ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Alhamisi, 16 Machi 2017

WIZARA YA ELIMU YAPOKEA VIFAA VYA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU.

KONTENA LENYE KEMIKALI KWA AJILI YA MASOMO YA KEMIA NA BIOLOJIA TAYARI KWA AJILI YA KUSAMBAZWA.
Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya leo amepokea vifaa vya wanafunzi wenye  mahitaji maalumu vyenye thamani ya Shilingi bilioni 3.6 ambavyo vinalenga  kutatua changamoto ya upungufu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia .

Akizungumza wakati wa makabidbiano hayo, mhandisi Manyanya amesema baadhi ya vifaa Vilivyopokelewa leo ni pamoja na mashine za kuandika maandishi ya nukta nundu 932,  karatasi za kuandikia maandishi ya nukta nundu ream 2548,karatasi ya kurudufishia maandishi ya nukta nundu ream 1150,shime  sikio ( hearing Aid) 1150, vifaa vya upimaji kielimu.

Naibu waziri manyanya amewataka maafisa Elimu nchini kote  kuhakikisha walimu waliopata mafunzo ya watu wenye mahutaji maalumu wanakwenda kufundisha katika shuke hizo na si vinginevyo.

Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Kesi Ya Kuzuia Uchaguzi TLS


Mahakama Kuu imetupilia mbali kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na Wakili Onesmo Mpinzila pamoja na mambo mengine akipinga Kanuni za Uchaguzi za Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) za mwaka 2016.

Kesi hiyo imetupiliwa mbali baada ya Mahakama kukubaliana na hoja za mapingamizi ya TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambao ndio waliokuwa wadaiwa katika kesi hiyo.

Hoja hizo ambao Mahakama imekubaliana nazo ni pamoja na kwamba mdai hakuwa na mamlaka kisheria kufungua kesi hiyo na kwamba hati yake ya kiapo kilichokuwa kikiunga mkono madai yake ilikuwa na kasoro za kisheria.

Uamuzi huo umesomwa na Jaji Ignasi Kitusi kwa niaba ya jopo la majaji watatu waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo. Majaji wengine walikuwa ni Rose Teemba(kiongozi wa jopo) na Beatrice Mutungi.

Tundu Akamatwa Na Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma

Mbunge Tundu Lissu amekamatwa na jeshi la polisi asubuhi hii nyumbani kwake na kupelekwa ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma.
 
==>Huu ni Ujumbe wa Tundu Lissu alioutumia mtandaoni
Wandugu wapendwa. Ninaandika haya nikiwa nyumbani kwangu Dodoma. Najiandaa kwenda mahakamani kwa ajili ya uamuzi wa Mahakama Kuu juu ya kesi ya kutaka kuzuia Uchaguzi wa TLS.

Ninawapa taarifa kwamba nimefuatwa nyumbani na askari wawili kutoka ofisi ya RPC Dodoma. Sijazungumza nao bado lakini ni wazi wana maagizo ya kunikamata na kunizuia kuja Arusha kwenye Uchaguzi wa TLS. Wameshindwa kuzuia uchaguzi wetu mahakamani. Sasa, kama kawaida ya serikali za kidikteta kila mahali, wanatumia mabavu ya kijeshi.

Wito wangu kwenu mawakili wa Tanzania:
Nendeni Arusha mkachague viongozi wa TLS watakaopigania haki za binadamu, utawala wa sheria na demokrasia. Msipofanya hivyo hakuna mtu yeyote, hata ninyi mawakili, atakayepona kwenye utawala wa aina hii.

Kumbuka, kama Nimrod Mkono anaweza kufungiwa ofisi na TRA ni wakili gani mwingine aliye salama??? Kama wakili anaweza kukamatwa mahakamani kwa kufanya kazi yake ya uwakili, ni nani miongoni mwetu aliye salama??? Nendeni mkapige kura kukataa mfumo wa aina hii.

Mimi naenda mahabusu, na pengine, gerezani. Nawaombeni kura zenu ili niweze kuwaongoza katika kipindi hiki kigumu. 
Hiki sio kipindi cha kuwa na viongozi wanaojipendekeza kwa wanaokandamiza haki za watu wetu na haki za mawakili wetu. 
Hiki ni kipindi cha kuwa na viongozi watakaopigania haki zenu na haki za watu wetu. Mnanifahamu. Nipeni jukumu hili la kuwaongoza kwenye giza hili nene. Msikubali kuyumbishwa.

Na wachagueni pia Makamu wa Rais, Mweka Hazina wajumbe wa Governing Council watakaokuwa na msimamo kama wa kwangu.

Nawatakieni kila la kheri. I'll think of you all wherever they'll take me to, wherever I'll be incarcerated. This too shall pass. The race of man shall rise again. It always has. Nimemwambia na mke wangu naye aende Arusha akapige kura. So, everybody to Arusha. Go vote your consciences.

All the best.

TL

Magazeti ya Leo Alhamisi ya tarehe 16/03/2017



Jumatano, 15 Machi 2017

Kauli ya Godbless Lema kuhusu wabunge CCM waliokwenda kumsalimia gerezani kuitwa wasaliti


Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ameibuka na kueleza kushangazwa na kauli ya Rais Dk. John Magufuli kwamba wabunge wa CCM waliotaka kwenda kumwona gerezani walikuwa wasaliti.

Lema alisema anatarajia Spika wa Bunge, Job Ndugai, atatoa msimamo juu ya kauli ya kiongozi huyo wa nchi.

Kauli hiyo ya Lema imekuja siku moja baada ya Rais Dk. John Magufuli, kuripotiwa na chombo kimoja cha habari  kwamba alishangazwa na hatua ya baadhi ya wabunge wa CCM waliounda kamati ya kutaka kwenda kumtembelea Lema gerezani.

Katika mkutano wake na wabunge hao juzi uliofanyika Ikulu ndogo ya Chamwino mkoani Dodoma, Rais Magufuli alisema amekuwa akielezwa kuwa kamati hiyo ilikuwa imepanga safari za kutaka kwenda kumwona Lema alipokuwa gerezani jambo ambalo alilifananisha ni sawa na usaliti kwa chama chake.

Katika taarifa aliyoitoa jana kwa vyombo vya habari, Lema alisema kitendo cha wabunge hao kutaka kumtembelea si usaliti bali ni upendo ambao ni muhimu kwa binadamu yeyote pale anapokuwa na matatizo.

Lema alikaa gerezani kwa muda wa miezi minne kwa kukosa dhamana kutokana na mashtaka yaliyokuwa yakimkabili.

“Mheshimiwa Rais Magufuli nakusalimu. Nimetoka gerezani hivi karibuni ambako nilikuwa huko kwa zaidi ya miezi minne kwa kunyimwa masharti ya dhamana kwa dhamana iliyokuwa wazi.

“Nimeona kwenye vyombo vya habari leo kwamba wale wabunge waliokuwa wanataka kunisalimia nilipokuwa magereza ni wasaliti wa chama cha CCM.

“Mheshimiwa Rais wengi walinisalimia wakiwemo wachungaji, masheikh, wabunge na viongozi mbalimbali, sidhani kama hatua hii ilikuwa ni usaliti isipokuwa upendo ambao ni muhimu kwa binadamu yeyote pale anapokuwa na matatizo.

“Mheshimiwa  Rais nimeogopa sana kwa kauli hii, je Taifa linakwenda wapi? Hivi kweli sisi wabunge ni maadui? Kama viongozi tutafikiri utengano ni moja ya njia ya kuimarisha vyama vyetu, bila shaka tutakuwa tunalitendea Taifa ubaya,” alisema Lema.

Mbunge huyo alisema dhambi hiyo ikikomaa ni wazi kwamba lugha za kidini, ukanda na ukabila hazitaacha kukomaa.

Alisema ni muhimu sasa wakajenga utamaduni wa kuhimiza mshikamano wa kitaifa bila kujali itikadi kama kweli wanapenda masikini na wanyonge.

“Nawaomba wabunge wenzangu walionijali wakati niko gerezani wasijisikie vibaya kwani walifanya jambo jema na muhimu kwa wakati muhimu sana katika maisha yangu ninatarajia kuwa Spika wa Bunge atatoa neon juu ya kauli hii ya Rais.

“Mheshimiwa Rais wakati wa msiba wa Christina Lissu dada yake na Tundu Lissu, nilikuona katika msiba ule wewe na mama yetu mke wako, je wewe ulikuwa unasaliti chama chako?

“Meshimiwa Rais neno la Mungu linasema wapendeni maadui zenu, waombeni wanaowadhi, wabarikini wanaowaonea kwani kufanya hivi ni kuishi kwa thawabu za Mwenyezi Mungu,”alisema Lema.

Mbunge huyo alisema pamoja na hali hiyo ya kuzuiwa lakini aliwashukuru wabunge wa CCM kwa kwenda kumjulia hali, akiwa nyumbani kwake baada ya kutoka gerezani.

“Sina la kusema katika hili kama Rais alikuwa anajua hawakuja kuniona gerezani lakini niwashukuru wabunge wa CCM wote waliokuja kunijulia hali nyumbani. Sisi kama nchi tunatakiwa kuwa na umoja badala ya kuanza kubaguana kwa itikadi zetu za vyama.

“Mdogo wangu wa kike amepata mchumba lakini familia ya huyo mchumba wake inatokana na CCM je tuvunje vikao vya harusi kwa sababu ya tofauti ya vyama?

“Jibu ni hapana sisi ni Watanzania ni lazima tuishi kwa kupenda na kwa umoja kama ambavyo utamaduni wetu unatutaka na si vinginevyo,” alisema.

Lema alikamatwa Novemba 2, mwaka jana mjini Dodoma nje ya viwanja vya Bunge na kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Novemba 4 mwaka jana akikabiliwa na kesi mbili namba 440 na 441 za uchochezi dhidi ya Rais Dk. John Magufuli.

Katika kesi ya kwanza ya jinai namba 440, anadaiwa kati ya Oktoba 22 mwaka jana maeneo ya Kambi ya Fisi, Kata ya Ngarenaro, katika mkutano wa hadhara alitoa maneno yenye kuleta tabaka miongoni mwa jamii kwa kutoa matamshi yenye chuki, kuibua nia ovu kwa jamii.

Katika kesi ya pili namba 441, alidaiwa kwamba, Oktoba 23, mwaka jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Shule ya Sekondari Baraa, Lema  alitoa maneno kuwa:

“Kiburi cha Rais kisipojirekebisha, Rais akiendelea kujiona yeye ni Mungu, nimeota  Mwaka 2020 haitafika Mungu atakuwa ameshamchukua maisha yake,”.

Februari 27,  mwaka huu, Mahakama ya Rufaa Tanzania ilifuta rufaa mbili za Jamhuri dhidi ya Lema baada ya mawakili wa Serikali kuieleza mahakama  hiyo kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), hana nia ya kuendelea na rufaa, hivyo kuiomba mahakama kuzifuta rufaa hizo zilizokuwa zinahusu dhamana ya mbunge huyo.

Mwaka Mmoja ya Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda kuwa madarakani.......Yote Aliyoyasema Yako Hapa

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda leo Machi 15, 2017 anatimiza mwaka mmoja tangu ateuliwe kuwa Mkuu wa Mkoa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli Machi 13, 2016 na kuapishwa Machi 15, 2016.

==>Haya ni Baadhi ya Maneno Yake
1.Namshukuru Rais Magufuli kwa kusikiliza kauli ya Mungu na kunikabidhi mamlaka ktk mkoa huu wa Dar.

2.Navishukuru sana Vyombo vya Habari kwa kuwa daraja kati ya Serikali ya Mkoa na wananchi. Wamefanya kazi kubwa!

3.Nawashukuru sana vijana tuliowakamata wa mwanzo(TID na wenzake), wamekuwa mfano mzuri kwa wenzao na Mungu awasaidie

4.Mwaka wangu wa II nikiwa kama RC wa Dar, kasi itaongezeka maana nimekomaa sasa. Nitahakikisha jiji linarudi kwny mstari.

5.Kuna makampuni ya barabara mawili nimeshayapiga marufuku kwa sababu ya kujenga barabara chini ya viwango.

6.Katika vitu nimeweka msingi mzuri ni kinondoni, kesi za ardhi zinasikilizwa mpaka jumamosi

7.Kazi hii nimepewa na Mungu, acha idadi ya wanaomchukia Makonda waongezeka lakini niwe na uhakika na Mungu wangu

8.Tumeamua kufanya vitu hadharani kwa sababu hatutaki kupokea rushwa wala fedha haramu

9.Hatuna kisasi na mtu, ndio maana upande huo wanapigana sisi tunacheka

10.Kupitia fedha za dawa za kulevya, watu wamejenga maghorofa yanakwenda kwa kasi sana na wamefanya hata thamani ya viwanja ipande

11.Fedha hizi za dawa za kulevya zinaenda kukauka DSM ili kila mtu ale kwa jasho lake

12.Tutaanza mfumo wa kutumia kadi ili tukusanye kodi yetu na kila mtu ale kwa jasho lake, kuna watu wanaficha fedha

13.Kipindi hiki ni cha kazi. Nawapongeza wote wanaofanya kazi kwa bidii na kuifanya Serikali isimame kidete

14.Changamoto mojawapo niliyokutana nayo ni MUDA! Muda hautoshi, nahitaji hata miaka kadhaa ili kumsikiliza kila mwananchi

15.Changamoto nyingine ni mazoea ya Watendaji wa Serikali ktk kutoa huduma. "Njoo kesho" imekuwa kero kwangu na kwa wananchi

16.Kuzungushwa kwa wananchi kunapelekea changamoto katika za Serikali za Mitaa kuletwa ofisini kwangu. Hili nalo ni tatizo!

17.Nampongeza sana Kamishna Sirro na Awadhi (wa Usalama barabarani) kwa kusimamia ulinzi na usalama jijini Dar

18.Milio ya risasi ilikuwa kawaida Dar, watu waliogopa hata kwenda Mlimani City kwa hofu ya kuporwa. Tumeyakomesha yote hayo

19.Mtu anataka nikae kimya wakati wananchi wangu Dar wanateseka kwa matumizi ya DawazaKulevya... Nauliza "Wewe ni NANI?"

20.Tunapambana kupigania ndoto za vijana na matumaini ya wazazi wao. Haijalishi tumechelewa kiasi gani lakini hatutoacha!

21.Wapiga dili wa Bandarini jijini Dar wamekuwa wakisumbua kwa fedha zisizo halali na kuwasumbua wafanyabiashara halali

22.Sibabaishwi na watu wanaonichukia wakati nikitekeleza majukumu niliyopangiwa na Rais Magufuli kama Mkuu wa Mkoa.

23.Bureau de Change zinatumika kufichia pesa haramu. Wiki ijayo moto utawaka, lazima tushughulikie maficho haya.

24.Sasa foleni jijini Dar imepunguzwa kwa kiwango kikubwa na askari. Ukifurahishwa na trafiki toa shukrani zako, tuwape moyo.

25.Mwaka huu wa pili tutakazia sana kwenye utumishi. Nitaanzia kwenye Serikali za Mitaa nione jinsi wanavyowasaidia wananchi.

26.Nataka mwananchi apate majibu kamili aendapo Ofisi ya Umma. Kama hawawezi kumsaidia waende wao ofisi ya juu sio mwananchi.

27.Wanaoishi mabondeni jijini Dar na wana hati halali nitawapa viwanja. Watendaji waliotoa hizo hati nitawashughulikia!

28.Najua wengi wanaoishi mabondeni wamepangishwa na waliolipwa fidia. Huwezi kuwa na akili timamu ukakubali kupanga bondeni

29.Hivi karibuni nitaelekeza wapi showroom za magari zinatakiwa ziwe jijini Dar. Nataka magari yote yauzwe eneo moja

30.Ninawashukuru wanasheria wetu 35 wanaotoa msaada na ushauri wa kisheria bure kwa wananchi wa jiji la Dar wasio na uwezo

31.Tumepewa eneo kubwa la kujenga kambi kwa ajili ya wahanga wa DawazaKulevya. Hii itatusaidia kufuatilia mienendo yao

32.Hadi sasa tuna watu 11,854 jijini Dar waliokubali kuacha matumizi ya DawaZaKulevya kwa hiari. Haya ni mafanikio makubwa

33.Wengine tukiwaita Kituo cha Polisi wanatumia Colgate na Chumvi ili wasigundulike ktk vipimo. Tuna mbinu mpya za kuwapima

34.Kuna wanaowatumia watoto wadogo kufanya uhalifu na kabla ya hapo wanawavutisha bangi. Tunawasaka na tutawakamata!