Jumapili, 26 Februari 2017
Jumamosi, 25 Februari 2017
Ijumaa, 24 Februari 2017
Wema Sepetu Avaa Rasmi Magwnda ya CHADEMA.....Aeleza Kilichomfanya Aihame CCM
Msanii
wa filamu nchi Tanzania Wema Sepetu ametangaza rasmi kukihama Chama cha
Mapinduzi CCM na kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Akizungumza
na waandishi wa habari leo akiwa ameambata na mama yake mzazi nyumbani
kwao Sinza Jijini Dar es Salaam, Wema amesema sababu kubwa ya kuhamia
CHADEMA ni ili kupata nafasi ya kupigania demokrasia anayodai kuwa
inapotea nchini Tanzania.
Sababu
nyingine aliyoieleza Wema ni kutelekezwa na CCM licha ya kujitolea
kutoa mchango wake kwa chama hicho wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa
mwaka 2015 kiasi cha kuwa hatarini kumwagiwa tindikali visiwani
Zanzibar.
"Kuanzia
sasa mimi siyo tena mwanachama wa CCM, na muda mfupi ujao nitachukua
kadi yangu ya CHADEMA... Nimeamua kuingia CHADEMA kwa sababu nataka
kupigania demokrasia, laiti ningejua, ningeingia zamani sana, najua
nimewahi kusema kuwa nitakufa nikiwa CCM, lakini sikujua kama itakuwa
hivi, laiti ningejua mapema basi nisingesema vile na ningejiunga CHADEMA
muda mrefu sana". Amesema Wema Sepetu
Amesisitiza
kuwa hajaamia CHADEMA kwa sababu ya pesa kama ambavo imekuwa ikidaiwa,
bali ni kwa ajili ya kupigania demokrasia, na kuweka wazi kuwa kuanzia
sasa ameingia kwenye mapambano ya kupigania demokrasia akiwa kwenye
chama ambacho anaamini kuwa ni chama peke chenye uwezo wa kurejesha
demokrasia inayopotea.
"Sijachukua
pesa yoyote kutoka CHADEMA, kama nimechukua hata shilingi 10,000 ya
CHADEMA basi kaburi la baba yangu huko Zanzibar litikisike" - Amesema Wema
Wema pia amejibu kuhusu baadhi ya wasanii kuidai CCm ambapo amesema "Ni kweli kuna madeni mengi wasanii tunaidai CCM, lakini kila wakati tukidai tunaambiwa tukamdai JK" - Wema Sepetu
Baada ya Wema kukabidhi kadi ya CCM, mama yake pia amerudisha kadi ya CCM na kusema "Tutatembea Tanzania nzima kuinadi CHADEMA". Kauli hiyo ilikuja baada ya mama huyo kueleza jinsi ambavyo CCM haikumtendea haki
Kuhusu sauti zilizosambazwa mitandani zikionesha Mama Wema akiongea na Steve Nyerere, mama Wema amesema "Kuhusu sauti zinazosemwa kuwa ni mimi na Steve Nyerere, siwezi kulizungumzia hilo maana sijazisikia"
==>Msikilize hapo chini akiongea
Alhamisi, 23 Februari 2017
Irene Uwoya kuwa mchungaji.....Atangaza kuanzisha kanisa
Msanii wa filamu Irene Uwoya amesema kuwa ana mpango wa kuwa Mchungaji pamoja na kumiliki kanisa lake yeye mwenyewe siku za usoni na kwamba anamuomba Mungu kila siku aweze kutimiza ndoto hizo.
Kauli
hii imetoka kinywani mwa msanii huyo pindi alipokuwa akijibu maswali
mubashara aliyokuwa anaulizwa na mashabiki zake kupitia katika ukurasa
wa Facebook wa EATV katika kipindi cha Kikaangoni
"Nina
ndoto ya kuwa mchungaji na kila siku huwa nina muomba Mungu
anifanikishie suala hilo niweze kutimiza japokuwa sasa hivi bado nipo
katika changamoto kubwa ila natumai ndoto zangu zitatimia. Natamani kuwa
pastor ambaye ni mwalimu, niwafundishe watu Mungu anataka nini, lakini
sitaki kuanzisha kanisa kama biashara, sitaki kucheza na Mungu, ndiyo
maana najipanga kwanza sitaki kukurupuka, nataka niwafundishe watu Mungu
anataka nini, na jinsi ya kumuomba Mungu". Alisema Uwoya
Uwoya
pia amefunguka na kueleza kuwa kazi yake ya sanaa huwa inamtesa kiimani
jambo ambalo linamfanya kila siku akiamka awe anatubu kwa ajili ya
mambo anayoyafanya akiwa katika kazi zake za uigizaji .
Amesema
katika tasnia ya uigizaji mara nyingi huwa wanaongea uongo na hata
mambo mengi wanayoyafanya kufikisha ujumbe huwa ni vitu ambavyo
havimpendezi Mungu.
"Mimi
nina hofu ya Mungu sana pia napenda kusali linapokuja suala la kazi
yangu ukweli naona kama inanisumbua imani yangu kwa sababu katika
uigizaji mambo mengi tunayoyafanya siyo ya kumpndeza Mungu lakini ndiyo
kazi sasa, kila siku asubuhi nikiamka huwa inabidi kumuomba msamaha
mungu wangu ndiyo niendelee na kazi". Amesema Irene Uwoya.
Kwa
waliotaka kujua kama Irene anatumia dawa za kulevya, amewajibu kuwa
hatumii dawa za kulevya na hajawahi kutumia kwa kuwa ni mkristo na dini
yake hairuhusu kutumia dawa za kulevya wala kushiriki katika ndoa za
jinsia moja lakini pombe anakunywa
"Situmii
dawa za kulevya lakini nakunywa bia, dini yangu haizuii kunywa, nina
uwezo wa kumaliza hata kreti nzima, hata mapadre kwenye dini yetu
wanakunywa, lakini hairuhusiwi kulewa"
Pia
amefunguka kuhusu mapenzi yake ya kuvaa nguo fupi, ambapo amesema
anapeda nguo fupi, kwa kuwa ana mzio 'allergy' na nguo ndefu, hivyo
hawezi kuvaa nguo ndefu.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)