ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Alhamisi, 10 Machi 2016

Wawekezaji wa Vietnam waalikwa

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewaalika wawekezaji kutoka Vietnam na kuwahakikishia kuwa Tanzania ni nchi inayoheshimu uwekezaji na kwamba Serikali imesaini mikataba mbalimbali ya kupinga kutaifisha mali za wawekezaji.
Majaliwa aliyasema hayo Dar es Salaam jana kwenye kongomano baina ya ujumbe wa Tanzania na Rais wa Vietnam, Truong Tan San aliyeongozana na ujumbe wake katika ziara ya siku nne nchini na wafanyabiashara wa Tanzania.
Waziri Majaliwa alisema Tanzania ni nchi yenye mazingira mazuri ya uwekezaji katika nyanja mbalimbali na kusisitiza kwamba wanaotaka kuwekeza nchini wanafurahia mazingira hayo na uwepo wa dhamana ya mitaji waliyowekeza.
“Ukiwekeza Tanzania una uhakika wa usalama wa mtaji na uwekezaji wako kwa sababu nchi imesaini mikataba mbalimbali ya kupinga utaifishaji mali za wawekezaji na kuhimiza uwekezaji wa kigeni katika mazingira salama na yenye amani,” alisema Majaliwa.
Alisema kila mara nchi imekuwa ikiboresha sheria na kuimarisha ushirikishwaji wa sekta binafsi ili kuchochea mazingira ya uwekezaji kwa lengo la kuimarisha uchumi na kuinua maisha ya wananchi wake.
Akizungumzia soko mara baada ya kuwekeza nchini, Waziri Majaliwa alisema, wawekezaji wanaowekeza nchini wana uhakika wa masoko ya zaidi ya watu milioni 300 waishio Mashariki na Kusini mwa Afrika, ambao hufurahia kuwepo kwa nchi katika Jumuiya kama ya SADC na EAC.
Aidha, nchi zaidi ya sita ambazo hazina bahari hutegemea bandari ya Tanzania kufanya biashara na masoko katika eneo hilo. Akizungumzia uwekezaji kutoka nje ya nchi, Waziri Majaliwa alisema serikali imekua ikiboresha mazingira ya uwekezaji na hiyo imeongeza uwekezaji kutoka nje.
Alisema mfano mzuri ni uwekezaji wa Kampuni ya Viettel Tanzania Ltd, ambao ni wawekezaji kutoka Vietnam

YASEMAVYO MAGAZETI TAR 10/03/2016Thursday, March 10, 2016 :

 Ndalichako: Vyeti Vya Form Six Vilivyo Katika Mfumo wa GPA Havitabadilishwa Kwenda Division 
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiX6Mpq_jhttge5s_qQ1IGLkZJQQ3rcc4-vMPf4F9RYAlyxZo0TfcZmhTh_qD0pydiPFlvxCDd7Ue7nDP44QYTPhiBB_JcGSDLRYSkKWBR4927_SkyXg6V8FF9VVhyphenhyphenqN8VvdRr46J63BgK5/s1600/ndalichako.jpg
Serikali imesema haina mpango wa kubadili vyeti vya wanafunzi waliomaliza kidato cha sita mwaka jana kutoka kwenye mfumo wa alama za GPA kwenda Divisheni.

Msimamo huo wa serikali, umetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako.
 
Amesema serikali haina mpango wa kubadili mfumo huo wa vyeti kwani tangu awali wanafunzi walisoma kwa mfumo wa GPA na vyeti vilitoka kwa mfumo huo.

“Hatuwezi kubadili vyeti hivyo, isipokuwa vimehitajika kwa ajili ya marekebisho madogo ambayo Katibu Mkuu wa Wizara, aliyasema lakini siyo kubadili kwenda mfumo wa divisheni,” alisema.

Februari mwaka huu, Baraza la Taifa la Mitihani (Necta), lilitangaza kusitishwa kwa ugawaji wa vyeti vya kidato cha sita kwa wanafunzi waliohitimu mwaka 2015, huku likiagiza kuwa vile vilivyokwisha gawanywa kwa wahitimu hao vinatakiwa kurejeshwa kwenye chombo hicho.

Hata hivyo, Katibu Mtendaji wa Necta, Dk, Charles Msonde, hakubainisha marekebisho ambayo wanatakiwa kuyafanya kwenye vyeti hivyo na badala yake kudai baraza linataka kujiridhisha na baadhi ya vitu.

Hatua hiyo ya kubadili vyeti hivyo iliibua utata mkubwa, huku baadhi ya wadau wakiwamo maofisa elimu, wakihisi Necta huenda inalenga kuvibadili vyeti hivyo kutoka kwenye mfumo wa wastani wa alama (GPA), kwenda kwenye ule wa jumla (division).

Atupwa Jela Miaka 7 kwa Kumkata Mkewe Sehemu za Siri Ili Apate Mali

Kikoti blog

Mkazi wa Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora, Mashaka Maziku (60) amehukumiwa kifungo cha miaka saba jela kwa kosa la kumkata sehemu za siri mkewe kwa imani za kishirikina ili apate mali.

Hakimu Joctan Rushwela alisema jana kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Tabora imeridhishwa na ushahidi uliotolewa upande wa mashtaka.

Hakimu Rushwela alisema anamhukumu mshtakiwa huyo kwenda jela ili iwe fundisho kwa wengine wanaokuwa na tamaa ya kujipatia mali kwa njia za kishirikina.

Awali wakili wa Serikali, Idd Mgeni alidai kuwa mshtakiwa huyo na mganga wa jadi, walitenda kosa hilo kati ya Oktoba 29 na Novemba 2, 2014 katika eneo la Kazaroho Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora.

Wakati wa tukio hilo, ilidaiwa kuwa Maziku aliambiwa na mganga huyo ambaye ni mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo, Kahele Paul kwamba akipeleka sehemu za siri za mkewe atapata Sh5milioni.

Alidai baada ya kupewa ushauri huo, alimchukua mkewe na kwenda kumnywesha pombe ili aweze kutimiza ukatili huo.

Alidai baada ya kunywa pombe nyingi, alichukua kisu na kumkata sehemu za siri mkewe na kuzihifadhi kwenye mfuko wa suruali yake na kutoweka. 
Alidai kwa mujibu wa mashahidi wanne, mwanamke huyo alikuwa akipiga kelele kutokana na maumivu makali aliyopata huku akivuja damu nyingi.

Jumamosi, 27 Februari 2016

AJIRA ZA WALIMU

            B1=Basic 419000
Cwt=8390.Pension=20950.Income=46090.Insur 12570
Take home 331000

C1=530000
Cwt 10600.Pension 26500.Income 58300.Insurance 15900
Take home=418700

D1=716000
Cwt 14320.Pension 35800.Income 78760.Insurance 21400
Take home= 565640

E1=940000
Cwt 18800.Pension 47000.Income 103400.Insurance 28200
Take home 742600

F1=1235000
Cwt 24700.Pension 61750.Income 135850.Insurance 37050
Take home 975650

Approved
TOA MAONI YAKO HAPA

Alhamisi, 18 Februari 2016

Jumamosi, 6 Februari 2016

India waomba radhi kwa Watanzania kudhalilishwa

Imeandikwa na Sifa Lubasi, Dodoma
Imechapishwa: 06 Februari 2016
SERIKALI ya India imeiomba radhi serikali ya Tanzania, kufuatia kudhalilishwa na kupigwa kwa wanafunzi wa Tanzania wanaosoma nchini humo.
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika, Kikanda na Uhusiano wa Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga, aliliambia Bunge, jana, mjini hapa, wakati akitoa taarifa ya serikali kuhusu hatua zilizochukuliwa serikali ya India kufuatia tukio hilo.
Alisema tayari serikali ya India, imewachukulia hatua wote waliohusika na tukio hilo na wamefikishwa mahakamani.
Balozi Mahiga alisema serikali ya India, imeagiza kuwa wanafunzi wa Watanzania wapewe ulinzi maalumu kwenye maeneo wanakoishi na wasindikizwe wanapokwenda masomoni.
Aidha alisema serikali ya India ilimtaka balozi wa Tanzania afuatane na maofisa waandamizi, wa Wizara ya Mambo ya Nje ya India kwenda Bangalore ili kukutana na wanafunzi wa Tanzania na wengine wa Afrika kufanya mikutano na wanafunzi hao.
Balozi Mahiga alisema tukio hilo lilitokea baada ya uendeshaji mbaya wa gari uliofanywa na mwanafunzi kutoka Sudan ambaye aligonga pikipiki tatu na baada ya hapo kumgonga mama wa kihindi aliyekufa papo hapo.
Alisema baada ya tukio hilo, mwanafunzi huyo alikimbia na wananchi waliokuwa jirani walichoma gari lake moto na kwamba baada ya muda lilitokea gari lingine likiwa na wanafunzi wanne Watanzania akiwemo msichana mmoja.
Balozi Mahiga alisema wananchi hao walilisimamisha gari hilo na kuwatoa nje wanafunzi hao ambapo mwanafunzi wa kike alivuliwa nguo na kutembezwa mitaani uchi, huku wanaume wakipigwa sehemu mbalimbali za miili yao na gari lao lilichomwa moto.
“Katika gari hilo kulikuwa na simu zao na document (nyaraka) mbalimbali ambazo ziliteketea,” alisema.
Alisema baada ya muda, polisi walifika lakini walishindwa kutoa ushirikiano ingawa waliwachukuwa na kuwapeleka hospitali. Balozi Mahiga alisema, “Kule hospitali walionekana wana majeraha makubwa, walitibiwa lakini ikabidi waondoke kwa sababu walikuwa hawana fedha za kutosha za kugharamia matibabu”.
Alisema baada ya hapo, Balozi wa Tanzania aliyeko India aliandika dokezo la kidiplomasia kwa serikali ya India kulaani kitendo hicho na kuitaka serikali ya India, ichukue hatua za kisheria na za haraka katika kupeleleza tukio hilo.