ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 23 Julai 2016

Kamati Kuu ya CHADEMA kukutana kwa dharura Dar es Salaam

Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), itakutana kwa dharura, jijini Dar es Salaam, chini ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe, ambapo pamoja na masuala mengine, itapokea taarifa na kujadili hali ya siasa nchini.

Katika siku za hivi karibuni, taifa limekuwa likipitia katika majaribu makubwa, ikiwa ni pamoja na uvunjifu mkubwa wa sheria na taratibu za kuongoza nchi unaofanywa waziwazi na mamlaka za juu/viongozi waandamizi wa nchi kupitia kauli na matendo mbalimbali kiasi cha kuwashtua Watanzania ambao wangependa kuona nchi yao ikiendeshwa katika misingi ya uwajibikaji wa kisheria na demokrasia.

Katika kikao hicho cha siku mbili, Julai 23-24, mwaka huu, Kamati Kuu pia itapokea taarifa na kujadili kabla ya kufanya maamuzi kuhusu mipango mbalimbali inayoendelea ya kukipanga chama ili kiendelee kufanya shughuli zake kwa ufanisi hususani kinapokwenda kuimarisha misingi kuanzia ngazi ya kitongoji nchi nzima, kupitia usimamizi wa kanda 10 za chama.

Imetolewa  Ijumaa, Julai 22, 2016 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Habari CHADEMA

Uamuzi wa Bodi ya Mikopo kuhusu Wanafunzi ambao hawajarejesha mikopo yao hadi leo

Uamuzi wa Bodi ya Mikopo kuhusu Wanafunzi ambao hawajarejesha mikopo yao hadi leo


Mnamo mwezi Machi, 2016, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ilitoa notisi ya siku 60 ikiwataka wanufaika wa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kujitokeza na kuanza kurejesha mikopo yao.  
Aidha, taarifa hiyo pia iliwataka waajiri kuwasilisha taarifa za waajiriwa wao na makato ya marejesho.  Baada ya kipindi hicho kumalizika, kipindi cha notisi hiyo kiliongezwa ambacho pia kimekwisha.

Kufuatia hatua hiyo, Bodi inapenda kuwataarifu wanufaika wote wa mikopo kwamba kuanzia wiki ijayo itaanza kutangaza majina ya wale wote ambao hawajaweza kujitokeza na kuanza kurejesha mikopo yao. 
Zoezi hili litajumuisha pia waajiri ambao hawajawasilisha taarifa za waajiriwa wao.  Hatua hiyo itafuatiwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote watakaoshindwa kutimiza matakwa hayo kwa mujibu wa kifungu cha 19A (1) cha sheria Na. 9 ya mwaka 2004.

Hivyo basi, wanufaika wa mikopo wanahimizwa kuanza kulipa madeni yao na waajiri kuwasilisha taarifa za waajiriwa au kufika kwenye ofisi za Bodi ya Mikopo ili kupata Ankara za madeni yao kabla ya zoezi la kutangaza majina halijafanyika. Marejesho yanaweza kufanyika kupitia Akaunti:

A/C No. 2011100205 – NMB

A/C No. 01J1028467503 – CRDB

A/C No. CCA0240000032 – TPB

Ni muhimu kuzingatia taarifa hii ili kuepuka usumbufu utakaojitokeza kutokana na hatua zitakazochukuliwa.

Imetolewa na:
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu

Magazeti ya Leo jumamosi ya tarehe 23/07/2016






















ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Magazeti ya Leo jumamosi ya tarehe 23/07/2016






















ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Ijumaa, 22 Julai 2016

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA WIZARA YA ELIMU


ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Hukumu ya Mwangosi yasogezwa Julai 25



Imeandikwa na Frank Leonard, Iringa


Marehemu Daudi Mwangosi
HUKUMU ya kesi ya mauaji ya mwanahabari Daudi Mwangosi inayomkabili askari Polisi, Pacificius Simoni iliyokuwa itolewe jana katika Mahakama Kuu, Kanda ya Iringa, imeahirishwa hadi Julai 25.
Akiahirisha hukumu hiyo, Kaimu Msajili wa Mahakama hiyo, Jofrey Isaya, alisema inaahirishwa kwa sababu Jaji Paulo Kiwehlo, aliyekuwa akiisikiliza yuko nje ya Iringa kwa majukumu mengine ya kikazi.
Jana katika eneo la Mahakama, nje na ndani, ulinzi uliimarishwa zaidi ya siku nyingine kesi hiyo ilipokuja kutajwa.
Mamia ya wananchi akiwemo Rais wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Deo Nsokolo, walionekana mahakamani hapo kufuatilia hukumu hiyo.
Mtuhumiwa kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo Septemba 12, 2012 akituhumiwa kumuua Mwangosi kwa kukusudia katika tukio lilitokea kwenye kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi, mkoani hapa.
Mwangosi aliuawa Septemba 2, 2012 akiwa kwenye kazi katika ufunguzi wa matawi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kijijini humo.
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

Katiba Mkuu Chadema Dkt Vicent Mashinji Awapatia Mbinu za Kushinda 2020 BAVICHA


Katibu Mkuu Chama cha Demokrasia na Maendeleo Dkt Vicent Mashinji amewataka vijana wa Bavicha kutokuwa wazembe wakufikiria bali kujipanga kwa ajili ya kushika dola mwaka wa uchaguzi mkuu 2020 huku akiwapatia kanuni za kushinda uchaguzi huo.

Akizungumza na vijana hao jana jijini Dar es salaam Mashinji aliwaambia vijana hao chama chao kimejipanga kushika dola hivyo wao kama vijana wanatakiwa kuhakikisha wanatekeleza majukumu ya kufanya uchaguzi na kuwatambua wanachama hai, pia kuhakikisha kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa vijana wanashiriki nafasi mbali mbali na kushinda

”Nataka niwape majukumu matatu ambayo mkiyafanya hayo 2020 tutashinda nakutangazwa, moja hakikisheni tunaingiza wanachama wapya na kuwahakiki walio hai, nendeni 2019 kwenye serikali za mitaa vijana mgombee na tupate viongozi ngazi ya chini viijana wasomi, na tatu kwa mwaka huu kila kijana ajue nafasi zitakozogombewa katika eneo lake hiyo itatusaidia kushinda nafasi nyingi za madiwani  kwa Tanzania bara na visiwani  na haya ndiyo majukumu makubwa ninayowapatia”   Alisema Mashinji.

Pamoja na hayo aliwataka vijana hao kuendelea kupigania haki za wanyonge na kushinda vita ya demokrasia bila kuvunja sheria huku akiwaasa kuwa askari mzuri na shujaa ni yule anayepambana bila risasi.

”Askari mzuri ni yule ashindaye vita bila kutumia risasi zake, mkawe mabalozi wa kuwatetea wanyonge na haki zao, msiwe waoga kudai katiba ya wananchi, pia kuna watu Geita, Shinyanga na Simiyu tunataarifa wanapigwa kisa itikadi ya upinzani wa vyama hivyo kama vijana mnatakiwa mpaze sauti kwa ajili yao”. aliwaambia Mashinji.

Hata hivyo Mashinji aliwaasa vijana hao kuwa wapole na kusubiri maamuzi ya viongozi wa chama kwani yanabusara. Aidha aliwapongeza vijana hao kwa kuwa na umoja wa kupigania haki na misingi ya demokrasia.

Mwenyekiti wa Bavicha Taifa Patrobas Katambi alimweleza Katibu huyo wa chama kuwa wao wapo tayari kwa pambano japo wanasikiliza na kutii kauli ya chama hivyo wao  watatoa msimamo wao.

Sisi vijana tupo tayari miili yetu ilale makaburini na tukumbukwe kama mashujaa waliokufa wakipigania haki, tumesikiliza maagizo ya viongozi wetu lakini pia sisi leo tutatoa msimamo wetu”.- Katambi
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu