ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 2 Septemba 2017

Mtokeo ya uchaguzi kenya yafutwa Uhuru kenyata asema Nitauheshimu uamuzi wa Mahakama

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema kuwa hakubaliani na uamuzi wa Mahakama ya Juu nchini humo ya kubatilisha uchaguzi wa urais uliopita na kuagiza kufanyika upya kwa uchaguzi lakini anaheshimu uamuzi huo wa mahakama.

Akizungumza na waandishi wa habari leo  kuhusu uamuzi huo wa Mahakama, Rais Kenyatta amesema kuwa Jubilee iko tayari kurejea kwenye uchaguzi kama Mahakama ilivyoamuru huku akiwataka Wakenya kudumisha amani.

“Wenzangu, amani… amani… amani. Mshike jirani yako mkono umwambie hii ni vita ya wale, sisi ni kitu kimoja. Sisi ni jamii ambayo inaitwa ‘Wakenya’ na hivyo ndivyo itakavyokuwa,” amesema Kenyatta.

“Na mimi namshukuru ndugu yangu hapa [Ruto] amesema yuko tayari kurudi uwanjani,” ameongeza.

Kenyatta amewataka Wakenya kujiandaa na uchaguzi mwingine na kwamba Jubilee wataingia tena barabarani ‘kupiga debe’ ili wachaguliwe tena.

Leo, Mahakama ya Juu iliamua kubatilisha uchaguzi wa Rais uliofanyika Agosti 8 mwaka huu ambao kwa mujibu wa Tume Huru ya Uchaguzi ya nchi hiyo, Kenyatta alishinda kwa zaidi ya asilimia 54 dhidi ya Raila Odinga (NASA) aliyepata asilimia 44.7.

Mahakama imeeleza kuwa kulikuwa na vitendo vya ukiukwaji wa sheria na katiba ya nchi hiyo uliopelekea uchaguzi huo kutofaa kuwa halali. Imeamuru uchaguzi huo kufanyika baada ya siku 60 (Novemba Mosi).

Magazeti ya Leo jumamosi ya tarehe 02/09/2017






















Alhamisi, 31 Agosti 2017

15,473 tu ndio waliokamilisha maombi Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu

 
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeongeza muda wa wanafunzi kuwasilisha maombi ya mikopo.

Hatua hiyo imeelezwa inalenga kutoa nafasi kwa wanafunzi walioshindwa kufuata masharti kuyakamilisha.

Mkurugenzi Mkuu wa bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru amesema muda huo umeongezwa hadi Septemba 11 badala ya Septemba 4.

"Tumesogeza mbele kwa siku saba zaidi ili walioshindwa kufuata vigezo wakati wa kujaza fomu wafanye hivyo," amesema.

Amesema hadi kufikia jana Agosti 29, wanafunzi waliojitokeza walikuwa 49,282 lakini ni 15,473 waliokamilisha maombi kwa njia ya mtandao. 
Aidha, Badru amewasisitiza waombaji wa mikopo kuzingatia mwongozo uliotolewa na Bodi unaowataka kuambatanisha nyaraka zote zilizothibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamimi (RITA), makamishina wa viapo, mawakili na serikali za mtaa na kuziwasilisha kwenye mtandao wa Bodi.
Maombi ya mikopo kwa mwaka wa masomo 2017/2018, yanayofanyika kwa njia ya mtandao olas.heslb.go.tz  yalifunguliwa Agosti 6, 2017.
Mpaka kufikia Agosti 29, 2017, maombi ya mkopo zaidi ya 50,000 yalikuwa yametumwa Bodi ya Mikopo kwa ajili ya uhakiki na baadaye kupangiwa mikopo kwa mwaka wa masomo 2017/2018.