Alhamisi, 23 Juni 2016
Jumatano, 22 Juni 2016
Jumanne, 21 Juni 2016
CHADEMA Wataka Mkutano Mkuu wa CCM Kumkabidhi Uenyekiti Magufuli Nao Uzuiliwe
Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetoa tamko zito kikitaka
Polisi kuzuia Mkutano Mkuu wa CCM utakaofanyika mwezi ujao, vinginevyo
watatumia nguvu ya umma kuuzuia.
CCM
kimeitisha mkutano mkuu maalumu unaotarajiwa kufanyika Julai 23 mjini
Dodoma, kwa lengo la Mwenyekiti wa chama hicho, Jakaya Kikwete
kumkabidhi uongozi wa chama, Rais John Magufuli.
Kauli
ya kutaka Polisi kuzuia mkutano huo kama inavyofanya kwa vyama vingine
vya siasa, ilitolewa juzi mjini Moshi na Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana
wa Chadema (Bavicha), Julius Mwita.
Msimamo
huo wa Chadema ambao uliungwa mkono na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho
Zanzibar, Salum Mwalim unafuatia Polisi kuzuia mahafali ya wahitimu wa
vyuo vikuu ambao ni wanachama wao.
Akizungumza
na wanahabari, Mwita alikwenda mbali na kudai kuwa, Chadema
watalifungulia Jeshi la Polisi kesi ya madai ya fidia kwa kuvuruga
mahafali ya Chaso mjini Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita.
“Ukisoma
barua yao wamesema wamezuia mikutano ya hadhara sasa kama wanakuja hadi
kwenye vikao vya ndani, hatuwezi kuendelea kukubali jambo
hili.Tumetumia busara sana,” alisema Mwita na kuongeza:
“Msipouzuia Mkutano Mkuu wa CCM Dodoma Julai 23 tunakuja kuuzuia sisi... yaani muwe tayari kusafiri kwenda Dodoma tukauzuie ule mkutano la sivyo, wauzuie kama walivyouzuia mikutano yetu.”
Mwita alimgeukia Mwalimu na kumweleza kuwa hiyo ni lugha ya ujana na inatekelezeka, akawahoji vijana wa Chaso waliokuwapo: “Wangapi mko tayari kuja Dodoma?” Wote wakaafiki.
“Msipouzuia Mkutano Mkuu wa CCM Dodoma Julai 23 tunakuja kuuzuia sisi... yaani muwe tayari kusafiri kwenda Dodoma tukauzuie ule mkutano la sivyo, wauzuie kama walivyouzuia mikutano yetu.”
Mwita alimgeukia Mwalimu na kumweleza kuwa hiyo ni lugha ya ujana na inatekelezeka, akawahoji vijana wa Chaso waliokuwapo: “Wangapi mko tayari kuja Dodoma?” Wote wakaafiki.
“Intelijensia
ya polisi ni ya kiumbea, inayoweza kujua tu Chadema wanakwenda kwenye
mkutano, haiwezi kujua watu wamejificha wana bunduki na risasi 300
kwenye mawe kule Mwanza,” alidai.
Mwalimu alisema utaratibu wa Polisi na Serikali lazima ukome na kwamba wao ni viongozi.
Kesi ya Mauaji ya Mwanahabari, Daud Mwangosi Kuendelea Leo
Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, jana iliahirisha kesi ya mauaji ya mwanahabari, Daud Mwangosi inayomkabili askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Mkoa wa Iringa (FFU), Pasificus Simon hadi leo.
Kesi
hiyo iliahirishwa baada ya upande wa Serikali kufunga ushahidi wake.
Kesi hiyo iliyoanza kusikilizwa Februari 12, mwaka 2012, leo inaendelea
kwa upande wa utetezi kuleta mashahidi wake mbele ya Jaji Paul Kihwelo
anayeisikiliza.
Katika
kesi hiyo ambayo haikuchukua muda mrefu mahakamani hapo jana, mawakili
wa Serikali wakiongozwa na Sandy Hyra na Ladislaus Komanya walisema
wamefunga ushahidi kwa mashahidi wanne wa awali.
Baada
ya wakili wa utetezi, Rwezaura Kaijage kukubaliana na maombi ya upande
wa Serikali kufunga ushahidi wao, Jaji Kihwelo aliiahirisha kesi hiyo
hadi leo.
Awali,
mtuhumiwa Simon alifikishwa mahakamani hapo akiwa chini ya ulinzi mkali
wa polisi ambao hawaruhusi apigwe picha na waandishi wa habari.
Mwangosi
aliuawa kwa kupigwa bomu Septemba 2, 2012 katika Kijiji cha Nyololo
Wilaya ya Mufindi alipokuwa akiwajibika kwa kazi za kihabari wakati wa
ufunguzi wa matawi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Wabunge wa Upinzani Watoka Bungeni Kimyakimya
Wabunge
wa Ukawa wameendelea kususia vikao vinavyoongozwa na Dk Tulia Ackson,
lakini leo wametoka kimyakimya bila mbwembwe kama za jana.
Kwa sasa kamati ya uongozi ya umoja huo imeingia kufanya kikao kujadili mustakabali wao.
Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia amesema watatoa taarifa kamili baada ya kumaliza kikao hicho.
Marais, maspika wastaafu watwishwa zigo la Bunge
MARAIS wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na maspika wastaafu, wametakiwa kusaidia kutoa ushauri ya namna bora ya uendeshaji wa shughuli za vikao vya Bunge kwa sasa, hususan katika kipindi hiki cha vyama vingi ili wananchi wawakilishwe vyema zaidi kuhusu mahitaji yao bungeni.
Pia Watanzania wametakiwa kufanya maombi maalumu, yenye lengo la kuombea Bunge ili lirudi katika misingi ya awali ya Utanzania kwa kujenga umoja, mshikamano na uvumilivu na kuweka mbele dhamira ya dhati ya kuwawakilisha wananchi katika mahitaji yao na si kutanguliza dhamira za kivyama wakati wa vikao vyake.
Hayo yalisemwa na Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Paulo wa Msalaba la mjini Dodoma, Padri Sebastian Mwaja wakati wa mahubiri ya ibada za Jumapili zilizofanyika kanisani hapo juzi.
Padri Mwaja alisema Bunge la sasa, linaloendelea na vikao vyake hapa linawanyong’onyesha wengi kwa kushindwa kujikita katika taratibu na desturi nzuri za Kitanzania za kujenga umoja, mshikamano na kuvumiliana katika mambo mbalimbali na badala yake limeshuhudia mvutano, mgawanyiko na kutovumiliana.
“Tunapofanya ufuatiliaji wa hoja za wabunge katika vikao vyake, hatupati kuona ile dhamira ya wazi ya kuwakilisha hoja na mahitaji ya Watanzania wa ngazi za chini ili mahitaji yao yapatiwe ufumbuzi na badala yake tunashuhudia hoja zenye mlengo wa kujipendelea mambo yao zaidi na kuwaacha wananchi na hofu ya kujiuliza endapo kweli dhamira ya kuwatumikia wananchi endapo ni kipaumbile cha kwanza,” alieleza Padri Mwaja.
Alieleza jinsi Bunge linavyojikita katika uvyama na kudhoofisha msingi wa umoja, mshikamano na usawa pamoja na kuvumiliana kama ilivyo tangu awali ambako Watanzania walisifiwa kimataifa kwa sifa hiyo lakini sasa, haipo hivyo, na kushauri juhudi za makusudi lazima zifanyike ili kurudi katika mstari huo mzuri.
Alifafanua kwa undani kwamba kujadili hoja bungeni kwa kuweka mbele dhamira za kivyama, kwa kushuhudia hoja za msingi za kuwatetea wananchi, zikiwekwa pembeni na kuweka mbele dhana ya uvyama, akisema hilo halitasaidia kuwatatulia wananchi kero zao nyingi kama Bunge halitarudi katika misingi ya kizalendo.
Alieleza kusikitishwa na mparaganyiko wa umoja bungeni na kutokuwa na mshikamano katika kuendesha shughuli za Bunge na kutoa mwito kwa marais wastaafu na maspika wastaafu kwa umoja wao kusaidia kulishauri Bunge njia nzuri zaidi ya kurejea katika misingi ya Kitanzania ili tumaini lililojengeka kwenye nyoyo za watu lisififie.
Padri Mwaja alisema wastaafu haswa marais na maspika ni hazina kubwa kwa Taifa, ambao wanaweza kutumika kama kisima cha hekima kwa taifa ili kutoa ushauri bora wa namna ya kurejea katika misingi ya kizalendo ya kitanzania na si kama mambo yanavyoendeshwa bungeni hivi sasa.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)