ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatano, 20 Julai 2016

Orodha ya wanachuo wanaorudi kusoma stashahada maalum ya ualimu UDOM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj6mWQMraVFnV5VtjTXsByqhExmgOrPJvviQcUMQzLH0NBS61muTjlWS_cFbhaYJuFpyBRzjF15lir-pecJGP7mdXD2Ds_XPDTSBfUqwd4jdSD7GjmCev50CIc5mHfP_h9RWWfjUjZBS3Y/s1600/1.jpg

==> Kuona Majina ya Waliohamishiwa Vyuo vingine  << BOFYA  HAPA>>
==> Kuona majina ya ambao hawajakidhi vigezo vya kurudishwa  << BOFYA HAPA>> 
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Magazeti ya Leo jumatano ya tarehe 20/07/2016



















Jumanne, 19 Julai 2016

TCU kuanza kudahili wanafunzi wa kujiunga vyuo vikuu kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh08-jAqkJHihehdulHCHWAObB6Bg943UDPT_WN50Whc0L-sX6AJYoxvOdBv2VLIzy_oDrZc_HHa_Qxsi5bZy2NJv3cl2UKyfpb7flJ5xV0cThMjgPNrWyZYcKXvUb0FO986JFIN46wCJo/s1600/1.jpg
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), itaanza kudahili wanafunzi waliomaliza kidato cha sita wanaoomba kujiunga na vyuo vikuu kuanzia kesho. 
Akizungumza jana, Kaimu Mkurugenzi wa Udahili na Nyaraka wa TCU, Dk Kokubelwa Mollel alisema udahili kwa wenye diploma utaanza Julai 31. 
Dk Mollel alisema kazi hiyo itaendelea kwa mwezi mzima ili kuruhusu wananchi wengi zaidi kupata fursa ya kuomba kudahiliwa na udahili huo utafanyika kwa njia ya mtandao.
Alisema ili wanafunzi waweze kuelewa programu zinazotolewa na vyuo vikuu, tume hiyo imeandaa maonyesho ya 11 yatakayofanyika kuanzia Julai 20 hadi 22, mwaka huu. 
Alisema maonyesho hayo yatafanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kufunguliwa na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako.
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Bavicha: Msimamo Wetu ni Ule Ule, Lazima Nasisi Tufanye Kikao Chetu Dodoma

Ikiwa zimebaki siku tatu kabla ya Mkutano Mkuu wa CCM kufanyika, Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) limesema azma yao ya kufanya kikao chao cha kamati ya utendaji mjini Dodoma ipo palepale. 
Julai 16, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alisema kikao cha Bavicha hakitofanyika kwa sababu itakuwa ni mwendelezo wa vurugu zao. 
Mkutano Mkuu wa CCM, utakuwa na ajenda mbalimbali ikiwamo ya Mwenyekiti wa chama hicho, Jakaya Kikwete kumkabidhi kijiti cha uongozi Rais John Magufuli. 
Katibu Mkuu wa Bavicha, Julius Mwita jana alisema  baraza hilo lipo kwenye hatua ya mwisho ya maandalizi ya kikao hicho kitakachohudhuriwa na zaidi ya wajumbe 50 kutoka mikoa yote. 

“Wajumbe wataanza kuwasili kesho (leo) mjini Dodoma. Hatuna wasiwasi na kikao hiki kwa sababu ni cha ndani siyo mkutano wa hadhara, ambao umepigwa marufuku na polisi,” alisema Mwita. 
Mwita alisema kikao hicho kitakuwa cha siku mbili kuanzia Julai 20 hadi 21 na kwamba, kitahudhuriwa na mameya na wenyeviti vijana wa halmshauri zinazoongozwa na Chadema. 
Alipotafutwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob ambaye ni mwanachama wa Bavicha kujua kama atahudhuria kikao hicho alijibu: “Nitakwenda kwa sababu mimi ni kijana, sina sababu ya kukataa wito wa viongozi wangu wa juu wa Bavicha taifa.” 
Kuhusu kauli ya Kamanda Mambosasa, Mwita alisema polisi ilishatoa maelekezo ya kuruhusu vikao vya ndani. 
“Taarifa ya Mambosasa hatujaishangaa kwa sababu ni desturi yake kujichanganya, leo anasema hivi kesho vile. Tunamtaka atulie asubiri tumpe taarifa ni wapi kikao chetu kitanyika kwa njia ya amani,” alisema Mwita
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Rais Magufuli Akataa Kuwapandisha vyeo Maofisa 17 wa Polisi

Rais John Magufuli, amekataa kuwapandisha vyeo maofisa 17 wa polisi waolipendekezwa na amewapa nafasi ya kujipanga zaidi. 

Rais Magufuli aliwapandisha vyeo maofisa 60 kuanzia Jumamosi iliyopita, kati yao 25 kutoka cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) kuwa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP). 

Wengine 35 aliwapandisha kutoa cheo cha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi. 
Akizungumza jana muda mfupi baada ya maofisa hao kuapa kiapo cha maadili ya umma, Rais Magufuli alisema waliokuwa makamishna wasaidizi waandamizi waliopelekwa kwake katika mapendekezo walikuwa 31, lakini wamerudi 25. 

Pia, alisema waliokuwa makamishna wasaidizi wa polisi waliopendekezwa kuwa makamishna wasaidizi waandamizi wa polisi walikuwa 46, “ wamerudi 35.” 
“Wale ambao hawakurudi tuwape nafasi ya kujipanga tena zaidi. Nataka niwaeleze ukweli kwa sababu inawezekana wako wengine walisikia kwamba majina yao yalipelekwa…Sasa mkawaambie hayakurudi kwa sababu yangu. Wala wasihangaike kutafuta mchawi,” alisema Rais Magufuli. 
Alisema baada ya kupata taarifa na data zote walizonazo, “Nikaona tuwape muda wa kujirekebisha. Kwa hiyo nyinyi mliofanikiwa mpaka mmefikia hapa nawapongeza sana. “Mchakato ulikuwa mrefu na mzito,” alisema Rais Magufuli. 
Aliongeza, “Nyinyi sasa ni makamanda tunaowategemea katika nchi hii. Mmechaguliwa siyo kwa makosa. Mnastahili. Katekelezeni wajibu wenu bila woga kwa kuzingatia sheria.” 
Kuhusu mchakato huo, Rais Magufuli alisema alimwagiza, IGP Ernest Mangu karibu miezi mitano iliyopita kuanza mchakato huo.

Alisema mchakato ulianzia na ukapita kwa wakuu wao (wa polisi) kwa kuangalia historia za wale ambayo majina yao yalikuwa pamoja na kazi zao. 
“Wakapita (majina ya wapendekezwa) mahali pengine mpaka yamefikia kwangu…Ninajua hamtaki kusema lakini mimi nimeumbwa kusema ukweli.” 
Watumishi ‘raia’ kuondolewa 
Katika hotuba yake ya takriban dakika 30 aliyotoa bila kusoma popote, Rais Magufuli alisema inawezekana wapo watendaji wachache ndani ya Jeshi la Polisi ambao aidha kwa makusudi au kwa nia yao mbaya wanalichafua jeshi hilo. 
“Ninawaomba mkawashauri na kuwaelekeza, ikishindikana mkawaondoe katika Jeshi la Polisi. Mfano mzuri ni mhasibu ambaye aliorodhesha watumishi ambao si maaskari kulipwa pensheni wanayolipwa maaskari. 

“Mtu mwenyewe siyo askari, la kujiuliza nyinyi lakini mmeshindwa kumshika,” alihoji. 
Mhasibu huyo, Frank Msaki (ambaye si polisi) alisimamishwa kazi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, kwa makosa ya kufanya malipo hewa ya posho ya chakula kwa watu wasio askari. 

Kutokana na hilo, Rais Magufuli alisema kama wanafikiri kuwa na raia kwenye Jeshi la Polisi wanaliharibia jeshi, wahamishwe na wapelekwe utumishi. 

“IGP kaorodheshe raia wote wanaofanya katika Jeshi la Polisi watoke. Tuwapangie kazi nyingine kazi za kiraia. Ili kusudi hawa raia wanaokaa kwenye nafasi za jeshi waondoke. Bila kufanya hivyo inawezekana wataendelea kuwachafulia. Naomba hilo lishughulikiwe,” alisema. 
Mbali na agizo hilo, alimtaka IGP kufuatilia mtu aliyelipwa kati ya Sh20 bilioni hadi Sh60 bilioni kwa ajili ya kutengeneza sare za polisi tangu mwaka jana, lakini hadi sasa bado hajakabidhi sare hizo. 
“Tupate hizo fedha zetu ili mkakomboe magari yenu. Ninategemea siku moja waliohusika na hilo watapelekwa mbele ya haki,” alisema. 

Mwigulu Nchemba
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba aliwataka walioapishwa kufanya kazi kwa bidii na uadilifu. “…Sheria isipofuata mkondo wake wananchi wanachukua sheria mkononi. Tuzuie hilo na kuhakikisha sheria zinafuatwa,” alisema. 
Kamishna wa maadili, Jaji mstaafu Salome Kaganda aliwashauri maofisa hao wa Jeshi la Polisi kuunda kamati za maadili kwa ajili ya kusikiliza manung’uniko yao. 
IGP, Mangu alimshukuru Rais kwa kupokea mapendekezo yao na kuahidi kuwa atahakikisha maofisa hao wanatekeleza kiapo walichokula. 
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Makonda: Mashoga wanataka kuniangamiza

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amesema tangu alipotangaza kuanza kukamatwa kwa mashoga, amebaini kuna mkakati unawaohusisha watu hao zaidi ya 150 kutaka kumwangamiza.

Kauli hiyo aliitoa jana Dar es Salaam baada ya kumaliza mahojiano katika kituo cha redio Clouds FM, ambako alikuwa akifafanua hoja na changamoto mbalimbali za mkoa wake.

Alisema kuwa baada ya kubainika kwa mipango hiyo, mashoga wanane wamekamatwa na Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi.

“Lazima watu wajue jitihada na harakati za kusimamia katiba na usawa hapa nchini. Hakuna anayezipenda, vita inakuwa kubwa… Nimebaini kuwa mashoga zaidi ya 150 waliketi katika baa moja Kinondoni wakipanga njama za kunimaliza kwa namna moja ama nyingine, lakini kutokana  na taarifa za kiintelijensia, watu kadhaa, wengi wao wakiwa ni mashoga wameshakamatwa,” alisema Makonda.

Katika hatua nyingine, Makonda aliwatolea uvivu watu wanaosambaza ujumbe wa tofauti juu ya maagizo yake katika mitandao ya kijamii, ikiwamo kutengeneza akaunti feki.

“Kwanza wanapaswa kujua kuwa sina akaunti ambayo inaanza na cheo changu, hivyo akaunti zote zangu zimeandikwa kwa jina langu Paul Makonda si vinginevyo, hivyo kila mtu anapaswa kuwa makini na hilo,” alisema Makonda.

Aliweka wazi kuwa kuna agizo batili lililowekwa katika mitandao ya kijamii, akidaiwa kusema kuwa watu wasiokuwa na kazi watakwenda jela, lakini ukweli ni kwamba ameagiza wenyeviti wa Serikali za mtaa kuhakikisha kuwa wanafanya uhakiki wa wakazi wao nyumba kwa nyumba kwa ajili ya usalama wa maeneo wanayoishi.

Aidha Makonda alisisitiza kuwa kutokana na matatizo yaliyopo, kamwe Hatoacha kupambana na mafisadi katika halmashauri zote tatu za mkoa wake, pamoja na wauza unga, wafanyabiashara wa shisha na mashoga
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Magazeti ya Leo jumanne ya tarehe 19/07/2016





KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu