ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 30 Januari 2016

Magufuli awateua Chagonja, Mtweve makatibu tawala

RAIS John Magufuli amefanya uteuzi wa makatibu tawala wawili wa mikoa ya Mwanza na Katavi, ili kujaza nafasi za makatibu tawala wa mikoa hiyo. Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema Dar es Salaam jana kuwa Rais amemteua Kamishna wa Polisi, Clodwing Mtweve kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, ambako anakwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Faisal Issa ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Kabla ya uteuzi huo, Kamishna Mtweve alikuwa Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Polisi Tanzania. Balozi Sefue alisema Rais Magufuli pia amemteua Kamishna wa Polisi, Paul Chagonja kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, ambako anakwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Madeni Kipande, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Kabla ya uteuzi huo, Kamishna Chagonja alikuwa Kamishna wa Mafunzo na Operesheni wa Jeshi la Polisi Tanzania. Aidha, Balozi Ombeni Sefue alisema Rais Magufuli ameamua kuwateua Makamishna hao wa Polisi, kama alivyowateua Majenerali wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania kuwa Makatibu Wakuu wa Wizara, kwa lengo la kujenga nidhamu katika utumishi wa umma.
Makamishna Clodwing Mtweve na Paul Chagonja pamoja na Mahadhi Juma Maalim ambaye ameteuliwa kuwa Balozi mpya wa Kuwait, wataapishwa jijini Dar es Salaam leo saa nne asubuhi.

Hakuna maoni: