ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Alhamisi, 9 Februari 2017

Yusuf Manji kawasili Polisi Leo akiwa na mawakili nane

Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuph Manji amefika kituo cha Polisi cha Kati leo saa 4:54 asubuhi kwa ajili ya mahojiano baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kumtaka afike polisi.


Manji amefika leo badala ya kesho ambapo yeye na wengine 64 walitakiwa kufika kituoni hapo.

Manji ambaye pia ni Mwenyekitu wa Klabu ya Yanga jana alizungumza na waandishi wa habari na kusema hatoweza kufika kituoni hapo siku ya Ijumaa.

Amewasili leo na gari aina ya Range Rover rangi nyeusi huku.

Manji amefika kituoni hapo  akiwa na wanasheria wake 8 ambapo wanasheria 6 ni raia wa Tanzania na wanasheria wawili ni raia wa Uingereza. Aidha, mashabiki wa Yanga wamejitokeza kwa wingi kituoni hapo kumuunga mkono kiongozi wao.

Mbali na Manji, wengine waliotajwa katika orodha hiyo ni Pamoja na Fremaan Mbowe, Askofu Josephat Gwajima, Iddi Azan.

Magazeti ya Leo Alhamisi ya tarehe 09/02/2017






















Jumatano, 8 Februari 2017

MAKONDA AITWA BUNGENI KOWAOMBA MSAMAHA WABUNGE

chanzo chetu cha habari kutoka Bungeni mjini Dodoma kinaeleza kuwa mchana wa leo katika ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega alisimama na kutoa hoja binafsi akitaka Bunge kumuwajibisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda, baada ya kauli aliyotoa RC Makonda mapema leo baada ya kumaliza kutaja orodha ya watuhumiwa wengine 65 kwenye sakata la madawa ya kulevya ambapo aliulizwa swali juu ya yale yanayozungumzwa Bungeni juu ya jinsi anavyoendesha kampeni hiyo ambapo Paul Makonda alijibu kuwa hajishughulishi na kauli za wabunge kwani kazi yao ni kulala na wengine kazi zao ni kuchekesha wenzao.
Baada ya kauli hii ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Mbunge wa Mkuranga amewasilisha hoja binafsi yenye mapendekezo matatu:
1. Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es salaam aende Bungeni mjini Dodoma na awaombe msamaha Wabunge kwa kulidhalilisha Bunge hilo.
2. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Kassim Majaliwa akiwa kama msimamizi wa shughuli zote za serikali Bungeni atoe tamko kuhusu kauli hii iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na kuliomba msamaha Bunge kwa niaba yake.
3. Bunge liandike barua kwenda Kamati ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakimtaka Mkuu huyo wa mkoa aitwe kwenda Bungeni mjini Dodoma ili akaliombe msamaha Bunge kwa kauli aliyoitoa.
Abdallah Ulega, Mbunge wa Mkuranga
Baada ya kuwasilisha hoja hii, wabunge kwa pamoja walikataa hoja namba mbili ya Waziri Mkuu kuzungumza kwa niaba ya serikali au kuomba msamaha kwa kauli alizotoa Paul Makonda na badala yake wamekubaliana kuwa Bunge liandike barua kwenda kwenye Kamati ya Maadili ya Uongozi wa Umma wakitaka Mkuu huyo wa Mkoa kwenda Bungeni akaombe msamaha yeye mwenyewe.
Taarifa zinasema kwamba kufikia jioni hii barua hiyo imeshaandikwa na kutumwa kwenda Kamati ya Maadili ya Watumishi wa Umma ili kutekeleza mchakato uliopendekezwa

Yusuf Manji Aapa Kumshitaki Makonda Kwa Kumchafulia Jina......

 
Manji: Nimesikia wakisema natakiwa kufika kituo cha Polisi siku ya Ijumaa.

Manji: Mimi nina nafasi mbili kwenye jamii, Mimi ni mtoto wa baba yangu na nafasi yangu ya pili mimi ni mwenyekiti wa Yanga na nyote mnajua ninavyoheshimiwa.

Manji: Na chaguzi zilizopita mimi nilichukuahukua fomu peke yangu ya kugombea Yanga hivyo naheshimika.

Manji: Huwezi kunitangaza kupitia radio kwamba niende kwenye kutuo cha polisi saa tano. Makonda ni mdogo kwangu kiumri.

Manji: Na katiba inasema kila mtu ana haki yake, Ukinichafua mimi kama Mwenyekiti wa Yanga unachafua Yanga nzima.

Manji: Ukinishutumu mimi ni mpumbavu tu wewe.

Manji: Kama unataka mimi nikusaidie kutaja wauzaji ni kuniweka kwenye hatari.

Manji: Mimi nitaenda Kituo cha Polisi kesho sisubiri hiyo Ijumaa.

Manji: Kifungu cha 66 katika katiba kinaeleze haki zangu na kufungu 32 pia. Vinanilinda.

Manji: Nataka nimshitaki Mahakamani na vyombo vyote vilivyoandika kunituhumu na madawa.

Manji: Kesho naenda Polisi asubuhi nihojiwe baada ya hapo naanza kutafuta haki yangu. Huwezi kuniita kaka huku unanitaja kwenye mambo mabaya.

Manji: Wapo watu kwenye mtandao wameanza kuandika vitu, Alichofanya mkuu wa mkoa ni kosa siwezi kukubali.

Manji: Na Wanayanga kama mnaona mimi sifai na kama hamna imani na mimi hata kesho naondoka Yanga. Siwezi kuchafua Club kubwa.

Manji: Kwanini RC Makonda hajamuita Askofu Pengo au Mashehe wamsaidie?

Manji: Hiwezi kuniita mimi kama mbwa njoo, Hii ni kutafuta masifa. Kesho utanikuta mimi kwenye gazeti na wengine 65 watasahaulika. Hii sio haki.

Manji: Zipo njia za kushughulikia vitu, Tukienda Comoro tunaenda na bendera ya Tanzania.

Manji: Kama unataka msaada omba msaasa sio unaagiza msaada, Unaniita na watu 65 nikae kwenye foleni, watu 65 watamaliza saa ngapi? Saa tano usiku nitoke? Sina kazi nyingine za kifanya?

Manji: Yupo mzee mmoja na wenyewe mnamjua, alinitukana nikamdai shilling moja. Unanihusisha mimi jina langu nloachiwa na baba kwenye huu upumbavu halafu unathubutu kiniita kaka yako?

Manji: Hii itanifanya nishindwe kwenda Comoro na Klabu ya Yanga sababu Wanacomoro watasema nimepeleka madawa. Wananichafua sana.

Manji: Hivi ni vita na wanahitaji msaada haraka na kama wana shutuma au ushahidi au huo msaada wanieleze. Kama vita kwanini isiwe leo wasubiri ijumaa. Mimi naenda kesho.

Manji: Kesho nyie watu wa magazeti na habari msitoe habari kwa upande mmoja.

Manji: Ambao hawatabalance habari. Cybercrime inasema ukiweka habari ya uongo unafungwa. "Ambaye ataandika makonda manji dawa za kulevya" kesho namshitaki.

Manji: Wakina Amina Chifupa walitaja majina, yalienda wapi? Hii jitihada hakuna mtu anakataa. Hata unayemchunguza humtaji kwenye vyombo vya habari. Hata TAKUKURU hawawataji wanaowachunguza. Mimi siwezi kwenda kutaja mshahara wa mfanyakazi. Nitakiwa namvunjia heshima.

Manji: Mimi nipo tayari kupimwa na kusearchiwa na Makonda naye apimwe kama anatumia na wamsearch pia.

Manji: Mimi sitaki kuchanganya vitu viwili kwenye mkutano mmoja. Kesho au keshokutwa ntafanya mkutano kuanzia PSPF, Coco Beach nk. Leo nakaa kwenye point moja tu ya madawa.

Manji: Mkuu wa mkoa kunasehemu nimegongana naye oysterbay na nlienda kuonanana naye kama diwani wa mbagala kuu kumuomba mkuu wa majeshi atakayekuja ahamishe kambi ya jeshi kutoka mbagala na kupelekwa nje ya mji. Kama diwani siwezi kumuandikia rais.

Makonda ataja majina mengine ya washukiwa wa madawa ya kulevya



Magazeti ya Leo jumatano ya tarehe 08/02/2017