Alhamisi, 16 Februari 2017
Jumatano, 15 Februari 2017
Jumanne, 14 Februari 2017
HONGERA WALIMU WA NYALUMBU SEKONDARI
Na Mwandishi wetu,
Katika makala yetu ya leo tunapenda kuwapongeza walimu, wanafunzi na wafanyakazi wote wa shule ya sekondari Nyalumbu inayopatikana wilaya ya kilolo katika mji mdogo wa ilula katika kata ya Nyalumbu Kwa mafanikio yao mema katika kutoa elimu.
Kwa
fursa hii, mwandishi wetu ameamua kuwapongeza na kuwatakia kazi
njema yenye kuwa mfano, yenye kuleta tija na ustawi katika taaluma
na maendeleo kwa ujumla.
Tunaamini, ingawaje mnakumbana na changamoto mbalimbali , bado mchango na jitihada zenu katika taaluma zimeonekana ndani na nje ya wilaya ya kilolo.
Sanjari na kuwapongeza walimu wote katika shule hiyo, pia mwandishi wetu anawaasa walimu wengine kutoka shule nyingine kama shule ya sekondary kiheka iliyoweza kuwa miongoni mwa shule mbili za mwisho kimkoa kuiga mfano huu na kujifunza namna walimu wa shule hii walivoweza kufanikiwa kupata ufaulu mzuri katika mitihani yao.
Tunaamini ufanisi huu unaooneshwa na shule hiyo unastahiri pongezi na motisha, na hasa wilaya kutazama namna yakuwapongeza walimu hawa ili kuleta hamasa ya ushindani zaidi.
Tunaamini, ingawaje mnakumbana na changamoto mbalimbali , bado mchango na jitihada zenu katika taaluma zimeonekana ndani na nje ya wilaya ya kilolo.
Sanjari na kuwapongeza walimu wote katika shule hiyo, pia mwandishi wetu anawaasa walimu wengine kutoka shule nyingine kama shule ya sekondary kiheka iliyoweza kuwa miongoni mwa shule mbili za mwisho kimkoa kuiga mfano huu na kujifunza namna walimu wa shule hii walivoweza kufanikiwa kupata ufaulu mzuri katika mitihani yao.
Tunaamini ufanisi huu unaooneshwa na shule hiyo unastahiri pongezi na motisha, na hasa wilaya kutazama namna yakuwapongeza walimu hawa ili kuleta hamasa ya ushindani zaidi.
Tunawapongeza sana utawala wa shule akiwemo Mkuu wa shule(Myinga), makamu mkuu wa shule, walimu wa taaluma(mwl mwangonela J, na mwl Shonde) kwa kuweza kuongoza walimu wenu kufanya kazi nzuri ya kufundisha bila hata kuzembea tunaamini ukiwa mtawala ni Adui wa wasiofuata sheria endeleeni kufanya kazi kwa weledi huo.
Pia kabisa tunawapongeza walimu wote kutoka Shule ya sekondari Nyalumbu kwa kuonesha ushupavu wa hali ya juu katika ufundishaji na hata kutumia muda wenu wa ziada kutoa elimu kwa wanafunzi.
Na mwisho wanafunzi wetu kwa jitihada zenu katika masomo yenu nikiwaona wanafunzi wa shule ya sekondari Nyalumbu wamejengwa katika mazingira ya kusoma na siyo kucheza, wafundisheni wanafunzi wenzenu namna ya kusoma ili waweze kufaulu vizuri
"mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni bila kuficha ukweli"
"mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni bila kuficha ukweli"
Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa
Hali
ya ulinzi imeimarishwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)
alikolazwa mfanyabiashara Yusuf Manji baada ya kuugua ghafla akiwa
polisi alikokuwa akihojiwa.
Manji
aliyekuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa
alipelekwa hospitalini hapo juzi jioni akiwa ndani ya gari la wagonjwa
aina ya Toyota Land Cruiser lenye nembo ya Shirika la Umoja wa Mataifa
la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) huku gari lake aina ya Range Rover
likifuata kwa nyuma.
Askari
wenye sare na wengine wakiwa na mavazi ya kiraia nje ya wodi aliyolazwa
mwenyekiti huyo wa klabu maarufu nchini ya Yanga walionekana
wakiimarisha ulinzi.
Ilipofika saa 4:13 asubuhi mfanyabiashara huyo alitoka kwenye chumba hicho na kuongozwa kuelekea upande mwingine wa jengo hilo.
Akiwa amevalia nguo za wagonjwa zenye rangi ya kijani, Manji alitembea taratibu kuelekea upande aliokuwa akielekezwa.
Alipoulizwa
kuhusu uwapo wa Manji hospitalini hapo, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI,
Profesa Mohamed Janabi alisema hawezi kuzungumzia taarifa za mgonjwa.
Februari
8, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitoa orodha ya watu
65, akiwamo Manji ambao aliwataka wafike Polisi kwa ajili ya mahojiano
kuhusu masuala ya dawa za kulevya.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)