ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 22 Julai 2016

Hukumu ya Mwangosi yasogezwa Julai 25



Imeandikwa na Frank Leonard, Iringa


Marehemu Daudi Mwangosi
HUKUMU ya kesi ya mauaji ya mwanahabari Daudi Mwangosi inayomkabili askari Polisi, Pacificius Simoni iliyokuwa itolewe jana katika Mahakama Kuu, Kanda ya Iringa, imeahirishwa hadi Julai 25.
Akiahirisha hukumu hiyo, Kaimu Msajili wa Mahakama hiyo, Jofrey Isaya, alisema inaahirishwa kwa sababu Jaji Paulo Kiwehlo, aliyekuwa akiisikiliza yuko nje ya Iringa kwa majukumu mengine ya kikazi.
Jana katika eneo la Mahakama, nje na ndani, ulinzi uliimarishwa zaidi ya siku nyingine kesi hiyo ilipokuja kutajwa.
Mamia ya wananchi akiwemo Rais wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Deo Nsokolo, walionekana mahakamani hapo kufuatilia hukumu hiyo.
Mtuhumiwa kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo Septemba 12, 2012 akituhumiwa kumuua Mwangosi kwa kukusudia katika tukio lilitokea kwenye kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi, mkoani hapa.
Mwangosi aliuawa Septemba 2, 2012 akiwa kwenye kazi katika ufunguzi wa matawi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kijijini humo.
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu

kuwa inaanza kutoa elimu ya pre-form one kwaajili ya maandalizi ya kidato cha kwanza. Kuanzia tarehe 09/09/2016.Kwa gharama ya shilingi elfu ishirini(20,000) tu kwa muda wa miezi mitatu(3), ambapo mwanafunzi atapewa vitu vifuatavyo:-
1) Tisheti yenye jina la kituo
2) Daftali, peni na pensel
3) Vitabu vya masomo husika yakiwemo biology, English,physic
4) Mitihani kila wiki kupima maendeleo ya mwanafunzi
Pia Kikoti education centre wanaendelea na kutoa tuition kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka cha sita kama kawaida
OUR MOTTO: EDUCATION FOR LIFE
Kwa mawasiliano zaidi tupigio kwa namba 0769694963

Hakuna maoni: