ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatano, 13 Aprili 2016

matokeo kati ya yanga na mwaadui

Yanga 2 mwadui1
Azam 1 mtibwa 0

Mrema akumbushia tena ahadi ya kupewa kazi na rais

Image result for agustino mrema
Mwenyekiti wa TLP taifa Dkt. Augustino Lyatonga Mrema amesisistiza ombi lake la kazi kwa kumkumbusha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwamba ampe kazi yoyote amsaidie kibarua kigumu alichonacho cha kuwahudumia wananchi

Dkt. Mrema ameyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na EATV kuhusu miaka 32 ya kifo cha aliyekuwa waziri mkuu wa Tanzania Edward Moringe Sokoine ambaye alihudumu kwenye awamu ya kwanza ya Mwl. Julius Nyerere ambapo alifariki akiwa na cheo cha waziri mkuu tarehe 12.04.1984 kwa ajali ya gari.

''Namkumbuka Sokoine kama mtu wa watu aliyehudumia watu, aliyepambana na ufisadi na magendo .Alikuwa anatenda haki kwa wananchi wote .

"Hata mimi nilipokuwa waziri wa mambo ya ndani na naibu waziri mkuu nilijaribu kufanya kama yeye bahati mbaya sikufanikiwa kama yeye kwa sababu sikuwa waziri mkuu au Rais''- Alisisistiza Mrema.

Kuhusu Mrema kuomba kazi kwa Dkt. Magufuli 
Mrema alisema kwa kutambua rekodi yake ya utendaji kazi wa  Rais Dkt. Magufuli, aliwahimiza wananchi wa Vunjo wamchague kipindi cha kampeni na yeye akampigia kampeni na Rais akawaambia wananchi wa Vunjo kwamba Mrema akikosa ubunge atapangiwa kazi nyingine ndiyo hiyo wananchi wanaulizia.

Aidha Mrema alisema kuna maeneo ambayo yeye anafiti siyo lazima apewe madaraka makubwa 

"Mimi sihitaji ukuu wa mkoa au uwaziri, anipe kazi yoyote na nikionana naye nitamkonyeza maeneo ambayo ninafiti ili nimsaidie kutumbua majipu." Alisema Mrema

Hata hivyo Dkt. Mrema alimpongeza Dkt. Magufuli kwamba ni mtendaji ambaye ameamua bila kusukumwa kupambana na mafisadi na kwamba yeye ni alfa na omega na kazi hiyo ameonyesha kwamba atafanya vizuri kuliko Sokoine na Mrema.

DC, DED Kishapu wamruka Anne Kilango kwa JPM

 Siku moja baada ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango kuvuliwa uongozi kwa kutosema ukweli, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Hawa Ng’humbi ameiruka taarifa ya kutokuwapo kwa watumishi hewa, ambayo amesema ilimshtua alipoiona kwenye televisheni. 
Mkoa wa Shinyanga unaundwa na wilaya tatu ambazo ni Shinyanga, Kishapu na Kahama zinazoundwa na halmashauri sita ambazo ni Kishapu, Manispaa ya Shinyanga, Mji wa Kahama, Ushetu, Msalala na Shinyanga Vijijini. 
Rais John Magufuli juzi alitengua uteuzi wa Kilango, ikiwa ni siku 30 tangu alipotangaza kumteua kwa maelezo kuwa alitoa taarifa isiyo ya kweli kuwa Shinyanga hakuna watumishi hewa kabla ya kujiridhisha.
 Pamoja na Kilango, Rais Magufuli pia alitengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Shinyanga, Abdul Dachi, kwa sababu hiyo ya kutoa taarifa za uongo.
 Dk Magufuli alichukua uamuzi huo baada ya kutuma timu mkoani Shinyanga kufanya uhakiki na kubaini kuwa kulikuwa na watumishi hewa 45 katika wilaya moja ya Shinyanga kabla ya kwenda wilaya nyingine za Kahama na Kishapu. 
Akizungumzia sakata hilo jana baada ya uamuzi wa Dk Magufuli, Ng’humbi alisema taarifa za kukosekana watumishi hewa kwenye wilaya yake alizisikia kwenye taarifa ya habari ya televisheni Machi 30 na zilimshtua.
 “Binafsi nilishtuka sana nilipoona ikitangazwa kuwa mkoa mzima wa Shinyanga, hakuna mfanyakazi hewa wakati mimi sikuwa hata nimeona taarifa kutoka wilayani kwangu iliyoandaliwa na uongozi wa halmashauri,” alisema Ng’humbi. 
“Nilijiuliza taarifa imefikaje kwa mkuu wa mkoa bila kupitia kwangu? Kusema kweli nilianza kuifanyia kazi taarifa hiyo na ninatarajia ifikapo Ijumaa nitakamilisha kazi hiyo.” 
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Alphonce Gagambobyaki alisema hadi sasa ofisi yake haijafahamu nani aliyempa mkuu wa mkoa taarifa ya ukaguzi wa wafanyakazi hewa kwa sababu taarifa aliyonayo mezani haijasainiwa.
 “Kuna tatizo la ofisi hii kukaimiwa na zaidi ya watu wanne tangu aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji, Dalikunda Kimulika alipostaafu Februari. Ni vigumu kujua nani alihusika nayo bila kuona saini,” alisema Bagambobyaki. 

Alisema taarifa hiyo inaonekana haikusainiwa kutokana na hofu baada ya watumishi waliobainika kutokuwapo kwenye vituo vyao vya kazi karibu wote kuonekana kuwa na ruhusa maalumu.
“Wakati bado tunajiridhisha kujua ni ruhusa ya aina gani na hawa watumishi wako wapi, ndipo taarifa ilipotangazwa kwamba mkoa hauna watumishi hewa,” alisema.

Hata hivyo, alisema anaamini taarifa sahihi itajulikana baada ya timu maalumu iliyotoka Tamisemi kukamilisha uhakiki wilayani humo jana. 
“Timu ile ya Tamisemi imekwenda mbele zaidi katika uhakiki wake kwa kukagua mtumishi mmoja mmoja hadi vijijini na imekamilisha kazi yake jana,” alisema Bagambobyaki. 

Kuhusu iwapo aliyekuwa mkuu wa mkoa alitumia taarifa zao au la? kaimu mkurugenzi huyo alisema: “Iwapo RC alitumia taarifa zetu au la, hilo siwezi kulisemea kwa sasa.”
Kilango ambaye juzi alisema hakuwa amepata taarifa hivyo asingeweza kuzungumzia kutenguliwa kwake, jana alisema hawezi kuzungumzia suala hilo kabisa na Dachi akaeleza kuwa ameupokea uamuzi huo kwa kuwa Rais ndiye mteule wake. 
Taarifa ya kutenguliwa kwa watumishi hao wa umma sasa imekuwa kaa la moto kwa wakuu wa wilaya makatibu tawala wao, na wakurugenzi watendaji wa halmashauri za mkoa huo.
Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo za watumishi hewa, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro alisema hawezi kuzungumzia lolote.
“Sisemi lolote na wala sizungumziii mkoa,” alisema na kukata simu ambayo haikupokewa tena. 

Kama ilivyokuwa kwa mkuu wake wa wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Shinyanga, Lewis Kalinjuna aligoma kuzungumzia uwezekano wa halmashauri yake kutoa taarifa zilizompotosha Kilango.
“Sitaki kulizungumzia hilo, nawaachia wanaolijua walizungumzie,” alisema Kalinjuna.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Vita Kawawa alikata simu yake mara kadhaa alipopigiwa na baadaye kutuma ujumbe mfupi wa maneno akisema yuko kwenye kikao na kuelekeza atumiwe ujumbe ambao hata alipotumiwa hakujibu.

Rais Magufuli aongoza mamia kumuaga mbunge mstaafu

Imeandikwa na Mwandishi Wetu RAIS John Magufuli ameungana na mamia ya waombolezaji kuaga mwili wa Mbunge mstaafu wa Mkoa wa Singida, Marehemu Christina Lissu Mughwai katika ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es Salaam.
Mughwai aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida katika kipindi cha kuanzia mwaka 2010 hadi 2015, aliagwa jana kabla ya kusafirishwa kwenda kijiji cha Mahambe mkoani Singida kwa maziko.
Pamoja na Rais Magufuli na mkewe Mama Janeth, viongozi wengine waliohudhuria shughuli ya kuaga ni Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bunge, Freeman Mbowe.
Akitoa salamu kwa niaba ya Rais Magufuli, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene aliwapa pole familia ya marehemu. Alisema katika kipindi chake cha ubunge, Mughwai alitoa mchango mkubwa kama mbunge na kama mtaalamu wa Uchumi.

Kutenguliwa Anne Kilango kwaendelea kuwa gumzo

KUTENGULIWA kwa uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela kumeendelea kuwa gumzo huku viongozi wengine wakiambiwa wawe macho kwa kuchukulia uamuzi huo wa Rais Magufuli, kama funzo la kutambua aina ya uongozi anaoutaka katika Serikali yake ya Awamu ya Tano.
Wakati viongozi hususani wa kuteuliwa wakitakiwa kuzingatia ukweli kwamba serikali ya awamu hii haihitaji wanaoficha mabaya wakitaka mazuri ndiyo yaonekane, baadhi wameshauri mfumo uliopo, hususani wa kupeana taarifa uangaliwe kwa kuwa una tatizo linalohitaji kufanyiwa kazi.
Miongoni mwa watu ambao gazeti hili lilizungumza nao jana kuhusu hatua hiyo ya Rais kutengua uteuzi wa Kilango, ni mwanasiasa mkongwe nchini, Paul Kimiti aliyetaka viongozi wengine kutambua kwamba, Magufuli ni kiongozi asiyependa unafiki.
“Uongozi wake tangu mwanzo umejidhihirisha wazi kuwa ni kiongozi anayependa uwazi na ukweli hataki short cut (njia za mkato),” alisema Kimiti. Kimiti aliyewahi kushika uwaziri katika Serikali zilizopita, alisema hatua hiyo ya Rais ni ishara na funzo kwa viongozi wengine hasa wale walio madarakani kuhakikisha kuwa wanawajibika ipasavyo kwa kufuata misingi ya uwazi na kutokimbilia njia za mkato.
Alisema kwa hali ilivyo, ni vyema viongozi waliopo wakaanza kufuata heshima na taratibu za kiongozi aliyewaweka madarakani, hali ambayo itawasaidia kutowajibishwa.
Mwanasiasa huyo ambaye alionesha kuguswa kwa mtazamo chanya na hatua anazochukua Rais, alisema kumekuwa na utaratibu wa watendaji kutoa taarifa zisizo sahihi na zisizo kamili kwa wakuu wao wa kazi kwa lengo la kuonesha kuwa mambo ni mazuri.
Alisema jambo hilo ni tatizo kubwa linalopaswa kukemewa. Utendaji wa kujikomba “Hii ni kero kubwa, watendaji wengi wanaficha taarifa za ukweli kwa wakuu wao ili kuonesha mambo ni mazuri, hili ni jambo baya kabisa kwani matokeo yake ndiyo haya; anakuja kuwajibishwa mtu mwingine ambaye huenda hakuhusika na taarifa hizo,” alisisitiza.
Alisema utendaji wa aina hiyo ni sawa na utendaji wa kujikomba ambao hauna tija, kwani pamoja na kuficha ukweli na uhalisia wa mambo, mwisho wake siku wananchi ndio waathirika na baadaye ukweli hufichuka.
Mhadhiri wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Haji Semboja alisema kilichotokea ni funzo kubwa kwa viongozi wengine kuhakikisha kuwa kila taarifa wanayopatiwa lazima wanaifanyia kazi na kujiridhisha kabla ya kuitoa kwa umma.
“Mama Kilango kwa vyovyote vile bado ndio alikuwa anaanza kazi ya ukuu wa mkoa, hivyo lazima atakuwa amepatiwa taarifa aliyoitoa kwa umma na watendaji wake. Hii ilikuwa ni kawaida, viongozi wengi huuamini mfumo unaowapatia taarifa,” alisema Semboja.
Hata hivyo, alisema kiongozi huyo alipaswa baada ya kupatiwa taarifa ya awali, angewasiliana na vyanzo mbalimbali kupata uhakika kwa kutumia madaraka aliyonayo wakiwemo waajiri na wanaofanya malipo kujiridhisha.
Alisema anaamini hatua aliyoichukua Dk Magufuli ni ishara na njia yake ya kutambulisha kwa umma mtindo wa uongozi unaozingatia uwazi na uwajibikaji. “Hiki kwetu ni kitu kipya hatujakizoea, lakini sasa ni vyema kila kiongozi awe makini na kutambua kuwa akikosea lazima awajibike,” alisisitiza.
Mfumo uangaliwe
Pamoja na hayo, alimuomba Rais Magufuli awe mvumilivu na atambue kuwa huenda tatizo kubwa bado lipo kwenye mfumo uliopo wa kupeana taarifa ambao utahitaji kuangaliwa kwa umakini na kuchukuliwa hatua stahiki.
Alisema Dk Magufuli ni kiongozi anayefuata mfumo wa kisheria na kwamba hatua zote alizochukua zinatokana na nia njema aliyonayo kwa watanzania. “Huyu ni mtakatifu baada ya Mungu, ana moyo mzuri na nia njema kwa watanzania,” alisema Profesa Semboja.
Akizungumzia watumishi hewa, Profesa Semboja alishauri baada ya operesheni ya kuwatafuta upande wa rasilimali watu ndani ya utumishi wa umma lazima utoe taarifa nzima na kufafanua kilichotokea.
Kwa upande wa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana, alisema hatua aliyoichukua Dk Magufuli ya kumvua uongozi Kilango ni ishara kuwa anatoa kipaumbele katika suala zima la uwajibikaji lakini pia hapendi viongozi wasiojishughulisha.
“Inaonesha dhahiri Dk Magufuli katika masuala nyeti yanayogusa taifa hapendi majibu mepesi wala njia za mkato. Hii inamaanisha kuwa viongozi hawana budi kuzifanyia kazi taarifa wanazopewa na kujiridhisha kwanza,” alisema Dk Bana.
Awali gazeti hili lilizungumza na Kilango kwa njia ya simu ili kuweza kupata upande wake kuhusu nini kilitokea na kusababisha kutoa taarifa hiyo isiyo sahihi kuhusu watumishi hewa mkoani Shinyanga, ambapo mara baada ya salamu, mwandishi alipojitambulisha alikata simu.
Juzi Rais Magufuli alitengua uteuzi wa mkuu huyo wa mkoa baada kutoa taarifa za uongo kwenye vyombo vya habari kuwa mkoani kwake hakuna watumishi hewa. Alisema baada ya taarifa hiyo, aliunda timu maalumu kwa ajili ya uhakiki wa watumishi hewa mkoani humo na ndani ya siku moja, walibaini kuwepo kwa watumishi hewa 45 waliokuwa tayari wamelipwa mishahara yenye gharama ya Sh milioni 339.9.

Mkataba wa Lugumi wawa kaa la moto

Imeandikwa na Mwandishi Wetu(Habari leo) BUNGE limetoa siku tatu kwa Jeshi la Polisi kuwasilisha kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) mkataba wa Kampuni Lugumi Enterprises wenye thamani ya Sh bilioni 37.
Hatua hii inakuja siku mbili baada ya jeshi hilo kudaiwa kukaidi agizo la kamati hiyo, iliyotaka likabidhi nyaraka za utekelezaji wa mkataba ufanyiwe tathmini kutokana na malalamiko yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali(CAG) katika hesabu za mwaka 2013/2014.
Akizungumza jana na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Aeshi Hilaly alisema agizo la kamati la kutaka mkataba huo, lilitolewa wiki iliyopita kuwezesha wabunge kuangalia utekelezaji wake.
“Jana (juzi) ilikuwa siku ya mwisho kwa jeshi kuwasilisha mkataba huo ofisi za Bunge, lakini mpaka leo (jana) muda huu ninapozungumza nanyi (saa 7:30 mchana) walikuwa hawajawasilisha. “
Siku zote tumekuwa tukitoa maagizo kwa mdomo na taasisi nyingi zimekuwa zikitekeleza, lakini hili la mkataba wa Lugumi naona kwa wenzetu limekuwa gumu, hivyo tumeamua kuwakumbusha kwa maandishi,” alisema.
Alisema kamati hiyo imetoa siku tatu tangu barua itakapopelekwa na ofisi za Bunge, kuhakikisha wanatekeleza agizo hilo ili kamati hiyo iweze kupitia utekelezaji wa mkataba huo na baadaye kupeleka mapendekezo kwenye Bunge.
“ Katika suala hili, Kamati haitarudi nyuma, hivyo tunawaomba wenzetu wa Jeshi la Polisi kutupa ushirikiano, si jambo la peke yangu kuamua, ni la Bunge, baada ya kupitia tunapeleka mapendekezo bungeni ambalo ndilo litakaloamua nini kifanyike,” alisisitiza.
Hata hivyo, habari zilizofikia HabariLeo jana zinasema jeshi hilo lilipeleka mkataba huo katika Kamati ya Mambo ya Nje na Usalama na juzi badala ya Kamati ya PAC iliyoagiza. “Kuna taarifa kuwa mkataba huo umepelekwa kwenye kamati ya Mambo ya Nje inayoongozwa na Mbunge wa Muheza, Balozi Adadi Rajabu,” kilisema chanzo chetu.
Hata hivyo, Adadi aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) alikanusha madai hayo kwa kujibu kifupi kwa ujumbe wa simu kuwa, “suala hilo limepelekwa PAC.” Kamati ya PAC ilipokuwa ikipitia hesabu za Jeshi la Polisi, ilibaini kuwapo mkataba tata wa Kampuni ya Lugumi Enterprises .
Kupitia mkataba huo wa mwaka 2011, Kampuni ya Lugumi Enterprises ilipewa zabuni ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya polisi 108 nchini kwa gharama ya Sh bilioni 37.
Inasadikiwa kampuni hiyo imekwishalipwa Sh bilioni 34 kati ya Sh bilioni 37 ikiwa ni sawa na asilimia 99 ya fedha zote, huku ikiwa imefunga mashine katika vituo 14 pekee katika jiji la Dar es Salaam, ambavyo pia inadaiwa havijulikani maeneo vilipo.

Magazeti ya Leo jumatano tarehe 13/04/2016

Headline za magazeti ya Leo zinaletwa kwenu Kwa hisani  ya New Mwalimu education centre inayopatikana eneo la ilula madizini _iringa Tanzania majengo ya kanisa catholic kigango cha madizini madizini