Wakati 
 wanasiasa na wasomi wakimnyooshea kidole Msajili wa Vyama vya Siasa, 
Jaji Francis Mutungi (pichani) kwa uamuzi wake wa kumtambua aliyekuwa 
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, mwenyewe ameibuka na kusema 
kuwa hatua yake hiyo haikulenga kumrudishia msomi huyo nafasi yake ya 
uenyekiti.
Jaji Mutungi  jana alisema kuwa alichofanya ni kukishauri chama hicho kuhusu mgogoro uliokuwa ukikisonga na Lipumba aliamua kutumia ushauri huo kurudi mwenyewe kwenye nafasi yake hiyo kinyemela.
Kauli
 hiyo ya Jaji Mutungi imekuja siku mbili tangu alipotoa waraka 
unaoelezwa kumtambua Profesa Lipumba kama kiongozi halali wa CUF licha 
ya kuandika barua ya kujiuzulu Agosti 6, mwaka jana akipinga vyama 
vinavyounda Ukawa kumpa fursa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa 
kugombea urais.
“Isome
 barua yangu…, mimi nimeamua watu waijadili umenielewa? Ni vizuri 
wanavyoijadili, ila nilitarajia waijadili kwa tija sio kwa hasira,” alisema Jaji Mutungi.
Alipoulizwa kuhusu polisi kumsaidia Profesa Lipumba kuingia katika makao makuu ya CUF kwa mtutu alisema: “Hizo ni taratibu ambazo (polisi) wanatumia kwa kuzingatia sheria nyingine za nchi.”
Juni
 mwaka huu, Profesa Lipumba alimwandikia barua Katibu Mkuu wa CUF, 
Maalim Seif Sharif Hamad kutengua barua yake ya kujiuzulu na kutaka 
arejee kwenye kiti chake, uamuzi uliozusha mtafaruku huku Mkutano Mkuu 
wa chama hicho ulioketi Agosti 21 ukiridhia kujiuzulu kwake licha ya 
kuwa ulivunjika.
“Barua
 yangu inajieleza sina haja ya kuichambua. Nimekujibu baada ya kuona 
mjadala huo (katika mitandao) nilitegemea (waliomtukana) wawashauri CUF 
cha kufanya badala ya kuanza kunitukana,” alisema Jaji Mutungi.
“Sasa huko mahakamani wanakotaka kwenda kama mahakama ikiamua kama Mutungi alivyoshauri huko nako watatukana pia?” alihoji.
Wanasiasa na wasomi 
Mwenyekiti
 wa Chama cha Kijamii (CCK), Constatine Akitanda alisema alichofanya 
msajili ni kupandikiza zogo ndani ya CUF jambo ambalo linasikitisha.
Akitanda
 alisema ndani ya CUF kuna bundi ambaye alikuwa anasumbua watu ila 
msajili ameongezea mgogoro huo na kuwa alichokifanya si sawa kwa mujibu 
wa mamlaka yake.
“Unajua
 hii nchi inachezewa sana hivi mtu anajiuzulu mwenyewe halafu anaamua 
kurejea mwenyewe bila kufuata taratibu ni aibu, lakini nadhani kuna 
mkono wa mtu,’ alisema.
Mwenyekiti
 wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira alisema anachokiona ndani ya 
CUF ni uwepo wa biashara haramu ambayo inaweza kuua chama hicho.
Alisema
 ni wakati mwafaka kwa wafanyabiashara haramu hao wakajulikana katika 
pande zote kwani ni aibu kuvumilia kasoro hizo zitawale vyama vya siasa.
Naibu
 Katibu Mkuu wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Dominata Rwechungura 
alisema migogoro ndani ya vyama vya siasa ipo, hivyo ni jukumu la CUF 
kutatua ili kurejesha amani na upendo kati yao.
Mwenyekiti
 wa Chama cha United People Democratic Party (UPDP), Fahimu Dovutwa 
alisema kinachotokea ni msiba unaoacha pengo ndani ya CUF na vyama vya 
siasa nchini.
Dovutwa
 alisema pia pengo la mwasisi wa CUF, marehemu Shaban Mloo linaonekana 
na kuwataka wazee wa chama hicho kukaa ili kukinusuru chama. 
“Huu
 ni msiba katika siasa za Tanzania, naomba CUF watafute wazee wao ili 
waweze kusuluhisha hali hiyo kwa maslahi ya chama chao kwani pengo la 
Mloo linaonekana,” alisema.
Katibu
 wa Habari na Uenezi wa NCCR Mageuzi, David Kafulila alisema mgogoro wa 
CUF unaweza kutolewa uamuzi na mahakama pekee kwa kuwa msajili hana 
mamlaka ya kufanya alichokifanya. Kafulila alisema msajili anapaswa 
kushauri kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa na si kama 
alivyoelekeza kwani anaongeza mgogoro zaidi.
Mwenyekiti
 wa ADC, Hamad Rashid alishauri CUF kutumia vikao kumaliza tofauti zao, 
huku akibainisha kuwa ndani ya chama hicho kuna viashiria vya udikteta 
na usultani.
Mbunge
 wa Tandahimba CUF, Katani Katani alisema kwa sasa wamethibitisha jinsi 
Lipumba anavyotumika kwani pamoja na Jeshi la Polisi kukataza 
maandamano, wafuasi wa Lipumba waliandamana bila kuzuiwa.
Alisema haiwezekani chama kikaendeshwa kwa ajenda za watu wachache ambao wanatumikia matumbo yao na makundi yao na si chama.
Mhadhiri
 Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kitivo cha Sheria, 
Dk. Onesmo Kyauke alisema msajili anakosea na kuwataka CUF wakimbilie 
mahakamani kupata haki.
Credit: Jamboleo
Credit: Jamboleo

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni