ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumapili, 13 Machi 2016

Dk. Vicent Mashinji ndiye Katibu Mkuu Chadema

Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema
Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema
DAKTARI Vicent Mashinji ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema, katika kikao chake kilichokaa jijini Mwanza, anaandika Mwandishi Wetu.
Katika Kikao hicho cha Baraza Kuu, Freeman Mbowe alitangaza jina la Dk. Mashinji na kuungwa mkono na wajumbe wa baraza hilo, hivyo anajaza nafasi iliyoachwa na Dk. Willibrod Slaa, aliyejienguwa ukatibu mkuu wa chama hicho.
Jina la Dk. Machinji halikuwa miongoni mwa wanachama wa Chadema ambao walikuwa wanatarajiwa kumrithi Dk. Slaa kwani waliokuwa wanatabiriwa kukatia kiti hicho ni Salum Ally Mwalimu, Frederick Sumaye, Benson Kigaila, John Mnyika, Dk. Marcus Albanie na Prof. Mwesiga Baregu.
Nafasi ya Katibu wa Chadema ilikuwa wazi tangu Dk. Slaa alipoondoka Chadema muda mfupi baada ya chama hicho kumpitisha Edward Lowassa aliyetokea CCM kuwa mgombea urais wa chama hicho na kuungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Wasifu wa Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Vincent B. Mashinji
Professional experience
Clinical Advisor & TB/HIV lead
UMSOM-IHV
July 2008 – Present
ART Program Doctor/IMA team lead
IMA Worldhealth
August 2006 – June 2008 (1 year 10 months)
Medical Officer/Anaesthesiology
Regency Medical Centre
October 2005 – August 2006 (10 months)
Medical Officer
Muhimbili National Hospital
August 2003 – October 2005 (2 years 2 months)
Research Assistant
Freelance
November 2002 – August 2003 (9 months)
Intern Docor
Muhimbili National Hospital
September 2001 – October 2002 (1 year 1 month)
Education history
Open University of Tanzania
PhD
August 2010 – Present
AMREF/UCLA Anderson School
MDI Certificate
April 2010 – April 2010
Blekinge Institute of Technology
MBA
September 2007 – March 2010 (2 years 6 months)
UMSOM-IHV
IPEP Certificate
May 2008 – May 2008
Evin School of Management
Certificate in CSR
October 2005 – October 2005
Muhimbili University College of Health Sciences
MMed/Anaesthesiology
September 2003 – April 2005 (1 year 7 months)
Muhimbili University College of Health Sciences
Certificate in Research Methodology
September 2004 – September 2004
Makerere University
MBChB
October 1995 – July 2001 (5 years 9 months)
Mzumbe High School
ACSEE
July 1992 – June 1994 (1 year 11 months)
St. Pius X Seminary, Makoko
GCSEE
January 1988 – October 1991 (3 years 9 months)
Iligamba Primary School
Leaving Certificate/Primary School
January 1981 – October 1987 (6 years 9 months

Breaking News: Rais Magufuli Afanya Uteuzi wa Wakuu wa Mikoa 26....Kati Yao 13 ni Wapya, 7 Wamebakizwa na 5 Wamehamishwa

Kikoti blog

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.
 
Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
  1. Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
  2. Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu wa Mkoa wa Geita.
  3. Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
  4. Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
  5. Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
  6. Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
  7. Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
  8. Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
  9. Mh. Anna Malecela Kilango - Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
  10. Mhandisi Methew Mtigumwe - Mkuu wa Mkoa wa Singida.
  11. Mh. Antony Mataka - Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
  12. Mh. Aggrey Mwanri - Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
  13. Mh. Martine Shigela - Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
  14. Mh. Jordan Mungire Rugimbana - Mkuu wa Mkoa Dodoma.
  15. Mh. Said Meck Sadick - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
  16. Mh. Magesa Mulongo - Mkuu wa Mkoa Mara.
  17. Mh. Amos Gabriel Makalla - Mkuu wa Mkoa Mbeya.
  18. Mh. John Vianey Mongella - Mkuu wa Mkoa Mwanza.
  19. Mh. Daudi Felix Ntibenda - Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
  20. Mh. Amina Juma Masenza - Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
  21. Mh. Joel Nkaya Bendera - Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
  22. Mh. Halima Omary Dendegu - Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
  23. Dkt. Rehema Nchimbi - Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
  24. Mhandisi Evarist Ndikilo - Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
  25. Mh. Said Thabit Mwambungu - Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
  26. Luteni Mstaafu Chiku Galawa - Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).
Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
13 Machi, 2016

Jumamosi, 12 Machi 2016

Vita ya ukatibu mkuu Chadema

freeman-mbowe-chadema
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, yupo katika wakati mgumu kutokana na wajumbe wa Baraza Kuu na wabunge wenye ushawishi kumtaka amteue Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho.
Hii inakuwa mara ya kwanza kutokea katika historia ya kuasisiwa kwa chama hicho kikuu cha upinzani kwa wajumbe wa Baraza Kuu kumshawishi Mwenyekiti kumteua mtu anayefaa kushika wadhifa huo.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu, linalotarajiwa kuketi leo wanaotajwa kujipanga kumshawishi Mwenyekiti kumteua Sumaye kuwa Katibu Mkuu ni Profesa Mwesiga Baregu, Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu na Mbunge wa Iringa, Mchungaji Peter Msigwa.
Wengine ni pamoja na Makamu Mwenyekiti Bara, Profesa Abdallah Safari, Makamu Mwenyekiti Zanzibar, Said Issa, Anthony Komu na  Benson Kigaila na Katibu Mkuu Baraza la Wanawake (Bawacha), Grace Tendega.
Katika orodha hiyo pia wamo wabunge wenye ushawishi mkubwa ambao ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara.
Katika orodha hiyo yumo Mbunge wa zamani wa Ilemela, Ezekia Wenje na baadhi ya waliokuwa wagombea ubunge wenye ushawishi mkubwa ndani ya chama.
Hadi jana Profesa Safari hakuwa amehudhuria vikao vya Mwanza kutokana na kile kilichoelezwa kukabiliwa na matatizo mbalimbali.
Juzi Lissu aliweka wazi sifa za kiongozi aliyekuwa akimtaka, jambo ambalo lilitafsiriwa na wachambuzi wa mambo kwamba alikuwa akimuelezea Sumaye.
Naye mmoja wa wajumbe ambaye hakupenda jina lake litajwe anayemuunga mkono Sumaye ashike nafasi ya Katibu Mkuu, alisema ukiondoa sifa alizotaja Lissu za kumtaka Katibu Mkuu anayeweza kuzungumza na Watanzania, vyama vya Ukawa, ndani na nje ya nchi wakamsikiliza, nyingine ni mtu aliyeingia Chadema kwa kutofuata cheo.
“Hakuna mwingine zaidi ya Sumaye, ambaye alijiunga na chama hiki wakati ambao nafasi nyingi zilikuwa zimeshanyakuliwa na wanachama wengine,” alisema mjumbe huyo.
Sababu kubwa ya wajumbe kumtaka Sumaye inaelezwa kutokana na kubaini kuwepo kwa mpango wa Mwenyekiti, Mbowe kumtaka Salum Mwalimu, anayekaimu nafasi hiyo.

Majipu tisa yaliyoiva Dawasco yatumbuka

WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji, Gerson Lwenge amewasimamisha kazi kupisha uchunguzi vigogo tisa wa Kampuni ya Maji Safi na Taka (Dawasco) na kutaka aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Jackson Midala kusakwa na kuchunguzwa na ikibainika alihusika kwenye ubadhirifu wa maji, afikishwe mahakamani.
Kadhalika,Waziri Lwenge ameitaka Bodi ya Dawasco, kuchunguza tuhuma za wizi wa maji zinazofanywa na baadhi ya watendaji wa kampuni hiyo kwa kuwaunganishia maji bure kampuni na viwanda kadhaa jijini Dar es Salaam na kulipwa ujira kila mwisho wa mwezi na viwanda hivyo.
Waziri Lwenge alitoa maagizo hayo jana jijini Dar es Salaam wakati alipotembelea Dawasco kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe, kuona utendaji wao na kuzungumza na watumishi hao.
Pia ameitaka bodi hiyo kuchunguza Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) na kampuni nyingine pamoja na viwanda jijini Dar es Salaam kama wana akaunti za maji ya Dawasco na kwamba madai ya kuwa wao wana visima vyao vya maji, lazima ukweli upatikane.
Alisema kama kampuni inasema ina visima vyake binafsi vya maji, ni lazima wawe na kibali walichopata kutoka Wizara ya Maji, kinachowaruhusu wao kuchimba na kinaonesha kiwango cha maji, na kwamba kuna madai mengi ya kampuni na viwanda kuwa na visima vyao, ila wizara haifahamu.
“Kama unadai una kisima cha maji cha kwako kibali kinatolewa na wizara yangu, sasa yapo madai mengi viwanda vinasema vinatumia maji yao, ila zipo taarifa kwamba wanajificha kwenye hilo na ukweli ni kwamba wanaiba maji ya Dawasco, sasa lazima mchunguze hayo,” alisema Lwenge.
Waliosimamishwa kazi ni Meneja Rasilimali Watu, Mvano Mandawa, Meneja Ufuatiliaji na Tathmini, Reinary Kapera, Teresia Mlengu, Emmanuel Guluba, Peter Chacha, Fred Mapunda, Reginald Kessy, Jumanne Ngelela na Bernard Nkenda.
“Sehemu kubwa ya upotevu wa maji ni wizi unaofanywa na wezi ambao ni baadhi ya viwanda na kampuni kubwa kwa kushirikiana na watendaji wa Dawasco, tuna taarifa na kila mwisho wa mwezi wako kwenye ‘payroll’ wanaenda kuchukua malipo, hawa ni majipu lazima yatumbuliwe,” alisema Waziri Lwenge.
Mara baada ya kusomewa taarifa fupi ya utendaji kazi wa Kampuni hiyo kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco, Cyprian Luhemeja, Waziri Lwenge alitoa maagizo hayo na kusema pamoja na Kampuni kuwa na malengo mazuri, lakini ni lazima ifanyiwe mabadiliko ili kupata watendaji waadilifu.
Alisema upotevu wa maji hivi sasa ni asilimia 47 na kwamba maji hayo yanapotea katika mazingira tatanishi na kuikosesha kampuni hiyo mapato. Strabag Alitoa mfano mzuri wa Kampuni ya Ujenzi wa Barabara ya Strabag, ambayo ilipewa zabuni ya kujenga barabara za mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), kwamba tangu kampuni hiyo ianze kufanya kazi hadi sasa, haijalipa Dawasco bili ya maji iliyotumia.
“Strabag walifanya wizi wa maji, wamejenga barabara lakini hakuna malipo yoyote waliyofanyika Dawasco, wanadaiwa zaidi ya Sh bilioni 2.9 pamoja na faini na natoa siku 14, wawe wamelipa vinginevyo wakamatwe wafikishwe mahakamani.
Waziri Lwenge alisema Serikali haiwezi kufanya kazi na wabadhirifu ambao wako ndani ya taasisi, kampuni au mashirika yake na kusisitiza kuwa ni lazima watendaji wasio waaminifu waondolewe ili kuleta ufanisi nchini.
“Tunafanya mageuzi ili tufanye kazi kwa ufanisi na lazima tuwe na watendaji waadilifu na wenye maadili, si wanaoangalia maslahi binafsi,” alisema Lwenge. Waziri Lwenge alitoa wiki mbili kwa bodi hiyo kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo na zile za wateja wakubwa wa Dawasco kutokuwa na akaunti za maji, ili kuthibitisha ukweli wa madai hayo.
Maagizo mengine ni kuitaka Dawasco ifikapo Juni, mwaka huu kuhakikisha wamefanikiwa kupunguza upotevu wa maji kwa asilimia 30 na ifikapo 2020 upotevu huo uwe chini ya asilimia 20.
Awali Ofisa Mtendaji wa Dawasco, Luhemeja alisema changamoto kubwa ya Dawasco ni upotevu wa maji na kubainisha katika maeneo 10 wanayohudumia maji Dar es Salaam na Pwani, Magomeni ni eneo korofi kwa wizi wa maji.
Alisema eneo hilo hivi sasa limebainishwa na wameweka mtandao ambao kuanzia mwisho wa mwezi huu, utabaini wezi wote lakini pia hatua nyingine walizochukua ni kuweka vituo vya kuuza maji kwenye eneo korofi, vinavyosimamiwa na jamii ya eneo husika.
Alisema kwa miezi kadhaa sasa, tangu kuanza kwa huduma hiyo wameweka vituo 47 vya kuuza ambavyo vimefungiwa mita na wauzaji hutakiwa kulipa Dawasco bili ya maji baada ya kuwauzia wateja wadogo wadogo.
Ofisa Mtendaji huyo mpya wa Dawasco, alisema kwa kipindi cha muda mfupi tangu aingie kwenye kampuni hiyo, wamefanikiwa kuongeza mapato ya maji kutoka Sh bilioni 2.9 mwaka jana hadi kufika Sh bilioni 7.1 Januari mwaka huu.
Aliongeza kwamba lengo lao ifikapo Juni mwaka huu, ni kukusanya Sh bilioni 12 kwa mwezi na hiyo ni kutokana na kuweka mifumo imara na dhabiti ya kufuatilia mita za maji na masharti waliyopewa mameneja wa maeneo husika ya kampuni hiyo.
Dawasco hivi sasa ina wateja waliounganishiwa mita zaidi ya 151,000 na lengo lao ni kuongeza idadi ya wateja baada ya kuongeza uzalishaji na usambazaji wa maji hasa baada ya kuimarika kwa mitambo miwili ya maji ya Ruvu Chini na Juu.

Alhamisi, 10 Machi 2016

Simba leo tena

TIMU ya soka ya Simba na Mbeya City leo zinashuka dimbani kwenye viwanja viwili tofauti kusaka pointi tatu muhimu katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu bara. Simba itakuwa mwenyeji wa Ndanda FC kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam wakati Mbeya City itakuwa mwenyeji wa Stand United kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya.
Wekundu hao wa Msimbazi huenda wakapanda kileleni tena iwapo watafanikiwa kuwafunga Ndanda Fc katika mchezo huo kwa kuwa watafikisha pointi 51 na kuishusha Yanga yenye pointi 50.
Mwishoni mwa wiki iliyopita Simba ilikaa kileleni kwa siku mbili kabla ya Yanga juzi kupanda na kumpiku kufuatia ushindi wake wa mabao 5-0 dhidi ya African Sports ya Tanga. Simba, Yanga na Azam FC zinatofautiana kwa pointi chache kiasi kwamba mmoja akishinda, mwingine anashuka.
Simba ina uwezekano wa kushinda mchezo wa Ndanda, kwani katika mchezo wake wa raundi ya kwanza ilishinda bao 1-0 ugenini mjini Mtwara. Hali itakuwa mbaya kwa Ndanda kama itakubali kichapo kwa mara nyingine kwani licha ya kuwa katika nafasi ya nane, ina pointi 24 ambazo hazitoshi kuihakikishia kubaki salama kwenye msimamo wa ligi kwa kuwa timu zilizoko chini yake zinaweza kupanda kutokana na kutofautiana pointi chache.
Kwa upande wa Mbeya City, huenda ikafanya vizuri leo baada ya kuonesha kiwango bora chenye mabadiliko katika mchezo dhidi ya Simba wiki iliyopita. Licha ya kufungwa mchezo huo, walicheza vizuri isipokuwa inayumbushwa na ubutu wa safu yake ya ushambuliaji.
Pengine kwa vile inacheza kwenye uwanja wake wa nyumbani wanaweza kutumia faida hiyo katika kufanya vizuri na kufuta machungu ya kufungwa na timu hiyo ya Shinyanga bao 1-0 katika mchezo wa raundi ya kwanza.

APR, Yanga watambiana

HOMA ya pambano la raundi ya kwanza la Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga na APR ya Rwanda, imezidi kupanda, kiasi cha kila moja kutamba kumshikisha adabu mpinzani wake.
Tayari makocha wa klabu hizo, Hans van der Pluijm wa Yanga na Nizar Khanfir wa APR aliyeweka rekodi ya kuwa mwarabu wa kwanza kufundisha soka Rwanda baada ya kuanza kazi rasmi jana, ameelezea utayari wake kushinda mechi ya Jumamosi wiki hii huko Kigali, Rwanda.
Khanfir amekaririwa jana kuwa, ameshawaona Yanga kupitia video mbalimbali na kwamba anataka kuwafunga Jumamosi. “Lengo letu ni kushinda huo mchezo,”amesema na kuongeza; “Nimeona baadhi ya video zao na tutaendelea kuwachambua katika siku chache zijazo kuelekea kwenye mechi”.
Kwa ujumla, Khanfir amesema malengo yake makuu katika miezi sita ya mwanzo ni kuiwezesha timu kutetea ubingwa wa Rwanda na pia kuifikisha mbali katika Ligi ya Mabingwa Afrika. Mtaalamu huyo wa Tunisia aliongoza mazoezi yake ya kwanza APR jana Uwanja wa Kicukiro akisaidiwa na kocha aliyemkuta kazini, Emmanuel Rubona.
“APR ni timu kubwa Rwanda na ina heshima kubwa Afrika na pia ina wachezaji wengi katika timu ya taifa, ambacho ndicho kilichonivutia mimi kukubali kazi hii,” amesema Khanfir. “Wachezaji ni vijana wadogo na timu ina uwiano mzuri ambao unafaa vizuri katika falsafa yangu. Tunaitaka kuipeleka timu katika kiwango kingine.
Ni wajuzi na tunataka kuongeza ufundi zaidi, lakini zaidi ya hapo nimevutiwa na timu kwa ujumla,” amesema. Wakati Khanfir akisema hayo, Pluijm kwa upande wake amesema anatambua wanakwenda Kigali kwenye mchezo mgumu wa ugenini dhidi ya APR, lakini watapambana wasipoteze.
“APR ni timu nzuri na watakuwa wamejiandaa vizuri, lakini sisi tuko vizuri, tutakwenda kupambana tusipoteze mchezo, ili tumalizie vizuri mchezo wa nyumbani,”amesema. Yanga SC inatarajiwa kuondoka leo nchini kwenda Kigali kwa ajili ya mchezo huo, unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua.
Mechi hiyo inatarajiwa kuchezeshwa na marefa wa Malawi Jumamosi Uwanja wa Amahoro, Kigali Rwanda. Duncan Lengani anatarajiwa kupuliza filimbi, wakati washika vibendera watakuwa Clemence Kanduku na Jonizio Luwizi.
Mchezo wa marudiano wiki moja baadaye Dar es Salaam, utachezeshwa na marefa wa Shelisheli; katikati Bernard Camille na pemebeni watakuwapo Eldrick Adelaide na Gerard Pool.
Mchezo wa kwanza utafanyika mjini Kigali, Rwanda Machi 12 kabla ya timu hizo kurudiana Dar es Salaam Machi 19 na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa mchezo mwingine wa raundi ya kwanza, kati ya Al Ahly ya Misri na Recreativo de Libolo ya Angola mwezi ujao.

St Joseph watakiwa kurudi darasani

WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ameingilia kati mgogoro wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. Joseph Dar es Salaam, waliogomea kufanya mitihani na kuwataka warejee madarasani wakati matatizo yao yakishughulikiwa.
Wanafunzi hao walikuwa katika siku ya tatu ya mgomo wao jana ambapo pamoja na mambo mengine walikuwa wakilalamikia mapungufu yaliyopo chuoni hapo, ikiwa ni pamoja na maabara za kufanyia mafunzo kwa vitendo, matatizo ya kiutawala, mitaala ya kufundishia pamoja na ada.
Profesa Ndalichako aliwasili chuoni hapo jana asubuhi na kukagua mazingira ya kufundishia ya chuo hicho kwa kutembelea maabara zote chuoni hapo na kisha kwenda kuzungumza na utawala, Serikali ya wanafunzi na mwisho alihutubia wanafunzi wote.
Ndalichako baada ya kuzungumza na pande zote mbili aliagiza wanafunzi hao warejee madarasani kuendelea na mitihani yao na kuutaka uongozi wa chuo uyafanyie marekebisho mapungufu ya kiutawala yaliyojitokeza.
Aidha ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), chini ya Katibu Mtendaji wake, Profesa Yunus Mgaya kufuatilia na kuchunguza kwa makini madai ya wanafunzi hao juu ya kuwepo kwa wahadhiri wasio na sifa zinazotakiwa.