ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 25 Aprili 2016

Magazeti ya Leo jumatatu ya tarehe 25/04/2016

Ndugu msomaji wa blog yetu  endelea kufuatana nasi kwa taarifa za uhakika na zenye ukweli kutoka vyanzo mhimu, vile vile kumbuka makala yetu ya wiki itaangazia masuala ya elimu kilolo katika mada itakayoenda kwa jina la "hili nalo jipu". Tutaangazia ni vipi walimu wakuu hasa kada sekondari wakishirikiana na walimu wao wameanza kuonesha nia ya kuhujumu elimu bure kaa nasi hapahapa


























Jumapili, 24 Aprili 2016

Magazeti ya Leo jumapili ya tarehe 24/04/2016

Ndugu msomaji wa blog yetu wiki hili katika makala ya wiki tutakuletea jipu jipya linaloonekana kuzinyemelea shule za sekondari za wilaya ya kilolo na kuonesha nia ya dhati ya wakuu wa shule kuhujumu mpango wa elimu Bure. Je hili nalo jipu? Utafahamu hapa hapa kwenye blog yako pendwa











Jumamosi, 23 Aprili 2016

fuatilia simulizi ya kusisimua

MIRATHI YA KAKA SEHEMU YA 1
Kiza kinene kilikuwa kimetanda pande zote za dunia, sikuelewa kama nipo peke yangu ama tupo wengi  kutokana na kutoona umbali hata wa sentimita moja mbele yangu.
Nilifikicha macho na kutazama huku na kule,
‘Mungu wangu! Nipo wapi huku, nimefikaje na nimefika saa ngapi?’ Nilishindwa kupata jibu.
Nilikodoa macho kwa nguvu kama mtu aliyeshikwa ugoni; bado nilikuwa sioni chochote mbele ya mboni za macho yangu zaidi ya weusi wa giza totoro lililokuwepo.
Niligeuka kushoto sikuona chochote, nikageuka kulia pia sikuona chochote. Niliamua kugeuka mzimamzima, bado sikupata picha hata kidogo, moyo wa woga ulianza kuniingia,  nikataka kukimbia lakini nikashindwa.
Nilipojaribu kunyanyua mguu wangu wa kuume nipige hatua kuelekea mbele, mguu ulikuwa mzito.
Ndipo nilipogundua kuwa nguvu zimeniishia, viungo vyote vya mwili nilivihisi vimelegea; vilikuwa vimekufa ngazi kabisa. Nilibaki nikitetemeka palepale, nikajaribu kufumbua kinywa changu angalau nipige yowe la kuomba msaada. Hata hivo nilijikuta nikishindwa kuongea, nikaishia kumung’unyamung’unya maneno utadhani anaongea bubu vile. Kinywa kilikuwa kizito kufumbuka.
Kijasho chembamba kilianza kunitoka, nikajikuta nimelowana chepechepe mwili mzima utadhani nimemwagiwa maji. Ghafla nikadondoka chini mzimamzima, nikaanguka  puu kama gunia la mtama liangukavyo linapotupiwa chini hasahasa na mtu mzembe ama aliyechoka kubeba.
Nilianza kuona mwanga mweupe, mwanga huo ulikuwa ni mkali mara kumi zaidi ya ule wa radi; mwanga huo ulizidi kujirudiarudia.
Ghafla mwanga ulisitisha kumulika; mara nikamuona mtu mbele yangu, mtu huyo alikuwa amevaa kanzu iliyong’aa japokuwa gizani. Nilijaribu kuinua kichwa changu nimwangalie huenda nitang’amua kuwa ni nani.
Nilijikuta nikipigwa na butwaa baada ya kuinua macho yangu kwani nilimuona mtu huyo ni wa ajabu mno. Ni miaka ishirini na saba sasa tangu nizaliwe lakini sijawahi kuona mtu mrefu namna hii hapa chini ya jua. Nilijaribu kukifuatilia kiwiliwili chake ili nione kichwa chake kilipoishia .
Niligundua kuwa mtu huyo alikuwa ni mrefu kuzidi maelezo kwani nilishindwa kuuona mwisho wake.
Sijakaa sawa mtu huyo akapotea, nilibaki nikiwaza bila kupata jawabu.                           ‘Nitasalimika kweli leo?’ Nilijiuliza kimoyomoyo bila kutoa sauti. Nikaangaza pande zote, giza lilikuwa bado lipo palepale. Nilijaribu kuinuka ili nikimbie, hata hivo  nilishindwa kwa vile mwili ulikuwa bado hauna nguvu. 

Sauti za ngurumo kama za radi zilianza kusikika kwenye ngoma za masikio yangu. Zilizidi kujirudiarudia kabla ya kusindikizwa na tetemeko kubwa la ardhi. Nilihisi ardhi yote inatikisika, woga ukazidi kuongezeka. Mapigo ya moyo wangu yakaanza kwenda kasi zaidi.
‘Nitapona kweli leo?’ Huu ni mfano wa baadhi ya maswali yaliyokuwa yanaisumbua akili yangu kwa wakati huo. Nilikosa majibu ya maswali yangu, nikaishia kujisemea kuwa Mungu yupo.
 

MIRATHI YA KAKA sehemu ya 2


Tetemeko lilikoma ghafla, pakawa shwari tena, lakini giza lilikuwa lipo palepale. Mvua kubwa ilianza kunyesha, mwanga na miungurumo ya radi nilizidi kuvishuhudia.  
Nilibaki nimeduwaa baada ya kugundua kuwa pale nilipokuwa silowi licha ya mvua kubwa kuendelea kunyesha. Hakuna hata tone moja la maji lililokuwa likinifikia utadhani nilikuwa chini ya mwamvuli, nilizidi kuchanganyikiwa.
Hata kwa chini maji hayakunigusa hivyo nyayo zangu zilikuwa kavu. Lakini mvua nilikuwa naishuhudia ikinyesha, tena ni bonge la mvua.
Nilibaini kuwa kumbe nilikuwa nipo juu ya kilima baada ya mwanga wa radi kumulika. Lakini hapakuwa hata na mwamvuli juu yangu licha ya kutoangukiwa na tone hata moja.
Mara niliona kitu kama shuka jeupe kikishuka kutoka angani. Nilikisubiri kwa hamu kitu hicho ili nione ni nini kitatokea.
Woga ulianza kupungua. Siyo kwa kuwa nilikuwa nimeyazoea mazingira; la hasha! Ulipungua kutokana na kukata tamaa nikijua kuwa kuokoka kwangu ni asilimia 0.0025. Nilijipa uhakika wa kupoteza uhai endapo kudura za Mwenyezi Mungu zisingechukua nafasi.
Kitu hicho kilizidi kuteremka taratibu, tena kilikuwa wima mithili ya kitambaa cha sinema. Japokuwa giza lilikuwa limetanda angani kote, kitu hicho kiling’ara na niliweza kuushuhudia mng’ao wake. Shauku ya kutaka kuona kitakachotokea ilizidi kunishika, moyo wa woga haukuwepo tena kwa wakati huo.
Kitu hicho kilianguka chini, moshi mwingi niliushuhudia kilipokuwa kimeangukia. Moshi uliendelea kutoka mahali hapo lakini kitu hicho mfano wa shuka kilikuwa hakionekani tena.
Kufumba na kufumbua niliwaona watu katikati ya moshi huo, nikashindwa kujua idadi yao kamili kwa sababu walikuwa wanatembeatembea bila ya kutulia. Licha ya moshi mwingi kutanda eneo hilo, watu hawa walionekana ‘live’ tena bila chenga.
Nilizidi kuchanganyikiwa nilipoanza kuwatambua baadhi yao, kilichokuwa kinanishangaza ni kwamba kila niliyemtambua alikuwa kashatangulia mbele ya haki tukamzika, yaani namaanisha alishakufa kitambo.
Itaendelea......

UKAWA watoa sababu tatu za kugomea bajeti

Tazama video ya mwenyekiti wa CHADEMA akizungumza na waandishi wa habari
Kambi ya Upinzani bungeni jana imesusia kuwasilisha na kujadili hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu, huku kiongozi wake, Freeman Mbowe akitoka nje ya ukumbi huo, akitaja kasoro tatu zilizosababisha wachukue uamuzi huo.

Staili ya kususia kujadili hotuba hiyo ya bajeti ni mpya kwa kambi hiyo ya upinzani baada ya kutumia njia ya kutoka nje ya ukumbi wakati wa vikao vya Bunge la Katiba na baadaye kutumia njia ya kupiga kelele kukwamisha shughuli za chombo hicho wakati wa Bunge la Kumi.

Jana, Mbowe aliwaambia waandishi nje ya ukumbi kuwa kasoro zilizofanya wachukue uamuzi huo ni kukiuka masuala ya kisheria katika utekelezaji wa bajeti, kutotangaza kwenye Gazeti la Serikali mabadiliko ya wizara na kutorushwa kwa vipindi vya Bunge kwenye televisheni. 
 

Mbowe, ambaye alikuwa akitarajiwa kusoma bajeti ya upinzani kuhusu Ofisi ya Waziri Mkuu, aliibuka na hoja hizo tatu kabla ya kuamua kutoka nje.

“Bajeti inakuwapo kwa sababu ni hitaji la kisheria. Inapokuwa Serikali inataka kupitisha bajeti, lakini haiheshimu bajeti hakuna sababu ya wabunge kukaa hapa kujadiliana, kutoa povu, kupitisha vifungu vya Katiba, halafu yenyewe haitekelezi wajibu wake kisheria,” alisema Mbowe nje ya ukumbi wa Bunge.

Alisema Serikali imekuwa ikikiuka sheria ya utekelezaji wa majukumu ya mawaziri inayomtaka Rais kutengeneza mwongozo wa muundo wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali yake, ikiwa ni pamoja na kutangaza katika gazeti la Serikali mabadiliko ya wizara zake. 
Alisema “Tulichelewa kuunda (Baraza Kivuli la Mawaziri) kwa sababu tulikosa instrument (nyaraka rasmi). Tukalazimika kuunda hivyohivyo. Sasa tumefika kwenye (Bunge bado Serikali haijaundwa officially (rasmi), kisheria. Haijawa gazetted (haijatangazwa kwenye Gazeti la Serikali),” alisema Mbowe.

“Mpaka leo Serikali hii inafanya kazi kwa kutumia instrument iliyosainiwa na Rais (wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya) Kikwete mwezi wa 12 mwaka 2010.

“Na wizara kuu kwa mujibu wa instrument ya mwaka 2010 ilikuwa ni Wizara ya Waziri Mkuu Tamisemi. Na Tamisemi ilikuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Kwa hiyo baada ya uchaguzi wa 2010, Tamisemi imerudishwa Ofisi ya Rais, haiku tena Ofisi ya Waziri Mkuu. Lakini haijawa gazetted.”

Alitaja hoja nyingine kuwa ni uvunjwaji wa Katiba na sheria za nchi kuhusiana na bajeti unaofanywa na Serikali pamoja na kuminya uhuru na madaraka ya mhimili wa Bunge kwa kuzuia matangazo ya wasusia Bunge kurushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni.

“Hatutashiriki mjadala tunaendelea kutafakari hatua nyingine za kuchukua kama Serikali na Bunge hawatatafuta ufumbuzi wa masuala hayo matatu,” alisema Mbowe.

Mbowe aliingia ukumbini saa 9:56 alasiri akiongozana na mbunge wa Momba, David Silinde na alikwenda kusalimiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) George Masaju na Waziri wa Kilimo, Mwigulu Nchemba.

Mara baada ya kupewa nafasi na Mwenyekiti wa Bunge Andrew Chenge, Mbowe alieleza sheria ya utekelezaji wa majukumu ya mawaziri ambapo alidai kifungu cha 5(1) kinaweka masharti kwa Rais kutengeneza mwongozo wa muundo na utekelezaji wa majukumu yake.

Alisema mpaka sasa Serikali inafanya kazi bila kuwa na mwongozo wa utendaji kwa wizara mbalimbali hivyo kazi nyingi za Serikali zinafanywa kwa kauli ya Rais.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo mpaka sasa mwongozo wa utendaji wa Serikali kwa kila wizara unaotumika ni uliochapishwa kwenye Gazeti la Serikali Namba 494 A la Desemba 17, 2010 ambao pia umetoa majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu. 
Kiongozi huyo alinukuu baadhi ya majukumu katika mwongozo huo kuwa ni kuratibu shughuli za Serikali, kiongozi wa Serikali ndani ya Bunge, kiungo kati ya Bunge na Serikali, shughuli za kisiasa na serikali na kuratibu sherehe na misaada mbalimbali.

“Kazi nyingine ni kusaidia urahisishaji wa mipango ya serikali katika kuhamishia makao makuu Dodoma, uwekezaji, uchumi, sekta binafsi na kusaidia maendeleo katika sekta za ndani,” alisema Mbowe.

Alisema Rais John Magufuli alifanya mabadiliko ya kuziunganisha wizara bila kubadili muongozo wa kisheria.

“Kitendo cha Serikali hii kuendesha kazi zake kwa mwongozo wa 2010 kina maana kwamba majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu bado ni yale yale ya mwaka 2010 kwa sababu gazeti hilo halijafutwa,” alisema.

Alifafanua kuwa jambo hilo ni uvunjwaji wa Katiba na sheria za nchi kuhusu bajeti unaofanywa na serikali na kwa mujibu wa Ibara ya 63 (3) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bunge limepewa mamlaka ya kujadili utekelezaji wa kila wizara na kuidhinisha bajeti ya Serikali.

Mbowe alisema ikiwa fedha zilizoidhinishwa na bunge hazikutosha kutekeleza majukumu, kifungu cha 41 (1) cha Sheria ya Bajeti ya mwaka 2015 kinaelekeza kuwa serikali itawasilisha bungeni maombi ya idhini, bajeti ya nyongeza ya fedha zilizotumika ambazo zimezidi kiwango.

Alituhumu kuwa kumekuwa na uvunjwaji wa kifungu hicho na kutolea mfano bajeti ya Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano ya mwaka wa 2015/16 ilikuwa Sh 883.8 bilioni ambazo kati ya hizo, fedha za ndani zilikuwa Sh191.6 bilioni. 
 “Jambo la kushangaza ni kwamba hadi kufikia mwezi Machi 2016 Wizara ilikuwa imeshapokea kutoka hazina Sh607.4 bilioni ikiwa ni fedha za ndani, kitendo kinachoonyesha kuwa na ongezeko kubwa la fedha za ndani,” alisema.

Alitaja kuwa tangu kuidhinishwa kwa bajeti ya Wizara ya Ujenzi, hakuna bajeti ya nyongeza iliyopelekwa bungeni na Serikali kwa ajili ya kupata idhini kutokana na matakwa ya Sheria ya Bajeti ya mwaka 2015 au sheria ya fedha ya 2015.
 “Kitendo cha Serikali kuamua kuhamisha kiasi cha fedha ya bajeti bila ya kupata idhini ya Bunge ni dharau kwa bunge lakini mbaya zaidi ni uvunjwaji wa Katiba na sheria.” alisema.
 Nje ya ukumbi wa Bunge alisema:”Ukiwauliza wanapata wapi hizi fedha, wanasema ni maelekezo ya Rais kwamba fedha ziondolewe kwenye fungu hili, zipelekwe wizara hii.”

Vipindi vya Bunge
 Kadhalika, Mbowe alisema uamuzi wa Serikali kuminya uhuru na madaraka ya Bunge umewapora wananchi haki yao ya kupata habari kwa kuzuia mijadala bungeni kurushwa moja kwa moja na vyombo vya habari.

Alisema jambo hilo ni uvunjwaji wa Ibara ya 18 ya Katiba inayotoa uhuru kwa kila mtu kutoa maoni na kueleza fikra zake, kutafuta, kupokea na kutoa habari.

“Bunge ndipo mahali ambapo wananchi wanahoji na kuiwajibisha Serikali na wanajadili hoja za maendeleo kupitia wabunge wao waliowachagua, hivyo huwafuatilia kupitia kwenye luninga zao pia ubadhirifu wa miradi mingi uibuliwa huko,” alisema.

Alisema wapinzani wataendelea kutafakari kwa kina na makini hatua za kufuata na kisha akawasilisha.

“Kwa mazingira kama hayo, kambi rasmi ya upinzani bungeni haiko tayari kuendelea kushiriki katika uvunjaji Katiba, sheria na haki za msingi za wananchi,” alisema.

“Kambi rasmi haitakuwa tayari kuwasilisha hotuba yake katika mazingira haya na inaushauri uongozi wa Bunge kutafuta ufumbuzi wa haraka wa kadhia hii ili kurejesha heshima ya Bunge na haki za msingi.”

Baadaye, Chenge aliipinga kauli ya Mbowe kuwa Katiba imevunjwa na kusema alitumia maneno mazito na badala yake alimtaka atumie maneno kuwa Katiba ilitaka kuvunjwa.

Chenge aliitaka kambi ya upinzani kufuata taratibu kama wanaona kuwa wameonewa, badala ya kutumia maneno hayo na pia akata watafakari kama wangependa kuendelea na mjadala.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge wa upinzani walionyesha kususia kwani hata walipoitwa na mwenyekiti hawakuchangia licha ya kuwapo ndani ya ukumbi wa Bunge.

Kauli ya Mbowe kwa wanahabari 
Akizungumza na wanahabari Mbowe alisema uamuzi huo haujakiuka sheria kwa sababu Bunge liko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kwamba hawawezi kwenda mahakamani ili kupata tafsiri kuhusu suala hilo kwa sababu shughuli za Bunge zinatatuliwa na Bunge lenyewe si mahakama.

“Rais kama kiongozi wa nchi ana mamlaka ya kulisemea hili, atueleze kama ni yeye ndiye aliyeruhusu Bunge lisirushwe moja kwa moja. Awali walisema TBC hawatarusha ila kwa sasa vyombo vyote vimezuiwa,” alisema.

“Hivi sasa luninga zilizopo ndani ya Bunge zilizokuwa zikionyesha matangazo  nazo hazionyeshi kinachoendelea. Sasa watumishi wa Bunge watafuatilia nini?” alihoji Mbowe.

Kauli ya AG 
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alisema: “Nitashukuru kama mtavuta subira majibu ya Serikali yatatolewa wakati wa kufanya majumuisho.”

Magazeti ya Leo tarehe 23/04/2016


Ndugu msomaji wetu  wiki hili katika makala maalumu tutakuletea jibu jipya linalo zinyemelea shule za sekondari kilolo linaloonesha nia ya dhati ya wakuu wa shule kuanza kuhujumu elimu bure : Tutatazama jipu hili limeiva au bado?