ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumapili, 20 Machi 2016

Dr Shein aongoza wazanzibar katika kupiga kura, Uchaguzi wa Marudio Zanzibar

Wananchi wa Zanzibar leo wanapiga kura katika uchanguzi wa marudio baada ya kufutwa kwa uchanguzi uliofanyika October 25,2025 kutokana na kasoro zilizojitokeza.

Katika baadhi ya vituo wananchi wamejitokeza na zoezi linaendelea vizuri huku hali ya usalama ikiwa imeimarishwa.

Katika kituo cha shule ya sekondari Muembeladu ambayo ina vituo sita,vituo vitano vinawatu 350 na kituo kimoja kina watu 91. Akizungumza na wanahabari, msimamizi wa kituo hicho amesema zoezi la upigaji kura linaendelea vizuri katika jimbo la Jangombe .

Kwa upande wa kituo cha skuli ya Muembeshauri nako hali ni shwari na zoezi linaendelea vizuri ambapo katika skul hiyo vituo 11 vinatumika watu kupiga kura.
Katika Jimbo la kikwajuni, zoezi  linaendelea vizuri huku mwitikio wa watu ukiwa ni mkubwa.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kupiga kura wamesema zoezi hilo limekua rahisi na la  amani tofauti na taarifa zilivyokua zinasambazwa.

Mkazi wa Muembeshauri aliyejitambulisha kwa jina la Hamidu Salum Haji ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kwani zoezi la kupiga kura linaendelea kwa amani na utulivu.

Ndugu zangu tusikubali kugombanishwa na watu ambao hawaitakii mema Zanzibar tusimame pamoja katika kutetea nchi yetu” amesema Haji
 
Wakati zoezi hilo linaendelea maduka mengi yamefunguliwa na wafanyabiashara wanaendelea na kazi kama kawaida
Rais wa Zanzibara na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Ali Mohammed Shein leo amepiga kura katika kituo cha skuli ya bungi
5607497e-aa8a-46b6-9e65-24e5da213e24
9c703d6a-0f99-42ea-a17d-935d411e8f87
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, amepiga kura katika kituo cha skuli ya Kiembe samaki
36086a57-dbef-464f-8d12-ae3b207940ab


Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar Dkt Ali Mohammed alizungumza na wanahabari baada ya kupiga kura yake katika kituo cha Bungi, Kibera kisiwani Unguja  ambapo alisema anaamini atashinda kwa kishindo na kuhusu kushindwa  alisema tusubiri matokeo ya uchaguzi ndiyo yataamua.
"Nimepata nafasi ya kupiga kura kama haki yangu ya  kimsingi na kumekuwa na utulivu mkubwa kwenye zoezi hili,hali ya ulinzi imeimarishwa. 
"Matumaini yangu ni kushinda kwa kishindo, kuhusu kushindwa ndugu muandishi tusubiri matokeo ndiyo yataamua".Alisema Dkt. Ali Mohammed Shein

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd amepiga kura katika kituo cha skuli ya Kitope
46bee29d-6ade-49ea-9377-a3a692b33b12
670502cb-700e-47f1-b9e9-fa44bea0f2db

Hakuna maoni: