- Na Fidelis Butahe, MwananchiKwa ufupi
- Ndiye amesababisha vyama hivyo vinne vishindwe kutangaza jina mapema kama vilivyoahidi
- Hali imeendelea kuwa ngumu kwa upande wa Ukawa ambao hadi sasa wameshindwa kumtaja mgombea wao
Dar es Salaam. Wakati wa hali ya sintofahamu ikiwa imetawala uteuzi wa mgombea atakayeungwa mkono na vyama vinne vya upinzani, imebainika kuwa mzozo unaochelewesha suala hilo ni mgombea ambaye Chadema haijamuweka bayana.Katibu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa ndiye ambaye anapewa nafasi kubwa ya kupitishwa kugombea urais kwa tiketi ya Ukawa mbele ya mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na kada wa NCCR-Mageuzi, Dk George Kahangwa, lakini hadi sasa vyama hivyo bado vinasita kumtangaza mteule wake.Profesa Lipumba alikuwa amewaahidi waandishi wa habari wiki iliyopita kuwa mgombea ambaye ataungwa mkono na vyama hivyo vya Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF na NLD angetangazwa Julai 14, lakini siku hiyo hakuna aliyetangazwa.Badala yake viongozi wa Chadema, NLD na NCCR ndio waliofika Hoteli ya Coloseum jijini Dar es Salaam ambako Profesa Lipumba aliahidi kuwa ndiko jina la mgombea huyo lingetajwa, wakati viongozi wa CUF hawakuonekana na baadaye jioni wakasema kuwa walikuwa na kikao cha ndani ya chama cha kutafuta ufumbuzi wa mambo ambayo walikuwa hawajakubaliana.Vyama hivyo vitatu vikaeleza baadaye kuwa jina hilo litatangazwa ndani ya siku saba kuanzia Julai 14, lakini siku iliyofuata CUF ilisema suala la kuachia chama kingine jukumu la kusimamisha mgombea urais litawasilishwa kwenye kikao cha Baraza Kuu la chama hicho ambacho kitafanyika Julai 25, jambo ambalo lilikubaliwa na vyama hivyo vitatu.Matamko hayo yamefanya suala la mgombea urais wa Ukawa kugubikwa na giza nene, lakini kwa siku tatu Mwananchi imefuatilia na kubaini kuwa mgombea ambaye yuko na hajatajwa rasmi kwa vyama hivyo vinne ndiye anayechelewesha mchakato huo na amesababisha kuwapo na hatari ya umoja huo kuparaganyika.Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka ndani ya vikao vya Ukawa vilivyoanza kufanyika takribani wiki mbili jijini Dar es Salaam, zinaeleza kuwa licha ya viongozi wa vyama hivyo kumpata mgombea wao wa urais katika kikao cha Julai 14 mwaka huu, walikwama kumtangaza kutokana na CUF kutokuwapo kikaoni ikielezwa kuwa wanapinga maendeleo ya mchakato huo.Taarifa hizo zinaeleza kuwa msimamo huo wa CUF umetokana na utata ulioibuka katika kikao cha Ukawa cha Julai 11 na 14, baada ya wagombea wawili kati ya watatu, kukubali mmoja wao agombee urais, lakini chama chake kikasema kuwa kinachotakiwa ni Ukawa kutangaza jina la chama kitakachotoa mgombea na si jina la mgombea.Tayari Profesa Lipumba ameshachukua fomu za kuwania urais kwa tiketi ya CUF, wakati Dk Kahangwa amechukua fomu kuwania urais kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi, huku mchakato wa Chadema ukiwa haujaanza.Habari hizo zinaeleza kuwa awali kulikuwa na mvutano mkali kati ya Profesa Lipumba na Dk Slaa na kwamba katika kikao cha Julai 11, Lipumba ambaye ni mwenyekiti wa CUF alikubali kumuachia Dk Slaa agombee urais kupitia Ukawa, lakini inaonekana hata ndani ya Chadema bado hawajaafikiana kuhusu jina la mgombea.Hata hivyo, chama hicho kimeeleza kuwa jina la mgombea urais limeshapatikana na linasubiri muda muafaka.“Tutamtangaza mgombea urais wa Ukawa ndani ya wiki moja kama tulivyosema awali,” alisema Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-Bara, John Mnyika jana.ananchi wanatakiwa kutulia tu, siku ikifika tutatangaza.”Mnyika alitoa ufafanuzi huo muda mfupi baada ya kulieleza gazeti hili jana kwamba wanaopaswa kuzungumzia suala hilo ni Dk Slaa na Profesa Lipumba.Jibu kama hilo la Mnyika lilitolewa pia na mwenyekiti wa NLD, Dk Emmanuel Makaidi alipoulizwa kuhusu habari kwamba kuna jina la mgombea urais linalosumbua Ukawa.“Sijui chochote kuhusu hilo. Ila watu hawa wawili, Mbowe na Dk Slaa watakusaidia kujua kuhusu jambo hilo.”Alipobanwa zaidi, alisema: “Unajua hata mimi nazisikia sana habari kama hizo pamoja na nyingine nyingi. Katika Ukawa watu wanazungumza ndani ya vikao na nje ya vikao, ila wa kulithibitisha hilo ni hao watu wawili niliokutajia.”Lakini mpashaji habari wetu alisema ugumu wa kumpata mgombea urais wa Ukawa kutoka Chadema unasababishwa na chama hicho kutotaka kuweka bayana jina la mtu atakayebeba jukumu hilo wakati wameshakubaliana kuwa Dk Slaa ndiye asimamishwe.“Inaonekana kama kuna mtu mwingine hivi. Wote tumekubali mgombea awe Dk Slaa, lakini Chadema wenyewe wanazuia asitangazwe,” alisema mpashaji huyo kutoka ndani ya vikao vya Ukawa.Habari zaidi zinaeleza kuwa ndani ya Chadema kuna mvutano, kwani wapo wanaotaka Dk Slaa atangazwe kuwa ndiye mgombea na wanaotaka asitangazwe lakini hawaweki bayana kuwa hawamtaki au wanataka mtu mwingine.Hata hivyo, habari hizo zinasema kuwa sababu nyingine inayochelewesha suala hilo ni Chadema kutotaka kumtangaza mgombea wake kutokana na mchakato wake wa uteuzi wa mgombea urais kutoanza. Mchakato huo utaanza Julai 20 na kumalizika Julai 25, siku ambayo CUF itakuwa na kikao chake cha Baraza Kuu kuamua mgombea urais.Habari zinasema kuwa Chadema imekuwa ikisisitiza kuwa Ukawa itaje jina la chama kitakachotoa mgombea urais na si jina la mwanachama atakayegombea nafasi hiyo.Habari hizo zinaeleza kuwa chama hicho kinachoongoza kambi ya upinzani, kinadai kuwa Ukawa kutangaza jina la mwanachama atakayegombea urais ni kuingilia mchakato wa Chadema ambao humalizika kwa kikao cha juu kupitisha mgombea urais wa chama.Awali baada ya kuchukua fomu ya kugombea urais kwa tiketi ya CUF, Profesa Lipumba alikuwa akisema kwenye mikutano ya hadhara kuwa vyama hivyo vinne vimekubaliana kuwa kila kimoja kifanye mchakato wake wa kupata mgombea. Alisema kila chama kitalazimika kupeleka Tume ya Uchaguzi (NEC) jina la mgombea wake ili kiwe na uhakika kuwa amepitishwa halafu ndipo vikutane na kuamua mmoja atakayeungwa mkono na vyama vyote.magazeti ya Tanzania yote sehemu moja. Read Tanzania News Headlines here. -
http://millardayo.com/Stori zote kwenye
Magazeti ya Tanzania July 18 2015 >>> Udaku, Michezo na Hardnews niko nazo hapa. Good morning mtu wa nguvu.. millardayo.com huwa ... - http://www.mwananchi.co.tz/Skip to the navigationchannel.links.navigation.skip.label. Skip to the content. MCL Blog | Daily Nation | NTV | Business Daily | The East African | Daily Monitor ...
-
http://www.mjengwablog.com/
Magazeti ya Leo.Magazeti ya leo. BOFYA HAPA KUISOMA. Matangazo Mapya. Website Design · Huduma. We provide the full IT solutions including web design ...
Jumamosi, 18 Julai 2015
magazeti ya leo tar 18/07/2015
-
http://www.magazetini.com/Soma vichwa vya habari vya
magazeti ya Tanzania yote sehemu moja. Read Tanzania News Headlines here. -
http://millardayo.com/Stori zote kwenye
Magazeti ya Tanzania July 18 2015 >>> Udaku, Michezo na Hardnews niko nazo hapa. Good morning mtu wa nguvu.. millardayo.com huwa ... - http://www.mwananchi.co.tz/Skip to the navigationchannel.links.navigation.skip.label. Skip to the content. MCL Blog | Daily Nation | NTV | Business Daily | The East African | Daily Monitor ...
-
http://www.mjengwablog.com/
Magazeti ya Leo.Magazeti ya leo. BOFYA HAPA KUISOMA. Matangazo Mapya. Website Design · Huduma. We provide the full IT solutions including web design ...
Ijumaa, 26 Juni 2015
Mwanafunzi chuo kikuu mkwawa kugundua dawa ya ukimwi, je kunani?
Wanafunzi wa chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa wamegundua dawa ya Maradhi ya Ukimwi, wamedai hadi sasa mtu mmoja Kapona. Ni wanafunzi wa Kitivo cha Sayansi chuoni hapo, nini maoni yako katika ugunduzi huu?
je unadhani kiunahaja ya kuendelezwa kama mataifa ya ulaya?
tanzania ni nchi nyenye watafiti wengi lakini changamoto ni ukasumba wa tasisi husika kushindwa kuwatumia
TUPE MAONI YAKO HAPA NINI KIFANYIKE, KUPITIA misaelkikoti11@yahoo.com
Wanafunzi waunda kondomu inayotambua magonjwa ya zinaa
Wanafunzi katika shule moja nchini Uingereza wameunda mipira ya kondomu inayowaonya watumiaji wanapojamiana na mtu aliyeambukizwa maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo inabadili rangi pindi inapokutana na majimaji ya mtu anayeugua maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
Kulingana na wanafunzi hao kondomu hiyo inabadili rangi tofauti kulingana na bakteria iliyopo.
Uvumbuzi huu ni wa Daanyaal Ali, 14, Muaz Nawaz, 13 na Chirag Shah, 14, ambao ni wanafunzi katika shule ya Isaac Newton Academy iliyoko Ilford, Essex, nchini Uingereza.
''tuliazimia kumpa onyo mtumiaji wa mipira hii kuwa mpenzi wake yuko salama ama ni mgonjwa bila ya wasiwasi wa kupimwa hospitalini''.
Wanafunzi hao tayari wametunukiwa, tuzo la ubunifu la ''the TeenTech'' .
Daanyall alisema kuwa "Walizindua kondomu hiyo ilikuifaidi kizazi kijacho''
''Kwa hakika swala la usalama wa mpenzi wako ni swala la kibinafsi kwa hivyo ni swala linalopaswa kupewa kipaombele haswa ikifahamika kuwa tunawajibu wa kuchochea ngono salama bila ya kuwashurutisha wapenzi wetu kufika hospitalini bila wao wenyewe kukusudia''
Wanafunzi hao waliwalitunukiwa pauni elfu moja pamoja na fursa ya kuzuru Kasri la Malkia wa Uingereza Buckingham Palace.
Muasisi wa kampuni ya ubunifu wa kiteknolojia, TeenTech, Bwana Maggie Philbin, alisema kuwa
"Ni wajibu wetu kama jamii kuchochea ubunifu unaopatikana madarasani kuchochewa na kupigwa msasa kwa minajili ya kuboresha maisha ya mwanadamu'
Joseph Mbilinyi ‘ Anena Bungeni
Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alivyosimama na maneno yake Bungeni baada ya ishu ya mtoto wake kuzungumzwa.
Kwenye
kilichosikika jana June 25 2015 toka ndani ya Kikao cha Bunge Dodoma
ilikuwepo pia ishu ya Mbunge Martha Mlata kuanzisha mjadala kuhusu amri
ya Mahakama kwamba Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi Sugu
akabidhiwe mtoto wake ambae amezaa na Faiza Ally kutokana na Mbunge huyo
kuonekana kutoridhwishwa na malezi ya mtoto akiwa kwenye mikono ya mama
yake.
Ombi likapokelewa kwenye meza ya Naibu Spika leo June 26 2015 >>>”Nimepokea ombi maalum la kuwasilisha maombi binafsi kutoka kwa Mbunge Joseph Mbilinyi kwa hiyo namruhusu” >>> Naibu Spika Job Ndugai.
“Asante
sana Naibu Spika, naomba nitoe maelezo binafsi jana tarehe 25 June 2015,
Mbunge Martha Mlata alidai kuwa kuna Mbunge wa CHADEMA amempora
mwanamke mmoja mtoto mdogo wa miaka miwili na amempora wakati Mbunge
huyo amekuwa hatoi matunzo kwa mama yake… Mlata aliwataka Wabunge wote
wanawake kuungana kukemea kitendo alichodai kimefanywa na Mbunge huyo”
“Hakutaja
jina la Mbunge aliyemhusisha na madai yake ila alidai kuwa ni msanii
mwenzake… hata hivyo alitaja jina la mwanamke anayedaiwa kunyang’anywa
mtoto kuwa ni Faiza. Mbunge aliyelengwa na mashambulizi ni mimi Joseph
Osmond Mbilinyi, mimi ndiye baba wa mtoto Sasha Desderia Mbilinyi
anaedaiwa kuporwa kwa mama yake, na Faiza aliyetajwa ni Faiza Abdallah
Ally ambaye ni mzazi mwenzangu na mama mzazi wa Sasha Desderia“
“Watu
wazima hawapendelei kuzungumzia mambo binafsi hadharani… Nadhani
sitakosea kusema hata Mheshimiwa Martha mwenyewe asingependa kuzungumzia
matatizo yaliyopelekea ndoa yake kuvunjika“
“Mimi ni
mmoja wa watu wazima wenye akili timamu ndio maana sijazungumzia
hadharani kuhusu uhusiano wangu na mzazi mwenzangu Faiza Ally na mtoto
wetu Sasha… Sasha ameishi na mama yake tangu alipozaliwa mwaka 2012,
katika kipindi chote nimempelekea mama yake laki tano kila mwezi,
nimemlipia ada ya shule Milioni 3 kila mwaka.. Mlata kama angekuwa
anataka kujua angeniuliza ningempatia taarifa hizi kabla hajarusha
tuhuma nzito“
“Mwanamke
anayedaiwa kuwa mnyonge anajulikana katika kumbi za starehe nchi nzima,
picha zake zilisambazwa katika Mitandao ya Kijamii na kuleta fedheha
kubwa kwa watu wanaojali maadili ya mavazi, picha zake nyingine akiwa
amevaa diapers zilisambaa mitandaoni na Martha Mlata angeweza kupata
ukweli wa mambo haya kabla hajarusha tuhuma mbele ya Bunge“
“Nilienda
Mahakama ya Mwanzo Manzese, niliwasilisha ushahidi kwamba mzazi
mwenzangu asingeweza kumlea mtoto.. Mahakama ilimwita akajitetea, June
23 Mahakama iliridhika na ushahidi wangu, ikaamua mtoto akabidhiwe
kwangu ili nimlee. Kilichodaiwa kuwa ni uporaji wa mtoto kiukweli ni
amri ya Mahakama, Mlata hakuwahi kuonekana Mahakamani, nina mashaka hata
kama anamfahamu mtoto mwenyewe au mama anayemwita mwanamke mnyonge“
“Mashauri
haya hayakupaswa kuwekwa hadharani kama alivyofanya Martha Mlata…
Nimesikitishwa na Martha Mlata kuzungumza mambo binafsi. Pamoja na
Mahakama kunipa haki, mtoto bado yuko kwa mama yake kwa sababu mimi ni
mstaarabu… nimetoa nafasi ili Majadiliano ya kifamilia yafanyike… Naomba
mjadala huu usiendelee zaidi ya hapa”
Jumatano, 24 Juni 2015
Ijumaa, 19 Juni 2015
Mamlaka ya Mji Mdogo Ilula
Na waandishi wetu, Longo na Kikoti
kata ya Ilula inamitaa ya Ilula-Itund, Masukanz, Igunga, Ikokoto, Madizini.
kata Nyalumbu ina mitaa ya Ilula-Mwaya,Ikuvala, Mtua, Ding'inayo, Ngelango, Ilula Sokoni,
Itabali,Matalawe
kata ya Mlafu ina mitaa ya Mlafu,Isagwa,Itungi
MATATIZO YANAYOUKUMBA MJI MDOGO WA ILULA
Tatizo la maji
Maji ni uhai na maji yana matumizi mengi katika maisha ya kila siku ya binadamu,
wanyama na hata viumbe vingine hai,ikiwemo mimea.Lakini kwa wakazi wa
Mji Mdogo wa Ilula uliopo Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, upatikanaji
wa maji kwao ni kitendawili cha miaka mingi sasa kwani ni tatizo sugu.
Ilula ni mji unaosifika kwa biashara mbalimbali hususan zao la nyanya na
vitunguu, hali inayoufanya uwe na mkusanyiko mkubwa wa watu kutoka
maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi wanaokwenda kwa shughuli
za kilimo na biashara.
Sababu za uhaba wa maji ilula
- kuongezeka kwa kasi kwa idadi ya watu ukiringanisha na miundo
mbinu ya maji iliyopo katika-mji huo, pia suala la ubovu wa miundo
mbinu ya maji imeonekana ni tatizo kwani mingi imeharibika na-
hakuna jitihada zozote za kuirekebisha .
- pia sababu inayochangia uhaba wa maji katika mji huu ni-
pamoja na uharibu wa vyanzo vya maji; hasa katika chanzo
cha idemule.
je jitihada gani zimechukuliwa na serikali?
Serikali imejitahidi kuboresha miundombinu ya chanzo cha Idembe,
na imeanza kufanya upembuzi wa-awali ili kutumia vyanzo mbadala
vya mto Mgombezi na milima ya Selebu na kuchimba visima vingi
vya maji katika mji huo. akizungumza na wananchi waziri wa maji
alisema Profesa Maghembe wizara yake imekwishatoa Sh Milioni -
150 na itaongeza nyingine Sh Milioni- 150 ili kuboresha miundombinu-
ya chanzo cha Idembe.
Tatizo jingine ni miundombinu ya barabara za mitaani.
barabara za mitaani katika mji huu wa ilula bado ni tatizo kubw
hasa katika maeneo ya mtua, sokoni na isele na hii inatokana na
kutokuwepo mipango yakinifu iliyoweka na serikali ili kuzuia
wanajamii kujenga katika maeneo hayo ambayo barabara za
mitaani zinapaswa kujengwa, hivyo kusababisha hatari kumbwa
hasa kwa wananchi ikiwa hatari ikitokea kama ajari ya moto,
uwepo wa wagonjwa wanaohitaji msaada wa gari inakuwa ni
tatizo kwani hakuna barabara zinazoruhusu- magari kupita
kwa urahisi.
Je serikali imefanya jitihada gani?
suala la barabara za mitaani linaonekana kuendelea kufumbiwa-
macho, licha ya baadhi ya mitaa hasa Majengo mpya serikali
kutengeneza barabara ili kuzuia wanaojenga wasijenge lakini
wanashinda kutatua changamoto ya sehemu ambazo tayari
watu wameziba barabara hizo za mitaani.
Je ungekuwa we ungeshauri nini?
Sheria za barabara za mitaani zinatambulika vizuri, kwa hiyo;
ni vizuri serikali ikachukua hatua mapema kwa kuangalia
watu waliojenga maeneo hayo ya hifadhi za barabara za
mitaani na kuwachukulia hatua, na kama serikali ilifanya
makosa katika ugawaji wa maeneo bila kuacha maeneo
ya hifadhi ya barabara itafute njia ya kupata ramani
ambapo barabara zinatakiwa kupita na kulipa fidia
kwa jamii itakayoathirika na zoezi la upitishaji wa
barabara za mitaani ilula.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)