Ndalichako: Vyeti Vya Form Six Vilivyo Katika Mfumo wa GPA Havitabadilishwa Kwenda Division 
 
  

Serikali
 imesema haina mpango wa kubadili vyeti vya wanafunzi waliomaliza kidato
 cha sita mwaka jana kutoka kwenye mfumo wa alama za GPA kwenda 
Divisheni.
Msimamo huo wa serikali, umetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako.
Amesema
 serikali haina mpango wa kubadili mfumo huo wa vyeti kwani tangu awali 
wanafunzi walisoma kwa mfumo wa GPA na vyeti vilitoka kwa mfumo huo.
“Hatuwezi
 kubadili vyeti hivyo, isipokuwa vimehitajika kwa ajili ya marekebisho 
madogo ambayo Katibu Mkuu wa Wizara, aliyasema lakini siyo kubadili 
kwenda mfumo wa divisheni,” alisema.
Februari
 mwaka huu, Baraza la Taifa la Mitihani (Necta), lilitangaza kusitishwa 
kwa ugawaji wa vyeti vya kidato cha sita kwa wanafunzi waliohitimu mwaka
 2015, huku likiagiza kuwa vile vilivyokwisha gawanywa kwa wahitimu hao 
vinatakiwa kurejeshwa kwenye chombo hicho.
Hata
 hivyo, Katibu Mtendaji wa Necta, Dk, Charles Msonde, hakubainisha 
marekebisho ambayo wanatakiwa kuyafanya kwenye vyeti hivyo na badala 
yake kudai baraza linataka kujiridhisha na baadhi ya vitu.
Hatua
 hiyo ya kubadili vyeti hivyo iliibua utata mkubwa, huku baadhi ya wadau
 wakiwamo maofisa elimu, wakihisi Necta huenda inalenga kuvibadili vyeti
 hivyo kutoka kwenye mfumo wa wastani wa alama (GPA), kwenda kwenye ule 
wa jumla (division).
Atupwa Jela Miaka 7 kwa Kumkata Mkewe Sehemu za Siri Ili Apate Mali
Kikoti blog
Mkazi
 wa Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora, Mashaka Maziku (60) amehukumiwa
 kifungo cha miaka saba jela kwa kosa la kumkata sehemu za siri mkewe 
kwa imani za kishirikina ili apate mali.
Hakimu
 Joctan Rushwela alisema jana kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa 
Tabora imeridhishwa na ushahidi uliotolewa upande wa mashtaka.
Hakimu
 Rushwela alisema anamhukumu mshtakiwa huyo kwenda jela ili iwe fundisho
 kwa wengine wanaokuwa na tamaa ya kujipatia mali kwa njia za 
kishirikina.
Awali
 wakili wa Serikali, Idd Mgeni alidai kuwa mshtakiwa huyo na mganga wa 
jadi, walitenda kosa hilo kati ya Oktoba 29 na Novemba 2, 2014 katika 
eneo la Kazaroho Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora.
Wakati
 wa tukio hilo, ilidaiwa kuwa Maziku aliambiwa na mganga huyo ambaye ni 
mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo, Kahele Paul kwamba akipeleka sehemu 
za siri za mkewe atapata Sh5milioni.
Alidai baada ya kupewa ushauri huo, alimchukua mkewe na kwenda kumnywesha pombe ili aweze kutimiza ukatili huo.
Alidai
 baada ya kunywa pombe nyingi, alichukua kisu na kumkata sehemu za siri 
mkewe na kuzihifadhi kwenye mfuko wa suruali yake na kutoweka. 
Alidai
 kwa mujibu wa mashahidi wanne, mwanamke huyo alikuwa akipiga kelele 
kutokana na maumivu makali aliyopata huku akivuja damu nyingi.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni