ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumapili, 17 Aprili 2016

Magazeti ya Leo jumapili ya tarehe 17/04/2016


Magazeti ya Leo yanaletwa kwenu  kwa hisani ya New mwalimu education centre ambao wanaofundisha tuition kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita wa masomo ya Jioni kuanzia SAA Tisa mpaka SAA moja mahali ni ilula madizini majengo ya kanisa katoliki kigango cha madizini karibuni sana








Jumamosi, 16 Aprili 2016

Magazeti ya Leo jumamosi ya tarehe 16/04/2016

Magazeti ya Leo yanaletwa kwenu Kwa hisani ya kikoti m Pesa ambao wanatoa huduma mbalimbali za kibiashara kama huduma ya mpesa  , tigo pesa , wanauza vocha za mitandao yote ya simu pia wanauza vifaa vya shuleni na ofisini Kwa bei rahisi nyote mnakaribishwa
Pia kikoti company inakituo cha tuition kinachojulikana kama New Mwalimu Education Centre kinachofundisha masomo ya ziada kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita kwa masomo yote Muda ni kuanzia saa kumi mpaka saa moja jioni  Eneo in majengo ya roman Catholic kigango cha madizini .Njoo upate elimu bora














Ijumaa, 15 Aprili 2016

Tatizo la maji katika mji mdogo wa ilula laendelea kufanyiwa kazi na mbunge kilolo





MBUNGE wa Jimbo la Kilolo, Venance Mwamoto ameiomba serikali kutumia maji ya mto Ruaha Mdogo kumaliza tatizo la muda mrefu la maji linaloukabili mji mdogo wa Ilula, wilayani Kilolo mkoani Iringa wenye wakazi zaidi ya 38,000.

Mto huo unaopita mjini Iringa ukijazwa na vyanzo mbalimbali vidogo vya maji vikiwemo vya wilayani Kilolo, upo zaidi ya kilomita 30 kutoka mji huo wa Ilula wenye kata tatu za Lugalo, Nyalumbu na Ilula yenyewe.

Mwamoto alitoa ombi hilo  wakati  Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Iringa Mjini (IRUWASA) ikikabidhi kwa Mamlaka  ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira ya Mji Mdogo Ilula, mradi mdogo wa maji yanayotumiwa na mji huo toka chanzo cha mto Idemle baada ya kusimamia ukarabati wake uliogharimu Sh Milioni 903.

“Ufumbuzi wa tatizo la maji katika mji mdogo wa Ilula ni kutumia maji ya Mto Ruaha Mdogo badala ya pendekezo la kutumia chanzo cha Mgombezi ambalo gharama zake ni kubwa,” Mwamoto alisema.

Alisema endapo serikali itaendelea na mpango wa kutumia chanzo cha Mgombezi wananchi wa Ilula wasitegemee kupata maji ndani ya kipindi kifupi kijacho.

“Kama tutang’ang’ania kutumia chanzo cha Mgombezi, inaweza kuichukua Ilula zaidi ya miaka 10 kupata huduma ya maji safi na salama, ombi langu tutumie chanzo cha mto Ruaha Mdogo kuleta maji Ilula, na nadhani hata gharama zake zinaweza kuwa ndogo,” alisema.

Akitoa taarifa ya ukarabati wa mradi wa maji wa chanzo cha mto Idemle, Mkurugenzi wa IRUWASA, Gilbert Kayange alisema; “baada ya ukarabati huo uliofanywa kati ya mwaka 2013 na 2015, chanzo hicho sasa kinazalisha mita za ujazo 940 kutoka mita za ujazo 600 zilizokuwa zikizalishwa awali wakati mahitaji kwa siku ni mita za ujazo 2,609.”

Ili kutatua tatizo la maji katika mji huo, Kayange alisema serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji wa chanzo cha Mgombezi ambao gharama yake inaelezwa kuwa ni zaidi ya Sh Bilioni 15.

“Tunaongelea suala la Mgombezi kwasababu mradi huo ulikwishasanifiwa, lakini hiyo haitufanyi wataalamu tusiendelee kutafuta vyanzo vingine mbadala vitakavyosaidia kukabiliana na changamoto ya maji katika mji wetu wa Ilula,” alisema.

Akizungumzia kazi zilizotekelezwa wakati wa ukarabati wa mradi huo wa chanzo cha Idemle, Kayange alizitaja baadhi yake kuwa ni pamoja na kukarabati kidaka maji katika mto Idemele, kukarabati tenki la kuhifadhi maji Mazombe na ujenzi wa vitolea hewa katika bomba kuu la usafirishaji na ukarabati wa njia ya usafirsiahaji maji wenye urefu wa kilomita 14.

Nyingine ni pamoja na ujenzi wa mabomba mapya ya kusambaza maji safi yenye urefu wa kilomita 16.7 ambayo hata hivyo yamekuwa yakihujumiwa kwa kutobolewa na watu wasiojulikana.

Mtendaji wa kijiji cha Mazombe, Joseph Nyoni alisema; “mambomba ya plastiki yamekuwa yakitobolewa nay ale ya chuma yamekuwa yakibondwa sehemu za maungio na kusababisha kuvuja na kupoteza maji mengi yanayotakiwa kwa matumizi ya wananchi.”

Nyoni alisema katika kukabiliana na changamoto hiyo, wamefanya mikutano ya hadhara ili kuwashirikisha wananchi kuwafichua waharibifu wa mitandao ya maji.

Mbunge wa Kilolo ameliomba jeshi la Polisi kuwasaidia kuwabaini watu hao ili wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa uharibifu huo.

Meneja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Ilula, Enock Ngoinde amesema wanahitaji zaidi ya Sh Milioni moja kukarabati mabomba hayo.

TAKUKURU yakabidhiwa Kampuni ya Lugumi


Image result for valentino mlowola
picha :Mkurugenzi Mkuu Takukuru-Valentino Mlowola
Sakata la kampuni ya Lugumi iliyoingia mkataba wa Sh37 bilioni na Jeshi la Polisi wa kufunga mashine za kielektroniki za kuchukua alama za vidole nchi nzima, sasa limetua Takukuru baada ya taasisi ya kupambana na rushwa kuchukua faili lake la usajili.

Kampuni hiyo ilibainika kutotimiza matakwa ya mkataba wake baada ya kufunga mashine 14 tu kati ya 108 ilizotakiwa kufunga, licha ya kulipwa  asilimia 99 ya fedha kwa mujibu wa mkataba.

Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) ya mwaka 2013/14 ndiyo iliyofichua udhaifu huo.

Wakati Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ikitaka nguvu itumike ili Jeshi la Polisi liwasilishe mkataba huo, utata umeibuka katika umiliki wa kampuni hiyo kutokana na kuwepo tuhuma kuwa baadhi ya vigogo wa Polisi na wanasiasa ni wanahisa wa Lugumi Enterprises.

Jana, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela), Frank Kanyusi alisema kuwa Takukuru inashughulikia suala hilo, huku akibainisha kuwa kwa sasa Brela hawana takwimu za kina za kampuni hiyo.

“Kampuni hii ilisajiliwa kihalali na kupewa cheti cha usajili. Ila ninachoweza kukueleza kwa sasa ni kwamba jalada la usajili la Lugumi lipo Takukuru kwa ajili ya uchunguzi zaidi,” alisema Kinyusi jana.

Kanyusi, ambaye hakutaka kuzungumzia kiundani kuhusu usajili wa kampuni hiyo, alisema: “Waandishi wa habari wamekuwa wakiniuliza maswali mengi kuhusu suala hili ila kwa sasa hali ndiyo hiyo. Jambo hili lipo Takukuru.”

Alisema kwa sasa kampuni zilizosajiliwa na Brela zipo 120,000 na zinakaribia kufika 130,000 na kwamba kampuni lazima zitoe taarifa zake kila mwaka, kinyume na hapo zinaweza kuchukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufutwa.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Brela zilieleza  kuwa taarifa za usajili wa kampuni hiyo zilitoweka takribani miezi miwili iliyopita.

Mwandishi  alipofika katika ofisi za wakala huyo kwa ajili ya kupata ukweli wa usajili, alielezwa na mmoja wa watumishi ambaye hakutaka jina lake kuwekwa wazi kwamba ni vigumu kupata hilo jalada kwa sababu ya mvutano ulioibuka.

Hata baada ya kufuata taratibu za kupewa jalada hilo kwa ajili ya kupitia masuala mbalimbali, alijibiwa kuwa jalada hilo halionekani ingawa baadaye Kanyusi alisema limechukuliwa na Takukuru.

Sakata la Lugumi liliibuka wiki iliyopita wakati PAC ilipokutana na Jeshi la Polisi kupitia taarifa ya hesabu zao za mwaka 2013/14 zilizokaguliwa na CAG.

Katika hesabu hizo ilibainika kuwa mwaka 2011, Polisi iliingia mkataba na Lugumi kwa ajili ya kufunga mashine hizo katika vituo 108 vya polisi kwa gharama ya Sh 37 bilioni.

Hata hivyo, ilibainika kuwa kampuni hiyo imefunga mitambo hiyo kwenye vituo 14 tu, huku ikilipwa asilimia 99 ya fedha hizo.

Kutokana na ukakasi huo, PAC ambayo ilibaini viashiria vya ufisadi katika mkataba huo, iliagiza watendaji wa Polisi kuwasilisha taarifa za mkataba huo pamoja na vielelezo vyake ili kamati hiyo iweze kuupitia na kujiridhisha.

Lakini hadi sasa Jeshi la Polisi halijawasilisha mkataba huo, jambo ambalo huenda likazua mjadala mkali katika mkutano wa Bunge unaoanza Jumanne ijayo.

Anne kilango malecela atoa ya moyoni

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela, ameibukia kanisani na kutoa ya moyoni, ikiwa siku tano baada ya Rais Dk. John Magufuli kutengua uteuzi wake.

Kilango, Jumatatu wiki hii uteuzi wake ulitenguliwa baada ya Machi 20, mwaka huu, kudai kuwa mkoa wa Shinyanga hauna mtumishi hewa wa serikali hata mmoja.

Hata hivyo, Ikulu ilifanya uchunguzi na kubaini kuwa katika taarifa za awali kuna watumishi hewa 45, huku kazi ya uhakiki ikiendelea katika wilaya za Ushetu na Shinyanga.

Rais Magufuli aliwaagiza wakuu wa mikoa wote, alipokuwa akiwaapisha kuwa wafanya uchunguzi kuhusu uwapo wa watumishi hewa katika mikoa yao na kutoa taarifa.

Kutokana na kutoa taarifa hizo zisizo za kweli, Jumatatu wiki hii, Rais Magufuli alitangaza kutengua uteuzi wake, akiwa amekaa kwenye nafasi hiyo kwa siku 27. Kilango amekuwa mkuu wa mkoa wa 19 tangu kuanzishwa kwa mkoa huo.

Mbali na Kilango, Rais Magufuli pia alimsimamisha kazi Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Abdul Dachi, kutokana na taarifa hizo za kutokuwapo watumishi hewa katika mkoa.

Alivyosema Kanisani
Akiwasalimia waumini wenzake juzi, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, mjini Shinyanga, baada ya kupewa fursa ya kusema neno, Kilango alisema anamshukuru Mungu kwa kila jambo kwa yote yaliyomtokea.

“Ndugu waumini wenzangu, hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu. Hata mtu unapojifungua mtoto akafariki dunia, unamshukuru Mungu kwani hayo ni mapenzi ya Mungu.

"Ukiona mzazi wako kafariki dunia pia, unamshuruku Mungu. Tunao wajibu wa kumshukuru Mungu kwa kila jambo,” alisema kwa maneno mafupi na kisha kuketi, huku akiacha simanzi miongoni mwa waumini wenzake, wakiwamo viongozi wa kanisa.

 
 
 Image result for anne kilango malecela
Alivyoanza Kazi
Mbele ya kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), muda mfupi baada ya kuanza kazi, Kilango alisema Shinyanga ni mkoa wenye changamto nyingi ambazo atazishughulikia, lakini atakuwa akilazimika kukimbia Dar es Salaam kumwona mwenzi wake, Mzee John Malecela ambaye ni mgonjwa, na pindi hali yake ikiimarika wataungana naye mjini Shinyanga.

Hayo aliyasema Machi 22, mbele ya wajumbe wa kikao cha kamati hiyo na Ijumaa Machi 25, alisali kanisani hapo.

Sambamba na hayo, aliahidi kupambana na watumishi wazembe na wale wanaoendekeza rushwa na ufisadi na kurejesha hadhi ya mkoa wa Shinyanga kimaendeleo.

Kilango ambaye yuko mjini Shinyanga, akisubiri kukabidhi ofisi kwa mrithi wake kwa mujibu wa utaratibu, bado anaishi hotelini kwa vile aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Ally Rufunga, hajaondoka katika nyumba ya serikali iliyoko Ikulu ndogo, eneo la Lubaga.

magazeti ya Leo ijumaa ya tarehe 15/04/2016

Magazeti haya yanaletwa kwenu Kwa hisani ya New Mwalimu Education Centre