ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 1 Januari 2016

Magufuli ateua makatibu wakuu 29, manaibu 21

Thursday, December 31, 2015


Rais John Magufuli 
By Mwandishi Wetu, Mwananchi
Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Makatibu wakuu na Manaibu Katibu wakuu wa wizara mbalimbali.
Aidha, Dkt Magufuli pia amemteua Eliakimu Maswi kuwa Kaimu Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na kutengua uteuzi wa Naibu Kamishina wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Lusekelo Mwaseba.
Miongoni mwa Makatibu walioteuliwa ni pamoja na nafasi ya Katibu Mkuu Kiongozi, ambaye amebaki Balozi Ombeni Sefue.
Baadhi ya Makatibu waku hao waliochaguliwa ni pamoja na Mhandisi Mussa Iyombewa ameteuliwa katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Ofisi ya Makamu wa Rais anakuwa Mbaraka A. Wakili.
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano waliochaguliwa ni Mhandisi Joseph. Nyamuhanga (Katibu Mkuu – Ujenzi), Dokta Leonard Chamuliho (Katibu Mkuu - Uchukuzi) na Profesa Faustine R. Kamuzora (Katibu Mkuu - Mawasiliano).
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ni Dokta Yamungu Kayandabira, Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi ni Maimuna Tarishi.
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wanakuwa ni Dokta Mpoki Ulisubisya atakayesimamia Afya na Sihaba Nkinga - Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
Wizara ya Nishati na Madini ni Profesa Justus W. Ntalikwa, Wizara ya Mambo ya Ndani ni Jaji Meja Jenerali Projest A. Rwegasira.
Wizara ya Fedha na Mipango anabaki kuwa Dokta Silvacius Likwelile , Wizara ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa ni Dkt Aziz Mlima. Huku Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa akiteuliwa Job D. Masima.

Hakuna maoni: