ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 3 Juni 2016

Magazeti ya Leo ijumaa ya tarehe 03/06/2016

 Endelea kupata taarifa mbalimbali kupitia kikoti.com blog pia unaweza kutangaza nasi Kwa bei nafuu kabisa wasiliana nasi Kwa na 0769694963 au email misaelkikoti@gmail.com.















Alhamisi, 2 Juni 2016

Rais Magufuli Azungumzia Sakata la Wanafunzi Waliotimuliwa UDOM.......


Image result for MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli amesema kuwa baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma walioondolewa chuoni hivi karibuni hawakuwa na sifa za kujiunga na masomo chuoni hapo.

Akizungumza leo katika uzinduzi wa Maktaba mpya ya Kisasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Magufuli amewataka watanzania kuweka siasa kando nakuzungumzia masuala ya msingi, huku akiwashangaa wanasiasa waliojitokeza kuwatetea wanafunzi hao.

“Nimeshukuru wale vijana wameondoka. Wanasiasa haohao, ‘eti ooh.. hao vijana wamekosa pa kulala.. it’s nonsense’. Taifa letu tuliweke mbele kwanza. Siasa zije nyuma,” alisema.

Alisema kuwa baadhi ya wanafunzi ambao walibainika kuwa na elimu ya kidato cha nne waliofeli masomo yao na kuruhusiwa kuendelea na masomo ya elimu ya juu ni watoto wa viongozi.

“Ukimchukua mtoto wa form four ukampeleka pale, hata kama atafanikiwa kupata degree… itakuwa ya ajabu. Na baadhi ya watoto waliopelekwa pale ni watoto wa viongozi. Watoto wa Maskini wenye qualification wamekosa nafasi za kwenda Chuo Kikuu. Watoto wa watu fulani fulani wanapelekwa wakati walifeli. It can’t be,” Dk. Magufuli alisisitiza.

Rais Magufuli aliongeza kuwa Serikali yake haitaruhusu fedha zinazopaswa kutumika kwa ajili ya maendeleo ya wananchi kupelekwa kwa ‘vilaza’ huku waliofaulu wakikosa mikopo ya elimu ya juu.

Dk. Magufuli ameahidi kuwa Serikali yake itahakikisha wanafunzi waliofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza na la pili (division 1 &2) wanajengewa mazingira mazuri ya kuendelea na masomo.

“Waliofeli watafute vyuo vyenye size yao,” alisisitiza.

Viongozi ‘waliochakachua’ fedha za Tasaf kukiona

Imeandikwa na Namsembaeli Mduma, Dodoma.
SERIKALI imesema itawachukulia hatua za kinidhamu watumishi wa halmashauri nchini waliohusika kusababisha watu wasio na sifa kulipwa fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf).
Aidha, imesema itahakikisha viongozi waliochaguliwa kushiriki utambuzi na ugawaji wa fedha hizo kwa kaya masikini, wakiwemo wa vijiji waliohusika kuwaingiza kwenye orodha watu wasio na sifa kwa makusudi, nao wanachukuliwa hatua zinazostahili. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene alisema hayo bungeni mjini hapa jana alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Sabreena Sungura (Chadema) aliyetaka kufahamu hatua zilizochukuliwa kwa waliofanya makosa hayo.
“Kwa kuwa mpango huo umeleta malalamiko mengi na kumekuwa na watumishi waliohusika kusababisha makosa hayo ya kuorodhesha wasio masikini, je, Serikali inawachukulia hatua gani?” alihoji.
Akijibu, Simbachawene alisema, baada ya kutambua udanganyifu katika kaya 25,446 kwamba hazikuwa na vigezo, Serikali imechukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kuagiza kuondolewa kwa watu hao kwenye orodha.
Alisema, kuhusu viongozi wa vijiji na wengine waliochaguliwa kushiriki mpango huo wa kugawa fedha kwa kaya masikini, itaangaliwa kuona endapo walifanya makusudi kuwaingiza watu wasio na sifa au ilitokea bahati mbaya kwa sababu ya kutokuwa na takwimu sahihi, ili hatua zichukuliwe.
Alisema kuwa makosa mengine yanaweza yakatokea lakini si kwa makusudi ya aliyoyatenda, hivyo wanaangalia suala hilo pia kabla ya kuchukua hatua zaidi. Katika swali lake la msingi, Sungura kupitia Mollel alitaka kujua Serikali imejipangaje kutatua kero ya mgawanyo wa fedha hizo, ambapo alieleza kuwa wananchi wengi wasio na uwezo wamekuwa hawazipati.
Simbachawene alisema, hasa katika Mkoa wa Kigoma, udanganyifu umefanyika kwa kiasi kikubwa na wahusika wote watachukuliwa hatua zinazostahili za kisheria, kuhakikisha suala hilo haliendelei kutokea.
Alieleza kuwa utambuzi wa kaya za walengwa wa mpango huo ulianza Novemba, 2013 na hadi sasa umekwishaandikisha kaya milioni moja na laki moja katika halmashauri 159 za Tanzania Bara, pamoja na wilaya zote za Unguja na Pemba.
Kwa mujibu wa Simbachawene, kaya hizo zinapata ruzuku kwa utaratibu wa uhawilishaji fedha baada ya kutimiza masharti ya kupeleka watoto shule na kliniki. Alisema, wakati mpango wa kunusuru kaya masikini unaanza ulipanga kufikia asilimia 70 ya vijiji, mitaa na shehia za halmashauri ambavyo vimefikiwa zilijaziwa dodoso ili kukusanya taarifa zaidi za kaya na hatimaye ziliandikishwa kwenye daftari la walengwa na kuanza kupokea ruzuku.
Alisema, maeneo yote 161 ya utekelezaji ambayo ni halmashauri 159 za Tanzania Bara, Unguja na Pemba, zimeshaondoa kaya zisizostahili kuwa kwenye orodha ya walengwa. “Jumla ya kaya 25,446 zimekwishaondolewa kwenye mpango huo kwa sababu mbalimbali zikiwemo vifo, kukosa vigezo vya kuwa kaya masikini na kuondolewa kwa wajumbe wa kamati za mpango na viongozi wa vijiji, mitaa na shehia katika orodha ya kaya masikini,”alisema.

Magazeti ya Leo Alhamisi ya tarehe 02/06/2016