Askofu
 wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amemjibu katibu mkuu wa 
zamani wa CCM, Yusuf Makamba aliyemtuhumu kuwa ni mwongo akisema leseni 
yake ni ya kuendesha magari makubwa na siyo vibajaji na maguta. 
Akihubiri katika kanisa lake jana, Gwajima bila kutaja jina la Makamba, alisema: “Siwezi kushughulika na vigari vidogovidogo nyie mnanifahamu, mimi nina leseni ya kuendesha semi trailer …nadhani mmenielewa,” alisema huku waumini wake wakimshangilia. 
Juzi,
 Makamba aliwaeleza wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM kuwa Askofu 
Gwajima ni kiongozi wa dini lakini ni muongo na kuwa uongo wake 
unawaudhi hata waumini wake ambao ni wanachama wa chama hicho. 
Alisema
 Gwajima amekuwa akisema uongo kuwa Rais mstaafu, Jakaya Kikwete hataki 
kuachia madaraka ya uenyekiti wa chama hicho, kitu ambacho Rais huyo 
mstaafu alikanusha akisema ni yeye alikwenda kumshawishi Dk John 
Magufuli kuchukua nafasi hiyo kabla ya muda wa uliopangwa kikatiba. 
Katika
 mahubiri hayo, Gwajima pia alisema mafunzo aliyoyapata tangu akiwa 
mdogo ni kuogopa kugombana na watu wa aina tatu, walevi, wazee na 
wagonjwa. 
“Baba yangu alinifundisha nisigombane na walevi, wazee na wagonjwa kwani ukimpiga kidogo mtu wa aina hiyo anaweza kufa,” alisema Gwajima. 
“Hata nyie waumini wangu nawaomba msigombane na watu wa aina hiyo kwani mnaweza kupata matatizo,” alisema. 
Kiongozi
 huyo aliongoza mamia ya waumini wake kumuombea Rais Magufuli kwa 
kushinda uenyekiti wa CCM akisema kofia hizo mbili zimempa meno ya 
kung’ata na zitamwongezea kasi ya kutatua matatizo ya wanyonge nchini.
Rais Magufuli juzi alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM baada ya kupata kura zote 2,398 alizopigiwa na wajumbe wa mkutano huo. 
Kutokana
 na ushindi huo, Gwajima alisema Magufuli amepewa meno ya `kung’ata’ 
kila upande tofauti na alipokuwa na kofia moja ya urais. 
Alisema
 kwa muda mfupi aliokaa madarakani, elimu ya msingi na sekondari 
zimeanza kutolewa bure kitendo ambacho maskini na wanyonge wa nchi hii 
wameanza kuuona mwanga. 
Alisema
 ataendelea kumwombea Magufuli kwa sababu kazi anazozifanya 
zinawanufaisha wanyonge na maskini ambao kwa muda mrefu walipuuzwa 
katika nchi yao.
“Kuchaguliwa
 kwake kuwa mwenyekiti ni zawadi kwetu Watanzania, tuendelee kumwombea 
kila siku ili aendelee kufanya kazi yake kwa ufanisi zaidi,” alisema. 
Alisema
 nafasi hiyo mpya itamwezesha kupambana na rushwa tatizo ambalo 
ameonyesha kuwa `atalivalia njuga’ hata ndani ya chama hicho. 
Mbali
 na Rais Magufuli, Gwajima aliwaombea pia Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, 
mawaziri na Spika wa Bunge kwamba Mungu awalinde ili wamsaidie Rais 
kutekeleza majukumu yake. 
Kwa
 mwezi mzima, Askofu Gwajima amekuwa akitafutwa na Polisi baada ya 
kusambaa kwa sauti inayosikika kama yake ikitaka Rais mstaafu Kikwete 
afikishwe mahakamani kwa makosa yote yaliyofanyika katika utawala wake. 
Katika
 mkanda huo, sauti hiyo inadai baadhi ya viongozi wa CCM wametuma watu 
mikoani kupiga kampeni ya kutaka Magufuli asipewe uenyekiti ambao 
umekuwa ukishikiliwa na Kikwete. 
Baada
 ya sauti hiyo, Gwajima aliondoka nchini kwenda Japan lakini Polisi 
waliendelea kumsaka hadi Julai 12 walipomkamata katika Uwanja wa Mwalimu
 Julius Nyerere (JNIA), aliporejea. Alihojiwa na kuachiwa siku hiyohiyo.
 

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni