alisema, “Bunge halikuweza kukutana Oktoba na Novemba kama kanuni hiyo inavyotaka kwa sababu kulikuwa na shughuli kubwa ya uchaguzi.
Alisema Serikali na Bunge hawakuwa na njia nyingine, jambo ambalo ilikuwa lazima mchakato ufanyike sasa ili Machi 11, serikali iwasilishe mbele ya wabunge kama ilivyofanyika mwaka jana katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam.
“Waziri mwenye dhamana anawasilisha mipango na ukomo wa bajeti. Wakishawasilisha, katibu wa bunge ndiye anapeleka kwa spika ili aelekeze ipelekwe kwenye kamati ya bajeti hadi watakapokuja kutoa taarifa,” alisema.
Kwa mujibu wa kanuni, siku ya kusoma bajeti ya serikali, waziri anawasilisha hoja yake ya mpango; utekelezaji wa hali ya mwaka jana na mwaka unaofuata. Hivyo kunakuwa na hoja mbili ambazo hujadiliwa kwa pamoja; hoja ya mpango na ya bajeti ya serikali.
“Haya ndiyo yanapaswa yafanyike,” alisema na kusihi wabunge kuelewa kanuni. Baada ya maelezo hayo, Chenge alimuita Waziri mtoa hoja; Waziri wa Fedha, aombe idhini ya Bunge ya kuondoa hoja. Kabla ya kutoa hoja hiyo, wabunge walihojiwa, na wote waliridhia.

Magufuli awateua Chagonja, Mtweve makatibu tawala

RAIS John Magufuli amefanya uteuzi wa makatibu tawala wawili wa mikoa ya Mwanza na Katavi, ili kujaza nafasi za makatibu tawala wa mikoa hiyo. Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema Dar es Salaam jana kuwa Rais amemteua Kamishna wa Polisi, Clodwing Mtweve kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, ambako anakwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Faisal Issa ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Kabla ya uteuzi huo, Kamishna Mtweve alikuwa Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Polisi Tanzania. Balozi Sefue alisema Rais Magufuli pia amemteua Kamishna wa Polisi, Paul Chagonja kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, ambako anakwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Madeni Kipande, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Kabla ya uteuzi huo, Kamishna Chagonja alikuwa Kamishna wa Mafunzo na Operesheni wa Jeshi la Polisi Tanzania. Aidha, Balozi Ombeni Sefue alisema Rais Magufuli ameamua kuwateua Makamishna hao wa Polisi, kama alivyowateua Majenerali wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania kuwa Makatibu Wakuu wa Wizara, kwa lengo la kujenga nidhamu katika utumishi wa umma.
Makamishna Clodwing Mtweve na Paul Chagonja pamoja na Mahadhi Juma Maalim ambaye ameteuliwa kuwa Balozi mpya wa Kuwait, wataapishwa jijini Dar es Salaam leo saa nne asubuhi.