ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 11 Julai 2016

Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson Asema Kura za Wabunge wa UKAWA Hazitoshi Kumvua Madaraka ya Unaibu Spika

Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson amesema hoja ya wabunge wa Ukawa kutaka aenguliwe kwenye wadhifa huo inafanyiwa kazi na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ambayo iwapo itaridhia, itarejeshwa bungeni kupigiwa kura ambazo hata hivyo, hazitatosha kwa uchache wao. 
Dk Tulia alisema hayo jana wakati akihojiwa na Tido Mhando katika kipindi cha Funguka kinachorushwa na Azam TV.

“Hoja ikishakuja bungeni hapo sasa huwa ni kampeni na baadaye kupigiwa kura. Kwa kuwa waliopeleka hoja ni wabunge wa upinzani, hivyo wanatakiwa kufikisha idadi fulani ambayo kiuhalisia wao kwa sasa hawana,” alisema.

Kwa karibu mwezi mzima kwenye Bunge la Bajeti, wabunge wa Ukawa walimsusia Dk Tulia na walikuwa wakitoka bungeni kila alipoingia, tayari wameanzisha mchakato wa kumuondoa madarakani kwa madai kuwa hawatendei haki na anaminya demokrasia ndani ya Bunge.

Dk Tulia alisema Katiba inatambua kwamba kiongozi aliyechaguliwa anaweza kuondolewa madarakani na wale waliomchagua, hivyo wabunge wa upinzani wametumia haki yao ya msingi na kinachosubiriwa ni hoja yao kufanyiwa kazi.

“Kanuni imeweka wazi na msingi ule umejengwa kwenye Katiba kwa sababu inatambua wale waliomchagua kiongozi wasiporidhika naye wanaweza kumuondoa madarakani. Nafarijika kuona wanachukua hatua, hivyo mimi sina malumbano nao,” alisema.

Hakuna maridhiano 
Dk Tulia alisema hakuna maridhiano yanayotakiwa baina yake na wabunge wa Ukawa kwa kuwa hana malumbano nao, bali kanuni na taratibu zinafuatwa kufanikisha hoja yao ya kumuondoa madarakani.

Naibu Spika huyo alisema maridhiano huwapo baina ya watu wanaolumbana na kwamba, baina yao hakutakuwa na suala hilo

Mwenyekiti wa Chadema Awazuia Vijana wa Chadema ( BAVICHA ) Kwenda Dodoma

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiacXY69F6eDNr-zExmYxmRgr1kuSWaSZVcMGRe1DJjVak36KkYZQLO67miRiC_s06FUu95oF0AMAphBc1uO2NRcy2eh1WmmIsuSVmANijrKdG_pQlGDwsCsW2iiJi5aRKHcG2mEm63eAE/s1600/1.jpg
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ametangaza kusitisha mpango wa vijana wa chama hicho kwenda Dodoma kuzuia Mkutano Mkuu wa CCM ili kuepusha maafa ambayo yanaweza kutokea. Badala yake, Mbowe amesema wataendelea kusaka haki ya kufanya mikutano ndani na nje ya nchi. 
Sambamba na uamuzi huo, chama hicho kimetaka viongozi sita wa Baraza la Vijana (Bavicha) wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi kuachiwa mara moja. 
Mbowe alitoa tamko hilo jana wakati akizungumza na wanahabari jijini Arusha, katika mkutano wa mameya na wenyeviti wa halmashauri 18 zinazoongozwa na Umoja wa Katiba ya wananchi (Ukawa).
 Sababu za kusitisha 
Mbowe alisema wamewataka vijana wa Chadema nchi nzima ambao walianza kujiandaa kwenda Dodoma kuisaidia polisi kuzuia mkutano huo wa Julai 23 kutokwenda kwa sababu polisi wamepewa maagizo ya kuwapiga na kuwajeruhi, hivyo wao hawataki kupambana nao. 
“Nawataka vijana wote wa Chadema waliokuwa wanajiandaa kwenda Dodoma wasitishe na wasubiri maelekezo mapya ya Chadema,” alisema Mbowe. 
Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alisema wana taarifa Jeshi la Polisi limejipanga kuwanyima dhamana viongozi wa Bavicha hadi baada ya mkutano wa CCM, ingawa viongozi wote wa chama hicho hawana hofu ya kukaa mahabusu. 
Aliwataka vijana hao kutokwenda Dodoma na wawaache CCM waendelee na mkutano wao kwa kuwa Chadema haina hofu na mkutano wa chama hicho, bali walitaka dunia ione jinsi polisi wanavyofanya kazi kwa maelezo ambayo yanakiuka Sheria ya Vyama vya Siasa na Katiba ya nchi. 
“Wakati sisi tunazuiwa kufanya siasa, Rais anafanya siasa, Waziri Mkuu anafanya siasa, mawaziri wanafanya siasa, wakuu wa mikoa na wilaya wanafanya siasa jambo ambalo si sahihi,” alisema.
 Alisema lengo la Bavicha kwenda Dodoma ni kuchoshwa na uonevu wa kuzuiwa kufanya mikutano ya ndani na hadhara wakati CCM wanaendelea na mikutano yao. 
“Waliona pengine itakuwa busara washinikize polisi kuona maagizo yao ya kuzuiwa mikutano yanatekelezwa kwa wote,” alisema. 
Alilitaka jeshi la polisi kufanya kazi kwa kufuata taratibu kwa kutoa haki sawa kwa wote, kwa kuruhusu vyama vyote kufanya mikutano yao. 
Apinga tamko la Mwigulu
Kuhusu tamko la Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kuhusu mikutano hiyo, Mbowe alisema hawakulielewa tamko hilo la Rais, kuwa mikutano ambayo imezuiwa ni ya hadhara na maandamano na si ya ndani. 
Alisema mikutano ya ndani ya chama hicho imezuiwa kwani Chadema Wilaya ya Kahama walikuwa na mkutano wa ndani wa uchaguzi ambao umezuiwa. 
 Alisema mkutano wa ndani na wabunge wa Chadema mkoani Shinyanga ulizuiwa na pia mahafali za Vijana wa Vyuo Vikuu wa Chadema (Chaso). 

“Lakini wakati haya yanafanyika, CCM waliendelea na mikutano yao na mahafali yao,” alisema. 
Alisema Chadema itaendelea kudai haki ya mikutano na maandamano katika mahakama za ndani na nje ikiwamo ya Afrika ya Mashariki. 
Viongozi wa madiwani 
Katika mkutano wa wenyeviti wa halmashauri 18 zinazoongozwa na Chadema, Mbowe alisema Calist Lazaro, Meya wa jiji la Arusha amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa wenyeviti wa madiwani wa Chadema nchini.
Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob alichaguliwa kuwa katibu wa madiwani wote wa chama hicho na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tarime, Moses Matiku alichaguliwa kuwa mnadhimu wao. Wote hao watakuwa wajumbe wa Kamati Kuu Chadema. 
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji alisema katika mkutano huo wenyeviti hao wamepatiwa elimu juu kuongoza vyema halmashauri zao ili kuchochea maendeleo. 
“Siku mbili za mkutano huu tumekaa na kuweka mikakati bora ya kuhakikisha halmashauri zinazoongozwa na upinzani zinafanya vizuri,” alisema.

Magazeti ya Leo jumatatu ya tarehe 11/07/2016












 Kwa hisani ya kikoti education centre









 Ukombozi wa Mtoto wako mlete kikoti education centre