ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Jumatano, 30 Machi 2016

Breaking news: Ajira za walimu kutolewa baada ya bajeti kupitishwa

 

Waziri wa TAMISEMI amesema ajira mpya za walimu mwaka huu zitatoka pale bajeti hiyo itakapopitishwa ili kuepuka usumbufu ameyasema hayo alipokuwa katika mahojiano na clouds tv leo tar 30/03/2016

Jumamosi, 26 Machi 2016

Kificho ang’oka uspika

ALIYEKUWA Spika wa Baraza la Wawakilishi kwa zaidi ya miaka 20 sasa, Pandu Ameir Kificho, ameng’olewa katika nafasi hiyo baada ya kushindwa katika kura za kuwania awamu nyingine ya uongozi wa baraza hilo.
Badala yake wajumbe wateule wa Baraza la Wawakilishi, wamemchagua Zubeir Ali Maulid, kuwa Spika mteule wa baraza hilo, baada ya kupata kura 55 na kumuacha kwa mbali Kificho aliyeambulia kura 11 katika uchaguzi uliofanyika jana katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar.
Aidha katika uchaguzi huo ambao wawakilishi 72 walipiga kura, Janeth Nora Sekihola ambaye ni hakimu mstaafu akipata kura 4 wakati kura mbili ziliharibika.
Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuangushwa katika uchaguzi huo, Kificho alisema amekubali kushindwa na yupo tayari kutoa ushirikiano akitakiwa kufanya hivyo.
“Hiyo ndiyo demokrasia, nimekubali kushindwa na nipo tayari kutoa ushirikiano mkubwa nikitakiwa kufanya hivyo kwa sababu ni ukweli kwamba ninao uzoefu mkubwa katika nafasi hiyo kwa zaidi ya miaka 20,” alisema.
Naye Spika mteule wa baraza hilo, Maulid alisema anakabiliwa na changamoto kubwa ya kuleta maendeleo na mabadiliko makubwa katika chombo hicho ambacho ni moja ya mihimili ya dola katika utekelezaji wa majukumu yake.
Amesema atatumia uzoefu alioupata kufanya kazi katika taasisi za kutunga sheria, kwa ajili ya kuleta mabadiliko hayo kwa kuhakikisha kwamba Baraza la Wawakilishi linafanya kazi inayotakiwa ya kuisimamia Serikali kwa mujibu wa Katiba.
“Nimekuwa Mwakilishi Shauri Moyo na Waziri mwaka 2000, pia nimekuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa miaka miwili na nusu kwa hivyo uwezo wa kufanya kazi katika mabunge ya Jumuiya ya Madola ninao mkubwa,” alisema.
Aliwaomba wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wateule kumpa kila aina ya ushirikiano utakaomwezesha kutekeleza na kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba, kwani chombo hicho ni moja ya mihimili ya dola.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliozungumza na gazeti hili, wamesema kwamba mabadiliko hayo ni ishara na ujumbe tosha kwa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kwamba wawakilishi wanataka mabadiliko makubwa kwa Serikali kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
“Mabadiliko makubwa tuliyoyafanya sisi wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa kumchagua Zubeir Ali Maulidi kuwa Spika mteule mpya, ni dalili tosha kwamba sasa tunataka mabadiliko makubwa ndani ya Serikali kwa kuwa na viongozi watakaowatumikia wananchi moja kwa moja,” alisema Rashid Ali Juma mwakilishi mteule wa jimbo la Amani.
Kificho ameweka historia kuwa Spika wa Kwanza katika Baraza la Wawakilishi la mfumo wa vyama vingi kuanzia mwaka 1995, ambapo kabla ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo, alikuwa mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi kuanzia 1988.
Zubeir Ali Maulid mwaka 2000 alichaguliwa kuwa Mwakilishi wa Shauri Moyo kwa tiketi ya CCM na kuteuliwa kuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, chini ya Serikali ya Rais mstaafu Amani Abeid Karume, ambapo alidumu katika wadhifa huo kwa miaka mitatu.
Mwaka 2005, Zubeir alichaguliwa kuwa Mbunge wa Kwamtipura kwa tiketi ya CCM ambapo akiwa bungeni katika kipindi cha miaka miwili na nusu, alikuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na kuongoza vikao mbali mbali kwa kusaidiana na spika na naibu spika.
Katika hatua nyingine, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein, amemteua Said Hassan Said, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Uteuzi huo ndio wa kwanza kufanyika, tangu Rais Shein alipokula kiapo cha kuongoza Zanzibar kwa miaka mitano ijayo Alhamisi ya wiki hii.

Jumanne, 22 Machi 2016

Ukawa kidedea Umeya wa jiji la Dar es Salaam

by kikoti blog




UCHAGUZI wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam ambao unaendele kufanyika muda huu katika ukumbi wa Kareemjee taarifa za ndani kutoka katika uchaguzi huo zimeeleza kuwa mgombea wa vyama vya UKAWA, kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  Mh. Isaya Mwita ameibuka kidedea kwa kupata kura 84 huku CCM wao wakipata kura 67 na kati ya jumla ya kura hizo 7 ziliaribikaambapo jumla ya kura za wajumbe wote ni 158.
Umeya jijiHali ilivyo muda huu ndani ya uchaguzi huo wa Umeya wa Jiji la Dar es Salaam muda huu leo Machi 22.2016, ambapo UKAWA wameibuka kidedea
DSCN3491 
Mhe. Issaya Mwita (mbele)  ambaye hadi sasa vyanzo vya ndani kutoka uchaguzi huo ameweza kupata kura 84 dhidi ya mshindani wake kutoka CCM ambaye alipata kura 67 huku kura 7 zikiharibika, hivyo kuibuka na ushindi wa Umeya wa Jiji. (Picha ya Maktaba).

Jumatatu, 21 Machi 2016

walimu wapya kwa mwaka 2016 wapewa mtihani na TAMISEMI

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEic6vbqzF0JJL9QfkTbpK_Xwtwpaf65r_pwIRgw2HphXih_46gKNnnFwdW-GQ79r8JjAPMg9jxEAQwEO9wWuJ91v8ipEE0qGVv9-I1qB2-7UKtKu3JHpAGUl0BJbXMhyqZuhNmNddjVr4Hf/s1600/1350.jpg
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, George Simbachawene ametangaza leo March 21, 2016 kuwashughulikia wale wote wanaofanya hujuma katika sekta ya elimu nchini, wakiwemo Walimu wanaokimbia sehemu zao za kazi hususani vijijini na kukimbilia mijini.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari leo March 21, 2016 alisema…‘Katika eneo la upangaji wa Walimu ni tatizo kubwa na nadiliki kusema hadharani kwamba upangaji wa walimu kwenye  shule zetu ni wa ovyo leo hii tunaupungufu wa ualimu kwenye vijiji kwa  asilimia zaidi ya 40%  na ongezeko  la walimu mijini ni kama asilimia 50%  kwa   maana ya kwamba walimu wengi wapo Dar es Salaam, walimu wengi wapo kwenye miji mikubwa makao makuu ya mikoa na makao makuu ya wilaya’George Simbachawene
‘Hata wanawake wanasema wanafuata wanaume zao huko ni  kukosa uzalendo kama ulikubali kuajiliwa lazima ukubali kufanya kazi mahala popote pale na watanzania ni wote mpaka waliopo kule vijijini haiwezekani kukubali kazi mjini na kukataa kijijini’George Simbachawene
kwa tafsiri hii ya waziri wa TAMISEM hakutokuwa na sababu zzisizona msingi zitakazokubalika kwa walimu wapya kwa mwaka 2016

Jumapili, 20 Machi 2016

TATIZO LA MAJI KATIKA MJI MDOGO WA ILULA KUISHA KABLA 2020

 MBUNGE  wa   jimbo la  Kilolo  Venance  Mwamoto ameahidi kuongozana na  wazee  wa mji  wa Ilula kwenda Dodoma kuonana na   waziri  mkuu Kassim Majaliwa  ili  kumfikishia ahadi ya  maji ya Rais Dr John Magufuli kwa  wananchi  wa mji  mdogo  wa Ilula .
  https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEganogblP_gVCgRkG9WDNjiGmgaKAifYWmTa2QBjcrUK3DmNOKvT2dQlSyKamiQbpJZcmDhxihrAM2_xHTsKYSRWFBdFoq4h51s2_Pi4txRVupOtV59XeiXS6613jzzTHtGGiQD7z7auNM-/s640/DSC_0972.JPG


Huku  akiwataka wananchi wa Ilula na Nyalumbu  kutomchagua mwaka 2020  iwapo atashindwa  kutekeleza ahadi ya maji katika mji  huo wa Ilula ndani ya  miaka  yake  mitano ya  ubunge.

Akizungumza  na  wananchi  wa kata ya  Nyalumbu na Ilula  wakati wa  mikutano yake ya  hadhara ya  kuwashukuru  wananchi  wake kwa kumchagua  kuwa mbunge wa  jimbo  hilo la Kilolo jana ,Mwamoto  alisema  kuwa  kero ya maji katika  mji wa Ilula  imekuwa ya muda murefu   jambo ambalo hatataka   kuona   wananchi  hao  wakiendelea kutabika.

Alisema  kuwa   kero hiyo  ya maji imeanza  kuwasumbua  wananchi hao toka nchi ipate  uhuru  wake mwaka 1961  hadi  leo wapo katika mahangaiko ya maji na  baadhi ya  viongozi  wameendelea  kufanya udanganyifu  wa mradi huo kama  ambavyo   mwaka 2010   viongozi  walivyomdanganya aliyekuwa makamu  wa Rais Dr Alli Mohamed  Shein  kwa  kupelekwa  kufungua  mradi wa maji ambao  viongozi  walimdanganya kwa  kujaza maji katika tanki hilo  ili azindue mradi huo.

Hivyo  alisema udanganyifu  huo hautapewa nafasi katika uongozi  wake wa miaka  mitano  lazima kero  hiyo imalizike na  wananchi hao  waweze kupata maji vinginevyo yupo tayari  kuongoza  wananchi  wake kumzuia waziri wa maji kupita Ilula kwenda jimboni kwake Njombe  iwapo  wananchi hao hawatatimiziwa ahadi yao ya maji  safi na salama .

Mbunge  huyo  alisema katika  kikao kijacho cha  bunge kinachoanza mwezi ujao ataomba  wananchi wa Ilula na Nyalumbu  kumteulia wazee watatu ama  wanne   ili kwenda nao bungeni Dodoma  kukutana na  waziri  mkuu ili  kwa ajili ya kumkumbusha ahadi ya Rais ya  maji katika mji  huo wa Ilula .
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhk7WxKewRYdjXwD8lX3crGfa8nBIOAo3SsF0Kg3ruaxfxMEciqaadCRdkopWqNhM03AgYUs8RsDLs9MZqzgf0JjCn8Pxy6UW5N8Q5pK1yZIREUxEtkSekyqD51VvReeSLegJODpoNpmcxU/s640/DSC_0966.JPG

Pia  aliagiza mamlaka ya maji ya mji  mdogo wa Ilula  kuchunguza vema mradi wa maji uliopo kama umejengwa kwa kiwango ama chini ya kiwango maana amesema mradi mdogo  uliopo kwa  sasa  bado umekuwa na kero  kubwa ikiwa ni pamoja na baadhi ya maeneo kuvujisha maji  huku  akiwataka  wananchi kwa  upande  wao kutunza miundombinu ya maji.

Mbunge wa Kilolo Bw  Venance Mwamoto (kushoto)  akisalimiana na mmoja kati ya  wazee wa mji wa Ilula  aliyetoka  kuchota maji


 

Katika  hatua nyingine  mbunge Mwamoto  alimshauri meneja wa maji wa IRUWASA katika mji wa Ilula Teodolah Mvungi  kuangalia uwezekano wa  kuboresha kituo  cha maji eneo la Ilula  ili  kiweze  kunufaisha  wananchi  wengi  na  kuwa iwapo wataanza uboreshaji kwa upande wake ataunga mkono .

Dr Shein aongoza wazanzibar katika kupiga kura, Uchaguzi wa Marudio Zanzibar

Wananchi wa Zanzibar leo wanapiga kura katika uchanguzi wa marudio baada ya kufutwa kwa uchanguzi uliofanyika October 25,2025 kutokana na kasoro zilizojitokeza.

Katika baadhi ya vituo wananchi wamejitokeza na zoezi linaendelea vizuri huku hali ya usalama ikiwa imeimarishwa.

Katika kituo cha shule ya sekondari Muembeladu ambayo ina vituo sita,vituo vitano vinawatu 350 na kituo kimoja kina watu 91. Akizungumza na wanahabari, msimamizi wa kituo hicho amesema zoezi la upigaji kura linaendelea vizuri katika jimbo la Jangombe .

Kwa upande wa kituo cha skuli ya Muembeshauri nako hali ni shwari na zoezi linaendelea vizuri ambapo katika skul hiyo vituo 11 vinatumika watu kupiga kura.
Katika Jimbo la kikwajuni, zoezi  linaendelea vizuri huku mwitikio wa watu ukiwa ni mkubwa.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kupiga kura wamesema zoezi hilo limekua rahisi na la  amani tofauti na taarifa zilivyokua zinasambazwa.

Mkazi wa Muembeshauri aliyejitambulisha kwa jina la Hamidu Salum Haji ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kwani zoezi la kupiga kura linaendelea kwa amani na utulivu.

Ndugu zangu tusikubali kugombanishwa na watu ambao hawaitakii mema Zanzibar tusimame pamoja katika kutetea nchi yetu” amesema Haji
 
Wakati zoezi hilo linaendelea maduka mengi yamefunguliwa na wafanyabiashara wanaendelea na kazi kama kawaida
Rais wa Zanzibara na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Ali Mohammed Shein leo amepiga kura katika kituo cha skuli ya bungi
5607497e-aa8a-46b6-9e65-24e5da213e24
9c703d6a-0f99-42ea-a17d-935d411e8f87
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, amepiga kura katika kituo cha skuli ya Kiembe samaki
36086a57-dbef-464f-8d12-ae3b207940ab


Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar Dkt Ali Mohammed alizungumza na wanahabari baada ya kupiga kura yake katika kituo cha Bungi, Kibera kisiwani Unguja  ambapo alisema anaamini atashinda kwa kishindo na kuhusu kushindwa  alisema tusubiri matokeo ya uchaguzi ndiyo yataamua.
"Nimepata nafasi ya kupiga kura kama haki yangu ya  kimsingi na kumekuwa na utulivu mkubwa kwenye zoezi hili,hali ya ulinzi imeimarishwa. 
"Matumaini yangu ni kushinda kwa kishindo, kuhusu kushindwa ndugu muandishi tusubiri matokeo ndiyo yataamua".Alisema Dkt. Ali Mohammed Shein

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd amepiga kura katika kituo cha skuli ya Kitope
46bee29d-6ade-49ea-9377-a3a692b33b12
670502cb-700e-47f1-b9e9-fa44bea0f2db

Jumapili, 13 Machi 2016

Dk. Vicent Mashinji ndiye Katibu Mkuu Chadema

Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema
Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chadema
DAKTARI Vicent Mashinji ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema, katika kikao chake kilichokaa jijini Mwanza, anaandika Mwandishi Wetu.
Katika Kikao hicho cha Baraza Kuu, Freeman Mbowe alitangaza jina la Dk. Mashinji na kuungwa mkono na wajumbe wa baraza hilo, hivyo anajaza nafasi iliyoachwa na Dk. Willibrod Slaa, aliyejienguwa ukatibu mkuu wa chama hicho.
Jina la Dk. Machinji halikuwa miongoni mwa wanachama wa Chadema ambao walikuwa wanatarajiwa kumrithi Dk. Slaa kwani waliokuwa wanatabiriwa kukatia kiti hicho ni Salum Ally Mwalimu, Frederick Sumaye, Benson Kigaila, John Mnyika, Dk. Marcus Albanie na Prof. Mwesiga Baregu.
Nafasi ya Katibu wa Chadema ilikuwa wazi tangu Dk. Slaa alipoondoka Chadema muda mfupi baada ya chama hicho kumpitisha Edward Lowassa aliyetokea CCM kuwa mgombea urais wa chama hicho na kuungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Wasifu wa Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Vincent B. Mashinji
Professional experience
Clinical Advisor & TB/HIV lead
UMSOM-IHV
July 2008 – Present
ART Program Doctor/IMA team lead
IMA Worldhealth
August 2006 – June 2008 (1 year 10 months)
Medical Officer/Anaesthesiology
Regency Medical Centre
October 2005 – August 2006 (10 months)
Medical Officer
Muhimbili National Hospital
August 2003 – October 2005 (2 years 2 months)
Research Assistant
Freelance
November 2002 – August 2003 (9 months)
Intern Docor
Muhimbili National Hospital
September 2001 – October 2002 (1 year 1 month)
Education history
Open University of Tanzania
PhD
August 2010 – Present
AMREF/UCLA Anderson School
MDI Certificate
April 2010 – April 2010
Blekinge Institute of Technology
MBA
September 2007 – March 2010 (2 years 6 months)
UMSOM-IHV
IPEP Certificate
May 2008 – May 2008
Evin School of Management
Certificate in CSR
October 2005 – October 2005
Muhimbili University College of Health Sciences
MMed/Anaesthesiology
September 2003 – April 2005 (1 year 7 months)
Muhimbili University College of Health Sciences
Certificate in Research Methodology
September 2004 – September 2004
Makerere University
MBChB
October 1995 – July 2001 (5 years 9 months)
Mzumbe High School
ACSEE
July 1992 – June 1994 (1 year 11 months)
St. Pius X Seminary, Makoko
GCSEE
January 1988 – October 1991 (3 years 9 months)
Iligamba Primary School
Leaving Certificate/Primary School
January 1981 – October 1987 (6 years 9 months