ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 27 Juni 2016

Madiwani Mwanza wapitisha mpango kabambe wa jiji


Imeandikwa na Mwandishi Wetu, Mwanza

MADIWANI wa Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela wamepitisha Mpango Kabambe wa Jiji la Mwanza.
Mpango huo utahakikisha jiji na manispaa, zimepangwa kisasa kuondoa migogoro na kuongeza kasi ya ukuaji wa kiuchumi.
Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano wa wadau wa mpango huo hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela alisema kuwa rasimu ya mpango huo, inahusisha mikakati na mapendekezo kutoka sekta tatu za maendeleo ya mji ambazo ni matumizi ya ardhi, usafirishaji na miundombinu.
“Huu ni mkutano wa sita wa mapendekezo ya rasimu ya mpango kabambe wa jiji la Mwanza na wa mwisho ili kuwa mpango kamili utakaotumika katika jiji la Mwanza kama sheria,” alisema Mongela.
Mongela alisema mpango huo wa kina wa matumizi ya ardhi, utatumiwa kama kichocheo cha kujumuisha ardhi inayohitajika kwa mapendekezo ya maendeleo mbalimbali katika sekta za usafirishaji na miundombinu.

Hakuna maoni: