ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Alhamisi, 22 Septemba 2016

Mikutano ya ndani vyama vya siasa ruksa

Imeandikwa na Mroki Mroki
JESHI la Polisi nchini limeondoa katazo lake la mikutano ya ndani kwa vyama vya siasa kuanzia leo.
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Nsato Mssanzya ametangaza kuondoa zuio hilo leo na kusema kuwa makatazo mengine ya mikutano ya vyama hivyo yako pale pale.
Kamishna Mssanzya amesema mikutano ya hadhara na maandamano bado hairuhusiwi lakini wabunge wanaruhusiwa kufanya mikutano yao katika majimbo yao kwa mujibu wa katiba. Polisi imesema imeamua kuruhusu mikutano hiyo ya ndani baada ya kuridhishwa na mwenendo wa shughuli za kisiasa nchini.
Soma Habarileo Septemba 23 kwa habari zaidi

Hakuna maoni: