Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ametangaza kusitisha 
mpango wa vijana wa chama hicho kwenda Dodoma kuzuia Mkutano Mkuu wa CCM
 ili kuepusha maafa ambayo yanaweza kutokea. Badala yake, Mbowe amesema 
wataendelea kusaka haki ya kufanya mikutano ndani na nje ya nchi. 
Sambamba na uamuzi huo, chama hicho kimetaka viongozi sita wa Baraza la 
Vijana (Bavicha) wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi kuachiwa mara moja. 
Mbowe alitoa tamko hilo jana wakati akizungumza na wanahabari jijini 
Arusha, katika mkutano wa mameya na wenyeviti wa halmashauri 18 
zinazoongozwa na Umoja wa Katiba ya wananchi (Ukawa).
 Sababu za 
kusitisha 
Mbowe alisema wamewataka vijana wa Chadema nchi nzima ambao walianza kujiandaa kwenda Dodoma kuisaidia polisi kuzuia mkutano huo wa Julai 23 kutokwenda kwa sababu polisi wamepewa maagizo ya kuwapiga na kuwajeruhi, hivyo wao hawataki kupambana nao.
Mbowe alisema wamewataka vijana wa Chadema nchi nzima ambao walianza kujiandaa kwenda Dodoma kuisaidia polisi kuzuia mkutano huo wa Julai 23 kutokwenda kwa sababu polisi wamepewa maagizo ya kuwapiga na kuwajeruhi, hivyo wao hawataki kupambana nao.
“Nawataka vijana wote wa 
Chadema waliokuwa wanajiandaa kwenda Dodoma wasitishe na wasubiri 
maelekezo mapya ya Chadema,” alisema Mbowe. 
Mbowe ambaye pia ni Kiongozi
 wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alisema wana taarifa Jeshi la Polisi
 limejipanga kuwanyima dhamana viongozi wa Bavicha hadi baada ya mkutano
 wa CCM, ingawa viongozi wote wa chama hicho hawana hofu ya kukaa 
mahabusu. 
Aliwataka vijana hao kutokwenda Dodoma na wawaache CCM 
waendelee na mkutano wao kwa kuwa Chadema haina hofu na mkutano wa chama
 hicho, bali walitaka dunia ione jinsi polisi wanavyofanya kazi kwa 
maelezo ambayo yanakiuka Sheria ya Vyama vya Siasa na Katiba ya nchi. 
“Wakati sisi tunazuiwa kufanya siasa, Rais anafanya siasa, Waziri Mkuu
 anafanya siasa, mawaziri wanafanya siasa, wakuu wa mikoa na wilaya 
wanafanya siasa jambo ambalo si sahihi,” alisema.
 Alisema lengo la 
Bavicha kwenda Dodoma ni kuchoshwa na uonevu wa kuzuiwa kufanya mikutano
 ya ndani na hadhara wakati CCM wanaendelea na mikutano yao. 
“Waliona 
pengine itakuwa busara washinikize polisi kuona maagizo yao ya kuzuiwa 
mikutano yanatekelezwa kwa wote,” alisema. 
Alilitaka jeshi la polisi 
kufanya kazi kwa kufuata taratibu kwa kutoa haki sawa kwa wote, kwa 
kuruhusu vyama vyote kufanya mikutano yao. 
Apinga tamko la Mwigulu
Kuhusu tamko la Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kuhusu mikutano hiyo, Mbowe alisema hawakulielewa tamko hilo la Rais, kuwa mikutano ambayo imezuiwa ni ya hadhara na maandamano na si ya ndani.
Kuhusu tamko la Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kuhusu mikutano hiyo, Mbowe alisema hawakulielewa tamko hilo la Rais, kuwa mikutano ambayo imezuiwa ni ya hadhara na maandamano na si ya ndani.
Alisema mikutano ya ndani ya chama hicho imezuiwa kwani Chadema Wilaya 
ya Kahama walikuwa na mkutano wa ndani wa uchaguzi ambao umezuiwa. 
 Alisema mkutano wa ndani na wabunge wa Chadema mkoani Shinyanga ulizuiwa
 na pia mahafali za Vijana wa Vyuo Vikuu wa Chadema (Chaso). 
“Lakini 
wakati haya yanafanyika, CCM waliendelea na mikutano yao na mahafali 
yao,” alisema. 
Alisema Chadema itaendelea kudai haki ya mikutano na 
maandamano katika mahakama za ndani na nje ikiwamo ya Afrika ya 
Mashariki. 
Viongozi wa madiwani 
Katika mkutano wa wenyeviti wa halmashauri 18 zinazoongozwa na Chadema, Mbowe alisema Calist Lazaro, Meya wa jiji la Arusha amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa wenyeviti wa madiwani wa Chadema nchini.
Katika mkutano wa wenyeviti wa halmashauri 18 zinazoongozwa na Chadema, Mbowe alisema Calist Lazaro, Meya wa jiji la Arusha amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa wenyeviti wa madiwani wa Chadema nchini.
Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob 
alichaguliwa kuwa katibu wa madiwani wote wa chama hicho na Mwenyekiti 
wa Halmashauri ya Tarime, Moses Matiku alichaguliwa kuwa mnadhimu wao. 
Wote hao watakuwa wajumbe wa Kamati Kuu Chadema. 
Katibu Mkuu wa Chadema,
 Dk Vincent Mashinji alisema katika mkutano huo wenyeviti hao wamepatiwa
 elimu juu kuongoza vyema halmashauri zao ili kuchochea maendeleo. 
“Siku
 mbili za mkutano huu tumekaa na kuweka mikakati bora ya kuhakikisha 
halmashauri zinazoongozwa na upinzani zinafanya vizuri,” alisema. 

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni