ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 21 Machi 2016

walimu wapya kwa mwaka 2016 wapewa mtihani na TAMISEMI

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEic6vbqzF0JJL9QfkTbpK_Xwtwpaf65r_pwIRgw2HphXih_46gKNnnFwdW-GQ79r8JjAPMg9jxEAQwEO9wWuJ91v8ipEE0qGVv9-I1qB2-7UKtKu3JHpAGUl0BJbXMhyqZuhNmNddjVr4Hf/s1600/1350.jpg
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, George Simbachawene ametangaza leo March 21, 2016 kuwashughulikia wale wote wanaofanya hujuma katika sekta ya elimu nchini, wakiwemo Walimu wanaokimbia sehemu zao za kazi hususani vijijini na kukimbilia mijini.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari leo March 21, 2016 alisema…‘Katika eneo la upangaji wa Walimu ni tatizo kubwa na nadiliki kusema hadharani kwamba upangaji wa walimu kwenye  shule zetu ni wa ovyo leo hii tunaupungufu wa ualimu kwenye vijiji kwa  asilimia zaidi ya 40%  na ongezeko  la walimu mijini ni kama asilimia 50%  kwa   maana ya kwamba walimu wengi wapo Dar es Salaam, walimu wengi wapo kwenye miji mikubwa makao makuu ya mikoa na makao makuu ya wilaya’George Simbachawene
‘Hata wanawake wanasema wanafuata wanaume zao huko ni  kukosa uzalendo kama ulikubali kuajiliwa lazima ukubali kufanya kazi mahala popote pale na watanzania ni wote mpaka waliopo kule vijijini haiwezekani kukubali kazi mjini na kukataa kijijini’George Simbachawene
kwa tafsiri hii ya waziri wa TAMISEM hakutokuwa na sababu zzisizona msingi zitakazokubalika kwa walimu wapya kwa mwaka 2016

Jumapili, 20 Machi 2016

TATIZO LA MAJI KATIKA MJI MDOGO WA ILULA KUISHA KABLA 2020

 MBUNGE  wa   jimbo la  Kilolo  Venance  Mwamoto ameahidi kuongozana na  wazee  wa mji  wa Ilula kwenda Dodoma kuonana na   waziri  mkuu Kassim Majaliwa  ili  kumfikishia ahadi ya  maji ya Rais Dr John Magufuli kwa  wananchi  wa mji  mdogo  wa Ilula .
  https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEganogblP_gVCgRkG9WDNjiGmgaKAifYWmTa2QBjcrUK3DmNOKvT2dQlSyKamiQbpJZcmDhxihrAM2_xHTsKYSRWFBdFoq4h51s2_Pi4txRVupOtV59XeiXS6613jzzTHtGGiQD7z7auNM-/s640/DSC_0972.JPG


Huku  akiwataka wananchi wa Ilula na Nyalumbu  kutomchagua mwaka 2020  iwapo atashindwa  kutekeleza ahadi ya maji katika mji  huo wa Ilula ndani ya  miaka  yake  mitano ya  ubunge.

Akizungumza  na  wananchi  wa kata ya  Nyalumbu na Ilula  wakati wa  mikutano yake ya  hadhara ya  kuwashukuru  wananchi  wake kwa kumchagua  kuwa mbunge wa  jimbo  hilo la Kilolo jana ,Mwamoto  alisema  kuwa  kero ya maji katika  mji wa Ilula  imekuwa ya muda murefu   jambo ambalo hatataka   kuona   wananchi  hao  wakiendelea kutabika.

Alisema  kuwa   kero hiyo  ya maji imeanza  kuwasumbua  wananchi hao toka nchi ipate  uhuru  wake mwaka 1961  hadi  leo wapo katika mahangaiko ya maji na  baadhi ya  viongozi  wameendelea  kufanya udanganyifu  wa mradi huo kama  ambavyo   mwaka 2010   viongozi  walivyomdanganya aliyekuwa makamu  wa Rais Dr Alli Mohamed  Shein  kwa  kupelekwa  kufungua  mradi wa maji ambao  viongozi  walimdanganya kwa  kujaza maji katika tanki hilo  ili azindue mradi huo.

Hivyo  alisema udanganyifu  huo hautapewa nafasi katika uongozi  wake wa miaka  mitano  lazima kero  hiyo imalizike na  wananchi hao  waweze kupata maji vinginevyo yupo tayari  kuongoza  wananchi  wake kumzuia waziri wa maji kupita Ilula kwenda jimboni kwake Njombe  iwapo  wananchi hao hawatatimiziwa ahadi yao ya maji  safi na salama .

Mbunge  huyo  alisema katika  kikao kijacho cha  bunge kinachoanza mwezi ujao ataomba  wananchi wa Ilula na Nyalumbu  kumteulia wazee watatu ama  wanne   ili kwenda nao bungeni Dodoma  kukutana na  waziri  mkuu ili  kwa ajili ya kumkumbusha ahadi ya Rais ya  maji katika mji  huo wa Ilula .
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhk7WxKewRYdjXwD8lX3crGfa8nBIOAo3SsF0Kg3ruaxfxMEciqaadCRdkopWqNhM03AgYUs8RsDLs9MZqzgf0JjCn8Pxy6UW5N8Q5pK1yZIREUxEtkSekyqD51VvReeSLegJODpoNpmcxU/s640/DSC_0966.JPG

Pia  aliagiza mamlaka ya maji ya mji  mdogo wa Ilula  kuchunguza vema mradi wa maji uliopo kama umejengwa kwa kiwango ama chini ya kiwango maana amesema mradi mdogo  uliopo kwa  sasa  bado umekuwa na kero  kubwa ikiwa ni pamoja na baadhi ya maeneo kuvujisha maji  huku  akiwataka  wananchi kwa  upande  wao kutunza miundombinu ya maji.

Mbunge wa Kilolo Bw  Venance Mwamoto (kushoto)  akisalimiana na mmoja kati ya  wazee wa mji wa Ilula  aliyetoka  kuchota maji


 

Katika  hatua nyingine  mbunge Mwamoto  alimshauri meneja wa maji wa IRUWASA katika mji wa Ilula Teodolah Mvungi  kuangalia uwezekano wa  kuboresha kituo  cha maji eneo la Ilula  ili  kiweze  kunufaisha  wananchi  wengi  na  kuwa iwapo wataanza uboreshaji kwa upande wake ataunga mkono .

Dr Shein aongoza wazanzibar katika kupiga kura, Uchaguzi wa Marudio Zanzibar

Wananchi wa Zanzibar leo wanapiga kura katika uchanguzi wa marudio baada ya kufutwa kwa uchanguzi uliofanyika October 25,2025 kutokana na kasoro zilizojitokeza.

Katika baadhi ya vituo wananchi wamejitokeza na zoezi linaendelea vizuri huku hali ya usalama ikiwa imeimarishwa.

Katika kituo cha shule ya sekondari Muembeladu ambayo ina vituo sita,vituo vitano vinawatu 350 na kituo kimoja kina watu 91. Akizungumza na wanahabari, msimamizi wa kituo hicho amesema zoezi la upigaji kura linaendelea vizuri katika jimbo la Jangombe .

Kwa upande wa kituo cha skuli ya Muembeshauri nako hali ni shwari na zoezi linaendelea vizuri ambapo katika skul hiyo vituo 11 vinatumika watu kupiga kura.
Katika Jimbo la kikwajuni, zoezi  linaendelea vizuri huku mwitikio wa watu ukiwa ni mkubwa.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kupiga kura wamesema zoezi hilo limekua rahisi na la  amani tofauti na taarifa zilivyokua zinasambazwa.

Mkazi wa Muembeshauri aliyejitambulisha kwa jina la Hamidu Salum Haji ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kwani zoezi la kupiga kura linaendelea kwa amani na utulivu.

Ndugu zangu tusikubali kugombanishwa na watu ambao hawaitakii mema Zanzibar tusimame pamoja katika kutetea nchi yetu” amesema Haji
 
Wakati zoezi hilo linaendelea maduka mengi yamefunguliwa na wafanyabiashara wanaendelea na kazi kama kawaida
Rais wa Zanzibara na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Ali Mohammed Shein leo amepiga kura katika kituo cha skuli ya bungi
5607497e-aa8a-46b6-9e65-24e5da213e24
9c703d6a-0f99-42ea-a17d-935d411e8f87
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, amepiga kura katika kituo cha skuli ya Kiembe samaki
36086a57-dbef-464f-8d12-ae3b207940ab


Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar Dkt Ali Mohammed alizungumza na wanahabari baada ya kupiga kura yake katika kituo cha Bungi, Kibera kisiwani Unguja  ambapo alisema anaamini atashinda kwa kishindo na kuhusu kushindwa  alisema tusubiri matokeo ya uchaguzi ndiyo yataamua.
"Nimepata nafasi ya kupiga kura kama haki yangu ya  kimsingi na kumekuwa na utulivu mkubwa kwenye zoezi hili,hali ya ulinzi imeimarishwa. 
"Matumaini yangu ni kushinda kwa kishindo, kuhusu kushindwa ndugu muandishi tusubiri matokeo ndiyo yataamua".Alisema Dkt. Ali Mohammed Shein

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd amepiga kura katika kituo cha skuli ya Kitope
46bee29d-6ade-49ea-9377-a3a692b33b12
670502cb-700e-47f1-b9e9-fa44bea0f2db

Jumapili, 13 Machi 2016

Dk. Vicent Mashinji ndiye Katibu Mkuu Chadema

Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema
Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema
DAKTARI Vicent Mashinji ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema, katika kikao chake kilichokaa jijini Mwanza, anaandika Mwandishi Wetu.
Katika Kikao hicho cha Baraza Kuu, Freeman Mbowe alitangaza jina la Dk. Mashinji na kuungwa mkono na wajumbe wa baraza hilo, hivyo anajaza nafasi iliyoachwa na Dk. Willibrod Slaa, aliyejienguwa ukatibu mkuu wa chama hicho.
Jina la Dk. Machinji halikuwa miongoni mwa wanachama wa Chadema ambao walikuwa wanatarajiwa kumrithi Dk. Slaa kwani waliokuwa wanatabiriwa kukatia kiti hicho ni Salum Ally Mwalimu, Frederick Sumaye, Benson Kigaila, John Mnyika, Dk. Marcus Albanie na Prof. Mwesiga Baregu.
Nafasi ya Katibu wa Chadema ilikuwa wazi tangu Dk. Slaa alipoondoka Chadema muda mfupi baada ya chama hicho kumpitisha Edward Lowassa aliyetokea CCM kuwa mgombea urais wa chama hicho na kuungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Wasifu wa Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Vincent B. Mashinji
Professional experience
Clinical Advisor & TB/HIV lead
UMSOM-IHV
July 2008 – Present
ART Program Doctor/IMA team lead
IMA Worldhealth
August 2006 – June 2008 (1 year 10 months)
Medical Officer/Anaesthesiology
Regency Medical Centre
October 2005 – August 2006 (10 months)
Medical Officer
Muhimbili National Hospital
August 2003 – October 2005 (2 years 2 months)
Research Assistant
Freelance
November 2002 – August 2003 (9 months)
Intern Docor
Muhimbili National Hospital
September 2001 – October 2002 (1 year 1 month)
Education history
Open University of Tanzania
PhD
August 2010 – Present
AMREF/UCLA Anderson School
MDI Certificate
April 2010 – April 2010
Blekinge Institute of Technology
MBA
September 2007 – March 2010 (2 years 6 months)
UMSOM-IHV
IPEP Certificate
May 2008 – May 2008
Evin School of Management
Certificate in CSR
October 2005 – October 2005
Muhimbili University College of Health Sciences
MMed/Anaesthesiology
September 2003 – April 2005 (1 year 7 months)
Muhimbili University College of Health Sciences
Certificate in Research Methodology
September 2004 – September 2004
Makerere University
MBChB
October 1995 – July 2001 (5 years 9 months)
Mzumbe High School
ACSEE
July 1992 – June 1994 (1 year 11 months)
St. Pius X Seminary, Makoko
GCSEE
January 1988 – October 1991 (3 years 9 months)
Iligamba Primary School
Leaving Certificate/Primary School
January 1981 – October 1987 (6 years 9 months

Breaking News: Rais Magufuli Afanya Uteuzi wa Wakuu wa Mikoa 26....Kati Yao 13 ni Wapya, 7 Wamebakizwa na 5 Wamehamishwa

Kikoti blog

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.
 
Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
  1. Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
  2. Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu wa Mkoa wa Geita.
  3. Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
  4. Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
  5. Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
  6. Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
  7. Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
  8. Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
  9. Mh. Anna Malecela Kilango - Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
  10. Mhandisi Methew Mtigumwe - Mkuu wa Mkoa wa Singida.
  11. Mh. Antony Mataka - Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
  12. Mh. Aggrey Mwanri - Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
  13. Mh. Martine Shigela - Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
  14. Mh. Jordan Mungire Rugimbana - Mkuu wa Mkoa Dodoma.
  15. Mh. Said Meck Sadick - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
  16. Mh. Magesa Mulongo - Mkuu wa Mkoa Mara.
  17. Mh. Amos Gabriel Makalla - Mkuu wa Mkoa Mbeya.
  18. Mh. John Vianey Mongella - Mkuu wa Mkoa Mwanza.
  19. Mh. Daudi Felix Ntibenda - Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
  20. Mh. Amina Juma Masenza - Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
  21. Mh. Joel Nkaya Bendera - Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
  22. Mh. Halima Omary Dendegu - Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
  23. Dkt. Rehema Nchimbi - Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
  24. Mhandisi Evarist Ndikilo - Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
  25. Mh. Said Thabit Mwambungu - Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
  26. Luteni Mstaafu Chiku Galawa - Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).
Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
13 Machi, 2016

Jumamosi, 12 Machi 2016

Vita ya ukatibu mkuu Chadema

freeman-mbowe-chadema
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, yupo katika wakati mgumu kutokana na wajumbe wa Baraza Kuu na wabunge wenye ushawishi kumtaka amteue Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho.
Hii inakuwa mara ya kwanza kutokea katika historia ya kuasisiwa kwa chama hicho kikuu cha upinzani kwa wajumbe wa Baraza Kuu kumshawishi Mwenyekiti kumteua mtu anayefaa kushika wadhifa huo.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu, linalotarajiwa kuketi leo wanaotajwa kujipanga kumshawishi Mwenyekiti kumteua Sumaye kuwa Katibu Mkuu ni Profesa Mwesiga Baregu, Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu na Mbunge wa Iringa, Mchungaji Peter Msigwa.
Wengine ni pamoja na Makamu Mwenyekiti Bara, Profesa Abdallah Safari, Makamu Mwenyekiti Zanzibar, Said Issa, Anthony Komu na  Benson Kigaila na Katibu Mkuu Baraza la Wanawake (Bawacha), Grace Tendega.
Katika orodha hiyo pia wamo wabunge wenye ushawishi mkubwa ambao ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara.
Katika orodha hiyo yumo Mbunge wa zamani wa Ilemela, Ezekia Wenje na baadhi ya waliokuwa wagombea ubunge wenye ushawishi mkubwa ndani ya chama.
Hadi jana Profesa Safari hakuwa amehudhuria vikao vya Mwanza kutokana na kile kilichoelezwa kukabiliwa na matatizo mbalimbali.
Juzi Lissu aliweka wazi sifa za kiongozi aliyekuwa akimtaka, jambo ambalo lilitafsiriwa na wachambuzi wa mambo kwamba alikuwa akimuelezea Sumaye.
Naye mmoja wa wajumbe ambaye hakupenda jina lake litajwe anayemuunga mkono Sumaye ashike nafasi ya Katibu Mkuu, alisema ukiondoa sifa alizotaja Lissu za kumtaka Katibu Mkuu anayeweza kuzungumza na Watanzania, vyama vya Ukawa, ndani na nje ya nchi wakamsikiliza, nyingine ni mtu aliyeingia Chadema kwa kutofuata cheo.
“Hakuna mwingine zaidi ya Sumaye, ambaye alijiunga na chama hiki wakati ambao nafasi nyingi zilikuwa zimeshanyakuliwa na wanachama wengine,” alisema mjumbe huyo.
Sababu kubwa ya wajumbe kumtaka Sumaye inaelezwa kutokana na kubaini kuwepo kwa mpango wa Mwenyekiti, Mbowe kumtaka Salum Mwalimu, anayekaimu nafasi hiyo.

Majipu tisa yaliyoiva Dawasco yatumbuka

WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji, Gerson Lwenge amewasimamisha kazi kupisha uchunguzi vigogo tisa wa Kampuni ya Maji Safi na Taka (Dawasco) na kutaka aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Jackson Midala kusakwa na kuchunguzwa na ikibainika alihusika kwenye ubadhirifu wa maji, afikishwe mahakamani.
Kadhalika,Waziri Lwenge ameitaka Bodi ya Dawasco, kuchunguza tuhuma za wizi wa maji zinazofanywa na baadhi ya watendaji wa kampuni hiyo kwa kuwaunganishia maji bure kampuni na viwanda kadhaa jijini Dar es Salaam na kulipwa ujira kila mwisho wa mwezi na viwanda hivyo.
Waziri Lwenge alitoa maagizo hayo jana jijini Dar es Salaam wakati alipotembelea Dawasco kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe, kuona utendaji wao na kuzungumza na watumishi hao.
Pia ameitaka bodi hiyo kuchunguza Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) na kampuni nyingine pamoja na viwanda jijini Dar es Salaam kama wana akaunti za maji ya Dawasco na kwamba madai ya kuwa wao wana visima vyao vya maji, lazima ukweli upatikane.
Alisema kama kampuni inasema ina visima vyake binafsi vya maji, ni lazima wawe na kibali walichopata kutoka Wizara ya Maji, kinachowaruhusu wao kuchimba na kinaonesha kiwango cha maji, na kwamba kuna madai mengi ya kampuni na viwanda kuwa na visima vyao, ila wizara haifahamu.
“Kama unadai una kisima cha maji cha kwako kibali kinatolewa na wizara yangu, sasa yapo madai mengi viwanda vinasema vinatumia maji yao, ila zipo taarifa kwamba wanajificha kwenye hilo na ukweli ni kwamba wanaiba maji ya Dawasco, sasa lazima mchunguze hayo,” alisema Lwenge.
Waliosimamishwa kazi ni Meneja Rasilimali Watu, Mvano Mandawa, Meneja Ufuatiliaji na Tathmini, Reinary Kapera, Teresia Mlengu, Emmanuel Guluba, Peter Chacha, Fred Mapunda, Reginald Kessy, Jumanne Ngelela na Bernard Nkenda.
“Sehemu kubwa ya upotevu wa maji ni wizi unaofanywa na wezi ambao ni baadhi ya viwanda na kampuni kubwa kwa kushirikiana na watendaji wa Dawasco, tuna taarifa na kila mwisho wa mwezi wako kwenye ‘payroll’ wanaenda kuchukua malipo, hawa ni majipu lazima yatumbuliwe,” alisema Waziri Lwenge.
Mara baada ya kusomewa taarifa fupi ya utendaji kazi wa Kampuni hiyo kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco, Cyprian Luhemeja, Waziri Lwenge alitoa maagizo hayo na kusema pamoja na Kampuni kuwa na malengo mazuri, lakini ni lazima ifanyiwe mabadiliko ili kupata watendaji waadilifu.
Alisema upotevu wa maji hivi sasa ni asilimia 47 na kwamba maji hayo yanapotea katika mazingira tatanishi na kuikosesha kampuni hiyo mapato. Strabag Alitoa mfano mzuri wa Kampuni ya Ujenzi wa Barabara ya Strabag, ambayo ilipewa zabuni ya kujenga barabara za mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), kwamba tangu kampuni hiyo ianze kufanya kazi hadi sasa, haijalipa Dawasco bili ya maji iliyotumia.
“Strabag walifanya wizi wa maji, wamejenga barabara lakini hakuna malipo yoyote waliyofanyika Dawasco, wanadaiwa zaidi ya Sh bilioni 2.9 pamoja na faini na natoa siku 14, wawe wamelipa vinginevyo wakamatwe wafikishwe mahakamani.
Waziri Lwenge alisema Serikali haiwezi kufanya kazi na wabadhirifu ambao wako ndani ya taasisi, kampuni au mashirika yake na kusisitiza kuwa ni lazima watendaji wasio waaminifu waondolewe ili kuleta ufanisi nchini.
“Tunafanya mageuzi ili tufanye kazi kwa ufanisi na lazima tuwe na watendaji waadilifu na wenye maadili, si wanaoangalia maslahi binafsi,” alisema Lwenge. Waziri Lwenge alitoa wiki mbili kwa bodi hiyo kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo na zile za wateja wakubwa wa Dawasco kutokuwa na akaunti za maji, ili kuthibitisha ukweli wa madai hayo.
Maagizo mengine ni kuitaka Dawasco ifikapo Juni, mwaka huu kuhakikisha wamefanikiwa kupunguza upotevu wa maji kwa asilimia 30 na ifikapo 2020 upotevu huo uwe chini ya asilimia 20.
Awali Ofisa Mtendaji wa Dawasco, Luhemeja alisema changamoto kubwa ya Dawasco ni upotevu wa maji na kubainisha katika maeneo 10 wanayohudumia maji Dar es Salaam na Pwani, Magomeni ni eneo korofi kwa wizi wa maji.
Alisema eneo hilo hivi sasa limebainishwa na wameweka mtandao ambao kuanzia mwisho wa mwezi huu, utabaini wezi wote lakini pia hatua nyingine walizochukua ni kuweka vituo vya kuuza maji kwenye eneo korofi, vinavyosimamiwa na jamii ya eneo husika.
Alisema kwa miezi kadhaa sasa, tangu kuanza kwa huduma hiyo wameweka vituo 47 vya kuuza ambavyo vimefungiwa mita na wauzaji hutakiwa kulipa Dawasco bili ya maji baada ya kuwauzia wateja wadogo wadogo.
Ofisa Mtendaji huyo mpya wa Dawasco, alisema kwa kipindi cha muda mfupi tangu aingie kwenye kampuni hiyo, wamefanikiwa kuongeza mapato ya maji kutoka Sh bilioni 2.9 mwaka jana hadi kufika Sh bilioni 7.1 Januari mwaka huu.
Aliongeza kwamba lengo lao ifikapo Juni mwaka huu, ni kukusanya Sh bilioni 12 kwa mwezi na hiyo ni kutokana na kuweka mifumo imara na dhabiti ya kufuatilia mita za maji na masharti waliyopewa mameneja wa maeneo husika ya kampuni hiyo.
Dawasco hivi sasa ina wateja waliounganishiwa mita zaidi ya 151,000 na lengo lao ni kuongeza idadi ya wateja baada ya kuongeza uzalishaji na usambazaji wa maji hasa baada ya kuimarika kwa mitambo miwili ya maji ya Ruvu Chini na Juu.