ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatatu, 21 Machi 2016

walimu wapya kwa mwaka 2016 wapewa mtihani na TAMISEMI

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEic6vbqzF0JJL9QfkTbpK_Xwtwpaf65r_pwIRgw2HphXih_46gKNnnFwdW-GQ79r8JjAPMg9jxEAQwEO9wWuJ91v8ipEE0qGVv9-I1qB2-7UKtKu3JHpAGUl0BJbXMhyqZuhNmNddjVr4Hf/s1600/1350.jpg
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, George Simbachawene ametangaza leo March 21, 2016 kuwashughulikia wale wote wanaofanya hujuma katika sekta ya elimu nchini, wakiwemo Walimu wanaokimbia sehemu zao za kazi hususani vijijini na kukimbilia mijini.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari leo March 21, 2016 alisema…‘Katika eneo la upangaji wa Walimu ni tatizo kubwa na nadiliki kusema hadharani kwamba upangaji wa walimu kwenye  shule zetu ni wa ovyo leo hii tunaupungufu wa ualimu kwenye vijiji kwa  asilimia zaidi ya 40%  na ongezeko  la walimu mijini ni kama asilimia 50%  kwa   maana ya kwamba walimu wengi wapo Dar es Salaam, walimu wengi wapo kwenye miji mikubwa makao makuu ya mikoa na makao makuu ya wilaya’George Simbachawene
‘Hata wanawake wanasema wanafuata wanaume zao huko ni  kukosa uzalendo kama ulikubali kuajiliwa lazima ukubali kufanya kazi mahala popote pale na watanzania ni wote mpaka waliopo kule vijijini haiwezekani kukubali kazi mjini na kukataa kijijini’George Simbachawene
kwa tafsiri hii ya waziri wa TAMISEM hakutokuwa na sababu zzisizona msingi zitakazokubalika kwa walimu wapya kwa mwaka 2016

Hakuna maoni: