Jumapili, 14 Agosti 2016
Jumamosi, 13 Agosti 2016
Magazeti ya Leo jumamosi ya tarehe 13/08/2016
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI:
ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI
Mzazi/Mlezi wa
………………………………………………,kikoti education centre inapenda kukutarifu kuwa
inatarajia kuaanza kutoa elimu ya pre-form
one kwaajili ya maandalizi ya kidato cha kwanza. Kuanzia tarehe
09/09/2016.Kwa gharama ya shilingi elfu ishirini(20,000) tu kwa muda wa
miezi mitatu(3), ambapo mwanafunzi atapewa vitu vifuatavyo:-
1)
Tisheti yenye jina la
kituo
2)
Daftali, peni na pensel
3)
Vitabu vya masomo husikaVitakuwepo
4)
Mitihani kila wiki kupima maendeleo ya mwanafunzi
5)
Masomo yatakayopewa kipaumbele ni masomo yote ya
sayansi(biology, chemistry,physics, mathematics na English ,GEOGRAPHY)
-
Mlete mwanao apate elimu bora kutoka kwa walimu bora na wenye
taaluma na maadili ya ualimu kutoka vyuo vikuu bora Tanzania
Pia kikoti
education centre wanaendelea na kutoa tuition kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka cha sita
kama kawaida
OUR MOTTO: EDUCATION FOR LIFE
Kwa mawasiliano
zaidi tupigio kwa namba 0769694963, 0625682117 au 0757927380 au fika kikoti
education centre kwa maelezo zaidi:
MAHALI : ilula madizini- majengo ya kanisa katoriki, mita 50 kutoka soko la TASAF.
Ijumaa, 12 Agosti 2016
TAHADHARI DHIDI YA MATAPELI KWA WAOMBAJI WA MIKOPO NA WADHAMINI WAO
Taarifa hizo za kitapeli zimekuwa
zikisambazwa katika siku za hivi karibuni kupitia mitandao mbalimbali ya
kijamii zikiwataka baadhi ya waombaji wa mikopo au wadhamini wao kutuma
fedha (Tshs 39,000/-) kwa namba ya simu 0716463190
ili fomu zao za maombi ya mikopo zilizowasilishwa Bodi zirekebishwe kwa
kuwa zimeonekana zina makosa na hivyo hawatapata mikopo.
Namba inayotumika kusambaza taarifa hiyo au kupiga simu kutoa taarifa hizo ni 0764640325 na mtu anayepiga anajitambulisha kwa jina la Charles Amos.
Bodi ya Mikopo inapenda kuwataarifu wadau wake wote, wakiwemo wale walioomba mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2016/2017 kuwa taarifa hizo si za kweli. Mtu huyo ni tapeli na si mtumishi wa Bodi ya Mikopo.
Iwapo waombaji watapigiwa simu na matapeli hao, watoe taarifa kwa vyombo vya dola kwa hatua zaidi.
Aidha, Bodi ya Mikopo inapenda
kuwataarifu waombaji wa mikopo kuwa utaratibu wa Bodi kuwasiliana na
waombaji wa mikopo ambao fomu zao za maombi hubainika kuwa na upungufu
haujabadilika. Mara baada ya kazi ya ukaguzi wa fomu kukamilika, Bodi ya
Mikopo itatoa taarifa kupitia vyombo mbalimbali vya habari, ikiwemo
tovuti hii ya Bodi na kuwaalika waombaji kufanya marekebisho.
Mwisho.
IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO,
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU,
IJUMAA, AGOSTI 12, 2016
Serikali: Hatuna ushahidi wa kuzihukumu shule za Feza, Hivyo Hatuwezi Kuzifunga

Kauli
hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga.
Alisema
walipokea madai kutoka Ubalozi wa Uturuki nchini kuwa shule hizo
zinamilikiwa na mmoja wa wananchi wa nchi hiyo anayejihusisha na ugaidi.
Balozi
Mahiga alisema katika madai ya ubalozi huo, shule hizo ni miongoni mwa
miradi inayomilikiwa na mtuhumiwa huyo na kwamba, baadhi ya walimu wake
hutumia mbinu za kigaidi kufundisha wanafunzi.
Akijibu
tuhuma hizo, Balozi Mahiga alisema serikali kabla ya kutoa kibali kwa
mwekezaji au mfanyabiashara yeyote kuendesha shughuli zake nchini,
vyombo vya usalama nchini, hufanya upelelezi wa kina na wamejiridhisha
kwamba wafanyabiashara wa Uturuki waliopo nchini wanafanya biashara
halali.
“Ni
kweli tumepokea tuhuma kutoka kwa Ubalozi wa Uturuki nchini kuhusu
shule za Feza kwamba ni sehemu ya makundi ya kigaidi, lakini hatuwezi
kuzitia hatiani shule hizo hadi tuletewe ushahidi wa kutosha,” alisema Balozi Mahiga.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya
Shule za Feza, Habib Miradji alisema shule hizo ni za asasi
iliyosajiliwa kisheria na Serikali ya Tanzania hivyo ni mali ya Tanzania
na endapo kuna kitu au tatizo ni lazima wawasiliane na serikali na
watafika kukagua ili kama kuna lolote baya hatua zichukuliwe.
Aidha alisema kwamba shule hazijafungwa.
Magazeti ya Leo ijumaa ya tarehe 12/08/206
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI:
ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI
Mzazi/Mlezi wa
………………………………………………,kikoti education centre inapenda kukutarifu kuwa
inatarajia kuaanza kutoa elimu ya pre-form
one kwaajili ya maandalizi ya kidato cha kwanza. Kuanzia tarehe
09/09/2016.Kwa gharama ya shilingi elfu ishirini(20,000) tu kwa muda wa miezi
mitatu(3), ambapo mwanafunzi atapewa vitu vifuatavyo:-
1)
Tisheti yenye jina la
kituo
2)
Daftali, peni na pensel
3)
Vitabu vya masomo husikaVitakuwepo
4)
Mitihani kila wiki kupima maendeleo ya mwanafunzi
5)
Masomo yatakayopewa kipaumbele ni masomo yote ya
sayansi(biology, chemistry,physics, mathematics na English ,GEOGRAPHY)
-
Mlete mwanao apate elimu bora kutoka kwa walimu bora na wenye
taaluma na maadili ya ualimu kutoka vyuo vikuu bora Tanzania
Pia kikoti
education centre wanaendelea na kutoa tuition kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka cha sita
kama kawaida
OUR MOTTO: EDUCATION FOR LIFE
Kwa mawasiliano
zaidi tupigio kwa namba 0769694963, 0625682117 au 0757927380 au fika kikoti
education centre kwa maelezo zaidi:
MAHALI : ilula madizini- majengo ya kanisa katoriki, mita 50 kutoka soko la TASAF.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)