ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 18 Aprili 2016

Bajeti ya Magufuli kusomwa Juni 9

Imeandikwa na Mwandishi Wetu KWA mara ya kwanza Bajeti ya Serikali ya Rais John Magufuli inatarajiwa kuwasilishwa Juni 9, mwaka huu, kwenye Mkutano wa Tatu wa Bunge la 11, unaoanza mjini Dodoma kesho.
Bajeti hiyo itawasilishwa rasmi na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango saa 10 kamili jioni siku ya Alhamisi baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya Hali ya Uchumi wa Nchi asubuhi siku hiyo.
Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano cha Bunge jana, ilieleza kuwa baada ya kuwasilishwa kwa bajeti hiyo, ambayo mapendekezo yake ya awali kwa wabunge yalibainisha kuwa itakuwa ni ya Sh trilioni 29, wabunge wataijadili kwa muda wa siku tisa kuanzia Juni 13 hadi Juni 21, mwaka huu.
Pamoja na bajeti hiyo, pia Dk Mpango atawasilisha Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano 2015/16 hadi 2020/21.
“Baada ya kuwasilishwa kwa mpango huo, Bunge pia litapokea na kujadili utekelezaji wa bajeti kwa wizara zote kwa mwaka wa fedha 2015/16 na makadirio ya matumizi ya Serikali 2016/17, kazi itakayofanyika kuanzia Aprili 22 hadi Juni 2, mwaka huu,” ilieleza taarifa ya Bunge.
Hivi karibuni, Dk Mpango aliwasilisha mapendekezo ya ukomo wa bajeti hiyo ya mwaka 2016/17 mbele ya wabunge jijini Dar es Salaam, na kubainisha kuwa inatarajiwa kuwa ya Sh trilioni 29.539 sawa na ongezeko la asilimia 31.32 ya bajeti iliyopita ya mwaka 2015/2016.
Kwa mujibu wa mapendekezo ya bajeti hiyo, Serikali inalenga kutumia Sh trilioni 15.105 sawa na asilimia 82 ya mapato ya ndani, mapato ya kodi na yasiyo na kodi na mapato kutoka halmashauri Sh trilioni 2.693 na Sh bilioni 665.4 na washirika wa maendeleo wanatarajiwa kuchangia Sh trilioni 3.600 ambayo ni sawa na asilimia 12 ya bajeti yote.
Akichanganua mapendekezo hayo, alisema kwa upande wa matumizi katika mwaka ujao wa fedha, Serikali inapanga kutumia Sh trilioni 17.719 kwa matumizi ya kawaida na Sh trilioni 11.820 kwa matumizi ya maendeleo sawa na asilimia 40 ya bajeti yote.
Aidha, alitaja vipaumbele vingine kuwa ni viwanda vya kukuza uchumi na ujenzi wa msingi wa uchumi wa viwanda, kufungamanisha maendeleo ya uchumi na rasilimali watu na mazingira wezeshi kwa uendeshaji biashara.
Pamoja na kuwasilishwa kwa bajeti hiyo, pia katika Mkutano huo Tatu wa Bunge unaoanza kesho, pamoja na kuwasilishwa hati za mezani, Bunge pia litapokea Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2014/15 ambayo hivi karibuni ilikabidhiwa kwa Rais Magufuli.
“Pia Bunge litapokea majibu ya Serikali kuhusu hoja zilizotolewa na CAG kwa hesabu za mwaka wa fedha 2014/15,” ilisema taarifa hiyo ya Kitengo cha Mawasiliano cha Bunge.
Taarifa hiyo ilisema pia katika mkutano huo, Bunge litajadili na kupitisha miswada miwili ambayo ni Muswada wa Sheria ya Matumizi wa Mwaka 2016 na Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2016.
“Vilevile inategemea kuwa Serikali itawasilisha bungeni miswada ya Sheria kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa bungeni mara baada ya shughuli ya kupitisha bajeti kukamilika,” ilisema taarifa hiyo.
Aidha, katika mkutano huo kutakuwa na shughuli ya uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge kwa ajili ya kuziba nafasi iliyoachwa wazi baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, kufanya mabadiliko ya baadhi ya wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge. Nafasi hiyo imeachwa wazi na Mbunge wa Viti Maalumu, Dk Mary Mwanjelwa.
Aidha, wabunge wapya wanne ambao ni Shamsi Vuai Nahodha wa Jimbo la Kijitoupele, Ritha Kabati na Oliver Semguruka wote Viti Maalumu CCM na Lucy Owenya wa Viti Maalumu Chadema, wanatarajiwa kuapishwa rasmi.

Makonda atangaza neema kwa walimu

Imeandikwa na Sophia Mwambe MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameahidi kutoa zawadi ya fedha kwa mwalimu atakayefaulisha mwanafunzi katika somo lake la sayansi, lengo likiwa ni kutoa motisha kwa walimu.
Makonda aliyasema hayo jana Dar es Salaam wakati akizindua programu ya kuwasaidia wanafunzi waliotoka katika familia masikini iliyoandaliwa na shule za Feza.
Feza wametoa Sh milioni 37.5 kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi 150 wanaotoka katika familia masikini.
Makonda alisema atatoa Sh milioni 15 kwa mwalimu wa sekondari atakayefaulisha mwanafunzi katika masomo ya Sayansi na Sh milioni 10 kwa mwalimu wa kidato cha pili atakayefaulisha mwanafunzi katika masomo ya sayansi na Sh milioni tano kwa mwalimu wa shule ya msingi atakayefaulisha mwanafunzi.
“Niseme sitaishia kwenye kutoa fedha pekee, mwalimu huyo na familia yake watachagua mbuga yoyote ya wanyama watakayoitaka na nitagharamia kila kitu, naamini kwa kufanya hivyo kutajenga motisha hata kwa walimu wengine kuongeza jitihada na kuhakikisha anafaulisha wanafunzi,” alisema Makonda.
Aidha, Makonda amewashukuru Feza kwa kuamua kuwasaidia wanafunzi hao na amewataka wazazi kuhakikisha wanasimamia vyema fedha hizo ili zifanye kazi iliyokusuduwa.
“Sitopenda kusikia mama ametumia fedha hizo tofauti na nyinyi wanafunzi muwalipe wafadhili hawa kwa kusoma kwa bidii, hakuna mtu atakubali kuendelea kutoa msaada kwa mtu ambaye haoneshi juhudi,” aliongeza Makonda.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shule hizo, Isa Otcu alisema shule hizo zimeamua kutoa msaada huo kwa ajili ya kumuunga mkono Rais John Magufuli katika harakati zake za elimu bure.
Alisema programu hiyo itatoa kiasi cha Sh 250,000 kwa kila mwanafunzi na tayari wameshaweka kiasi cha Sh 100,000 katika akaunti za wanafunzi hao kuanzia Januari mpaka Aprili.
Aliongeza kuwa wameamua kuwateua kina mama kwa ajili ya kusimamia fedha hizo ambazo zitawekwa katika akaunti zao za benki, kwani wanaamini mama ana uwezo wa kuhifadhi kwa faida ya watoto wake.

magazeti ya Leo jumatatu ya tarehe 18/04/2016


 Magazeti haya yanakujia Kwa hisani ya kikoti MPESA and stationery








Jumapili, 17 Aprili 2016

Magazeti ya Leo jumapili ya tarehe 17/04/2016


Magazeti ya Leo yanaletwa kwenu  kwa hisani ya New mwalimu education centre ambao wanaofundisha tuition kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita wa masomo ya Jioni kuanzia SAA Tisa mpaka SAA moja mahali ni ilula madizini majengo ya kanisa katoliki kigango cha madizini karibuni sana








Jumamosi, 16 Aprili 2016

Magazeti ya Leo jumamosi ya tarehe 16/04/2016

Magazeti ya Leo yanaletwa kwenu Kwa hisani ya kikoti m Pesa ambao wanatoa huduma mbalimbali za kibiashara kama huduma ya mpesa  , tigo pesa , wanauza vocha za mitandao yote ya simu pia wanauza vifaa vya shuleni na ofisini Kwa bei rahisi nyote mnakaribishwa
Pia kikoti company inakituo cha tuition kinachojulikana kama New Mwalimu Education Centre kinachofundisha masomo ya ziada kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita kwa masomo yote Muda ni kuanzia saa kumi mpaka saa moja jioni  Eneo in majengo ya roman Catholic kigango cha madizini .Njoo upate elimu bora














Ijumaa, 15 Aprili 2016

Tatizo la maji katika mji mdogo wa ilula laendelea kufanyiwa kazi na mbunge kilolo





MBUNGE wa Jimbo la Kilolo, Venance Mwamoto ameiomba serikali kutumia maji ya mto Ruaha Mdogo kumaliza tatizo la muda mrefu la maji linaloukabili mji mdogo wa Ilula, wilayani Kilolo mkoani Iringa wenye wakazi zaidi ya 38,000.

Mto huo unaopita mjini Iringa ukijazwa na vyanzo mbalimbali vidogo vya maji vikiwemo vya wilayani Kilolo, upo zaidi ya kilomita 30 kutoka mji huo wa Ilula wenye kata tatu za Lugalo, Nyalumbu na Ilula yenyewe.

Mwamoto alitoa ombi hilo  wakati  Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Iringa Mjini (IRUWASA) ikikabidhi kwa Mamlaka  ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira ya Mji Mdogo Ilula, mradi mdogo wa maji yanayotumiwa na mji huo toka chanzo cha mto Idemle baada ya kusimamia ukarabati wake uliogharimu Sh Milioni 903.

“Ufumbuzi wa tatizo la maji katika mji mdogo wa Ilula ni kutumia maji ya Mto Ruaha Mdogo badala ya pendekezo la kutumia chanzo cha Mgombezi ambalo gharama zake ni kubwa,” Mwamoto alisema.

Alisema endapo serikali itaendelea na mpango wa kutumia chanzo cha Mgombezi wananchi wa Ilula wasitegemee kupata maji ndani ya kipindi kifupi kijacho.

“Kama tutang’ang’ania kutumia chanzo cha Mgombezi, inaweza kuichukua Ilula zaidi ya miaka 10 kupata huduma ya maji safi na salama, ombi langu tutumie chanzo cha mto Ruaha Mdogo kuleta maji Ilula, na nadhani hata gharama zake zinaweza kuwa ndogo,” alisema.

Akitoa taarifa ya ukarabati wa mradi wa maji wa chanzo cha mto Idemle, Mkurugenzi wa IRUWASA, Gilbert Kayange alisema; “baada ya ukarabati huo uliofanywa kati ya mwaka 2013 na 2015, chanzo hicho sasa kinazalisha mita za ujazo 940 kutoka mita za ujazo 600 zilizokuwa zikizalishwa awali wakati mahitaji kwa siku ni mita za ujazo 2,609.”

Ili kutatua tatizo la maji katika mji huo, Kayange alisema serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji wa chanzo cha Mgombezi ambao gharama yake inaelezwa kuwa ni zaidi ya Sh Bilioni 15.

“Tunaongelea suala la Mgombezi kwasababu mradi huo ulikwishasanifiwa, lakini hiyo haitufanyi wataalamu tusiendelee kutafuta vyanzo vingine mbadala vitakavyosaidia kukabiliana na changamoto ya maji katika mji wetu wa Ilula,” alisema.

Akizungumzia kazi zilizotekelezwa wakati wa ukarabati wa mradi huo wa chanzo cha Idemle, Kayange alizitaja baadhi yake kuwa ni pamoja na kukarabati kidaka maji katika mto Idemele, kukarabati tenki la kuhifadhi maji Mazombe na ujenzi wa vitolea hewa katika bomba kuu la usafirishaji na ukarabati wa njia ya usafirsiahaji maji wenye urefu wa kilomita 14.

Nyingine ni pamoja na ujenzi wa mabomba mapya ya kusambaza maji safi yenye urefu wa kilomita 16.7 ambayo hata hivyo yamekuwa yakihujumiwa kwa kutobolewa na watu wasiojulikana.

Mtendaji wa kijiji cha Mazombe, Joseph Nyoni alisema; “mambomba ya plastiki yamekuwa yakitobolewa nay ale ya chuma yamekuwa yakibondwa sehemu za maungio na kusababisha kuvuja na kupoteza maji mengi yanayotakiwa kwa matumizi ya wananchi.”

Nyoni alisema katika kukabiliana na changamoto hiyo, wamefanya mikutano ya hadhara ili kuwashirikisha wananchi kuwafichua waharibifu wa mitandao ya maji.

Mbunge wa Kilolo ameliomba jeshi la Polisi kuwasaidia kuwabaini watu hao ili wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa uharibifu huo.

Meneja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Ilula, Enock Ngoinde amesema wanahitaji zaidi ya Sh Milioni moja kukarabati mabomba hayo.

TAKUKURU yakabidhiwa Kampuni ya Lugumi


Image result for valentino mlowola
picha :Mkurugenzi Mkuu Takukuru-Valentino Mlowola
Sakata la kampuni ya Lugumi iliyoingia mkataba wa Sh37 bilioni na Jeshi la Polisi wa kufunga mashine za kielektroniki za kuchukua alama za vidole nchi nzima, sasa limetua Takukuru baada ya taasisi ya kupambana na rushwa kuchukua faili lake la usajili.

Kampuni hiyo ilibainika kutotimiza matakwa ya mkataba wake baada ya kufunga mashine 14 tu kati ya 108 ilizotakiwa kufunga, licha ya kulipwa  asilimia 99 ya fedha kwa mujibu wa mkataba.

Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) ya mwaka 2013/14 ndiyo iliyofichua udhaifu huo.

Wakati Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ikitaka nguvu itumike ili Jeshi la Polisi liwasilishe mkataba huo, utata umeibuka katika umiliki wa kampuni hiyo kutokana na kuwepo tuhuma kuwa baadhi ya vigogo wa Polisi na wanasiasa ni wanahisa wa Lugumi Enterprises.

Jana, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela), Frank Kanyusi alisema kuwa Takukuru inashughulikia suala hilo, huku akibainisha kuwa kwa sasa Brela hawana takwimu za kina za kampuni hiyo.

“Kampuni hii ilisajiliwa kihalali na kupewa cheti cha usajili. Ila ninachoweza kukueleza kwa sasa ni kwamba jalada la usajili la Lugumi lipo Takukuru kwa ajili ya uchunguzi zaidi,” alisema Kinyusi jana.

Kanyusi, ambaye hakutaka kuzungumzia kiundani kuhusu usajili wa kampuni hiyo, alisema: “Waandishi wa habari wamekuwa wakiniuliza maswali mengi kuhusu suala hili ila kwa sasa hali ndiyo hiyo. Jambo hili lipo Takukuru.”

Alisema kwa sasa kampuni zilizosajiliwa na Brela zipo 120,000 na zinakaribia kufika 130,000 na kwamba kampuni lazima zitoe taarifa zake kila mwaka, kinyume na hapo zinaweza kuchukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufutwa.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Brela zilieleza  kuwa taarifa za usajili wa kampuni hiyo zilitoweka takribani miezi miwili iliyopita.

Mwandishi  alipofika katika ofisi za wakala huyo kwa ajili ya kupata ukweli wa usajili, alielezwa na mmoja wa watumishi ambaye hakutaka jina lake kuwekwa wazi kwamba ni vigumu kupata hilo jalada kwa sababu ya mvutano ulioibuka.

Hata baada ya kufuata taratibu za kupewa jalada hilo kwa ajili ya kupitia masuala mbalimbali, alijibiwa kuwa jalada hilo halionekani ingawa baadaye Kanyusi alisema limechukuliwa na Takukuru.

Sakata la Lugumi liliibuka wiki iliyopita wakati PAC ilipokutana na Jeshi la Polisi kupitia taarifa ya hesabu zao za mwaka 2013/14 zilizokaguliwa na CAG.

Katika hesabu hizo ilibainika kuwa mwaka 2011, Polisi iliingia mkataba na Lugumi kwa ajili ya kufunga mashine hizo katika vituo 108 vya polisi kwa gharama ya Sh 37 bilioni.

Hata hivyo, ilibainika kuwa kampuni hiyo imefunga mitambo hiyo kwenye vituo 14 tu, huku ikilipwa asilimia 99 ya fedha hizo.

Kutokana na ukakasi huo, PAC ambayo ilibaini viashiria vya ufisadi katika mkataba huo, iliagiza watendaji wa Polisi kuwasilisha taarifa za mkataba huo pamoja na vielelezo vyake ili kamati hiyo iweze kuupitia na kujiridhisha.

Lakini hadi sasa Jeshi la Polisi halijawasilisha mkataba huo, jambo ambalo huenda likazua mjadala mkali katika mkutano wa Bunge unaoanza Jumanne ijayo.