ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 1 Januari 2016

Yanga, Azam kamili kwa Mapinduzi

YANGA na Azam FC zinatarajia kuondoka leo kwenda Zanzibar kwa ajili ya kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kuanza keshokutwa mpaka Januari 13 kwenye uwanja wa Amani mjini Zanzibar.
Akizungumza na gazeti hili jana Meneja wa Yanga, Hafidh Salehe alisema timu yao inaondoka na wachezaji wote isipokuwa Nadir Haroub ambaye ni majeruhi. “Mchezaji ambaye hataungana na sisi ni Haroub peke yake ambaye ni majeruhi,” alisema.
Katika michuano hiyo, Yanga imepangwa Kundi B pamoja na Azam FC, Mtibwa Sugar na Mafunzo, wakati Kundi A lina timu za Simba, ambao ni mabingwa watetezi, URA ya Uganda, JKU na Jamhuri ya Pemba.
Yanga watafungua dimba kwa kucheza na Mafunzo keshokutwa, mchezo ambao utafuatiwa na mechi kati ya Mtibwa Sugar na Azam FC usiku. Mabingwa watetezi, Simba SC watateremka uwanjani kwa mara ya kwanza Januari 4, kumenyana na Jamhuri usiku, mchezo ambao utatanguliwa na mechi kati ya URA na JKU.
Nusu fainali zitachezwa Januari 10, wakati fainali itachezwa Januari 13 sambamba na kilele cha sherehe za Kombe la Mapinduzi 2016.

Hakuna maoni: