ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Ijumaa, 19 Juni 2015

Mamlaka ya Mji Mdogo Ilula

  

Na waandishi wetu, Longo na Kikoti


kata ya Ilula inamitaa ya Ilula-Itund, Masukanz, Igunga, Ikokoto, Madizini.


kata Nyalumbu ina mitaa ya Ilula-Mwaya,Ikuvala, Mtua, Ding'inayo, Ngelango, Ilula Sokoni,

Itabali,Matalawe


kata ya Mlafu ina mitaa ya Mlafu,Isagwa,Itungi

MATATIZO YANAYOUKUMBA MJI MDOGO WA ILULA


Tatizo la maji



Maji ni uhai na maji yana matumizi mengi katika maisha ya kila siku ya binadamu,

wanyama na hata viumbe vingine hai,ikiwemo mimea.Lakini kwa wakazi wa

Mji Mdogo wa Ilula uliopo Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, upatikanaji

wa maji kwao ni kitendawili cha miaka mingi sasa kwani ni tatizo sugu.

Ilula ni mji unaosifika kwa biashara mbalimbali hususan zao la nyanya na

vitunguu, hali inayoufanya uwe na mkusanyiko mkubwa wa watu kutoka

maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi wanaokwenda kwa shughuli

za kilimo na biashara.

Sababu za uhaba wa maji ilula

- kuongezeka kwa kasi kwa idadi ya watu ukiringanisha na miundo

mbinu ya maji iliyopo katika-mji huo, pia suala la ubovu wa miundo

mbinu ya maji imeonekana ni tatizo kwani mingi imeharibika na-

hakuna jitihada zozote za kuirekebisha .

- pia sababu inayochangia uhaba wa maji katika mji huu ni-

pamoja na uharibu wa vyanzo vya maji; hasa katika chanzo

cha idemule.

je jitihada gani zimechukuliwa na serikali?

Serikali imejitahidi kuboresha miundombinu ya chanzo cha Idembe,

na imeanza kufanya upembuzi wa-awali ili kutumia vyanzo mbadala

vya mto Mgombezi na milima ya Selebu na kuchimba visima vingi

vya maji katika mji huo. akizungumza na wananchi waziri wa maji

alisema Profesa Maghembe wizara yake imekwishatoa Sh Milioni -

150 na itaongeza nyingine Sh Milioni- 150 ili kuboresha miundombinu-

ya chanzo cha Idembe.

Tatizo jingine ni miundombinu ya barabara za mitaani.

barabara za mitaani katika mji huu wa ilula bado ni tatizo kubw

hasa katika maeneo ya mtua, sokoni na isele na hii inatokana na

kutokuwepo mipango yakinifu iliyoweka na serikali ili kuzuia

wanajamii kujenga katika maeneo hayo ambayo barabara za


mitaani zinapaswa kujengwa, hivyo kusababisha hatari kumbwa

hasa kwa wananchi ikiwa hatari ikitokea kama ajari ya moto,

uwepo wa wagonjwa wanaohitaji msaada wa gari inakuwa ni

tatizo kwani hakuna barabara zinazoruhusu- magari kupita

kwa urahisi.


Je serikali imefanya jitihada gani?


suala la barabara za mitaani linaonekana kuendelea kufumbiwa-

macho, licha ya baadhi ya mitaa hasa Majengo mpya serikali

kutengeneza barabara ili kuzuia wanaojenga wasijenge lakini

wanashinda kutatua changamoto ya sehemu ambazo tayari

watu wameziba barabara hizo za mitaani.


Je ungekuwa we ungeshauri nini?


Sheria za barabara za mitaani zinatambulika vizuri, kwa hiyo;

ni vizuri serikali ikachukua hatua mapema kwa kuangalia

watu waliojenga maeneo hayo ya hifadhi za barabara za

mitaani na kuwachukulia hatua, na kama serikali ilifanya

makosa katika ugawaji wa maeneo bila kuacha maeneo

ya hifadhi ya barabara itafute njia ya kupata ramani

ambapo barabara zinatakiwa kupita na kulipa fidia

kwa jamii itakayoathirika na zoezi la upitishaji wa

barabara za mitaani ilula.













Hakuna maoni: