
Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, George Simbachawene ametangaza leo 
March 21, 2016 kuwashughulikia wale wote wanaofanya hujuma katika sekta 
ya elimu nchini, wakiwemo Walimu wanaokimbia sehemu zao za kazi hususani
 vijijini na kukimbilia mijini.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari leo March 21, 2016 alisema…‘Katika
 eneo la upangaji wa Walimu ni tatizo kubwa na nadiliki kusema hadharani
 kwamba upangaji wa walimu kwenye  shule zetu ni wa ovyo leo hii 
tunaupungufu wa ualimu kwenye vijiji kwa  asilimia zaidi ya 40%  na 
ongezeko  la walimu mijini ni kama asilimia 50%  kwa   maana ya kwamba 
walimu wengi wapo Dar es Salaam, walimu wengi wapo kwenye miji mikubwa 
makao makuu ya mikoa na makao makuu ya wilaya’ – George Simbachawene
‘Hata 
wanawake wanasema wanafuata wanaume zao huko ni  kukosa uzalendo kama 
ulikubali kuajiliwa lazima ukubali kufanya kazi mahala popote pale na 
watanzania ni wote mpaka waliopo kule vijijini haiwezekani kukubali kazi
 mjini na kukataa kijijini’ – George Simbachawene
kwa tafsiri hii ya waziri wa TAMISEM hakutokuwa na sababu zzisizona msingi zitakazokubalika kwa walimu wapya kwa mwaka 2016 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni