ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumanne, 19 Julai 2016

Bavicha: Msimamo Wetu ni Ule Ule, Lazima Nasisi Tufanye Kikao Chetu Dodoma

Ikiwa zimebaki siku tatu kabla ya Mkutano Mkuu wa CCM kufanyika, Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) limesema azma yao ya kufanya kikao chao cha kamati ya utendaji mjini Dodoma ipo palepale. 
Julai 16, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alisema kikao cha Bavicha hakitofanyika kwa sababu itakuwa ni mwendelezo wa vurugu zao. 
Mkutano Mkuu wa CCM, utakuwa na ajenda mbalimbali ikiwamo ya Mwenyekiti wa chama hicho, Jakaya Kikwete kumkabidhi kijiti cha uongozi Rais John Magufuli. 
Katibu Mkuu wa Bavicha, Julius Mwita jana alisema  baraza hilo lipo kwenye hatua ya mwisho ya maandalizi ya kikao hicho kitakachohudhuriwa na zaidi ya wajumbe 50 kutoka mikoa yote. 

“Wajumbe wataanza kuwasili kesho (leo) mjini Dodoma. Hatuna wasiwasi na kikao hiki kwa sababu ni cha ndani siyo mkutano wa hadhara, ambao umepigwa marufuku na polisi,” alisema Mwita. 
Mwita alisema kikao hicho kitakuwa cha siku mbili kuanzia Julai 20 hadi 21 na kwamba, kitahudhuriwa na mameya na wenyeviti vijana wa halmshauri zinazoongozwa na Chadema. 
Alipotafutwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob ambaye ni mwanachama wa Bavicha kujua kama atahudhuria kikao hicho alijibu: “Nitakwenda kwa sababu mimi ni kijana, sina sababu ya kukataa wito wa viongozi wangu wa juu wa Bavicha taifa.” 
Kuhusu kauli ya Kamanda Mambosasa, Mwita alisema polisi ilishatoa maelekezo ya kuruhusu vikao vya ndani. 
“Taarifa ya Mambosasa hatujaishangaa kwa sababu ni desturi yake kujichanganya, leo anasema hivi kesho vile. Tunamtaka atulie asubiri tumpe taarifa ni wapi kikao chetu kitanyika kwa njia ya amani,” alisema Mwita
ADVATISMENT   kikoti education centre
KIKOTI EDUCATION CENTRE (K.E.C)
MAHALI: ILULA MADIZINI KARIBU MAJENGO YA KANISA KATORIKI

Mzazi/Mlezi wa ……………………………………………….kikoti education centre inapenda kukutarifu
kuwa inaanza kutoa elimu ya pre-form one kwaajili ya maandalizi ya kidato cha kwanza. Kuanzia tarehe 09/09/2016.Kwa gharama ya shilingi elfu ishirini(20,000) tu kwa muda wa miezi mitatu(3), ambapo mwanafunzi atapewa vitu vifuatavyo:-
1) Tisheti yenye jina la kituo
2) Daftali, peni na pensel
3) Vitabu vya masomo husika yakiwemo biology, English,physic
4) Mitihani kila wiki kupima maendeleo ya mwanafunzi
Pia Kikoti education centre wanaendelea na kutoa tuition kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka cha sita kama kawaida
OUR MOTTO: EDUCATION FOR LIFE
Kwa mawasiliano zaidi tupigio kwa namba 0769694963

Hakuna maoni: