ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatano, 20 Aprili 2016

Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam aliesimamishwa kazi atoa ya moyoni

Wednesday, April 20, 2016

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe amesema uchunguzi wa tuhuma zilizomfanya Rais John Magufuli kumsimamisha kazi jana utabainisha ukweli huku akihoji; “ikiwa itabainika kwamba nilionewa nitalipwa fidia?”

Alisema hayo mara baada ya Dk Magufuli kutangaza kumsimamisha kazi wakati wa uzinduzi wa Daraja la NSSF Kigamboni ambalo sasa litaitwa Daraja la Nyerere baada ya kumwita Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kueleza tuhuma dhidi ya mkurugenzi.

Alipoulizwa jana, Kabwe alisema hakuwa na taarifa za kusimamishwa kwake na mazungumzo yake na mwandishi wetu yalikuwa kama ifuatavyo:

Mwandishi: Habari mkurugenzi?
Kabwe: Salama.

Mwandishi: Tumepata taarifa za kusimamishwa kwako kazi na Rais kutokana na tuhuma zilizotolewa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Makonda tunaomba maoni yako. Kabwe: Sijasikia ndiyo kwanza unaniambia wewe, kasema lini Rais?

Mwandishi:Leo wakati akizindua Daraja la Kigamboni. Kabwe: Alitamka palepale au?

Mwandishi: Ndiyo.
Kabwe: Sasa kama ameshasema yeye ndiyo mkubwa mimi sina la kusema tena.

Mwandishi: Nataka kujua unazungumziaje uamuzi huo? Kabwe: Nimekwambia sina la kukwambia kwa sasa lakini nimesema tu sina shida na hilo, uchunguzi ufanyike nina uhakika ukweli utajulikana tu. Lakini kama ukijulikana na ikibainika nimeonewa je, kuna fidia yoyote nitalipwa?

Magazeti ya Leo jumatano ya tarehe 20/04/2016

Headline hizi za magazeti ya Leo zinaletwa Kwa hisani kubwa ya new Mwalimu education centre tunatoa huduma za tuition kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita mda wa masomo ni kuanzia SAA saba Kwa kidato cha tano(pre form five) na SAA kumi Kwa kidato vha kwanza mpaka cha NNE na wale wa kidato cha sita Karibuni sana















Jumatatu, 18 Aprili 2016

Mwenge wa Uhuru kuwashwa leo

Imeandikwa na John Nditi, Morogoro

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan leo atawasha Mwenge wa Uhuru na kuzindua rasmi mbio zake ili kukimbizwa katika halmashauri za wilaya na Manispaa zipatazo 179 za mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani.
Uzinduzi huo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro ambao utatanguliwa na shamrashamra za halaiki kutoka kwa vijana zaidi ya 1,000 na vikundi vya utamaduni kutoka wilaya za Morogoro na nje ya mkoa huo.
Katika uzinduzi huo, viongozi mbalimbali wa Serikali, dini na vyama vya siasa wamealikwa kushiriki wakiwemo pia mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Waziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Miongoni mwa mawaziri ambao hadi jana walikuwa tayari wamewasili mkoani hapa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Bunge, Sera, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama na Waziri wa Kazi, Uwezeshaji Wazee, Wanawake na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mouldine Castico.
Mawaziri hao jana waliungana na Makamu wa Rais kutembelea mradi wa vijana wajasiriamali wa mafundi seremala eneo la Mtaa wa Betero, Kata ya Sabasaba, Manispaa ya Morogoro. Kaulimbiu za Mwenge wa Uhuru mwaka huu ni “Vijana ni Nguvu kazi ya Taifa, Washirikishwe na Kuwezeshwa.”
Baada ya kuwashwa leo, Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na kuhitimishwa wilayani Gairo ambako Aprili 25, mwaka huu utakabidhiwa mpakani mwa wilaya hiyo na Kilindi ya Mkoa wa Tanga ili kuendelea na mbio zake.
Kwa mujibu wa ratiba ya mbio za Mwenge wa Uhuru za mwaka huu, utakimbizwa katika Halmashauri na Manispaa zipatazo 179 na kilele cha mbio hizo ni Oktoba 14, mwaka huu katika Mkoa wa Simiyu.
Mwenge wa Uhuru uliwashwa kwa mara ya kwanza Desemba 9, 1961 kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro, kutimiza ahadi ya Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere wakati wa kudai Uhuru wa Tanganyika.

DC aagiza kusakwa aliyempa mimba mwanafunzi

Imeandikwa na Angela Sebastian, Bukoba MKUU wa Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, Jackson Msome ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kumsaka na kumtia mbaroni kisha kumfikisha mahakamani mtu aliyempa mimba mwanafunzi wa Kidato cha Nne katika Shule ya Sekondari Karabagaine iliyoko wilayani humo.
Msome alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati alipofanya ziara ya kushtukiza shuleni hapo na kupewa taarifa kuwa mwanafunzi huyo ni mjamzito.
“Vyombo vya ulinzi na usalama kaeni na mwanafunzi huyo anamtambua aliyempa mimba, mhoji na hakikisheni mnamkamata mtu huyo kisha afikishwe mahakamani kujibu tuhuma hiyo,” alisema na kuongeza: “Pia jamii fichueni wale wanaowapa mimba watoto wetu wa kike, wanaowaoa na kuwaozesha waweze kutiwa mbaroni na kupambana na mkono wa sheria.”
Alisema kutokana na tabia hizo, watu wawili wamekamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuwapa wanafunzi mimba katika shule za sekondari za Nyakibimbili ambako wanafunzi wawili wa kidato cha kwanza, Alicia Vedasto na Dominatha Jacob wamepewa ujauzito.