ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Alhamisi, 23 Juni 2016

Breaking News: Rais Magufuli aonya wanasiasa wanaomchelewesha kufanya kazi

Imeandikwa na Selemani Nzaro
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli amewaonya wanasiasa wanaomchelewesha kufanya kazi ya kuwatumikia Watanzania.
Rais Magufuli ameyasema hayo muda mfupi uliopita baada ya kupokea ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kutoka kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Amesema haiwezekani uchaguzi umepita na mshindi amepatikana lakini wanasiasa hao wanaendeleza siasa ilhali wananchi wanataka watumikiwe wapate maendeleo.
Rais amesema hatawavumilia viongozi wa siasa wenye lengo baya na nchi na kuwataka waweke maslahi ya Taifa mbele badala ya vyama vyao. Amewataka kufanya siasa baada ya miaka mitano ambapo wananchi watawapima kile walichokifanya kwa muda wote huo.
Awali Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Damian Lubuva alisema suala la Kura ya Maoni halikusitishwa kama baadhi ya watu wanavyosema bali iliahirishwa kwa kuwa wakati kura hiyo ilipotakiwa kupigwa Aprili Mwaka jana, Tume ilikuwa na jukumu kubwa la kuandaa uchaguzi Mkuu.
Kutokana na hali hiyo, Jaji Lubuva alisema Tume haikuwa na uwezo wa kubeba mambo mawili makubwa kwa wakati mmoja. Jaji Lubuva amesema kutokana na zoezi la Uchaguzi Mkuu kumalizika rasmi, Tume iko tayari kuanza mchakato wa kura ya maoni.
Kuhusu suala hilo la Kura ya Maoni, Rais Dk Magufuli amemhakikishia Jaji Lubuva kuwa serikali italiamualia mara baada ya Tume kulifikisha serikalni.

TCU yaita wenye kero

Imeandikwa na Lucy Ngowi
TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imetoa fursa kwa wananchi wenye kero, maoni na changamoto kuhusu masuala ya elimu ya juu hususani udahili na uendeshaji wa vyuo vikuu, wayawasilishe kwao.
Ofisa Habari Mwandamizi wa tume, Edward Mkaku alisema jana mkakati huo umefanyika kutekeleza agizo kutoka Ofisi ya Rais –Menejimenti na Utumishi wa Umma, lililotaka taasisi hiyo iadhimishe wiki ya utumishi wa umma kwa kusikiliza kero, maoni na changamoto.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Mkaku alisema tangu jana saa 3 asubuhi hadi saa 7 mchana, walipokea wananchi 44 waliowasilisha maoni yao.
Wengi wao ni waliokuwa wakiulizia mwongozo wa kudahiliwa vyuo vikuu ambao kwa mwaka huu haujatoka.
Pia waliulizia mfumo wa kuhama kutoka chuo kimoja kwenda kingine, mfumo wa udahili unavyofanya kazi na utambuzi wa vyeti.
Hata hivyo, alisema wamebaini wananchi wengi wamekuwa wakichanganya kazi za tume na za Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).

Serikali yataja kodi mpya zitakazokatwa

Imeandikwa na Joseph Lugendo, Dodoma

WAKATI muswada wa Sheria ya Fedha ya Mwaka 2016 ukitarajiwa kuanza kujadiliwa bungeni leo ambao unaoipa serikali mamlaka ya kisheria kutoza kodi na kutumia fedha hizo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, ametaja kodi ambazo zitalazimika kukatwa.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi kufafanua hoja ambazo hakuzielezea kwa kina bungeni, Dk Mpango alisema miongoni mwa kodi hizo ambazo baadhi ya wabunge na vyombo vya habari vilitetea zisikatwe ni pamoja na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika utalii.
Nyingine ni kutoza kodi katika migahawa na maduka katika majeshi baada ya kufuta msamaha wake na kuhamisha jukumu la utozaji kodi za majengo kutoka halmashauri kwenda katika Mamlaka ya Mapato (TRA).
Akizungumzia VAT katika utalii, Dk Mpango alisema kodi hiyo haihusiani na ongezeko au kupungua kwa watalii nchini kwa kuwa watalii hao hawatazami kodi hiyo kama kigezo kikuu cha kwenda kuangalia vivutio vya utalii.
Alitoa mfano wa idadi ya watalii waliotembelea mbuga za wanyama kwa kipindi 2011 hadi 2014 katika nchi za Tanzania, Kenya na Afrika Kusini, ambayo inaonesha Tanzania licha ya kwamba haikuwa ikitoza VAT, bado ilitembelewa na watalii wachache kuliko nchi hizo ambazo zilikuwa zikitoza kodi.
Aliendelea kusisitiza kuwa mpaka kabla ya hotuba yake ya Bajeti ya Serikali ya 2016/17, nchi zote wanachama wa Jumuiya Afrika Mashariki zilikuwa zikitoza kodi hiyo kwenye huduma ya utalii isipokuwa Tanzania ambayo imependekeza kutoza katika bajeti yake ya mwaka 2016/17.
Kuhusu uamuzi wa serikali kuhamisha jukumu la kukusanya kodi za majengo kutoka katika halmashauri kwenda TRA, Dk Mpango alisema mamlaka hiyo ya kodi ndiyo yenye uzoefu wa kutosha katika ukusanyaji kodi za serikali na ndiyo yenye vituo vya ukusanyaji kodi katika wilaya na mikoa yote Tanzania.
Kuhusu viwango vya kodi ya majengo, alisema Waziri wa Fedha na Mipango ataweka viwango vya kodi ya majengo baada ya kushauriana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili kuweka uwazi na kujumuisha maoni ya wadau wote muhimu zikiwemo halmashauri husika.
Katika msisitizo mwingine alisema kuwa, mapato kutokana na kodi ya majengo yataingizwa katika mfuko mkuu ambao mawaziri wenye dhamana ya fedha na Tamisemi, ndio watakaoshauriana kuhusu mgawanyo wa fedha hizo kwa kuzingatia bajeti za halmashauri husika.
Kuhusu madai kwamba kuondolewa kwa misamaha ya kodi katika maduka na migahawa ya vyombo vya ulinzi na usalama kunaondoa motisha katika taasisi hizo, alisema uamuzi huo wa serikali upo palepale kwa kuwa misamaha hiyo ilikuwa ikitumika vibaya.
“Ili kuondoa kasoro hiyo, serikali imeamua kuweka utaratibu wa kuwalipa posho watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama ili wanufaike moja kwa moja kama walengwa. Kiasi cha posho atakayolipwa askari kitakokotolewa baada ya mashauriano na vyombo husika,” alisisitiza.
Kuhusu ushuru wa bidhaa kutozwa kwenye ada ya miamala ya uhawilishaji wa fedha, kama utaathiri mtumiaji wa mwisho, Dk Mpango alisema ushuru huo hautakatwa kwenye fedha zinazotumwa au kupokewa, bali katika ada inayotozwa na benki au kampuni ya simu.
Alifafanua kuwa kwa sasa sheria inatamka kwamba ada hiyo itatozwa katika kutuma fedha tu, hivyo baadhi ya kampuni za simu na benki zilikuwa zikitumia mwanya wa sheria hiyo kupunguza wigo wa kodi kwa kutoza ada wakati wa kupokea tu.

#Magazeti ya Leo Alhamisi ya tarehe 23/06/2016








 Pamoja tunaweza aaaa













Endelea kutembelea blog yetu 
Kwa Matangazo wasiliana nasi Kwa namba +255 769694963

Jumatano, 22 Juni 2016

Jumanne, 21 Juni 2016

CHADEMA Wataka Mkutano Mkuu wa CCM Kumkabidhi Uenyekiti Magufuli Nao Uzuiliwe

Image result for mbowe

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetoa tamko zito kikitaka Polisi kuzuia Mkutano Mkuu wa CCM utakaofanyika mwezi ujao, vinginevyo watatumia nguvu ya umma kuuzuia.

CCM kimeitisha mkutano mkuu maalumu unaotarajiwa kufanyika Julai 23 mjini Dodoma, kwa lengo la Mwenyekiti wa chama hicho, Jakaya Kikwete kumkabidhi uongozi wa chama, Rais John Magufuli.

Kauli ya kutaka Polisi kuzuia mkutano huo kama inavyofanya kwa vyama vingine vya siasa, ilitolewa juzi mjini Moshi na Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), Julius Mwita.

Msimamo huo wa Chadema ambao uliungwa mkono na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Salum Mwalim unafuatia Polisi kuzuia mahafali ya wahitimu wa vyuo vikuu ambao ni wanachama wao.

Akizungumza na wanahabari, Mwita alikwenda mbali na kudai kuwa, Chadema watalifungulia Jeshi la Polisi kesi ya madai ya fidia kwa kuvuruga mahafali ya Chaso mjini Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita.

“Ukisoma barua yao wamesema wamezuia mikutano ya hadhara sasa kama wanakuja hadi kwenye vikao vya ndani, hatuwezi kuendelea kukubali jambo hili.Tumetumia busara sana,” alisema Mwita na kuongeza: 

“Msipouzuia Mkutano Mkuu wa CCM Dodoma Julai 23 tunakuja kuuzuia sisi... yaani muwe tayari kusafiri kwenda Dodoma tukauzuie ule mkutano la sivyo, wauzuie kama walivyouzuia mikutano yetu.” 

Mwita alimgeukia Mwalimu na kumweleza kuwa hiyo ni lugha ya ujana na inatekelezeka, akawahoji vijana wa Chaso waliokuwapo: “Wangapi mko tayari kuja Dodoma?” Wote wakaafiki.

“Intelijensia ya polisi ni ya kiumbea, inayoweza kujua tu Chadema wanakwenda kwenye mkutano, haiwezi kujua watu wamejificha wana bunduki na risasi 300 kwenye mawe kule Mwanza,” alidai.

Mwalimu alisema utaratibu wa Polisi na Serikali lazima ukome na kwamba wao ni viongozi.