ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 24 Machi 2017

Maneno ya na Nape Nnauye hapo jana

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj8KcrRG0_eqHZNs60l_XB-iOO8NBmDyhurB9v1m2DE11HKsXityJdhyphenhyphenDc7IJ_JzoeL7wVKPkgMPq4NRAMJmikKC5jpd0UT_3OVhwboF33ubBWEHIebuAt3yICTZ2OFD73FTGi3TYcP04LP/s1600/1.jpgAliyekuwa Waziri wa Habari,  Nape Nnauye amezungumza na Waandishi wa habari akiwa juu ya gari lake leo maeneo ya St. Peter Osterbay Dar es salaam  ikiwa ni saa chache baada ya taarifa kutoka Ikulu kutangaza kwamba uteuzi wake umetenguliwa.

Hali hiyo imetokana na Jeshi la Polisi kuuzuia mkutano huo ambapo RPC Kinondoni alifunga barabara kwa gari kuzuia Gari ya Nape huku akiwataka waandishi wa habari watawanyike mara moja.

==> Haya ni machache ambayo Nape kayaongea

1.Nia ya mkutano wangu haikuwa mbaya. Nilitaka kuzungumza na waandishi wa habari lakini Polisi wanakuja kunizuia.

2.Mnajua ni kiasi gani nimepigana kuirudisha CCM madarakani? Miezi 28 nimelala porini leo mtu anakuja kunitolea bastola.

3.Jana nilisema kuwa kuna gharama za kulipa wakati unatetea haki za watu. Na nilisema kuwa nipo tayari kuilipa gharama hiyo.

4.Sina kinyongo na serikali wala chama changu. Sikumuuliza Rais siku aliniteua na sitamlaumu kwa kuamua kuniondoa.

5.Niliikuta CCM iko shimoni nikaitoa huko. Uzalendo wangu ndani wa CCM si wa kutiliwa shaka.

6.Kina Kawawa walikuwepo wakapita, sisi tutapita, lakini tujiulize tutawaachia watoto wetu Tanzania ya namna gani?

7.Namshukuru Rais kwa mwaka mmoja alioniamini. Nampongeza kaka yangu Dkt Mwakyembe. Nawaomba mumuunge mkono Waziri Mwakyembe.

8.Nawaomba mtulie maisha yaendelee. Nape ni mdogo sana kuliko nchi. Kuna mambo mazuri mbele hivyo tuiunge mkono serikali.

9.Nilitamani sana kuendelea kufanya kazi na ninyi waandishi wa habari lakini muda wa aliyeniweka umefika akaamua niondoke.
10.Mimi niliwahi kufukuzwa CCM kwa kusimamia nilichokiamini. Ili mbegu iote na kuchanua, sharti ioze kwanza
11.Vijana naomba msimamie haki yenu

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba Aagiza aliyemtolea bastola Nape Nnauye Achukuliwe Hatua Kali za Kisheria

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj70rZLWw2h6d0PX-TvxmU8_aQg0Zjw4L1XndPo5vtwYgLTVfKzXJ3CnKdot8BM4sF4IEcghvSJOxyjhsj70vjhXW179c4eaTyoL-NgberZWyQJORP31hTz94dbH16zEb_0brv6A2kU3QrG/s1600/1.jpgKufuatia tukio la mtu mmoja aliyedaiwa kuwa ni Askari kumtishia Mbunge Nape Nnauye kwa kutumia bastola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi amesema tukio lile halikuwa sahihi na kuagiza hatua zichukuliwe.

Waziri Mwigulu Nchemba ambaye ndiye mwenye dhamana ya kusimamia usalama wa raia na mali zao amesema kuwa, Nape Nnauye si jambazi, hakuwahi kuwa na taarifa za uhalifu, sasa kwanini mtu amtishe kwa bastola tena mbele ya umati mkubwa uliojaa waandishi wa habari?

“Mh.Nape Moses Nnauye sio jambazi, ni mtanzania, ni mbunge, mjumbe wa NEC wa CCM, hana record ya uhalifu. Kitendo cha mtu kumtolea Bastola, Sio cha kiasikari, sio cha kitanzania na sio cha ki Mungu, kama mtu ameweza kutoa Bastola mbele ya Kamera nawaza mbali ingekuwa kwenye uchochoro angefanya nini.”

Aidha, Waziri Nchemba amesema kuwa amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Ernest Mangu kumbaini mtu huyo aliyefanya kitendo hicho na kumchukulia hatua stahiki.

“Nahusika na Usalama wa Raia wote wa Tanzania, nimemwelekeza IGP atumie picha kumsaka mtu yule aliyeinua kufanya kitu cha kihalifu kwa kofia ya uaskari. Na kama ni Askari basi sheria zinazoongoza taasisi husika zichukue mkondo wake.”

Nape Nnauye alitishwa na bastola hiyo jana alipofika katika Hoteli ya Protea Dar es Salaam kwa lengo la kuzungumza na waandishi wa habari baada ya Rais Dkt John Pombe Magufuli kumvua Uwaziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Magazeti ya Leo Ijumaa ya tarehe 24/03/2017

Angalia video ya nape alipooneshwa bunduki