ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Alhamisi, 7 Julai 2016

wakurugenzi walioteuliwa leo na Rais Magufuli


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo July 07 2016 amefanya uteuzi wa wakurugenzi wa halmashauri za majiji 5, Manispaa 21, Miji 22 na Wilaya (DC) 137 za Tanzania Bara.

Uteuzi huo umetangazwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe ambapo kati ya wakurugenzi wote 185 walioteuliwa, 65 wameteuliwa kutoka orodha ya wakurugenzi wa zamani na 120 ni wakurugenzi wapya.

Orodha ya wakurugenzi walioteuliwa kulingana na mikoa yao ni kama ifuatavyo;

ARUSHA
⦁ Arusha Jiji – Athumani Juma Kihamia
⦁ Arusha DC – Dkt. Wilson Mahera Charles
⦁ Karatu DC – Banda Kamwande Sonoko
⦁ Longido DC – Jumaa Mohamed Mhiwapijei
⦁ Meru DC – Kazeri Christopher Japhet
⦁ Monduli DC – Stephen Anderson Ulaya
⦁ Ngorongoro DC – Raphael John Siumbu

DAR ES SALAAM
⦁ Dar es salaam Jiji – Siporah Jonathan Liana
⦁ Kinondoni Manispaa – Aron Titus Kagurumjuli
⦁ Temeke Manispaa – Nassibu Bakari Mmbaga
⦁ Ilala Manispaa – Msongela Nitu Palela
⦁ Kigamboni Manispaa – Stephen Edward Katemba
⦁ Ubungo Manispaa – Kayombo Lipesi John

DODOMA
⦁ Dodoma Manispaa – Dkt. Leonard M. Masale
⦁ Kondoa DC – Kibasa Falesy Mohamed
⦁ Kondoa Mji – Khalifa Kondo Mponda
⦁ Mpwapwa DC – Mohamed Ahamed Maje
⦁ Kongwa DC – Mhandisi Ngusa Laurent Izengo
⦁ Chemba DC – Semistatus Hussein Mashimba
⦁ Chamwino DC – Athuman Hamis Masasi
⦁ Bahi DC – Rachel Marcel Chuwa

GEITA
⦁ Bukombe DC – Dionis Maternus Nyinga
⦁ Chato DC – Mhandisi Joel Bahahari
⦁ Geita DC – Ally Abdallah Kidwaka
⦁ Geita Mji – Modest J. Apolinaly
⦁ Mbogwe DC – Mahwago Elias Kayandabila
⦁ Nyang’wale DC – Carlos K. Gwamagobe

IRINGA
⦁ Iringa Manispaa – William Donald Mafwele
⦁ Mafinga Mji – Saada S. Mwaruka
⦁ Mufindi DC – Riziki Salas Shemdoe
⦁ Iringa DC – Robert Mgendi Magunya
⦁ Kilolo DC – Aloyce Kwezi

KAGERA
⦁ Biharamulo DC – Wende Israel Ng’ahala
⦁ Bukoba DC – Abdulaaziz Jaad Hussein
⦁ Bukoba Manispaa – Makonda Kelvin Stephen
⦁ Karagwe DC – Godwin Moses Kitonka
⦁ Kyerwa DC – Shedrack M. Mhagama
⦁ Missenyi DC – Limbe Berbad Maurice
⦁ Muleba DC – Emmanuel Shelembi Luponya
⦁ Ngara DC – Aidan John Bahama

KATAVI

⦁ Mlele DC – Alex Revocatus Kagunze
⦁ Mpimbwe DC – Erasto Nehemia Kiwale
⦁ Mpanda DC – Ngalinda Hawamu Ahmada
⦁ Mpanda Manispaa – Michael Francis Nzyungu
⦁ Nsimbo DC – Joachim Jimmy Nchunda

KIGOMA
⦁ Buhigwe DC – Anosta Lazaro Nyamoga
⦁ Kakonko DC – Lusubilo Joel Mwakabibi
⦁ Kasulu DC – Godfrey Msongwe Masekenya
⦁ Kasulu Mji – Fatina Hussein Laay
⦁ Kigoma Ujiji – Manispaa – Judethadeus Joseph Mboya
⦁ Kigoma DC – Hanji Yusuf Godigodi
⦁ Kibondo DC – Shelembi Felician Manolo
⦁ Uvinza DC – Weja Lutobola Ng’olo

KILIMANJARO
⦁ Manispaa ya Moshi – Michael Nelson Mwandezi
⦁ Hai DC – Yohana Elia Sintoo
⦁ Siha DC – Valerian Mwargwe Juwal
⦁ Same DC – Shija Anaclaire
⦁ Mwanga DC – Golden A. Mgonzo
⦁ Rombo DC – Magreth Longino John
⦁ Moshi DC – Emalieza Sekwao Chilemeji

LINDI
⦁ Kilwa DC – Bugingo I. N. Zabron
⦁ Lindi DC – Samwel Warioba Gunzar
⦁ Lindi Manispaa – Jomaary Mrisho Satura
⦁ Liwale DC – Justine Joseph Monko
⦁ Nachingwea DC – Bakari Mohamed Bakari
⦁ Ruangwa DC – Andrea Godfrey Chezue

MANYARA
⦁ Babati Mji – Fortunatus Hilario Fwema
⦁ Hanang DC – Bryceson Paul Kibasa
⦁ Mbulu DC – Festi Fungameza Fwema
⦁ Mbulu Mji – Anna Philip Mbogo
⦁ Simanjiro DC – Yefred Edson Myezi
⦁ Kiteto DC – Tamim Kambona
⦁ Babati DC – Hamis Iddi Malinga

MARA
⦁ Manispaa ya Musoma – Fidelica Gabriel Myovela
⦁ Bunda DC – Amos Jeremiah Kusaja
⦁ Bunda Mji – Janeth Peter Mayanja
⦁ Butiama DC – Solomon Kamlule Ngiliule
⦁ Musoma DC – Flora Rajab Yongolo
⦁ Serengeti DC – Juma Hamsini Seph
⦁ Rorya DC – Charles Kitanuru Chacha
⦁ Tarime DC – Apoo Castro Tindwa
⦁ Tarime Mji – Hidaya Adam Usanga

MBEYA
⦁ Busokelo DC – Eston Paul Ngilangwa
⦁ Chunya DC – Sofia Kumbuli
⦁ Kyela DC – Mussa Joseph Mgata
⦁ Mbarali DC – Kivuma Hamis Msangi
⦁ Mbeya DC – Ameichiory Biyengo Josephat
⦁ Mbeya Jiji – Zacharia Nachoa Ntandu
⦁ Rungwe DC – Loema Isaya Peter

SONGWE
⦁ Momba DC – Adrian Jovin Jungu
⦁ Tunduma Mji – Valery Alberth Kwemba
⦁ Mbozi DC – Edna Amulike Mwaigomole
⦁ Ileje DC – Haji Mussa Mnasi
⦁ Songwe DC – Elias Philemon Nawela

MOROGORO
⦁ Gairo DC – Agnes Martin Mkandya
⦁ Kilombero DC – Dennis Lazaro Londo
⦁ Ifakara Mji – Francis Kumba Ndulane
⦁ Kilosa DC – Kessy Juma Mkambala
⦁ Morogoro DC – Sudi Mussa Mpili
⦁ Morogoro Manispaa – John Kulwa Magalula
⦁ Mvomero DC – Florent Laurent Kyombo
⦁ Ulanga DC – Audax Christian Rukonge
⦁ Malinyi DC – Marcelin Rafael Ndimbwa

MTWARA
⦁ Mtwara DC – Omari Juma Kipanga
⦁ Mtwara Mikindani Manispaa – Beatrice Dominic Kwai
⦁ Masasi Mji – Gimbana Emmanuel Ntayo
⦁ Masasi DC – Mkwazu M. Changwa
⦁ Nanyumbu DC – Hamis Hassan Dambaya
⦁ Newala DC – Mussa Mohamed Chimae
⦁ Newala Mji – Andrew Frank Mgaya
⦁ Tandahimba DC – Said Ally Msomoka
⦁ Nanyamba Mji – Oscar Anatory Ng’itu

MWANZA
⦁ Mwanza Jiji – Kiomoni Kibamba Kiburwa
⦁ Ilemela Manispaa – John Paul Wanga
⦁ Kwimba DC – Pendo Anangisye Malabeja
⦁ Magu DC – Lutengano George Mwalwiba
⦁ Misungwi DC – Eliud Leonard Mwaiteleke
⦁ Ukerewe DC – Tumaini Sekwa Shija
⦁ Buchosa DC – Crispian Methew Luanda
⦁ Sengerema DC – Magesa M. Boniphace

NJOMBE
⦁ Njombe Mji – Iluminata Leonald Mwenda
⦁ Makambako Mji – Paul Sostenes Malala
⦁ Makete DC – Francis Emmanuel Namaumbo
⦁ Njombe DC – Monica Peter Kwiluhya
⦁ Ludewa DC – Ng’wilabuzu Ndatwa Ludigija
⦁ Wanging’ombe DC – Amina Mohamed Kiwanuka

PWANI
⦁ Bagamoyo DC – Azimina A. Mbilinyi
⦁ Chalinze DC – Edes Philip Lukoa
⦁ Kibaha DC – Tatu Seleman Kikwete
⦁ Kibaha Mji – Jenifer Christian Omolo
⦁ Kisarawe DC – Mussa L. Gama
⦁ Mafia DC – Erick Mapunda
⦁ Mkuranga DC – Mshamu Ally Munde
⦁ Kibiti DC – Alvera Kigongo Ndabagoye
⦁ Rufiji DC – Salum Rashid Salum

RUKWA
⦁ Kalambo DC – Simon Ngagani Lyamubo
⦁ Sumbawanga DC – Nyangi John Msemakweli
⦁ Sumbawanga Manispaa – Hamid Ahmed Njovu
⦁ Nkasi DC – Julius M. Kaondo

RUVUMA
⦁ Mbinga DC – Gumbo Samanditu Gumbo
⦁ Mbinga Mji – Robert Kadaso Mageni
⦁ Namtumbo DC – Christopher Michael Kilungu
⦁ Nyasa DC – Oscar Albano Mbuzi
⦁ Songea DC – Simon Michael Bulenganija
⦁ Madaba DC – Shafi Kassim Mpenda
⦁ Tunduru DC – Abdallah Hussein Mussa
⦁ Songea Manispaa – Tina Emelye Sekambo

SHINYANGA
⦁ Kishapu DC – Stephen Murimi Magoiga
⦁ Msalala DC – Berege Sales Simon
⦁ Shinyanga DC – Mark Emmanuel Malembeka
⦁ Kahama Mji – Anderson David Msumba
⦁ Shinyanga Manispaa – Lewis Kweyemba Kalinjuna
⦁ Ushetu DC – Michael Augustino Matomola

SIMIYU
⦁ Bariadi DC – Abdallah Mohamed Malela
⦁ Bariadi Mji – Melkizedek Oscar Humbe
⦁ Itilima DC – Mariano Manyingu
⦁ Maswa DC – Fredrick Damas Sagamiko
⦁ Busega DC – Anderson Njiginya
⦁ Meatu DC – Said F. Manoza

SINGIDA
⦁ Ikungi DC – Rustika William Turuka
⦁ Iramba DC – Linno Pius Mwageni
⦁ Mkalama DC – Martin Msuha Mtanda
⦁ Manyoni DC – Charles Edward Fussi
⦁ Itigi DC – Luhende Pius Gerald
⦁ Singida DC – Rashid Mohamed Mandoa
⦁ Singida Manispaa – Kizito L. Brava

TABORA
⦁ Igunga DC – Revocatus Lubigili Kuuli
⦁ Kaliua DC – John Marco Pima
⦁ Nzega DC – Jacob James Mtalitinya
⦁ Nzega Mji – Phillimon Mwita Magesa
⦁ Sikonge DC – Simon Saulo Ngatunga
⦁ Tabora Manispaa – Bosco Addo Ndunguru
⦁ Urambo DC – Magreth Nakainga
⦁ Tabora -Uyui – Hadija Maulid Makuani

TANGA
⦁ Tanga Jiji – Daudi R. Mayeji
⦁ Korogwe DC – George John Nyaronga
⦁ Korogwe Mji – Jumanne Kiangoshauri
⦁ Muheza DC – Luiza Osmin Mlelwa
⦁ Handeni Mji – Keneth K. Haule
⦁ Handeni DC – William Methew Mafukwe
⦁ Pangani DC – Sabas Damian Chambasi
⦁ Mkinga DC – Mkumbo Emmanuel Barnabas
⦁ Bumbuli DC – Peter Isaiah Nyalali
⦁ Kilindi DC – Clemence Andagile Mwakasenda
⦁ Lushoto DC – Kazimbaya Makwega Adeladius

Wakurugenzi wote walioteuliwa wametakiwa kufika Ikulu Jijini Dar es salaam siku ya Jumanne July 12 2016 saa tatu asubuhi kwa ajili ya kula kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma.

Magazeti ya Leo Alhamisi ya tarehe 07/07/2016

 





Jumatano, 6 Julai 2016

BARAZA LA VIJANA MKOA WA IRINGA (BAVICHA) 06/07/2016


Taarifa kwa vyombo vya habari!
Ndugu waandishi wa habari, Awali ya yote naomba nianze Kwa kumshukuru Mungu Kwa kutujalia afya na uzima hata tukaweza kukutana hapa asubuhi ya leo tukiwa salama. Pia tunamshukuru Mungu kwaajili ya ndugu zetu waisilam kwa kufanikiwa kutimiza nguzo yao muhimu ya kiimani ya mfungo, Hivyo tunawatakia sikukuu njema ya EID EL FITRI.

PILI, Naomba kwa moyo mkunjufu na wa dhati kabisa, kutumia fursa hii ya kipekee kuwashukuruni ninyi waandishi wa habari kwa kukubali wito wetu na kuja kutusikiliza. Ni matumaini yetu kuwa mtatusikiliza kwa makini na kwa uhakika ili kuhakikisha ujumbe wetu unaifikia hadhira kubwa si tu ya wana-Iringa bali watanzania wote na dunia kwa ujumla.

Aidha, Baraza la vijana la Chadema mkoa wa Iringa chini ya uongozi wa BAVICHA mkoa iringa na viongozi wote wa baraza kwa ngazi zote za wilaya, majimbo, kata, matawi na misingi tumekubaliana na kuunga mkono kwa asilimia mia moja tamko la baraza la vijana Taifa lililotolewa na makamu mwkt ndugu Patrick Sosopi la Tarehe 02/07/2016 la kukutana Dodoma Tarehe 23/07/2016 ili kulisaidia jeshi la polisi kuwataka wenzetu CCM kutii sheria bila shuruti.
Na kwa mantiki hiyo tunatangaza rasmi kuanzia leo tarehe 06-15/07/2016 zoezi la kuandikisha vijana kwa ngazi zote za uongozi litafanyika mkoa wa Iringa na kwakuwa vijana wengi wamekuwa wakitupigia simu kuonyesha utayari wao basi sasa tunawaalika rasmi kujiandikisha.

Ndugu, Wanahabari mtakumbuka mwkt wa kamati ya siasa ya CCM Iringa mjini ndugu Kiponza aliwaita na kuzungumza nanyi, pamoja na mambo mengine alieleza kile alichoita kuwa ndoto za bavicha kuzuia mkutano wa CCM haziwezekani.sisi tunawaambia wenzetu waache kuweweseka na wasubiri tarehe 23 ili wajue jinsi nguvu ya umma inavyoweza kusimamia amri ya jeshi la police pamoja rais wao ya kuzuia shughuli za kisiasa mpaka 2020 . Pia watambue kuwa kupingana na bavicha ni sawa na kupingana na agizo la mh. Rais tena aliyetokana na chama Chao, jambo ambalo si heshima kwa kiongozi wetu wa nchi. Pia niwakumbushe ccm sisi bavicha mkoa wa Iringa hatuendi Dodoma kufanya vurugu na uchochezi kama wanavyosema wao bali tunaenda kuwasaidia police kuzuia mkusanyiko harama wa ccm



Ndugu Wanahabari, Naomba ieleweke kuwa ninyi wenyewe ni mashahidi wa Tamko lilitolewa na mkuu wetu wa nchi ambalo lilikwenda sambamba na tamko la jeshi la polisi kuvitaka vyama vyote vya siasa na wanasiasa wasijihusishe na shughuli za kisiasa mpaka mwaka 2020 ili kuwapa fursa viongozi waliochaguliwa kutekeleza ilani na ahadi zao kwa wananchi. Sasa sisi tunajiuliza kwanini CCM wanataka kukaidi agizo hili wakati vyama vingine vimekubali na kutii? Havana, ni lazima twende Dodoma tukawaambie CCM wajifunze kutii maagizo ya vyombo vya dola na viongozi wa nchi.
KWANINI TUNAKWENDA DODOMA?

Ndugu Wanahabari tunakwenda Dodoma kwakuwa,
01. Mpaka sasa si rais wala jeshi la polisi aliyetengua kauai au tamko la kuzuia shughuli za kisiasa kwa maana ya vikao vya ndani, makongamano, mkutano ya hadhara au maandamano n.k

02. Haki ya kufanya shughuli za kisiasa haiwezi kuwa ya chama kimoja kwenye nchi yenye mfumo wa vyama vingi tena unaotambulika kikatiba kama Tanzania.

03.kwa mujibu wa katiba yetu ni wajibu wa kila raia kuhakikisha anatii sheria za nchi, Hivyo sisi kama raia wema na tunaowapenda wenzetu hatutaki wapigwe na kuumizwa na virungu vya polisi, tunakwenda kuwasaidia na kuwakumbusha umuhimu wa kutii sheria bila shuruti ( Coercion without appliances)

04. Mkutano mkuu wa CCM huwakutanisha watu wengi sana na Hivyo jeshi la polisi ambao kwa nchi nzima hawazidi 50,000 pekee yao hawataweza kuwazuia. Tumejitolea hasa kwa kuzingatia ile dhana ya ulinzi shirikishi ili wasipate kazi kubwa sana ya kufanya siku hiyo ya tarehe 23.

05.Tunakwenda Dodoma kusaidia utekelezaji wa kipaumbele muhimu sana kwetu kama Chadema na ambacho kimekuwa hakitekelezwi kikamilifu na kuleta matatizo mengi ambacho ni haki na usawa mbele ya sheria ( Law and order before the law).

Ndugu wanahabari tangu kutolewa kwa tamko la viongozi wetu wa baraza ngazi ya Taifa kumekuwepo na upotoshaji mkubwa eti bavicha wanakwenda Dodoma kufanya fujo. Fujo! Kwanini tufanye Fujo? Tunasisitiza tunakwenda Dodoma kama raia wema na lengo kuu ni kulisaidia jeshi la polisi ili wasitumie nguvu kubwa kuwazuia CCM.Hivyo basi tunatoa wito kwa IGP Mangu na RPC wa mkoa wa Dodoma kutupokea na kutupongeza kwa uzalendo wetu.

Mwisho ndugu wanahabari, nimalizie kwa kumnukuu aliyekuwa rais wa Kwanza mweusi na baba wa Taifa la Afrika kusini Nelson Mandela aliwahi kusema " mahali popote hakuna njia rahisi ya ukombozi na wengi wetu itabidi tupitie, tena na tena kwenye bonde la uvuli wa Martin kabla ya kufikia kilele cha mafanikio". Sisi vijana wa bavicha mkoa wa Iringa tuko tayari kwa gharama kwenda Dodoma ili kusaidia kulinda sharia na katiba yetu isifinyangle finyangwe na chama cha mapinduzi kwa kuamua kwa makusudi kukiuka na kupuuza agizo la rais wetu na Jeshi la polisi.


Ahsanteni kwa kunisikiliza.
Imesomwa kwenu
Na, Jackson mnyawami
Katibu Bavicha Mkoa Iringa
Simu: 0762725088
0716884988

#MAGAZETINI:Kampuni za simu zaadhibiwa, zatozwa milioni 650/-

Imeandikwa na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezitoza faini ya jumla ya Sh milioni 649 kampuni sita za simu nchini kwa kosa la kukiuka masharti ya usajili na matumizi ya laini za simu.
Aidha, TCRA imetoa siku saba kwa kampuni za simu kuzima laini zote zilizokiuka masharti ya usajili zilizoko sokoni ambazo zimewashwa na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wake kwa mamlaka hiyo.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba alisema hatua hiyo imetokana na mamlaka hiyo kufanya ukaguzi katika mifumo ya usajili wa laini za simu na kugundua baadhi ya namba kutolewa bila mteja kujisajili, kusajiliwa kwa majina, vitambulisho na nyaraka za watu wengine.
“Pia TCRA imebaini baadhi ya kampuni kutofunga namba hadi usajili ukamilike na kusajiliwa usajili wa awali ikiwa ni kinyume na Kanuni ya 33 ya Kanuni za Leseni za mwaka 2011 zilizotolewa chini ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya mwaka 2010,” alisema Kilaba.
Kampuni zilizopata adhabu hiyo ni Airtel Tanzania Limited, Benson Informatics Limited, MIC Tanzania Limited, Viettel Tanzania Limited, Vodacom Tanzania Limited na Zanzibar Telecom Limited.
Akifafanua adhabu hizo kwa kila kampuni, Kilaba alisema Airtel imetozwa faini ya Sh milioni 182.7.
Akichanganua faini hiyo ya Airtel, alisema Sh milioni 74 ni kwa kuruhusu kuuzwa kwa laini 148 bila kutumia kitambulisho halisi cha mnunuzi, Sh milioni 33.5 kwa kuruhusu laini 67 ziuzwe bila kujaza fomu, Sh milioni 32.5 kwa kuruhusu laini 65 ziwashwe kabla ya kuuzwa na Sh milioni 42.5 kwa kuruhusu laini 85 zifanyiwe usajili wa awali na kutumika kwenye mtandao wake.
Alisema kwa upande wa Benson Informatics Limited imetozwa faini ya Sh milioni 17. Sh milioni saba kwa kuruhusu kuuzwa kwa laini 14 bila kitambulisho halisi, Sh milioni saba kwa kuruhusu laini 14 ziuzwe bila kujaza fomu na Sh milioni tatu kwa kuruhusu laini sita ziwashwe kabla ya kuuzwa.
Kilaba alisema kwa Kampuni ya MIC Tazania Limited, imetakiwa kulipa faini ya Sh milioni 189 ikiwa ni Sh milioni 93.5 kwa kuruhusu kuuzwa kwa laini 187 bila kutumia kitambulisho halisi cha mnunuzi, Sh milioni 43.5 kwa kuruhusu laini 87 ziuzwe bila kujaza fomu ya usajili, Sh milioni 41 kwa kuruhusu laini 82 ziwashwe kabla ya kuuzwa na Sh milioni 11 kwa kuruhusu laini 22 zifanyiwe usajili wa awali na kutumika kwenye mtandao wake.
Alisema Viettel Tanzania Limited wametozwa faini ya Sh milioni 107 ikiwa ni Sh milioni 36.5 kwa kuruhusu kuuzwa kwa laini 73 bila kutumia kitambulisho halisi cha ununuzi, Sh milioni 36 imeruhusu laini 72 ziuzwe bila kujaza fomu ya usajili na Sh milioni 34.5 kwa kuachia laini 69 ziwashwe kabla ya kuuzwa.
Alisema Vodacom Tanzania Limited imetozwa faini ya Sh milioni 96.5 ikihusisha Sh milioni 49 kwa kuacha laini 98 zisajiliwe bila kutumia kitambulisho halisi cha mnunuzi, Sh milioni 24 kwa kuruhusu laini 38 ziwashwe kabla ya kuuzwa na Sh milioni 4.5 kwa kuruhusu laini tisa zifanyiwe usajili wa awali kwa kutumika kwenye mtandao wake.
Alisema kwa upande wa Zanzibar Telecom Limited imetakiwa kulipa faini ya Sh milioni 57 ikiwa ni Sh milioni 36.5 kwa kuruhusu kuuzwa kwa laini 73 bila kutumia kitambulisho halisi cha mnunuzi, Sh milioni 11.5 kwa kuruhusu laini 23 ziuzwe bila kujaza fomu ya usajili na Sh milioni saba kwa kuruhusu laini 14 ziwashwe kabla ya kuuzwa na Sh milioni mbili kwa kuruhusu laini nne zifanyiwe usajili wa awali na kutumika kwenye mtandao wake.
“Kabla ya kutolewa hukumu hii, tuliziita kampuni za simu zilizogundulika kutenda makosa hayo na kutakiwa kutoa utetezi wao kuhusu ukiukwaji wa masharti ya usajili wa namba za simu. “Ikumbukwe kuwa Aprili 2013, TCRA na kampuni walikubaliana kuondoa kasoro zilizojitokeza katika usajili wa namba za simu kwa kutowezesha laini kutumika kabla ya usajili kukamilika na taarifa za mteja kuhakikiwa na kutofanya kile kinachoitwa usajili wa awali,” alisema.
Sheria ya EPOCA ya 2010 inataka kampuni za simu kusajili laini ili kumlinda mtumiaji kutokana na matumizi mabaya ya huduma za mawasiliano, kuwezesha kuwatambua watumiaji wa huduma za ziada za simu na kuimarisha usalama wa taifa.
Pia kuwawezesha watoa huduma za mawasiliano kuwafahamu wateja wao na kuwa na taarifa za matumizi ya simu za mkononi kwa ajili ya mipango ya maendeleo.
Akizungumzia ukomo wa matumizi ya simu bandia na uanzishwaji wa rajisi kuu ya namba tambulishi, Kilaba alisema mpaka sasa namba tambulishi ambazo hazikidhi viwango 1,713,337 na zilizonakiliwa 117,389 zimezimwa.