ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 4 Julai 2016

Chadema: Maandalizi ya Kuuzuia Mkutano wa CCM Yameanza


KATIKA kutekeleza tamko la Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) la kufika Dodoma kusaidiana na Jeshi la Polisi kuzuia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bavicha Dodoma wameanza maandalizi ya kupokea vijana zaidi ya 2000.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana Malambaya Manyanya, Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Dodoma alisema, kwa sasa viongozi wa mkoa wameanza maadalizi ya kuwapokea wageni wao ambao wanatarajiwa kuanza kuwasili tarehe 21 na 22 Julai mwaka huu.

Alisema, maadalizi hayo ni ya kuwapokea vijana ambao watatoka katika mikoa yote ya Tanzania kwa lengo la kutimiza tamko la Bavicha taifa la kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma kuzuia mikutano na vikao vya CCM.

Alisema, kwa sasa mkoa tayari umeunda kikosi cha kufanya kazi ya maadalizi ya ugeni huo ambapo kwa nia njema utafika mjini Dodoma kutekeleza kauli ya Rais John Magufuli ya kuzuia vikao vyote na mikutano ya vyama vya siasa.

Alisema, maadalizi hayo ya kuwapokea vijana hao ni pamoja na viongozi wa kitaifa wa Bavicha kwa maana ya kutafuta mahali pa kulala na maandalizi ya chakula.

“Wapo watu ambao wanadhani Bavicha wana mpango wa kufanya fujo, sisi tunataka kurejesha Demokrasia nchini na kutekeleza kauli ya mkuu wa nchi.

“Tumekuwa tukiona jinsi mikutano ya Chadema inavyozuiliwa, na sasa msimamo wa Bavicha ni  kuzuia mkutano ya CCM unaotarajiwa kufanyika Julai 23 kwa lengo la kubadilishana uongozi kati ya mwenyekiti wa sasa wa CCM na rais msitaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete na Rais John Magufuli.

“Tumeandaa vijana takribani 2000 kutoka mikoa yote nchini watakaokuja Dodoma kusaidiana na Jeshi la Polisi kutawanya mkutano usio halali wa CCM.

“Kwa sababau mkuu wa nchi ametoa tamko la kuzuia mikutano yote ya siasa ikiwa ni pamoja na vikao vya ndani na mikutano ya hadhara hadi 2020.” Alisema Malambaya.

Alisema, Jeshi la Polisi lilizuia mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani na mahafali ya Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Chadema (CHASO) na kuwa, sasa wanashirikiana na polisi kuhakikisha mikutano ya CCM haitafanyika.

UVCCM yanena kuhusu BAVICHA kuzua mkutano Dodoma

Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) umeingia katika mvutano mkubwa na Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA) kuhusu Mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho tawala uliopangwa kufanyika Julai 23 mwaka huu mjini Dodoma.

UVCCM wameionya BAVICHA kuhusu mpango wao wa kutaka kukusanyika mjini Dodoma siku hiyo kwa lengo la kuzuia mkutano huo kwa madai kuwa unakiuka amri halali ya polisi ya kupiga marufuku kufanyika kwa mikutano yote ya kisiasa nchini.

Onyo hiyo limetolewa na  Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamda Shaka ambaye aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuwa watawakabili kwa nguvu zote BAVICHA endapo wataamua kuendesha siasa zinazolenga kuvuruga amani na kuleta hofu katika jamii na kutishia maisha.

Alisema umoja huo hautaona shaka kutumia mbinu zilizotumiwa na wapiganaji wa Maumau miongo kadhaa iliyopita nchini Kenya.

“Hatutaona muhali kupita njia zilizotumiwa na wapiganaji wa Maumau wa Kenya ili kukihami chama, kulinda viongozi wake na kupigania hadhi na heshima yetu,” alisema Kaimu Katibu Mkuu huyo wa UVCCM.

CCM inatarajia kufanya mkutano mkuu maalum Julai 23 mwaka huu ambapo Rais John Magufuli atakabidhiwa rasmi uenyekiti wa chama hicho kutoka kwa mtangulizi wake, Dk. Jakaya Kikwete.

Shelukindo Kuzikwa Alhamis Jijini Arusha


MWILI wa Mbunge wa zamani wa Kilindi, Beatrice Shelukindo (CCM), unatarajiwa kuzikwa Alhamis wiki hii.

Taarifa iliyotolewa jana na kaka wa marehemu, Enock Madimilo, ilisema taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa nyumbani kwa marehemu Dar as Salaam na Arusha.

“Tunaendelea na mipango ya mazishi hapa Arusha na nyumbani kwa marehemu, Ada Estate jijini Dar es Salaam.

“Mazishi yatafanyika hapa Arusha Alhamisi wii hii. Kwa hiyo, tunawaomba ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu, waje kumuaga mpendwa na kiongozi wao,” alisema Madimilo.

Shelukindo alifariki juzi usiku saa 2:30 akiwa nyumbani kwa mama yake mzazi, katika eneo la Olorien, jijini Arusha baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Mwili wa marehemu Beatrice uliondolewa nyumbani kwa mama yake huyo alipokuwa akiuguzwa usiku huo huo na kupelekwa Hospitali ya Mount Meru.

Kutokana na msiba huo, tayari waombolezaji mbalimbali wameendelea kufika nyumbani kwa mama wa marehemu kwa ajili ya kutoa pole.

Kesi za mafisadi kutozidi miezi 9

Imeandikwa na Theopista Nsanzugwanko
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohammed Chande Othman (katikati), akipewa maelezo na Msajili wa Mahakama Kuu, Ilvin Mugeta (kulia) wakati alipotembelea banda la mahakama hiyo kwenye Maonesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea katika viwanja vya maonesho hayo, Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam, jana. Alifuatana na Jaji Kiongozi, Ferdinand Wambali (kushoto), Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage (wa pili kulia) na viongozi wengine. (Picha na Yusuf Badi).
JAJI Mkuu, Mohammed Chande Othman, amesema Mahakama Maalumu ya Uhujumu Uchumi na Ufisadi itaamua kesi kwa muda usiozidi miezi tisa na kwamba itaanza na majaji 14.
Aidha, wameandaa kozi maalumu kwa majaji 14 watakaofanya kazi katika mahakama hiyo itakayoanza Julai 11 hadi 15, mwaka huu, kwenye Chuo cha Mahakama Lushoto mkoani Tanga, ili kupeana mwongozo juu ya uendeshaji wa mahakama hiyo.
Jaji Mkuu alisema, kesi zitakazoendeshwa katika mahakama hiyo ni zile ambazo upelelezi wake umekamilika ili uamuzi utolewe mapema. Kwa mujibu wa Jaji Mkuu, dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kupambana na uhalifu huo.
Aliyasema hayo jana wakati alipotembelea Maonesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo katika Barabara ya Kilwa, ambayo alisema yamezidi kuwa bora kuliko miaka mingine. Alisema baada ya sheria hiyo ya uhujumu uchumi kupitishwa na Bunge, imekuwa na marekebisho mengi na kuboreshwa kwa kiasi kikubwa.
Jaji Mkuu alisema pia, hatua inayofuata ni Rais kutoa idhini ya sheria hiyo na baadaye kupitishwa kwa kutangazwa katika Gazeti la Serikali ili ianze kutumika.
Alieleza kuwa baada ya kutangazwa katika Gazeti hilo la Serikali, Jaji anatakiwa kutunga kanuni mbalimbali, mojawapo ikiwa ya kulinda mashahidi kutokana na kuwa sheria hiyo inahusu makosa makubwa na hatari ya ugaidi, rushwa na uhujumu uchumi.
“Tuko mbioni kutunga kanuni hizo na kuhakikisha mashahidi wanalindwa. Jengo la mahakama hii litakuwa katika Chuo cha Sheria karibu na Mlimani City na tayari tumepeleka wasajili watendaji,” alisema.
Mwishoni mwa wiki, Jaji Mkuu huyo alisema kuwa majengo ya mahakama hiyo yatakabidhiwa leo. Kutokana na maelezo yake, Mahakama iko tayari kuendesha divisheni hiyo, baada ya kukabidhiwa majengo hayo.
Alisema wataanza kutoa semina kwa majaji na watumishi wengine wa mahakama hiyo juu ya namna divisheni hiyo itakavyoendesha shughuli zake. Aidha, aliweka wazi kuwa hadi sasa hakuna kesi hata moja iliyokwishatambuliwa kwamba itashughulikiwa na mahakama hiyo.

Habari za magazetini Leo jumatatu ya tarehe 04/07/






















Jumapili, 3 Julai 2016

Michezo:Kikoti Education Centre Cup

Ilula mtua 2 na Ilula Madizini 2
Ilula sokoni 1 na Ilula isele 2
Kwa matokeo hayo timu ya ilula isele inaongoza katika ligi hiyo ikiwa na jumla ya point tatu na magoli mawili ikifuatiwa na ilula Madizini na ilula mtua zote zikiwa na point Moja na magori mawili na nafasi ya mwisho ikishikiliwa na ilula sokoni ambayo haina point
Mdhamini wa mashindano hayo amepongeza wachezaji wote Kwa kuonesha kiwango cha hali ya Juu na kuwaasa kuendelea na mashindano hayo Kwa nidhamu na utulivu mkubwa ili kufanisha zoezi hill 
Ratiba za mechi zijazo ni kama zifuatazo 
Isele vs Madizini saa name siku ya jumamosi ijayo 
Sokoni vs Mtua saa kumi ya jumamosi ijayo
Na siku ya jumapili ijayo 
Madizini vs Sokoni saa Nane 
Mtua vs Isele saa kumi Jioni
Wapenzi watazamaji mnakaribishwa sana kuangalia vijana wenu wanavoonesha vipaji

Magazeti ya Leo jumapili ya tarehe 03/07/2016