ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatano, 25 Mei 2016

Serikali kurejea viwango vya chakula shuleni

Imeandikwa na Theopista Nsanzugwanko, Dodoma
SERIKALI imesema inaendelea kufanya rejeo ya viwango vya chakula shuleni ili kuwezesha wanafunzi wa kidato cha tano na sita kupata elimu bora pamoja na lishe bora.
Aidha imesema serikali imeanza kuwekea miundombinu shule kongwe za kitaifa za kidato cha tano na sita.
Waziri wa Nchi katika ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jaffo alisema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftaha Nachuma (CUF) aliyetaka kujua mpango wa serikali katika kuhakikisha wanatatua matatizo ya shule za sekondari za kidato cha tano na sita, ikiwemo kupata chakula kisicho na matatizo.
Akijibu swali hilo, Jaffo alisema kwa kutambua changamoto hizo hasa ya chakula serikali inafanya marejeo ya posho kwa kila shule ili kuboresha kiwango cha elimu, ikiwa ni pamoja na shule kongwe kuwekewa miundombinu ya kuwapatia lishe bora.

Hakuna maoni: