ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumanne, 27 Septemba 2016

Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu : +255-22-2114512, 2116898
Email : press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi : 255-22-2113425
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 27 Septemba, 2016 amepokea msaada wa Shilingi Milioni 545 kutoka kwa Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi kwa ajili ya kusaidia wananchi wa Mkoa wa Kagera waliopatwa na maafa ya tetemeko la ardhi lililotokea tarehe 10 Septemba, 2016.
Hundi ya fedha hizo imekabidhiwa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam na Balozi wa India hapa nchini Mhe. Sandeep Arya na baadaye Rais Magufuli akaikabidhi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.
Katika barua yake kwa Rais Magufuli iliyosomwa na Balozi Sandeep Arya, Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi amesema Serikali na Wananchi wa India wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kutokea kwa maafa hayo yaliyosababisha vifo vya watu na uharibifu wa mali.
"Tunaziombea amani na uvumilivu familia zote zilizopatwa na madhara na pia tunapenda kuwahakikishia kuwa tupo pamoja na marafiki zetu Serikali ya Tanzania katika kipindi hiki kigumu" amesema Waziri Mkuu Modi.
Kwa Upande wake Rais Magufuli amemshukuru Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi na Serikali yake kwa kutoa mchango huo na kutuma salamu za rambirambi, na amesema Serikali yake imeguswa na moyo wa upendo waliounesha.
"Mhe. Balozi Sandeep Arya naomba unifikishie shukrani zangu za dhati kwa Waziri Mkuu Mhe. Narendra Modi, mwambie kwa niaba ya Serikali yangu tunamshukuru sana kwa kutoa msaada huu muhimu kwa ajili ya Watanzania wenzetu waliopatwa na maafa kule Kagera.
"Mwambie ameonesha moyo wa upendo na ushirikiano kwetu na tumefarijika kwamba marafiki zetu mmeguswa kwa namna ya kipekee na tatizo lililoipata nchi yetu" amesema Rais Magufuli.
Wakati huo huo, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. Amantius Msole na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Bw. Steven Makonda baada ya kubaini kuwa wamefungua akaunti nyingine ya benki kwa kutumia jina linalofanana na akaunti rasmi ya kuchangia maafa iitwayo "Kamati Maafa Kagera" kwa lengo la kujipatia fedha.
Taarifa iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa muda mfupi baada ya kupokea hundi ya msaada kutoka kwa Waziri Mkuu wa India imeeleza kuwa pamoja na kutengua uteuzi huo Rais Magufuli ameagiza vyombo vya dola vichukue hatua dhidi ya wote waliohusika katika njama za kufungua akaunti hiyo.
Aidha, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Bw. Simbaufoo Swai kutokana na kuhusika katika njama hizo.
Hata hivyo Mhe. Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali kuendelea kuchangia misaada kwa ajili ya walioathirika kwa kutumia akaunti rasmi ya "Kamati Maafa Kagera" ambayo imetangazwa na Serikali.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
27 Septemba, 2016

Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu : +255-22-2114512, 2116898
Email : press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi : 255-22-2113425
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 27 Septemba, 2016 amepokea msaada wa Shilingi Milioni 545 kutoka kwa Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi kwa ajili ya kusaidia wananchi wa Mkoa wa Kagera waliopatwa na maafa ya tetemeko la ardhi lililotokea tarehe 10 Septemba, 2016.
Hundi ya fedha hizo imekabidhiwa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam na Balozi wa India hapa nchini Mhe. Sandeep Arya na baadaye Rais Magufuli akaikabidhi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.
Katika barua yake kwa Rais Magufuli iliyosomwa na Balozi Sandeep Arya, Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi amesema Serikali na Wananchi wa India wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kutokea kwa maafa hayo yaliyosababisha vifo vya watu na uharibifu wa mali.
"Tunaziombea amani na uvumilivu familia zote zilizopatwa na madhara na pia tunapenda kuwahakikishia kuwa tupo pamoja na marafiki zetu Serikali ya Tanzania katika kipindi hiki kigumu" amesema Waziri Mkuu Modi.
Kwa Upande wake Rais Magufuli amemshukuru Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi na Serikali yake kwa kutoa mchango huo na kutuma salamu za rambirambi, na amesema Serikali yake imeguswa na moyo wa upendo waliounesha.
"Mhe. Balozi Sandeep Arya naomba unifikishie shukrani zangu za dhati kwa Waziri Mkuu Mhe. Narendra Modi, mwambie kwa niaba ya Serikali yangu tunamshukuru sana kwa kutoa msaada huu muhimu kwa ajili ya Watanzania wenzetu waliopatwa na maafa kule Kagera.
"Mwambie ameonesha moyo wa upendo na ushirikiano kwetu na tumefarijika kwamba marafiki zetu mmeguswa kwa namna ya kipekee na tatizo lililoipata nchi yetu" amesema Rais Magufuli.
Wakati huo huo, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. Amantius Msole na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Bw. Steven Makonda baada ya kubaini kuwa wamefungua akaunti nyingine ya benki kwa kutumia jina linalofanana na akaunti rasmi ya kuchangia maafa iitwayo "Kamati Maafa Kagera" kwa lengo la kujipatia fedha.
Taarifa iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa muda mfupi baada ya kupokea hundi ya msaada kutoka kwa Waziri Mkuu wa India imeeleza kuwa pamoja na kutengua uteuzi huo Rais Magufuli ameagiza vyombo vya dola vichukue hatua dhidi ya wote waliohusika katika njama za kufungua akaunti hiyo.
Aidha, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Bw. Simbaufoo Swai kutokana na kuhusika katika njama hizo.
Hata hivyo Mhe. Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali kuendelea kuchangia misaada kwa ajili ya walioathirika kwa kutumia akaunti rasmi ya "Kamati Maafa Kagera" ambayo imetangazwa na Serikali.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
27 Septemba, 2016

Majina ya Waliochaguliwa Kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam Degree-2016/2017



The following applicants have been selected to join various undergraduate degree programmes for the 2016/2017 academic year. 
The selected applicants should report at the Mwl. J.K. Nyerere Mlimani Campus on Saturday 8th October 2016 for the orientation week which will start on Monday 10th October 2016. 
Applicants selected for admission into Dar es Salaam University College of Education (DUCE) and Mkwawa University College of Education (MUCE) should report directly to the college's campuses in Chang'ombe and Iringa respectively on the same dates. 
Joining instructions and admission letters should be collected at the University campuses where one is admitted. Joining instructions and other important information can also be downloaded from the University website.

UDSM SELECTION: KUONA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU CHA UDSM 2016/2017,

 Image result for TCU.GO 

Kuona Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Chuo Kikuu 2016/2017,
 
==>Chuo  Kikuu Cha Mwalimu Nyerere   <<bonyeza Hapa>> 

==>Chuo  Kikuu Cha  Udsm,duce Na Muce   <<bonyeza Hapa>> 

==>Chuo  Kikuu Cha  Tumaini Makumira    <<Bonyeza Hapa>>   

==>Chuo  Kikuu Cha Udom  <<bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo  Kikuu Cha Ifm <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Marian << Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo Kikuu Cbe        << Bonyeza Hapa>>

==>Tumaini-mbeya     << Bonyeza Hapa>> & <<hapa>>

 ==>Chuo Kikuu Mum         << Bonyeza Hapa>>

==>Chuo Mum(Diploma) <<Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo- Stella Maris   << Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo- Kampala-kiu  << Bonyeza Hapa>>

Magazeti ya Leo jumanne ya tarehe 27/09/2016




















Jumatatu, 26 Septemba 2016

Msajili: Sikumrudishia Lipumba uenyekiti CUF, Kajirudisha Mwenyewe Kinyemela

Wakati  wanasiasa na wasomi wakimnyooshea kidole Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi (pichani) kwa uamuzi wake wa kumtambua aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, mwenyewe ameibuka na kusema kuwa hatua yake hiyo haikulenga kumrudishia msomi huyo nafasi yake ya uenyekiti.

Jaji Mutungi  jana alisema kuwa alichofanya ni kukishauri chama hicho kuhusu mgogoro uliokuwa ukikisonga na Lipumba aliamua kutumia ushauri huo kurudi mwenyewe kwenye nafasi yake hiyo kinyemela.

Kauli hiyo ya Jaji Mutungi imekuja siku mbili tangu alipotoa waraka unaoelezwa kumtambua Profesa Lipumba kama kiongozi halali wa CUF licha ya kuandika barua ya kujiuzulu Agosti 6, mwaka jana akipinga vyama vinavyounda Ukawa kumpa fursa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kugombea urais.

“Isome barua yangu…, mimi nimeamua watu waijadili umenielewa? Ni vizuri wanavyoijadili, ila nilitarajia waijadili kwa tija sio kwa hasira,” alisema Jaji Mutungi.

Alipoulizwa kuhusu polisi kumsaidia Profesa Lipumba kuingia katika makao makuu ya CUF kwa mtutu alisema: “Hizo ni taratibu ambazo (polisi) wanatumia kwa kuzingatia sheria nyingine za nchi.”

Juni mwaka huu, Profesa Lipumba alimwandikia barua Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kutengua barua yake ya kujiuzulu na kutaka arejee kwenye kiti chake, uamuzi uliozusha mtafaruku huku Mkutano Mkuu wa chama hicho ulioketi Agosti 21 ukiridhia kujiuzulu kwake licha ya kuwa ulivunjika.

“Barua yangu inajieleza sina haja ya kuichambua. Nimekujibu baada ya kuona mjadala huo (katika mitandao) nilitegemea (waliomtukana) wawashauri CUF cha kufanya badala ya kuanza kunitukana,” alisema Jaji Mutungi.

“Sasa huko mahakamani wanakotaka kwenda kama mahakama ikiamua kama Mutungi alivyoshauri huko nako watatukana pia?” alihoji.

Wanasiasa na wasomi 
Mwenyekiti wa Chama cha Kijamii (CCK), Constatine Akitanda alisema alichofanya msajili ni kupandikiza zogo ndani ya CUF jambo ambalo linasikitisha.

Akitanda alisema ndani ya CUF kuna bundi ambaye alikuwa anasumbua watu ila msajili ameongezea mgogoro huo na kuwa alichokifanya si sawa kwa mujibu wa mamlaka yake.

“Unajua hii nchi inachezewa sana hivi mtu anajiuzulu mwenyewe halafu anaamua kurejea mwenyewe bila kufuata taratibu ni aibu, lakini nadhani kuna mkono wa mtu,’ alisema.

Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira alisema anachokiona ndani ya CUF ni uwepo wa biashara haramu ambayo inaweza kuua chama hicho.

Alisema ni wakati mwafaka kwa wafanyabiashara haramu hao wakajulikana katika pande zote kwani ni aibu kuvumilia kasoro hizo zitawale vyama vya siasa.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Dominata Rwechungura alisema migogoro ndani ya vyama vya siasa ipo, hivyo ni jukumu la CUF kutatua ili kurejesha amani na upendo kati yao.

Mwenyekiti wa Chama cha United People Democratic Party (UPDP), Fahimu Dovutwa alisema kinachotokea ni msiba unaoacha pengo ndani ya CUF na vyama vya siasa nchini.

Dovutwa alisema pia pengo la mwasisi wa CUF, marehemu Shaban Mloo linaonekana na kuwataka wazee wa chama hicho kukaa ili kukinusuru chama. 
“Huu ni msiba katika siasa za Tanzania, naomba CUF watafute wazee wao ili waweze kusuluhisha hali hiyo kwa maslahi ya chama chao kwani pengo la Mloo linaonekana,” alisema.

Katibu wa Habari na Uenezi wa NCCR Mageuzi, David Kafulila alisema mgogoro wa CUF unaweza kutolewa uamuzi na mahakama pekee kwa kuwa msajili hana mamlaka ya kufanya alichokifanya. Kafulila alisema msajili anapaswa kushauri kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa na si kama alivyoelekeza kwani anaongeza mgogoro zaidi.

Mwenyekiti wa ADC, Hamad Rashid alishauri CUF kutumia vikao kumaliza tofauti zao, huku akibainisha kuwa ndani ya chama hicho kuna viashiria vya udikteta na usultani.

Mbunge wa Tandahimba CUF, Katani Katani alisema kwa sasa wamethibitisha jinsi Lipumba anavyotumika kwani pamoja na Jeshi la Polisi kukataza maandamano, wafuasi wa Lipumba waliandamana bila kuzuiwa.

Alisema haiwezekani chama kikaendeshwa kwa ajenda za watu wachache ambao wanatumikia matumbo yao na makundi yao na si chama.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kitivo cha Sheria, Dk. Onesmo Kyauke alisema msajili anakosea na kuwataka CUF wakimbilie mahakamani kupata haki.

Credit: Jamboleo

Magazeti ya Leo jumatatu ya tarehe 26/09/2016

















 O