ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumapili, 9 Oktoba 2016

NECTA KUANZA KIKAGUA VYETI KWA WATUMISHI KESHO


Hatua ya Baraza la Mitihani nchini (Necta) kutoa ratiba ya kufanya uhakiki wa vyeti vya kidato cha nne, sita na ualimu kwa watumishi wote wa umma sasa ni wazi imezidi kupandisha joto kwa vigogo na watumishi mbalimbali ambao hawana sifa za kielimu kushika nafasi walizo nazo.

Katika taarifa yake ya sasa Baraza la Mitihani nchini, limetangaza kuwafuata katika maeneo yao ya kazi watumishi wote walioko katika mamlaka za mikoa, halmashauri na manispaa kwa ajili ya kufanya uhakiki wa vyeti vyao hivyo vya kitaaluma.

Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na  Edga Kasuga kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Baraza hilo kwenda kwa Makatibu tawala wa Mikoa, uhakiki utafanyika katika ofisi za Makatibu Tawala wa mikoa kuanzia Oktoba 10 hadi 14 mwaka huu, ingawa ratiba nyingine ya uhakiki imeonyesha zoezi hilo litafikia tamati Novemba 7 mwaka huu.

“Ili kufanikisha zoezi hilo Baraza limetaka kupata orodha (nakala- laini ya soft copy) ya watumishi wote wa umma waliopo katika Mkoa, Halmashauri na Manispaa.

“Nakala za vyeti vya kidato cha nne, cha sita na ualimu vya watumishi wote walioandikishwa na chumba cha kufanyia uhakiki,” inaeleza taarifa hiyo ya Baraza la Mitihani.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la Mitihani, uhakiki huo utafanywa katika makundi matano katika mikoa tofauti tofauti.

Oktoba 10, mwaka huu kundi la kwanza litafanya uhakiki katika Mkoa wa Mtwara, kundi la pili Singida, kundi la tatu Rukwa, kundi la nne Katavi na kundi la tano litakuwa Geita.

Oktoba 17 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Lindi, la pili Manyara la tatu Songwe, la nne Kigoma na la tano litakuwa Mwanza.

Oktoba 24 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Morogoro, la pili Arusha, la tatu Mbeya, la nne Tabora na la tano Mara.

Oktoba 31 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Pwani, la pili Kilimanjaro, tatu Ruvuma, la nne Shinyanga na la tano Simiyu.

Novemba 7 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Dar es Salaam, la pili Tanga, la tatu Njombe, la nne Dodoma na la tano Iringa.
==

Majina ya waliochaguliwa kujiunga na vyuo mbali mbali kwa awamu ya pili


 Majina ya waliochaguliwa kujiunga na vyuo mbali mbali kwa awamu ya pili

==>Chuo Kikuu Eckern Ford  (2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Ruaha-iringa 2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Mwl. nyerere Dar (2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Tumaini-dar  (2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu St.john (2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Mwenge (2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Zanzbar (2nd Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Iringa (2nd Round)    <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Mipango Dodoma(2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Ifm  (2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Udsm,muce&duce(2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Makumira-arusha (Second Round)<<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Arusha University(2nd Round)<<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Stefano Moshi(1st &2nd Round)<<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Marian (Second Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Saut-mwanza (Second Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Teku(Second Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Muccobs/mocu(Second Round)<<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Bugando(Second Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Jordan (Second Round)   <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Amucta(Second Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Kiu(Second Round) <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Mum(Second Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Mweka Second Round)  <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Cha Ajuco Songea( 2nd Round) <<bonyeza Hapa>>

Taarifa kutoka Ikulu: Rais Magufuli afanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Mhandisi James Mitayakingi Kilaba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Mhandisi James Mitayakingi Kilaba umeanza jana Jumamosi tarehe 08 Oktoba, 2016.

Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi James Mitayakingi Kilaba alikuwa akikaimu nafasi hiyo, baada ya uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Ally Yahaya Simba kutenguliwa.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

09 Oktoba, 2016

Magazeti ya Leo jumapili ya tarehe 09/10/2016