ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatano, 11 Mei 2016

Magazeti ya Leo jumatano ya tarehe 11/05/206

Magazeti ya Leo
- watanzania wajiunga Is
-Rostam na manji wajieleza sakata la panama
- Serikari sukari iuzwe 1800
- 


















Jumanne, 10 Mei 2016

Makonda Awasimamisha Kazi Vigogo wawili wa Manispaa Kwa Tuhuma za Kushindwa kutoa Maelezo kuhusu Watumishi Hewa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEggzSbSXfXoIdSb-6Rj_3JaG6FUisiSQsIkd08CvnLCcYSBoG-oFj-uxzCzpGCMhXSURmTCdsHIxf-iz-al0d9oaursWSggE6BVWx6UmWM4c6JqYEiFuHRviQDa0uMZQ19JhUD2-pon8bw/s1600/1.jpg
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewasimamisha kazi wakuu wawili wa idara katika manispaa mbili kwa tuhuma za kushindwa kutoa maelezo kuhusu watumishi hewa katika idara zao, huku wakiendelea kuidhinisha mishahara yao kwa miaka mingi.

Makonda aliwataja watumishi hao waliosimamishwa kazi kuwa ni Mkuu wa Idara ya Utumishi wa Manispaa ya Ilala, Francis Kilawe na Mkuu wa Idara ya Afya Temeke, Syrivia Mamkwe na kuagiza uchunguzi dhidi ya tuhuma zao ufanyike haraka.

Kiongozi huyo alichukua uamuzi huo baada ya hivi karibuni kuwaapisha wakuu wa idara kutoka manispaa tatu ili kusema ukweli na kuwapa wiki moja kuhakiki watumishi hewa katika maeneo yao ya kazi.

Makonda alisema hadi kufikia jana, jumla ya watumishi hewa 39 waligundulika na kufikisha 248 kutoka 209 wa takwimu za awali. 
Kati yao, 26 wanatoka Ilala, wawili (Kinondoni) na 11 (Temeke) na kulisababishia jiji hilo kupata hasara ya zaidi Sh3 bilioni.

“Kilawe ameshindwa kujieleza kuhusu watumishi hewa 11 ambao hajui wako wapi, lakini wanapokea mishahara tangu mwaka 2010.Huku yeye akisaini mishahara yao,” alisema Makonda.

Makonda ambaye pia aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni aliongeza kuwa Mamkwe alishindwa kujieleza walipo watumishi hewa wawili ambao bado wanaendelea kupata mishahara huku akiwa kiongozi wa idara husika.

Kutokana na hali hiyo, Makonda amewaongezea wiki mbili maofisa wanaochunguza suala hilo ili kuwabaini zaidi watumishi hewa kwa madai kuwa bado wanaonekana katika mfumo wa kupokea malipo kutoka Hazina kwenda katika manispaa. 
“Huu ndiyo mkutano wangu wa mwisho kwenu.Wiki hizi mbili zikiisha tutaanza uchunguzi dhidi yenu na tukibaini watumishi hewa katika idara yako utawajibishwa ,” alisema Makonda ambaye pia ni Katibu wa Chipukizi na Uhamasishaji wa UVCCM.

Tanesco: Nchi haitaingia gizani

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco) limewatoa hofu wananchi kuwa nchi haitaingia gizani baada ya Kampuni ya uzalishaji umeme ya Songas kutishia kuzima mitambo yake kutokana na kulidai shirika hilo.

Aidha, imeelezwa kuwa tayari kampuni hiyo inayozalisha megawati 178 za umeme imeshazima asilimia 81 ya mitambo yake na hivyo kufanya uzalishaji wake wa sasa kuwa megawati 35.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Felchesmi Mramba alisema kampuni hiyo imeenda kinyume cha mkataba wao kwa kuzima mitambo yake bila majadiliano.
Mramba alisema Tanesco itachukua hatua za kisheria kama inavyoelekezwa kwenye mkataba wao, ingawa alikiri Songas inawadai kulingana na mkataba lakini si kweli kuwa wanadai Dola za Marekani milioni 90.
“Kampuni ya Songas imezima asilimia 81 ya mitambo yake ya kuzalisha umeme kwa madai ya kutolipwa na Tanesco. Vilevile kampuni hii imekwenda kwenye vyombo vya habari na kutishia kuzima mtambo mmoja uliosalia ifikapo Mei 11 na kujaribu kuwatia hofu Watanzania kwamba kutakuwa na uhaba wa umeme,” alisema Mramba.
Mramba alisema kampuni hiyo inazalisha megawati 178 lakini imezima mitambo yake na kubakiza megawati 35, pia Tanesco isingependa mitambo hiyo izimwe lakini isiwatishe wananchi kuwa nchi itaingia gizani.
Alisema mahitaji ya umeme ni megawati 1,000 kwa siku na kwamba mitambo ya maji inazalisha megawati 500, Kinyerezi megawati 150, Ubungo (I) 100, Ubungo (II) 29, Tegeta 42, Nyakato, Mwanza 42 pamoja na mitambo mingine.
Mramba alifafanua kuwa hatua zilizochukuliwa na kampuni ya Songas ni kinyume cha makubaliano ya mkataba na imekiuka mkataba wake yenyewe. Aidha, kampuni hiyo pia imefanya kosa kubwa kuzungumza na vyombo vya habari na kujaribu kuwatisha wananchi juu ya kukosekana kwa umeme.
Alifafanua kuwa kwa mujibu wa kifungu namba 4.4 kinaitaka Songas kutoa notisi ya siku 90 za kuwa na majadiliano na Tanesco endapo itakuwa haijaridhishwa na jambo lolote la kimkataba.
Aidha, kifungu cha 4.6 cha mkataba huo kinaitaka kampuni hiyo kutoa notisi kwa Serikali na Tanesco baada ya notisi ya awali ya siku 90 kumalizika kabla ya kuzima mitambo yao.
“Lakini pia kifungu cha 17 cha mkataba kinakataza na kuzuia upande wowote unaohusika na mkataba huu kutoa taarifa za mkataba au masuala yanayohusiana na mkataba kwa vyombo vya habari au kwa asiyehusika na mkataba huo pasipo kupata ridhaa ya upande wa pili,” alisema.

Mabasi yaendayo haraka hatimaye kuanza leo

Imeandikwa na Anastazia Anyimike MAMLAKA ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imetangaza nauli zitakazotumika kwa mabasi yaendayo haraka kuwa ni Sh 800 kutoka Mbezi hadi Kivukoni huku mwanafunzi akilipa Sh 200 kwa njia zote.
Aidha, usafiri huo unatarajia kuanza leo kwa mabasi machache na kwa siku mbili wananchi hawatalipa nauli kazi itakayofanywa na Kampuni ya UDA-RT. Akizungumza jana Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe alisema nauli hizo zimepitishwa na Bodi ya Sumatra baada ya kutafakari viwango vilivyotokana na ukokotoaji uliozingatia masuala muhimu ya uendeshaji na kuwa nauli hizo zitaanza kutumika keshokutwa Alhamisi.
Ngewe alisema njia ya pembezoni (kutoka Mbezi Mwisho hadi Kimara Mwisho) itakuwa Sh 400, njia kuu ya Kimara-Kivukoni, Kimara-Kariakoo, Kimara-Morocco, Morocco- Kivukoni, Morocco- Kariakoo na Kariakoo- Kivukoni itakuwa Sh 650.
Alisema pia nauli ya pembezoni wameweka Sh 400 kutokana na kuwa UDA-RT itakuwa ikitoa huduma sambamba na mabasi ya kawaida ya daladala hivyo kuweka usawa wa nauli na kusisitiza kuwa mpango wa biashara uliowasilishwa na UDA-RT ulikuwa na mapungufu.
Awali, UDA-RT ilipeleka mapendekezo ya nauli Sumatra ikionesha njia za pembezoni kuwa Sh 700, njia kuu Sh 1,200 na njia kuu na pembezoni kuwa Sh 1,400 na mwanafunzi akitakiwa kulipa nusu ya nauli ya mtu mzima.
Hata hivyo, Sumatra ilifanya mkutano wa kupokea maombi kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo watumiaji wa huduma hii kwa mujibu wa sheria, uliofanyika Januari 5, mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Aidha, Sumatra imekabidhi UDART leseni ya kutoa huduma hiyo ya mwaka mmoja itakayoishia Mei 8, mwakani. “Tunajua kuwa Kampuni ya UDA-RT inatakiwa kuendesha kwa miaka mwili kabla ya kuipata kampuni halisi itakayofanya kazi hiyo, tumempa leseni ya mwaka mmoja na wiki nne kabla ya kuisha kwa leseni hiyo wanatakiwa kuja kuomba tena kama wanaona wanataka kuendelea,” alisema Ngewe.
Naye Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi yaendayo Haraka (DART), Ronald Lwakatare alisema usafiri wa mabasi ya haraka utaanza leo kwa kuanza na mabasi machache ambapo wananchi watapanda mabasi hayo bure kwa siku mbili lengo ni kutumia fursa hiyo kutoa elimu kwa wananchi.
“Tutatumia siku mbili kutoa elimu kwa wananchi wakiwa ndani ya mabasi, hivyo watasafiri bure na wakiwa humo watapewa elimu ya matumizi ya mabasi hayo,” alisema Lwakatare.

Sukari kaa la moto

SUALA la uhaba bandia wa sukari limeendelea kuitikisa nchi, lakini vyombo vya ulinzi na usalama vikifanya kazi nzuri baada ya kuwatia nguvuni wafanyabiashara wengine, waliohodhi bidhaa hiyo kinyume cha sheria huku ikiwamo kukamata tani 622.4 za mfanyabiashara Haruni Zakaria mkoani Morogoro.
Mwishoni mwa wiki, mfanyabiashara huyo anayemiliki Kampuni ya Al Naeem, alikutwa akiwa ‘ameficha’ tani 4,579.2 za bidhaa hiyo katika maghala yake yaliyoko Tabata, Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), wachunguzi wa taasisi hiyo na wa Jeshi la Polisi, walifanya ukachero wao katika maghala ya kampuni hiyo yaliyopo Mbagala na Tabata, Mei 5, mwaka huu.
Lakini siku chache baada ya kunasa sukari hiyo. Kikosi kazi cha Vyombo vya Ulinzi na Usalama mkoa wa Morogoro kilichoundwa na Mkuu wa Mkoa huo, Dk Kebwe Steven Kebwe kufuatilia wafanyabiashara walioficha sukari, kimebaini kiasi cha tani 622.4 za sukari zilizofichwa katika maghala mbalimbali yaliyomo mkoani humo. Dk Kebwe amemwagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Ulrich Matei kuweka ulinzi kwenye maghala hayo yaliyokutwa yameficha sukari hiyo na kuhakikisha inauzwa kwa bei elekezi, iliyowekwa na serikali kwa wananchi.
Pia alimwagiza kuwafikisha wafanyabiashara walioficha sukari hiyo mahakamani mara moja na kumsaka mfanyabiashara Sadick Yassin ambaye alifunga duka lake wakati wa ukaguzi na kutokomea kusipojulikana.
Mali ya Zakaria wa Dar
Akizungumza jana, Dk Kebwe alisema sukari hiyo imebainika kuwa ni mali ya mfanyabiashara mmiliki wa Kampuni ya Al Naeem Enterprises na kuhifadhiwa katika maghala mbalimbali ya Kiwanda cha Sukari Kilombero (K1) tani 429, Kiwanda cha Sukari Kilombero (K2) tani 135 na katika Manispaa ya Morogoro tani 58.4, jumla kuwa ni tani 622.4.
“Nimeunda kikosi kazi cha kufuatilia wafanyabiashara walioficha sukari katika maghala yao katika ukaguzi wa awali, jumla ya tani 622.4 za sukari zimebainika kwenye maghala mbalimbali na sukari yote iliyobainika ni mali ya Al-Naeem Enterprises na tayari maghala hayo yenye sukari yapo chini ya ulinzi wa vyombo vya dola,” alisema.
Licha ya kumwagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa kuweka ulinzi katika maghala hayo na kusimamia sukari hiyo inauzwa kwa bei elekezi ya serikali, pia alimwagiza Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakiki iwapo sukari hiyo imelipiwa kodi ya serikali.
Dk Kebwe pia aliwataka wananchi katika maeneo mbalimbali mkoani humo, kutoa taarifa za wafanyabiashara au watu walioficha sukari ili hatua zichukuliwe mara moja dhidi yao. Kabla ya kuweka msimamo wa Serikali ya Mkoa dhidi ya wafanyabiashara dhalimu, Dk Kebwe na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa walifanya ziara ya kushtukiza ya kuhakiki upya maghala ya wafanyabiashara wa maduka ya jumla katika Manispaa ya Morogoro.
Katika ghala la Kampuni ya Sukari Kilombero lililipo mjini Morogoro lilikuwa na tani 58.4 za sukari ambayo ni mali ya Al Naeem Enterprises. Msimamizi wa ghala hilo, Robert Charles alimfahamisha Mkuu wa Mkoa na timu yake kuwa sukari hiyo ipo kwa muda wa mwezi mmoja sasa baada ya kununuliwa na mfanyabiashara huyo kutoka kiwandani Kilombero.
Alisema sukari tani 58.4 iliyokutwa ndani ya ghala hilo ni mali ya mfanyabiashara Zakaria aliyeinunua kutoka kiwandani Kilombero na kuihifadhi hapo akisubiri kusafirishwa na kuwauzia wanunuzi wa jumla. Baadhi ya wauzaji wa maduka ya jumla waliokaguliwa na timu ya Mkuu wa Mkoa, Thabit Islam na Hassan Binzoo walisema hali ya upatikanaji wa sukari katika kipindi hiki ni mgumu kutokana na kuadimika ghafla.
Dar yanaswa nyingine
Katika Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam, zimekamatwa tani 2,700 za sukari zikiwa zimefichwa katika ghala moja eneo la Mbagala. Akitoa taarifa hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam jana, Paul Makonda, Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo, Photidas Kagimbo alisema sukari hiyo imekamatwa baada ya Rais kutoa agizo la kuwabaini wale wote walioficha sukari na kusababisha wananchi kuteseka kupata bidhaa hiyo.
Kagimbo alisema licha ya kukamatwa kwa sukari hiyo Manispaa hiyo bado inaendelea na msako ili kuwabaini na wafanyabiashara wengine waliohodhi bidhaa hiyo.
Msako mkali Kahama
Wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Polisi imefanya upekuzi katika baadhi ya maghala ya kuhifadhia sukari na kuwabaini baadhi ya wafanyabiashara wanne wanaojihusisha na kazi hiyo.
Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Michael Nyange alisema wamefanya ukaguzi katika maghala ya wafanyabiashara wakubwa wa sukari, ambayo ni ya wafanyabiashara John Hango (walikuta mifuko miwili ya kilo 50), Nyorobi Kisabu (hakuna kilichokutwa), Mshaka Kaziro (hakuna kilichopatikana) na Alex Magina (mifuko 40, yenye kilo 50 kila mfuko). Alisema kazi hiyo itakuwa endelevu.
RC Dodoma aagiza iuzwe
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana ameagiza tani 154 kuuzwa kwa wananchi kwa bei elekezi, huku akiwataka wafanyabiashara ambao bado wameficha sukari kuitoa mara moja kabla rungu halijawashukia.
Takukuru kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani hapa walikamata na kuzifungia tani 154 za sukari katika ghala la mfanyabiashara Haidary Gulamali na sasa Rugimbana ametoa agizo la kufunguliwa kwa ghala hilo ili litoe huduma kwa wananchi.
Mkuu wa Mkoa akiwa amefuatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa alisema wameamua kufungua ghala na kuanza kutoa huduma kwa wananchi ambao wanauhitaji mkubwa kwa sasa wa sukari.
Lindi yagawiwa kwa shule
Mkoani Lindi, TRA mkoani humo imegawa sukari ya magendo mifuko 5,319 yenye thamani ya Sh 373,521 kwa taasisi mbalimbali za mkoani humo baada ya kuthibitishwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa kubaini kuwa ni salama.
Sukari hiyo ilikamatwa Februari mwaka huu katika bandari ya Lindi ikiingizwa nchini kinyume cha sheria kutoka Brazil kupitia bandari ya Zanzibar, na imegawiwa kwa shule za sekondari, Magereza na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, alisema sukari hiyo ilikamatwa kwa ushirikiano na taasisi nyinginezo.
Taasisi hizo mojawapo ni shule ya Ilulu Sekondari ya Kilwa mifuko 300, Chuo cha Maendeleo Kilwa mifuko 149, shule maalumu Kilwa mifuko 80, Hospitali Kilwa mifuko 50, Mitole Sekondari mifuko 42, Njinjo Sekondari mifuko 73, Nyangao Sekondari mifuko 150, Hospitali ya Nyangao mifuko 150, Lindi Sekondari mifuko 166, Hospitali ya Sokoine mifuko 216, Kambi ya Wazee mifuko 16 Shule ya Sekondari Mahiwa mifuko 210, Shule maalumu ya Nyangao mifuko 44, Veta Lindi 156, Mnolela Sekondari mifuko 57 na Mtama Sekondari mifuko 49.
Kawambwa, Serukamba wanena
Mbunge wa Bagamoyo, Dk Shukuru Kawambwa (CCM) amemtaka Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage kumuondolea adha Rais John Magufuli ya kugombana na wafanyabiashara wa sukari kwa kusaidia kuanza uzalishaji kwa Kiwanda cha Sukari cha Bagamoyo.
Dk Kawambwa alisema “Ni aibu wananchi wanakuwa na uhaba wa sukari, Rais (Magufuli) anaangaliwaje nchi inapokuwa na uhaba wa sukari, mwondolee aibu hii Rais, serikali isaidie Kiwanda cha Sukari Bagamoyo kianze kazi, kimesubiri mwaka wa 11 sasa…kina uwezo wa kuzalisha tani 150,000 kwa mwaka.”
Dk Kawambwa alitoa maelezo hayo bungeni jana wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka 2016/2017. Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba (CCM) aliitaka serikali kuachana na mpango wa kuanzisha viwanda vingi vya kila aina, badala yake ijikite kwenye viwanda vya sukari kwani vina uwezekano wa kuzalishwa tani milioni mbili na kiwanda cha mbolea kuwa na uhakika wa soko kwenye nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Zitto awasilisha hoja mahsusi
Mbunge wa Kigoma Mjini, Kabwe Zitto (ACT-Wazalendo), jana jioni aliwasilisha hoja ya kuomba mjadala wa bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, uahirishwe ili mawaziri wa Kilimo na Viwanda wakapange mikakati ya kuondoa tatizo la sukari. Alisema mikakati hiyo iwe ni kuongeza uzalishaji miwa pamoja na uzalishaji wa sukari ili miaka mitatu baadaye Tanzania isiwe na tatizo la sukari.
Alitumia Kanuni ya 69 kutaka Bunge liahirishwe. Hata hivyo, hoja iliungwa mkono na wabunge wa upinzani pekee na Waziri William Lukuvi alisimama kwa niaba ya serikali na kusema hoja hiyo haiwezekani kuahirishwa na kumtaka Zitto ashike mshahara wa waziri.
Komu, Kubenea watetea, wabanwa Kwa upande wao, Chadema imeonekana kuwatetea wafanyabiashara wanaoficha sukari na kudai kuwa agizo la Rais Magufuli la kuzuia sukari kutoka nje kuingizwa nchini, ndio sababu ya bidhaa hiyo kupotea sokoni.
Pia chama hicho kimedai kuwa kitendo cha serikali kuwataifisha sukari wafanyabiashara walioficha, kinaharibu mazingira ya biashara nchini, lakini pia kinaweza kusababisha benki kufilisika kwa kuwa wafanyabiashara wengi wamechukua mikopo kwenye benki hizo.
Kutokana na hali hiyo kiliitaka Serikali iwaruhusu wafanyabiashara waendelee kuagiza sukari kutoka nje kwa kuwa kuna uhaba mkubwa wa bidhaa hiyo tangu Februari, mwaka huu.
Waziri Kivuli wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Anthony Komu aliyefuatana na Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea walijikuta wakikanusha vikali baada ya waandishi wa habari kuwahoji kama wamelipwa fedha na wafanyabiashara ili kuwaunga mkono katika suala hilo la sukari.
Komu ambaye pia ni Mbunge wa Moshi Vijijini alimtupia lawama Rais Magufuli, na kueleza kuwa suluhisho la kudumu ni kuwaruhusu wafanyabiashara hao waendelee kuagiza sukari kutoka nje, kuliko kuendeleza hatua za kuwaadhibu wale walioficha sukari kwenye maghala yao kwa kuwa hilo si suluhisho.
Naye Kubenea aliwataka waandishi hao wakague hata simu zao, kuona kama kuna fedha yoyote iliyoingia kwani lengo lao ni kufikisha ujumbe kwa serikali kuwa wao ndio chanzo cha gharama kupanda kwa bidhaa hiyo.
Kwa upande wake, Mtafiti wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Haji Semboja alisema serikali imekosea kuingilia soko hilo pamoja na kupanga bei elekezi, jambo ambalo alisema limechangia kupanda bei kwa bidhaa hiyo muhimu kwa matumizi ya nyumbani na viwandani.
“Unapozungumzia sukari, ni bidhaa muhimu kwa matumizi ya nyumbani na viwandani, hili sio soko la nchi moja, ni soko linalohusisha nchi nyingi; ambalo likiingiliwa hata kwa kutekenywa kidogo tu kunalifanya soko lenyewe lishtuke na bei inaweza kuongezeka kama ilivyotokea sasa,” alisema Profesa Semboja wakati akizungumzia mfumuko wa bei wa taifa ambao ulitangazwa jana na NBS.
Habari imeandikwa na John Nditi, Moro, Halima Mlacha, Maulid Ahmed na Sifa Lubasi, Dodoma, Raymond Mihayo, Kahama, Kennedy Kisula, Lindi na Sophia Mwambe na Shadrack Sagati, Dar.

Wabunge wanawake walaani kejeli dhidi yao

Imeandikwa na Maulid Ahmed, Dodoma.
UMOJA wa Wabunge Wanawake Tanzania (TWPG) umelaani na kueleza kutokubaliana na tabia ya baadhi ya wabunge ya kutumia lugha za matusi, kejeli, dharau na udhalilishaji wa wabunge wanawake kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa wamepata nafasi hiyo kwa njia ya mapenzi.
Mwenyekiti wa TWPG, Margaret Sitta alibainisha hayo wakati akiwasilisha maelezo binafsi bungeni jana, akisema lengo la kutoa maelezo hayo ni kuhitimisha mjadala wa kauli hiyo dhidi ya wabunge wanawake wa Chadema uliotokea Mei 5, mwaka huu na kusababisha wabunge hao kutoka nje ya Bunge na kutishia kujitoa TWPG.
Kauli ya kuwadhalilisha wabunge hao wa Chadema ilitolewa bungeni na Mbunge wa Ulanga mkoani Morogoro, Goodluck Mlinga (CCM) ambaye alisema wabunge hao wanawake wamekuwa wakipata nafasi hiyo hadi wawe ‘baby’ (wapenzi) wa wanaume ndani ya chama hicho.
Sambamba na hilo, alisema wabunge wa ndani ya chama hicho wamo pia wenye uhusiano wa jinsia moja. Hata hivyo, hakuwataja kwa majina wabunge hao. “Chadema kuna wanachama wengi wa kike, iweje ichukue wa CCM.
Chadema ndiyo inakandamiza demokrasia, Tundu Lissu anajua sheria lakini ndani ya Chadema kuna wapenzi wa jinsia moja”. Hata hivyo, kauli hiyo ilifutwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson na baadaye Mlinga aliifuta, lakini wabunge wa Chadema hawakukubaliana na kuonesha kukerwa sana.
Jana, Sitta alisema licha ya kauli hizo kufutwa, inasisitiza kuwa inalaani tabia hiyo dhidi ya wanawake inayofanywa ndani na nje ya Bunge na kushauri wabunge wote kuzingatia kanuni zote za Bunge hasa kanuni ya 64(1)(f) na (g) inayokataza lugha ya matusi na ya kuudhi dhidi ya mbunge mwingine.
“TWPG inashauri mara inapotokea mbunge amekiuka kanuni hizi, kiti kichukue hatua za haraka kudhibiti hali hiyo…Tunashauri wabunge wote kuheshimiana ili kulinda hadhi ya Bunge letu na tuwe mfano wa kuigwa katika jamii yetu, tukio hili liwe la mwisho na wakati huohuo liwe fursa kwetu wanawake na kuimarisha umoja wetu, kamwe tusikubali kugawanywa,” alisema.

Magazeti ya Leo Jumanne ya tarehe 10/05/2016




Magazeti ya Leo
- sukari yawa kaa La moto ni baada ya tani zaidi ya 400 kukamatwa
-yanga kama diamond simba kama alikiba ni katika uchezaji wake 
-vigogo wagawana Tazara ni katika mikataba kusoma magazeti haya update taarifa zaidi Kwa hisani ya Airtel Tanzania