ILULA IRINGA TANZANIA

ILULA IRINGA TANZANIA
KIKOTI.COM BLOG - ILULA IRINGA TANZANIA / 0769694963 .......................................

Alhamisi, 16 Machi 2017

WIZARA YA ELIMU YAPOKEA VIFAA VYA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU.

KONTENA LENYE KEMIKALI KWA AJILI YA MASOMO YA KEMIA NA BIOLOJIA TAYARI KWA AJILI YA KUSAMBAZWA.
Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya leo amepokea vifaa vya wanafunzi wenye  mahitaji maalumu vyenye thamani ya Shilingi bilioni 3.6 ambavyo vinalenga  kutatua changamoto ya upungufu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia .

Akizungumza wakati wa makabidbiano hayo, mhandisi Manyanya amesema baadhi ya vifaa Vilivyopokelewa leo ni pamoja na mashine za kuandika maandishi ya nukta nundu 932,  karatasi za kuandikia maandishi ya nukta nundu ream 2548,karatasi ya kurudufishia maandishi ya nukta nundu ream 1150,shime  sikio ( hearing Aid) 1150, vifaa vya upimaji kielimu.

Naibu waziri manyanya amewataka maafisa Elimu nchini kote  kuhakikisha walimu waliopata mafunzo ya watu wenye mahutaji maalumu wanakwenda kufundisha katika shuke hizo na si vinginevyo.

Hakuna maoni: