ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumamosi, 9 Januari 2016

Yanga SC yamkuna Pluijm

KOCHA wa timu wa Yanga, Hans Van Pluijm amesema kuwa ameridhishwa na kiwango kinachoendelea kuoneshwa na wachezaji wake katika michuano ya Kombe la Mapinduzi mjini hapa.
Yanga imetinga hatua ya nusu fainali baada ya kumaliza michezo ya makundi wakiwa na pointi saba na kushika nafasi ya kwanza katika msimamo wa kundi A huku Mtibwa Sugar ikishika nafasi ya pili ikiwa na pointi nne.
Akizungumza baada ya kumaliza mchezo baina yake na Mtibwa, Pluijm alisema kuwa wachezaji wake wanacheza kwa jinsi alivyowaelekeza. “Naridhika na kiwango chao hasa kwa vile wanafuata maelekezo yangu na wanacheza vile ninavyotaka wacheze,”alisema.
Hata hivyo, alisema kuwa mashindano hayo ya Kombe la Mapinduzi ni mazuri kutokana na kuwa na ushindani ambao unazidi kuongeza uimara wa timu yake. Katika mchezo huo, Yanga ilishinda mabao 2-1 na mabao yake yalifungwa na Yussuf Abubakar dakika ya 42 na Mwalimi Busungu dakika ya 82, wakati lile la Mtibwa lilifungwa na Shiza Kichuya katika dakika ya 10. I

Hakuna maoni: